Mkapa above the law?: Allegations

Mkapa above the law?: Allegations


....kitila Mkumbo Una Akili Sana ...wala Haikuwa Ajabu Pale Ulipopewa Nafasi Ya Kufanya Kazi Pale Udsm ..mara Tu Baada Ya Ku Graduate....

Nafikiri Umetoa Mwelekeo Wa Namna Tunavyotakiwa Kuyachambua Mambo Hapa Jf.........maana Wengi Hapa Wanapenda Tu Kusema ...mkapa Hakufanya Kitu!!!....au Mkapa Sio Fisadi !!!

Naomba Wachambuzi Mfuate Msingi Alioleta Kitila Ili Hii Mada Ichambuliwe Kitaaluma Zaidi.....naomba Kuwasikia Wachambuzi Maarufi ..kama Rev Kishoka ,kichuguu,fmes,....na Wengine.....woote!!

phillemon mikael,

Mimi si maarufu lakini nakumbuka siku Mkapa amewaita waandishi wa habari na kueleza nia yake ya kutaka kugombea Uraisi, alizungukwa na watu wawili. Kwa upande moja alikuwapo Waziri Mkuu mstaafu, Judge Sinde Waryoba na upande wa pili alikuwepo aliyekuwa Mtendaji Mkuu wa wakati huo wa Habari Corporation, Jenerali Ulimwengu. Nakumbuka Watanzania wengi, pamoja na kutoridhika na utendaji wa CCM, tulikuwa na kila sababu ya kuwa na "HOPE" especially baada ya utawala wa Ali Hasan Mwinyi. Na kilichowaongezea matumaini wananchi wengi ni kule kuungwa mkono na Baba wa Taifa, Mwl. J.K. Nyerere. Hata hivyo kuna wachache kati yetu tuliojiuliza mara mbili hivi huyu Mkapa anatokea wapi na sifa zipi zinamfanya awe chaguo bora. Wenzetu walio ughaibuni na hasa nchi ya Marekani alikowahi kuwa balozi walitueleza jinsi alivyojumuika nao kwenye shughuli mbalimbali. Sifa zilianza kutafutwa ili aweze kuuzika na moja tu ilipatikana, hakuwa na kashfa iliyojulikana. Iweje hii iwe sifa pekee na itoshe kumkabidhi any Tom, Dick na Harry jukumu la kuongoza nchi - kosa namba moja.

Nakumbuka pia siku alipokutana na waandishi wa habari, kwa mara ya kwanza na ya mwisho, baada tu ya kuchaguliwa kuwa Rais. Ubabe aliouonyesha siku hiyo did not befit mtu aliyewahi kuwa balozi wa nyumba kumi leave alone balozi wa nchi. Tabia hii ilitosha kabisa kuwasha taa nyekundu of what was in store for us lakini kama kawaida ya Watanzania tulifunikwa na wingu la uCCM ambalo liko tayari kuita koleo kijiko. Rais huchaguliwa na kuapishwa kuwa ataitetea na atailinda katiba ya nchi ambayo kimsingi ni kulinda haki za wananchi wake. Katika mwaka wake wa kwanza tu Mkapa alivunja katiba kwa kukatisha maisha ya wananchi waliokuwa wanadai haki huko Pemba. Pia alishindwa kuwalinda wananchi waliokuwa wakishangilia ushindi wa Mbunge wao wa Temeke na kusababisha wengine wapate vilema vya maisha.

Madhambi mengine yamekwishatajwa lakini kuna mawili zaidi. Moja, katika kipindi chake mkewe alinunua jengo lililokuwa likitumika kama tawi la benki NBC kwa njia ambayo kwa nchi zenye sheria, hutafsiriwa kama fraudulent. Pili, katika utawala wa Mkapa, pamoja na kuigeuza Ikulu sehemu ya biashara, hasara ambayo nchi iliipata kutokana moto mkubwa uliounguza sehemu muhimu ya Ikulu bado haijulikani.

Hitimisho: Kujaribu kumtetea Mkapa kwa kutaja mazuri aliyoyafanya (ambayo ni wajibu wake) na kulinganisha na mabaya (ambayo si wajibu wake) ni ujuha usio mfano.Watu wamefungwa na wengine kunyongwa kwa sababu kuna siku walienda kinyume cha wajibu wao licha ya waliyotenda awali. Mabaya aliyofanya Mkapa akiwa Rais wa Tanzania hayasameheki.
 
