Mgomo wa madaktari - Updates

Mgomo wa madaktari - Updates

Hivi kati ya Pinda na Dk Mponda na Dk Nkya nani anastahili kujiuzulu?
 
Pinda alisema serikali imejipanga. Tuendelee kusubiri huku wagonjwa wakifa ili tuone jinsi ilivyojipanga?? Wafe watanzania wangapi ndio tuone hili likitatuliwa?
 
Hivi kati ya Pinda na Dk Mponda na Dk Nkya nani anastahili kujiuzulu?

Kilaza aliyepanga mjengo wetu wa Magogoni, Al hajj, Dr. Dr. Dr. Professor to be Kikwete naye aondoke na wakina mponda au mpondwa, ahame na nchi kabisa wengine tukimuona hatuwezi kumvumilia ujinga wange, tunatamaani tu*********
 
...kuunganisha suala la kugoma na kujiuzulu kwa Mawziri ni UKILAZA USIO NA KIFANI.............. [/QUOTE] Kwa hiyo wewe una akili nyingi kuliko madaktari wakiwekwa pamoja? Usilolijuwa ni sawa na usiku wa giza. Ina maana hata kama wewe ungekuwa kwenye nafasi ya Mponda ungegoma kujiuzuru kwa kuwa huoni mantiki?
 
Na hao watakaokufa kwa kugoma kwako uletewe watoto wao?

Miaka 10 ninatibu sasa,nilijitolea kuishi kwa prophylaxis ya TB pale kibong'oto for 8yrs lkn ugonjwa kama HEPATITIS B ambao chanjo yake ipo siwezi kuvumilia!!!Kama kauli imekukwaza I'm really sorry lkn inauma kuona watu wakidhani kuwa daktari ni kujitolea kufa kizembe.
 
Wewe mwenyewe si uwa unajisema..Kuna post yako kule jukwaa la malalamiko umejiita hivyo.
natoa pongezi kwa serikali yetu ilivyojipanga kupambana na mgomo wa madaktari kwa kuwaajiza warusi,waquba na wahindi huziba pengo habari za ndani ya carpet wapo kwenye maandalizi ya mwisho kesho kutwa wanawasili hongera mh.pinda kwa ulivyojipanga.:A S 465:
 
inasikitisha hadi sasa hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa kuokoa hali hii... tunaumia ni sisi wananchi na ndo tuliowapa dhamana ya uongozi , je ndo malipo mtulipayo haya???
 
Ni upuuzi kumpa masharti rais.

Wewe ndio huelewi Rais mpuuzi ndio anapewa masharti, elewa kuwa kuna aliyevaa bango limeandikwa "mimi ni mpuuzi" kila asomaye humcheka, kama anachukia kuchekwa, simpo!!!! vua bango walk freeeee, kamwe hatutajivika ujinga kuutetea ujinga uliofungamanishwa na taasisi ya urais.
 
Taarifa zilizonifikia kutoka vyanzo vya kuaminiaka bugando wamebandika tangazo likisomeka hivi

"KUTOKANA NA SERIKALI KUTOKUWA TAYARI KUSHUGHULIKIA MADAI YA MADAKTARI IPASAVYO SISI MADAKTARI TUMESIKITISHWA SANA. KUANZIA LEO TAREHE 7 MACHI 2012 SAA 2; 00 ASUBUHI,MADAKTARI WA HOSPITALI YA BUGANDO TUNASITISHA KUTOA HUDUMA ZOTE MPAKA HAPO SERIKALI ITAKAPOSHUGHULIKIA MADAI HAYO.
JUMUIYA YA MADAKTARI BUGANDO (INTERN,REGISTRARS,RESIDENTS)
NAKALA KWA WAKUU WA IDARA,UTAWALA BMC"

MUHIMBILI
EMD-KITENGO CHA WAGONJWA WA DHARURA KIMEFUGWA

OPD-WAGONJWA WAMEJAA LAKINI HAWAONI

THETRE HAZIFANYI KAZI NA MASPECIALIST WAPO RUSSIAN CULTURE TO PUT LAST NAIL IN THE COFFIN. WAMEUNGANA NA WATAANZA MGOMO RASMI LEO.

