Meremeta & TANGOLD Revealed!

Meremeta & TANGOLD Revealed!

Pinda has nothing to loose... nikitoa sbb nitaambiawa na mnyanyapaa....hamjui alichofanya kwenye part ya kupongezwa kuwa cheo fulani hivi miaka ya nyuma na rafikie Paul Kimiti... aibu..
 
Maskini mafisadi wamemchukua na huyu PM wetu tuliyemuamini sana.......sasa tutakimbilia kwa nani???
 
...Ukiona wanapaaza sauti zao bila woga ujue hayo ni mabadiliko makubwa maana wakati wa lile dude liitwalo Mkapa walikuwa kama watoto wa shule ya msingi.

...Wakati wa Nyerere Bunge la Chama kimoja wabunge walikuwa ni waumini na Nyerere alikuwa Mungu mtu....

...This is a step forward in the awakening the peoples minds.

Tanzania haikuwahi kuwa na Bunge.

Niliwahi kusema institutions zilizojengwa na Nyerere zilikuwa kazi yake ku rubber stamp his policies and sermons.

It's been a presidential one man's show all along.

Think about it: The Pindas of Tanzania ndio walikuwa wamemzunguka Nyerere na Marais wengine. Sasa huyu Mtoto wa Mkulima masikini angeweza kumwambia nini Nyerere au Mkapa jamani?
 
Ninavyoelewa mimi jambo technical ni jambo lenye ugumu wa kiufundi, kama ukimuuliza Pinda kwa mfano kuhusu mambo ya wagonjwa Muhimbili ambayo yanahitaji ujuzi wa ufundi wa kidaktari anaweza kukwambia "mimi siwezi kujibu jambo technical"

Lakini hii ni excuse kwa sababu Waziri Mkuu ana washauri wenye kujua technical detail, anaweza asiweze kujibu hapo kwa papo, lakini kama ni kitu anachotakiwa kujibu hii siyo excuse ya kutojibu, anaweza kushauriana na washauri wake.

Anatuonyesha zaidi asivyoijua kazi yake.


OOh asante sana nimekupata..
 
CHEYO akataa hoja ya waziri mkuu kuwa meremeta ni mali ya jeshi.

Amesema kuwa meremeta ya kwanza ilikuwa sahihi ila ya sasa ni meremeta ya pili.

ameshika shilingi.
 
Maskini mafisadi wamemchukua na huyu PM wetu tuliyemuamini sana.......sasa tutakimbilia kwa nani???

Kama ulimuamini hiyo ni sehemu ya tatizo, Watanzania tunaamini amini watu kirahisi rahisi tu.

Tunaletewa rais anayekenua meno bila merit, tunaamini, PM mwenye shady and corrupt past kama Lowasa, tunaamini, hatujui hata kujifunza huyu Pinda naye jina lake tu Mizengwe Pinda lilitosha kutushtua (joking), hana rekodi wala nini, wapi, tunafurahiii.

Tukae tukijua matatizo ya Watanzania yatatatuliwa na Watanzania wenyewe, hamna kiongozi atakayeleta utatuzi sehemu yenye corruption kama hii mpaka alazimike kufanya hivyo.

Na tukiamini amini tu tunakuwa hatufanyi kazi yetu ya kuwashurutisha kufanya kazi yao kwa uadilifu.
 
Tanzania haikuwahi kuwa na Bunge.

Niliwahi kusema institutions zilizojengwa na Nyerere zilikuwa kazi yake ku rubber stamp his policies and sermons.

It's been a presidential one man's show all along.

Think about it: The Pindas of Tanzania ndio walikuwa wamemzunguka Nyerere na Marais wengine. Sasa huyu Mtoto wa Mkulima masikini angeweza kumwambia nini Nyerere au Mkapa jamani?

Tatizo la Pinda ni yeye kukubali kudanganya kuhusu hili.Na ukitaka kujua nini nini Pinda angezungmza leo.Kama ulikuwa po bungeni angalia aliongea na kina nani jana.