Kama tulikataa hawa mafisadi wasijisafishe kwenye majukwaa ya kisiasa...Wakakimbilia vijijini na huko majimboni mwao...Hiyo haiukutosha.

Wakayatumia majukwa ya Dini husasan Kanisa.

Sasa wanajuwa kuwa mjadala huu unakwenda Bungeni...Na wabunge hawana ujanja kwani wanahitajika kutaja interests zao zote ili tusikie kama kweli maslahi wanayopigania ni ya Taifa.

Wabunge hao kama wananchi walio wengi...Wanaufuatilia mjadala huu na mingineyo pia.

Hivyo MSIMAMO WETU HAPA NI KUWA MAHAKAMA ITASAFISHA WATU MARA BAADA YA BUNGE KUSOMA RIPOTI NA KUZIJADILI VILE INAVYOPASWA.

Mkapa ana tuhuma za jinai...Hazitafutwa kwa mijadala kama hii ya kusema eti ni msafi.Period. What a crap!

Hata hivyo siwezi kumlaumu mtu kwani ni weekend hii na wabunge wanatingisha KIBERITI ama ni wanamtandao.

Nadhani watakutana na askari wa JF.
 
Sina haja ya kwenda kumuuliza yoyote kuhusiana na 'mazuri' ya Mkapa. Hao wafanyakazi unaowataja wamejaa tele hapa JF na sijasikia hata siku moja wakimtetea fisadi Mkapa. Wewe unayemtetea labda ulinufaika kwa namna moja au nyingine na ufisadi wa Mkapa, lakini Watanzania walio wengi hawakunufaika na chochote.

Nimeuliza mazuri aliyoyafanya fisadi Mkapa ni yepi? Je, yanaweza kuwekwa hapa? 😕
Ooh! Kamuulize huyu kamuulize yule! Nyerere ameng'atuka miaka 23 iliyopita pamoja na kuwa alikuwa na makosa yake lakini leo hii ukiuliza Watanzania wengi mazuri aliyoyafanya Nyerere basi hawatapata kigugumizi na kukwambia labda nenda kawaulize watu wa Butiama au wale waliokuwa Ikulu wakati alipokuwa madarakani. Toka kona moja ya nchi mpaka kona nyingine ya nchi Nyerere mazuri yake hayajifichi pamoja na kuwa mengine hayakuwa na mafanikio makubwa kutokana na sababu ambazo zilikuwa nje ya uwezo wake kama kupigwa vita na mataifa ya magharibi kwa kufuata siasa za ujamaa na pia kupanda kwa bei kubwa ya mafuta duniani mwaka 1973, vita dhidi ya nduli Idi Amini 1979, na ukame mkubwa ulioikumba Tanzania mwaka 1975.

Sasa uliza matatizo ya Mkapa yote yamesababishwa na wizi na ufisadi wake na sera ambazo zilitowa upendeleo dhahiri kwa wageni wachukuaji badala ya Watanzania.

Kwa Watanzania wengi Mkapa ni fisadi tu na wengi tungependa afikishwe Mahakamani kushtakiwa dhidi ya wizi alioufanya na hatimaye kufilisiwa. Sheria za nchi ni lazima ziwabane wote bila upendeleo wowote wa kujali wana utajiri mkubwa kiasi gani au walikuwa na wadhifa mkubwa kiasi gani ndani ya chama au serikali.


mazuri nimekuorodheshea lakini kwa vile una jibu tayari ndio inakua vigumu kuyaona.
1.ametia uhai elimu iliyokua inaelekea kuzimu.
2.ameanza kuajili walimu walikua wamepigwa lumba kali zaidi ya miaka 5bila ajira
3.Wafanya kazi walianza kulipwa mishahara kwa wakati
4.wafanyakazi walianza kulipwa malimbikizo yao
5.wafanya kazi walisogezewa huduma kwa kuletewa mishaharra katani na si kuzifuata wilayani zaidi ya mile 50.
6.wanafunzi waliongezeka mashule kwa ailimia 90%
7.karibu kila mtoto mwenye kwenda shule alikwenda
8.alfuta michango ya upe shuleni
9.ndio chachu cha ongezeko la shule
10.amerudisha hali ya watanzania kupenda kuajiliwa na kuitumikia serikali yao
11.amerejesha heshima ya serikali
12.amekuza uchumi kwa 6%
13.amefufua viwanda na makampuni yaliyokufa
 
mkandara,

upande niliosimama mie ni kutaka kuona wale wote wanaohusika na ufisadi wafikishwe kunako chombo cha haki (sijui kama hili linawezekana). sina hata chembe ya nia ya kumtetea fisadi yeyote yule.

