Mkuu Mwanakijiji,
Umenena Ya liyo ya kweli ,ila nachokwambia na walichoamua baada ya kikao kilichopita cha Baraza la Mawaziri,wameweka msimamo wa Serikali.Ni Pinda alishatoa Muungozo wa nini Kitakachojiri leo.na Mambo ambayo wameamua kufanya kwa kifupi
Wameshindwa kutuzuga na wameamua kutulazimisha tukubali
Rejea kauli ya Pinda kuhusu suala la Meremeta,walishatuzuga sana kipindi kile kuhusu Kampuni hii,alijaribu karamagi akashindwa na njia ambayo wametumia sasa ni kutumia Ubabe wa kutulazimisha tukabalia hata kaam hatutaki.Ndiyo maana Pinda akapindisha kwa kusema Merermeta ilikuwa ni mali ya Jeshi na Usalama.Sian uhakika ni lini Nchii hii ilishaanzisha Vyombo vya Usalama kwa Ajili ya Biashara.
Na hili la leo watatulazimisha tukubali kile ambacho hatukitaki na tunakijua kwamba walihujumu na kuchukua mali zetu.Kama Jana Ulimsikia Ngeleja akitoa Muhtasari utajua ni nini leo atazungumza
Kuhusu DOWANS na Richmond
Leo tutegeme mambo ambayo hatukuwahi kabisa kujua ila tutalazimishwa kuyameza,Jana Ngeleja akihojiwa na TBC! alisema seriklali haiikuwahi kuwa na Mkataba na Dowans na wameuvunja,cha kujiuliza hapa ni hiki
1.Je serikali ambayo tunaiamini iliwezaje kulipa pesa nyingi kiasi hicho bila ya kuwa na mkataba na kampuni hii.Kama ni hivyo ina maana hata malipo yaliyofanyika haijulikani yalilipwa kwa nani.Huku ni kutulazimisha kwa nguvu baada ya uzugaji kushindikana
2.Mkataba ulivunjwa na TANESCO,ila ukiangalia mwanzoni serikali ilikuwa ya kwanza kufanya nao mazungumzo,ilikuwaje TANESCO haikufanya hivyo ila baadaye waje wavunje mkataba.
3.Dr. Idrisa Rashid Alisema kwamba Wamevunja Mkataba,Serilai inasema kulikuwa hakuna Mkataba,sasa tumuelewe nani?Leo tutapata Majibu
Tumuachie Ngeleja azungumze Msimamo wa Serikali,ila siyo mawazo yake na hii ndiyo mbinu mpya ya serikali iliyobuniwa ili kujibu mapigo.Ndiyo maana hata Rais kwa sasa hatoi Hotuba za mwisho wa Mwezi na kamuachia Rweyemamu ambaye atakuwa akipewa maelekezo kutoka kikao cha Baraza la mawziri na makatibu wakuu.
Naomba nijibiwe leo,Msimamo wa serikali ni kitu Gani,Je Serikali imechaguliwa na Nani,Bila sisi kuna Serikali??Ikiwa Kama ni sisi tunasababisha inakuwapo serikali Je Msimamo wetu ni upi?