Aliongea na Thomas Mwang'onda na baadhi ya watu..Hivi wamiliki wa Meremeta ni kina tena ??
 
Cheyo:
Kwa jibu. Meremeta ya kwanza ilikua inahusu jeshi, meremeta ya pili katika task force,, iliyokua reported na Mwanahalisi,,, mfano inaonyesha kuna fedha ambazo ziko tangold bilioni 11 kwenda Meremeta na inaonyeshwa katika takwimu na imepokea fedha kutoka BoT na sio hivyo, Meremeta ina Anthony Buler ambao ni wageni sasa hao hawahusiki na Meremeta ya zamani. Ningeshauri jambo hili lifanyiwe uchunguzi wa kina pameonyeshwa kuna fedha Dola laki nne na 57 kwenda kwenye akaunti ya mtu anayetajwa na kuihusisha na jeshi tunakosea,… Serikali imefambwa sana na ,,,, hili limeulizwa hata na kamati ya madini… Tutendee haki Watanzania, kama kuna bilioni hazina wenyewe tunazihitaji tukachimbie visima…..


Marmo: Kwanza nafarijika kusikia kwamba…. Hakuna Meremeta mbili ni moja tu…. Kama alifuatilia vyema ni kwamba kwa kweli Waziri Mkuu alipofikia amefungwa mikono, lijadiliwe mahali na kama ni lazima sana. Si vyema kutafuta nyaraka kinyemela

CHEYO: Hata Gavana wa BoT alisema walioshiriki Meremeta ya pili walishiriki under their personal capacity.
 
bADO CHEYO asimamia hoja na naibu spika anaitetea serikali kuwa hoja ni wizi wa meremeta bado anaendelea kushikilia shilingi.

Agoma na anasema kuwa ni afadhali serikali ikubali na iende kuliangalia hili jambo na source ya information wanayo anataka kuupata ukweli juu ya jambo hili.

waziri mkuu kasimama sasa.
 
...Kama ulikuwa po bungeni angalia aliongea na kina nani jana.

Aliongea na Thomas Mwang'onda na baadhi ya watu..Hivi wamiliki wa Meremeta ni kina tena ??

Kwa hiyo jana ndio alipo anza kuuliza Meremeta ya nani?
 
SEHEMU YA HOTUBA YA DR SLAA ALIYOWASILISHA BUNGENNI

"Pamoja na Taarifa ya Ufisadi ndani ya BOT pia hakuna hatua yeyote iliyochukuliwa kuhusu maeneo mengine tuliyoyaibua mathalan Ufisadi kupitia Kampuni ya Meremeta na Tangold. Waziri wa Fedha ambaye ndiye mwenye dhamana na makampuni hayo katika majibu yake siku ya ijumaa amerusha maswala hayo kwa Mawaziri wa Kisekta. Inawezekana Serikali inasubiri Bunge liunde tena Kamati Teule nyingine kwa lengo la kupitia makampuni haya ambayo umiliki wake umegubikwa na utata mkubwa kutokana na Meremeta kuandikishwa Uingereza ikiwa na Hati ya Usajili na 3424504 ya Tarehe 19 August,1997 na kupata Hati ya Kutimiza Masharti (Certificate of Compliance) nchini Tanzania kama Tawi la Kampuni ya Kigeni yenye na 32755 ya tarehe 3 Oktoba, 1997. Kinachoshangaza katika Kampuni hii ni kuwa wenye hisa wake tofauti na Bunge lilivyoelezwa mara nyingi, ni Triennex(PTY) Ltd ya Afrika Kusini yenye hisa asilimia 50%, Msajili wa Hazina mwenye hisa asilimia 50% kwa niaba ya Serikali ya Tanzania na Kampuni mbili za London Law Services Ltd wa Temple Avenue, wenye hisa 1% na London Law Secretarial Services Ltd ambao anuani yao ni sawa na hao wenzao, nao pia wana hisa 1%. Hii Meremeta hasa ni ya nani, na hawa London Law Services na London Secretarial Services ni akina nani hasa. Kampuni ya Meremeta ina hisa asilimia ngapi? Haya ni mambo yanatufanya tuwe na mashaka makubwa sana. Hivi Serikali inaogopa nini kuweka mambo haya wazi hadharani, angalau kwa Kamati husika ya Bunge basi ili kama kuna sababu ya msingi wawakilishi wa Wananchi waweze kufahamu.