naafikiana nawe kwamba ufisadi wa bot haukuanza na awamu ya nne bali toka enzi ya bwm ulikuwepo. na nina hakika upekuzi wa kina ukifanyika utavumbua mengi zaidi hadi yale yaliyopelekea benki kuu kuunguzwa na moto.

ndio maana nimesema kama hoja ni kurutubisha mchenguo wa wanayoendelea sasa basi namuombea mzee butiku mafanikio (na sio kejeli bali ni maombi ya dhati). ila wasiwasi wangu pia ni uwezekano wa hoja zake kukwamua uhusiano wa bot na uchaguzi na awamu ya nne na kulengesha fikra za watu kwa bwm. sasa haya ni mawazo tuu na yaweza kuwa kweli au yasiwe na ukweli binafsi naomba sana mawazo yangu yasiwe na ukweli.

Mchango mzuri Kafara.
 
Mkamap,
Mkuu nashinda hata kuelewa ulichosimamia hapa..
Umezungumzia viwanda kuwa makazi ya nguchiro kama utani ama una uhakika wa hilo maanake kusema rahisi sana!.. Imekuwaje viwanda hivyo viendelee kuzalisha bila wawekeshaji kuweka mashine mpya!.. Na vile vilivyouzwa vingine baadhi mashine kung'olewa na kusafirishwa Kenya ambako na kuuzwa kama vipuri, kisha walionunua viwanda kutumia viwanja hivyo kuanszisha miradi mipya.. Je walichouziwa ni kiwanda kukiendeleza ama ilikuwa kuondoa taka!..Umemsikia mwenyewe Mizengo Pinda akilaumu kuhusu Reli, tazama ATC, NBC bado kitu gani unataka hasa kutuelezea hapa!..Kuna shirika hata moja ambalo limefikia hata kiwango cha juu wakati wa mwalimu?

Kama alivyosema Jasusi, siku zote kizuri kujiuza!
Mkuu kama Mkapa alifanya lolote bora ingeonekana wazi kabisa. Mchango wa vitu hivyo vyote alivyouza ktk mfuko wa Taifa % leo hii umepungua kuliko wakati wowote ule!... hili ni somo mojawapo..Sasa hivi tunategemea vitu vingine kabisa ambavyo havina faida kwa mwananchi..
Kama kweli kuna mazuri sii myaseme? kuonyesha ubovu wa vitu vilivyokuwepo haiwezi kudhihirisha UBORA ikiwa hakuna matunda ya kufanya hivyo!..
Hata mguu unapopata matatizo makubwa na kuanza kuharibika, unaweza kuondolewa ikiwa kuondolewa kwa mguu huo utasababisha kupona kwa mtu huyo, lakini ni ujinga mkubwa kuondoa mguu wa mtu bila kutazama replacement za mguu huo! kuzama ndani kiutaalam na kupata jibu sahihi la maradhi ya mguu na afya nzima ya mhusika kabla hujaondolewa.... hatukufanya hivyo.

Kichekesho cha mfumo wa Mkapa ni kwamba mguu huo ulioondolewa umeenda kutumiwa na mtu mwingine mwenye maradhi kama yetu na umefanya kazi....tulichofanya sisi mkuu ni kutoa donation ya kiungo chetu. Hii ndio lugha mnashindwa kuifahamu kwa sababu upeo wenu wa kutazama unaishia pale mguu ulikuwa una matatizo na tulishindwa kutembea... Hivyo kata hakuna haja ya kumwona daktari..Hii ndio taabu ya WANASIASA wanapoingilia UCHUMI..
IMF ni soko la kukusanya hizi organs kwa hiyo mawazo yao kwanza yatakuwa kuwaponyesha kina Trump kabla hawajakufikiria wewe ngozi ya tako..Mawazo ya Mkapa yahana tofauti na Mhindi anayetoa organ yake kuiuza kwa sababu hana kazi nayo....Leo tunatembelea magongo tunashindwa hata kuyatupa!.. pona yenyewe tunamwomba Mungu bado wewe unaona bora uzima wa magongo..

