.... Hapa Tanzania, Kuna haja kubwa ya migomo makazini kuanza kutumika kama mashinikizo kwa serikali yetu... Bunge na kanuni zake naona hazitoshi na hazitoshelezi!!
....Migomo makazini kwa nchi nzima is an unexplored option ambayo ni "salama" na huleta matumaini kwa wanyonge pale ambapo haki hazitendeki au zinakiukwa makusudi!!
....Kama migomo inakubalika, Watanzania tukubali kusafa kwa hata wiki moja alimradi tu hatuanzishi uasi baina yetu ili kuonesha kutoridhishwa kwetu... at the end of the day, tunasafa tayari na kupotea kwa hela hizi ambazo nyingi zinaendelea kupotea bila hata wanaohusika kuona adha inayowapata walalahoi.
Hii ni bonge ya point.....
Unajua hawa wanasiasa wetu....hawana uchungu kabisa na rasilimali za taifa letu.
Cha kwanza hawalipi kodi katika asilimia 90 ya matumizi na mapato yao. Hivyo sisi wafanyakazi ambao kila tunachokifanya tunakatwa kodi lazima tusikie uchungu tunapoona kodi zetu zinachezewa.
Wao wananunuliwa magari, tena 4WDs, wanayatumia kutoka kwenye nyumba za kupewa bure oysterbay na Masaki, mafuta wanajariwa kila siku, kila kikao wanalipwa (hata huko bungeni.....safari, malazi pamoja na chakula na chenchi kubaki juu).
Sisi walalahoi, gari ukinunua ndo utalipia kodi mpaka ulie, mshahara unakatwa, ukipewa bonus inakatwa, ukinunua mafuta kuna mikodi kibao, chakula ghali coz ya mikodi kibao,,,, etc etc.
Wao wamekalia tu kutumia, hawajui kuchangia kuongeza kipato cha nchi...ndo maana walipoona EPA wakafikiria jinsi ya kuitumia, Meremeta nayo hivyo hivyo,,,na mengine mengi.
Hawa mafisi-hadi washatuona sisi wananchi ni wapumbavu sana, kwanza nashangaa kwa nini tuwaite waheshimiwa....tumewachagua sisi ni sawa na kuwapa kazi watutumikie sisi, watuheshimu sisi, wawe answerable kwetu, na ndo maana tunawalipa, lakini wao washaona ni haki yao kuwa viongozi na sisi vibaraka wao.
Sasa ni wakati tuamue tusizalishe......tuone watakula wapi, watapata wapi kodi....by the way nimekuwa nikifikiria hakuna njia ya mtu kukataa kukatwa kodi???? kama hawa watu hawako wazi na tayari kuonyesha matumizi ya jasho langu, je nalazimishwa kulitoa???