Vivyo hivyo kwa Kampuni ya Tangold ambayo ilisajiliwa katika kisiwa cha Mauritius tarehe 05 April,2005 Ikiwa na Hati ya Usajili na 553334 na kupata Global Business Licence( C2/ GBL) tarehe 08 April,2005. na kupata Hati ya Kutimiza Masharti hapa nchini tarehe 20 February 2006. Hata hivyo Mhe. Spika, Taarifa zilizoko ni kuwa Tangold imekuwa na akaunti NBC Corporate Branch, no. 0lll03024840 iliyofunguliwa Tarehe 1 January, 2003, yaani miaka miwili kabla Kampuni hiyo haiijasajiliwa Mauritius na takriban miaka 4 tangu imepata Hati ya ‘Kutimiza Masharti’ Tanzania. Ni kwa vipi, kampuni hii kufanya kazi wakati Bunge lilijulishwa na Mhe. Waziri Karamagi kuwa ndiyo iliyorithi Meremeta baada ya Meremeta kufilisika? Mhe. Spika haya maswali yanahitaji kujibiwa kinagaubaga ili kuwarudishia Watanzania imani kuhusu kinachojiri na usalama wa Rasilimali na fedha zao. Waziri Mkuu ndiye mtu stahiki wa kurudisha imani hii kama Kiongozi wa Shughuli za Serikali Bungeni, baada ya Waziri wa Fedha kushindwa kutoa majibu ya kuridhisha jana. Isitoshe, Makampuni haya tangu yaliposajiliwa nchi za nje na hata hapa Tanzania japo yamekuwa na akaunti katika Benki za nje na za Ndani Hesabu zao hazijakaguliwa na chombo chochote hadi leo (hatujui kama itakuwa imekaguliwa na CAG katika Taarifa ya BOT ya 2007/2008 ambayo haijawasilishwa Bungeni bado).

Wahusika wa Tangold ni Bodi ya Wakurugenzi ambayo ni viongozi au waliokuwa viongozi waandamizi katika Serikali. Wakurugenzi hao ni pamoja na hayati Daudi Balali aliyekuwa Governor wa Benki Kuu (BOT), Andrew Chenge aliyekuwa Waziri wa Miundombinu, Gray Mgonja, Katibu Mkuu-Wizara ya Fedha, Patrick Rutabanzibwa- Katibu Mkuu-Maji na Vincent Mrisho-Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu."


MIMI SWALI LANGU HAPA NI KWAMBA MBONA KWENYE HAO WANAHISA WA MEREMETA SIONI JESHI? CHA KUSHANGAZA ZAIDI JESHI HUWA HALIFANYI WALA HALIJIHUSISHI NA BISHARA, KAZI YA JESJI NI KULINDA NA KUHAKIKISHA TAIFA NI SALAMA, SASA JESHI NALO SIKUHIZI LIMEJIINGIZA KWENYE KUANZISHA MAKAMPUNI? WAZIRI MKUU BADO HAJATOA MAJIBU HAPO. TUNAOMBA WAZIRI MKUU AJIBU HOJA KAMA ILIVOULIZWA NA DR SLAA KWENYE HOTUBA YAKE HAPO JUU
 
On this one tuko ukurasa mmoja, hatutaacha jiwe hata moja un-turned! Waache kwanza wamalize kudanganyana huko bungeni halafu ndio tuanze kazi rasmi hapa Jambo Forum ya kuwaanika mafisadi na watoto wao, wake zao, wajomba zao, mama zao, mpaka baba zao wadogo,

Oooh yeah I said it, wote wamenufaika na this misery of our nation!