Haya hayo mazuri uliyoyataja unaweza kutupa takwimu zake maanake tunarudia mada iliyokwisha siku nyingi..unavuta vitu ambavyo nina hakika huwezi kuvielezea zaidi ya kuandika juu juu..
 
Huyu mtu anayedai kuwa someone ni safi namuuliza swali moja!
MEREMETA NI YA NANI?
Kwasababu ndiyo maana hatutaki kuwasaidia wabunge kwenye mjadala wao.
Kuna maswali mengi ambayo hata huyu bongotz mwenyewe hawezi kuyajibu hapa...Na hivyo kuufanya mjadala huu kuwa BUTU!
Kwani ukiambiwa ni mchafu kwasababu hizi ama zile...Huwezi kuja na sababu za kupingana na sababu tutakazozitowa hapa!
Ndugu yangu uliyeleta mada hii naomba uendelee kuomba Mungu tu.
Huo ndio ushauri wangu...Zaidi ya hapo unajitafutia presha ya bure.
 
mazuri nimekuorodheshea lakini kwa vile una jibu tayari ndio inakua vigumu kuyaona.
1.ametia uhai elimu iliyokua inaelekea kuzimu.

Mpango wa shinikizo la kusamehewa madeni. Conditions za kusamehewa madeni zilitaka fedha zinasamehewa ziende kwenye afya, elimu. Siyo ugenious wa Mkapa. Na ukilinganisha utaona pia kuwa hakuweza kwa kiasi kikubwa kwenye elimu zaidi ya kuongeza kilichoambacho kilikuwa kimepungua.

2.ameanza kuajili walimu walikua wamepigwa lumba kali zaidi ya miaka 5bila ajira

Kuwaajiri walimu ambao ni substandard kwa kuteremsha kiwango cha elimu wanayotakiwa kuwa nayo na pia kwa kushindwa kutoa motisha wa kutosha kupeleka walimu maeneo ya vijijini na ya pembezoni mwa nchi yetu hayo si mafanikio.

3.Wafanya kazi walianza kulipwa mishahara kwa wakati
Ndio walianza which has nothing to do with being paid on time!

4.wafanyakazi walianza kulipwa malimbikizo yao
kwa miaka kumi ameshindwa kulipatia ufumbuzi suala la wastaafu wa Afrika ya Mashariki. Leo hii mstaafu wa Tanzania yuko nyuma sana katika malipo wakati chini ya utawala Rais mstaafu akajitengenezea kipackage chake cha kustaafu!


5.wafanya kazi walisogezewa huduma kwa kuletewa mishaharra katani na si kuzifuata wilayani zaidi ya mile 50.
Haya siyo mafanikio, hili ni jambo ambalo lilitakiwa kufanyika na hata hivyo bado kuna kazi kubwa sana katika kulipa watumishi wa serikali hasa walio mbali na mabenki na makao makuu ya wilaya.


6.wanafunzi waliongezeka mashule kwa ailimia 90%
Natural increase.

7.karibu kila mtoto mwenye kwenda shule alikwenda
Wangali walifaulu na kuendelea na wangapi walielemika. Chini ya utawala wake illiteracy level ilifikia asilimia 31!


10.amerudisha hali ya watanzania kupenda kuajiliwa na kuitumikia serikali yao
of course.. do you really want to know why?

11.amerejesha heshima ya serikali
Absolutely, wao wenyewe kuheshimiana na kuoneana aibu!

12.amekuza uchumi kwa 6%
The best spin.. uchumi umekua in relation to uchumi wa nani? Unajua sasa hivi ni maskini zaidi kuliko tulivyokuwa miaka mingi iliyopita. Kukua uchumi siyo sawasawa na kuondoa umaskini!

13.amefufua viwanda na makampuni yaliyokufa
Kwa kujiuzia yeye mwenyewe mengine na kuwaacha wezi waje waibe viwanda vyetu mbele ya macho yetu. Ni chini ya mkapa TTCL, NBC, ATC.... zote zilifufuliwa!
 
