Hapo ndipo ninaposhangaa...nchi inaendeshwa kienyeji-enyeji, kijinga-jinga, kiusanii-sanii, kiwizi-wizi...na katika yote hayo ni wananchi ndio wanaolipia gharama kwa kutaabika. Nchi nzima tunajua hilo, tunalilalamikia kila siku/saa/dakika/sekunde...angalia vyombo vya habari vyote ikiwemo mtandaoni! Tunapiga-piga kelele tu...tumeshashushuliwa kelele za mlango (wananchi) hazimnyimi usingizi mwenye nyumba (wenyenchi), bado tu tupo-tupo kama mazuzu!
Leo hii madaktari wametuonyesha ya kuaddress sensitive issues kwa serikali hii 'kiziwi' na 'pofu'...na kwa kubanwa huko serikali inaanza angalau kusikia na kuona....watu wanaona wivu na kuwabeza! Eti kwa nini maDaktari!? waTanzania mnataka nini!? Kama mnamsubiri 'mesiya' aje kuondoa kilio chenu sisi waKwere tunasema 'kalagha baho', endeleeni kusubiri!