AMANA
TOTAL TOOLS DOWN

MWANANYAMALA
TOTAL TOOLS DOWN EXCEPT 4 COs

TEMEKE
TOTAL TOOLS DOWN

MBEYA
WANAENDELEA PALE WALIPOISHI MAANA MGOMO KAMA KAWA

IFAKARA
TOTAL TOOLS DOWN

TUMBI
HALI TETE

BOMBO
WASALITI WACHACHE,TOOLS DOWN

KCMC
RESIDENT ROHO KWATU,INTERNS SOLIDARITY FOREVER. TOOLS DOWN

IKULU-TISS TUKIMWONDOA MPONDA NA NKYA WATAOMBA ATAKAYEFUATA NI PM (MR CROCODILE-JINA LAKE JIPYA) THEN MBAYUWAYU.
KWA UFUPI HALI NI TETE UMOJA WAO NI WA MFANO KESHO NITAWAPA MAMBO MAKUBWA YANAYO KUJA
 
Vimon,
Tunashukuru sana kwa update! Msalimie Dk Ulimboka!
 
Kwa hiyo wewe una akili nyingi kuliko madaktari wakiwekwa pamoja? Usilolijuwa ni sawa na usiku wa giza. Ina maana hata kama wewe ungekuwa kwenye nafasi ya Mponda ungegoma kujiuzuru kwa kuwa huoni mantiki?
Mkuu kwa hiyo wewe unataka mawaziri wajiuzuru kwa sababu madaktari wenye akili saana wametaka hivyo?.. Kwa nini wewe mwananchi mwajiri wa hawa wote usitake kujua hao mawaziri wamekosea nini kikubwa hadi ifikie wajiuzuru?
Kwa nini mazungumzo baina yao yanakuwa na usiri fulani wakati bunge lipo na mahakama zipo kwani vyombo hivi kazi yake ni nini? Hivi kweli leo hatma ya nchi yetu imeshikwa mikononi mwa watu sijui wasomi ambao ndio watoa hukumu bila kupitia hatua za kisheria.

Kugoma wagome hatuwakazi ni maamuzi yao lakini wasitegemee wananchi wote tunawaunga mkono kwa sababu waliua watu na wanaendelea kuua watu ati kwa sababu ya Mponda na Nkya. Kwa nini wasiseme JK ajiuzuru maana huyu ndiye kawawekea kifua mawaziri wote nchini. Yaani namkumbuka sana mwalimu Nyerere na tutamkosa sana!
 
kwani kujiuzulu kwa hawa mawaziri ni dhambi au ni aibu ? Mbona ni jambo la kawaida jamani. Kama vile alivyojiuzulu mkurugunzi wa IMF japo hakuwa na kosa lolote. Jamani watanzani hasa mliopo kwenye ngazi ya juu embu kuweni na utamaduni wa kuwajibika
 
kwani kujiuzulu kwa hawa mawaziri ni dhambi au ni aibu ? Mbona ni jambo la kawaida jamani. Kama vile alivyojiuzulu mkurugunzi wa IMF japo hakuwa na kosa lolote. Jamani watanzani hasa mliopo kwenye ngazi ya juu embu kuweni na utamaduni wa kuwajibika
Kama mnadai wana dhambi ni lazima dhambi zenyewe zitajwe.. Huyo mkurugenzi wa IMF kajiuzuru kwa sababu zake mwenyewe, hata wewe ukiwa mgonjwa unaweza jiuzuru kazi lakini sii kwa tuhuma za wizi au kumbaka mtu..
Kama makosa yapo kweli basi madai yafikishwe ktk vyombo vya sheria au hata kamati ya Bunge iwasikilize madai yao kutaka mawaziri hao wajiuzuru kisha kisha ndio maamuzi yatafuata. Kina Lowassa, Karamagi na wengineo wasingejiuzuru kama swala lile lisingefika bungeni, huu utaratibu kwa nini leo mnataka kukiuka na kuchukua mamlaka mikononi mwenu kama kumpiga mwizi wa Manzese!
 
Back
Top Bottom