Mkamap,
Mkuu nashinda hata kuelewa ulichosimamia hapa..
Umezungumzia viwanda kuwa makazi ya nguchiro kama utani ama una uhakika wa hilo maanake kusema rahisi sana!.. Imekuwaje viwanda hivyo viendelee kuzalisha bila wawekeshaji kuweka mashine mpya!.. Na vile vilivyouzwa vingine baadhi mashine kung'olewa na kusafirishwa Kenya ambako na kuuzwa kama vipuri, kisha walionunua viwanda kutumia viwanja hivyo kuanszisha miradi mipya.. Je walichouziwa ni kiwanda kukiendeleza ama ilikuwa kuondoa taka!..Umemsikia mwenyewe Mizengo Pinda akilaumu kuhusu Reli, tazama ATC, NBC bado kitu gani unataka hasa kutuelezea hapa!..Kuna shirika hata moja ambalo limefikia hata kiwango cha juu wakati wa mwalimu?

Kama alivyosema Jasusi, siku zote kizuri kujiuza!
Mkuu kama Mkapa alifanya lolote bora ingeonekana manufaa yake. Mchango wa vitu hivyo vyote alivyouza ktk mfuko wa Taifa % umepungua kuliko wakati wowote ule!... hili ni somo mojawapo..
Kama kweli kuna mazuri sii myaseme? kuonyesha ubovu wa vitu vilivyokuwepo haiwezi kudhihirisha UBORA ikiwa hakuna matunda ya kufanya hivyo!..
Hata mguu unapopata matatizo makubwa na kuanza kuharibika, unaweza kuondolewa ikiwa kuondolewa kwa mguu huo utasababisha kupona kwa mtu huyo, lakini ni ujinga mkubwa kuondoa mguu wa mtu bila kutazama replacement za mguu huo! kuzama ndani kiutaalam na kupata jibu sahihi la maradhi ya mguu huo kabla hujaondolewa.

Kichekesho cha mfumo wa Mkapa ni kwamba mguu huo ulioondolewa umeenda kutumiwa na mtu mwingine mwenye maradhi kama yetu na umefanya kazi....tulichofanya sisi mkuu ni kutoa donation ya kiungo chetu. Hii ndio lugha mnashindwa kuifahamu kwa sababu upeo wenu wa kutazama unaishia pale mguu ulikuwa una matatizo ya tulishindwa kutembea... Hivyo kata hakuna haja ya kumwona daktari..Hii ndio taabu ya WANASIASA wanapoingilia UCHUMI..
IMF ni soko la kukusanya hizi organs kwa hiyo mawazo yao kwanza yatakuwa kuwaponyesha kina Trump kabla hawajakufikiria wewe ngozi ya tako..
Mawazo ya Mkapa yahana tofauti na Mhindi anayetoa organ yake kuiuza kwa sababu hana kazi nayo....
Hayo mazuri uliyoyataja unaweza kutupa takwimu zake maanake tunarudia mada iliyokwisha siku nyingi..unavuta vitu ambavyo nina hakika huwezi kuvielezea zaidi ya kuandika juu juu..

Mkapa is the best president.
Ila kosa lake tu nikuongoza Taifa bovu kama Tanzania.

Ngoja nitoke nje ya maada kidogo
Kama wa marekani na waingereza wangekua werevu kama Watanzania
BREA,BUSH mwana na BABA leo hii wangekuwa wananyea SEGELEA ama GWATANAMO.
 
Mkapa is the best president.
Ila kosa lake tu nikuongoza Taifa bovu kama Tanzania.

Ngoja nitoke nje ya maada kidogo
Kama wa marekani na waingereza wangekua werevu kama Watanzania
BREA,BUSH mwana na BABA leo hii wangekuwa wananyea SEGELEA ama GWATANAMO.

Kwahiyo Mwalimu alipokufa ama kuuwawa..Alimwachia maagizo Andy Chande ampe MKAPA?

Na uzuri wa Rais wanausema wananchi ama wewe ama manyapara wengine pamoja na MAFIOSO WA FREEMANSON?
 
Mkamap,
Blea na Bush wanatazama maslahi ya nchi zao kwanza.. Ubaya wao ni mtazamo wa haki za kibinadamu lakini wanachokitaka Iraq, Iran, Venezuela Korea na kwingineko kote ni faida kwa nchi zao..
Tatizo kubwa linalowakaribiri watu hawa ni gharama ya kuvipata vitu hivyo!..hili ndio somo kubwa Marekani na Uingereza!
Bush wala Blea hakuna mwizi kati yao na wasingechukua hata siku 100 Ikulu kama wangekuwa na mfano mdogo tu wa Mkapa..
Mkuu umeshindwa kuitazama picha na nini wana JF wanakizungumza hapa.
 
Mkapa is the best president.
Ila kosa lake tu nikuongoza Taifa bovu kama Tanzania.

Ngoja nitoke nje ya maada kidogo
Kama wa marekani na waingereza wangekua werevu kama Watanzania
BREA,BUSH mwana na BABA leo hii wangekuwa wananyea SEGELEA ama GWATANAMO.

Mkapa will always remain a fisadi, corrupt leader and very selfish who did nothing to benefit Tanzanians. Na Tanzania kwa taarifa yako si Taifa bovu bali tuna viongozi wabovu na mafisadi kama fisadi Mkapa na wengineo wengi.
 
Mkamap,
Blea na Bush wanatazama maslahi ya nchi zao kwanza.. Ubaya wao ni mtazamo wa haki za kibinadamu lakini wanachokitaka Iraq, Iran, Venezuela Korea na kwingineko kote ni faida kwa nchi zao..
Tatizo kubwa linalowakaribiri watu hawa ni gharama ya kuvipata vitu hivyo!..hili ndio somo kubwa Marekani na Uingereza!
Bush wala Blea hakuna mwizi kati yao na wasingechukua hata siku 100 Ikulu kama wangekuwa na mfano mdogo tu wa Mkapa..
Mkuu umeshindwa kuitazama picha na nini wana JF wanakizungumza hapa.

Wamesahau mambo ya Freemanson...!

Wanadhani JF ni kijijini...Hapa data zote ziko na watu wanajuwa kila kitu.

Wao saa nyingine wakipita hapa wanakuta watu saa nyingine wanapiga soga basi wanafikiri ni kila taimu!

Hawajuwi kuwa sasa sisi FOCUS yetu ni huko bungeni.

Mimi namlaumu sana mwalimu.

Aliwakumbatia wahindi na Watutsi na sasa ni balaa!

Hata kuna wakati kina Mtikila wakaanza kusema huyu mwalimu ni Mnyarwanda...Na yeye na Museveni ndio basi tena usiseme!

Museveni yeye alikuwa Butiama nafikir karibia kila weekend.

Yeye akifikiri anasuluhisha mgogoro wa Rwanda na Burundi na kumbe wenzake wanautumia ukarimu wake kwa watu wengine wasiokuwa watanzania kwa kumpangia mkakati!

Sasa tukisema Mwalimu aliuwawa kuna atakeyebisha?

Kama huyu Andy na Kahama wote wana heshima ya U SIR waliyopewa na Malkia...Na mwalimu mwenyewe akawa anawaheshimu na kuwapa mustakabali waTaifa na huku akiwa hajuwi kuwa hao watu ni watumishi wa Mkoloni yule yule ambaye anapingana nao tena bado kwa fikra zake za kijamaa!

Hakujiuliza hayo?

Sir Chande alisimamia wakati wa Nyerere...Labda alisaidia kuuangusha ujamaa...Mwalimu mbishi..Akamwachia aendelee kuwa kinara wa Mwinyi...Bado tu combination ya Kahama na Chande.

Baada ya Mwinyi kufanya mambo si mambo...Mwalimu akapiga kelele kuwa ikulu ni pango la wanyang'anyi...Bado hakujuwa tatizo ni Chande na kahama?

Ama na yeye alikuwa na yake?

Haya...Mkapa akasaidiwa tena na hao hao...Sasa wakaongezeka kina RA na wanamtandao.

Sasa Nasikia tu ni mambo ya ukabila na Mwalimu mwenyewe alikufa na baada ya hapo ni champaigne tu kati ya Andy Chande Na Ben Mkapa maybe na hata kina Kahama na Mfisadi wengine ambao sasa wamejikita kwenye UTAJIRI WA HALI YA JUU!

Sasa na hao watutsi nao walihusika?

Mkapa anaweza kutupa data?
 
Tatizo tuangalie ukweli na fact harafu sio kulaumu kila kitu.

Mtu huwezi kuja na hoja eti kizuri cha jitembeza kwa kuchukua maoni ya wana JF na wanachama wa upinzani wa chache ambao msmamo wao wajulikana.

Uetembelea Tz yote ukatambua kua Mkapa hajiuzi ama unatumia sera za hisia ??

Mkapa
kama naye angekuja na kukumbatia hizi nyumba za nguchiro na kuacha madini yakae ardhini mpaka Watanzania wapate elimu leo hii TZ ingekua moja ya mahala pa ajabu sana duniani saizi palivyo ni infinity ahueni.
Kwa maana elimu inayosubiliwa isingekuwepo wala kuja maana walimu tayari walikua wamenza kukimbia.

Filosofia nzuri ni-
Kama wewe ni kibabu cha miaka 80 huwezi shika jembe na huna mtaji wala jinsi ya kuishi na wajukuu wako 10 walio na miaka chini ya 5 wanakutegemea wewe .Na hapo hapo wewe kibabu unashamba la hekali 100.

Sasa wewe kama una akili nzuri ni kumtafuta mtu mwenye uwezo wa kulilima na kumwambia bwana chukua shamba hili bure lima hili shamba lakini ktk mavuno utakayopata wewe nipe mavuno yatakayo niwezesha kula mwaka mzima na wajukuu wangu pia vijisenti vidogo vya matibabu na kuwawezesha hawa wajukuu kwenda shule.

Sasa wewe kama babu ukijifanya mkono wa birika eti unataka kukodisha kwa ma bilioni na kama akikosa likae hivyohivyo mpaka wajukuu wako watakapopata uwezo wa kulilima
Kwanza utakufa kwa Njaa wewe mwenyewe pia wajukuu wako hawatakua nao watakufa kwa njaa harafu shamba litabaki wazi na watu watakuja kulilima bure.

Kumbe babu yule alilotoa bure ni mwerevu kwanza anauhakika japo ananyonywa lakini ktk wajukuu wale wanaokwenda shule lazima wapo wataoendelea vizuri na kuja kulidai shamba lao kisomi zaidi na pia kuliendeleza shamba lao kisomi zaidi.

Sasa hawa wajukuu nao wata kapokua na kuanza kumlaumu babu yao kwanini alilitoa shamba lao bure >Na kwanini asingelikondisha tangu ezi hizo mamilion ya fedha leo hii sisi wajukuuu tungekua mamilionea na malalamiko ya aina hiyo kutoka kwa wajukuu .Kama babu bado yupo atawaelezea hali ilivyokua na bado wakiendelea kuhoji ,Haina shaka babu kuanza kuhoji UELEWA WAO yani IQ yao.
 
Mkapa will always remain a fisadi, corrupt leader and very selfish who did nothing to benefit Tanzanians. Na Tanzania kwa taarifa yako si Taifa bovu bali tuna viongozi wabovu na mafisadi kama fisadi Mkapa na wengineo wengi.
Tanzania sio mbovu ila wabovu ni watanzania
 
Maneno yako hayo mazuri ila tunasubiri yasemwe Bungeni na Mahakamani.
Then tutajuwa sasa itakuwa vipi...Then kama Msafi..tutajuwa still.
Ila naomba unijibu kuhusu huo uhusiano wa Mkapa na Chande.
 
Mkapa is the best president.
Ila kosa lake tu nikuongoza Taifa bovu kama Tanzania.

Mkamap,

Umeniacha hoi hapa - hebu elezea kidogo una maana gani na Taifa bovu. Halafu huo ubovu wa taifa unasababishwa ama umesababishwa na nini. Kama Mkapa alikubali kuwa president wa taifa bovu na hakuweza kuikwamua kutoka kwenye ubovu, atakuwaje Best President. Hakika hapo unajikanganya.
 
Ninaposoma kuwa kuna watu wanatetea utawala wa Mkapa, ukweli huwa nasikia kizunguzungu sana. Ni kweli kuwa kuna makosa yatokanayo na upungufu wa kibinadamu ambayo ni vigumu mtu mwenyewe kuyathibiti. Mkapa alikuwa nalo moja la namna hiyo kama vile kile kiburi chake cha kuamaini kuwa yeye ndiye mwenye akili tu na wengine wote wasiokubaliana naye ni wajinga; na tabia hii alikuwa nayo tangu hata kabla hajawa rais. Nadhani sote tunakumbuka onyo lililotolewa na balozi Mwakasakufya (sina uhakika na spelling) aliyewahi kufanya naye kazi kwa muda mrefu sana kuhusu tabi hiyo hata kabla ya uchaguzi wa mwaka 1995. Makosa haya bado anaweza kuyafanya hadi leo hata kama hayuko madarakani kwa vile hayo ni inherent kwake

Hata hivyo makosa tunayomlaumu bwana Mkapa siyo ya aina hiyo, bali yale aliyofanya kwa makusudi huku akijua kuwa ni makosa ila kwa vile alikuwa na madaraka hakuna ambaye angemfanya lolote; ni makosa ya dhidi ya ethics za madaraka aliyokuwa amekabidhiwa. Na kwa vile madaraka hayo ndiyo yalikuwa ultimate, yaani hakuna zaidi yake, ni lazima tutamlamu sana kwa vile makosa yake yaliitia nchi hii katika matatazio makubwa sana kwa kipindi cha miaka mingi ijayo. Sitaki kuyataja makosa hayo kwa vile yameshaandikwa sana na yote yameacha athari ambazo zitavikumba vizazi na vizazi vijavyo.

Si sahihi kujaribu kumtetea Mkapa kwa kumlumu Nyerere kwa vile Mkapa aliaza kuvuruga nchi baada ya Nyerere kufariki na kuwa ameoshaondoka madarakani takriban miaka kumi na tano. Wakati Nyerere akiwa hai, Mkapa alikuwa anazingatia sana maadili yake ya kazi (japo kwa kinafiki.) Tangu Nyerere atoke madarakani, kuna matukio mengi duniani hapa ambayo yamebadili sana mwelekeo wa uchumi wa dunia, la muhimu likiwa ni lile la kuisha kwa vita baridi. Kama bwana Mkapa ndiye angekuwa kiongozi wa nchi hii wakati wa vita baridi, sina wasiwasi kuwa huenda bwana huyu angekuwa kama Mobutu tu.
 
Mkamap,
Mkapa
kama naye angekuja na kukumbatia hizi nyumba za nguchiro na kuacha madini yakae ardhini mpaka Watanzania wapate elimu leo hii TZ ingekua moja ya mahala pa ajabu sana duniani saizi palivyo ni infinity ahueni.
Kwa maana elimu inayosubiliwa isingekuwepo wala kuja maana walimu tayari walikua wamenza kukimbia.

Filosofia nzuri ni-
Kama wewe ni kibabu cha miaka 80 huwezi shika jembe na huna mtaji wala jinsi ya kuishi na wajukuu wako 10 walio na miaka chini ya 5 wanakutegemea wewe .Na hapo hapo wewe kibabu unashamba la hekali 100.

Sasa wewe kama una akili nzuri ni kumtafuta mtu mwenye uwezo wa kulilima na kumwambia bwana chukua shamba hili bure lima hili shamba lakini ktk mavuno utakayopata wewe nipe mavuno yatakayo niwezesha kula mwaka mzima na wajukuu wangu pia vijisenti vidogo vya matibabu na kuwawezesha hawa wajukuu kwenda shule.
Mfano wako mzuri sana mkuu tena hapo nakupa pongezi..
Na ndio maana nimesema umeshindwa kuona wanachozungumza wana JF..
Alichofanya Mkapa ni kuwaozesha wale wajukuu kwa watu wenye fedha kisha ule mtaji akauweka benki na kutangaza maendeleo.. hao wajukuu ambao walikuwa miaka 8, 9 na 10..
Na kila naposoma maandishi yako yananipa hisia kwamba hata wewe ungefanya hivyo hivyo kwa sababu kusubiri mtoto wa miaka 8 apate elimu ya msingi, sekondary kisha sijui chuo kikuu loooh sii utakuwa umesha kufa?... kwa hiyo solution ni kuwaozesha mapema kabla hujafa..mnachotazama ni maisha yenu nyie vizee sio ya kizazi kijacho!..
Ndicho alichofanya Mkapa ktk maendeleo ya Tanzania... period!
 
Back
Top Bottom