Niliwahi kugusia hapo nyuma kuhusu varangati kati ya mtoto wa mboma na yona iliyotokea baa moja huko sinza siku za nyuma.
Cha kushangaza uligeuka kuwa mzozo ambao ulisuluhishwa na Che Nkapa..

Just imagine watoto wanakwaruzana baa kwenye kinywaji inakuwa ni kesi ya kusuhishwa na presidaa..nadhani katika usuluhishi wake aliwaambia nyie ni watoto wa familia moja na baba mmoja hivyo msigombane baa mtawa watu picha ya bure wapate ya kuzungumza mtaani..maana watoto walikuwa wanataka kuonyeshana nani zaidi!!

Ngoja niendelee kuunganisha dot...si jambo la kupuuzia
 
waziri mkuu asisistiza kuwa hawezi kusema kwani meremeta ,deepgreen finance,Nedbank,Trinex na Tangold zote zilikuwa zinahusika na jambo moja .

amesema kuwa hawezi kusema ni ulinzi gani wa nchi ...no way thank you Pinda
 
bADO CHEYO asimamia hoja na naibu spika anaitetea serikali kuwa hoja ni wizi wa meremeta bado anaendelea kushikilia shilingi.

Agoma na anasema kuwa ni afadhali serikali ikubali na iende kuliangalia hili jambo na source ya information wanayo anataka kuupata ukweli juu ya jambo hili.

waziri mkuu kasimama sasa.

Lete habari...Maana data zote na ushaidi UKO WAZI.
Na huyo CHEYO NAMSIKILIZA TU!
KAMA AMEAMUA KUBADILI MAWAZO baada ya kuona kuwa sasa ni wazi kunawaka moto...Basi aprove hivyo kabla hajatoka huko bungeni na kurudi kwa wananchi kuomba kura kwani tunawafuatilia kwa makini sasa ili tujuwe nani ni nani,kwanini,na wanataka nini.
 
Cheyo:
Kwa jibu. Meremeta ya kwanza ilikua inahusu jeshi, meremeta ya pili katika task force,, iliyokua reported na Mwanahalisi,,, mfano inaonyesha kuna fedha ambazo ziko tangold bilioni 11 kwenda Meremeta na inaonyeshwa katika takwimu na imepokea fedha kutoka BoT na sio hivyo, Meremeta ina Anthony Buler ambao ni wageni sasa hao hawahusiki na Meremeta ya zamani. Ningeshauri jambo hili lifanyiwe uchunguzi wa kina pameonyeshwa kuna fedha Dola laki nne na 57 kwenda kwenye akaunti ya mtu anayetajwa na kuihusisha na jeshi tunakosea,… Serikali imefambwa sana na ,,,, hili limeulizwa hata na kamati ya madini… Tutendee haki Watanzania, kama kuna bilioni hazina wenyewe tunazihitaji tukachimbie visima…..


Marmo: Kwanza nafarijika kusikia kwamba…. Hakuna Meremeta mbili ni moja tu…. Kama alifuatilia vyema ni kwamba kwa kweli Waziri Mkuu alipofikia amefungwa mikono, lijadiliwe mahali na kama ni lazima sana. Si vyema kutafuta nyaraka kinyemela

Cheyo: tusionee JWTZ hapa kuna tatizo

Pinda: Inapofikia mahali unashindwa hapa tuseme nini, Hakuna cha Meremeta moja au mbili, kuna TRINEX kuna Deep Green kuna task force: Cheyo anataka kutuambia tusema hawa wote walikua wana deal na nini, nasema NO!!!
 
waziri Mkuu Asisistiza Kuwa Hawezi Kusema Kwani Meremeta ,deepgreen Finance,nedbank,trinex Na Tangold Zote Zilikuwa Zinahusika Na Jambo Moja .

Amesema Kuwa Hawezi Kusema Ni Ulinzi Gani Wa Nchi ...no Way Thank You Pinda

Ni ulinzi Wa Mjangili Mwambie Kama Hasemi Mtasema!
 
Hii safi sana kwani naona hata sisi wana jf tuko DODOMA!
LETA MAMO KIELEWEKE!
 
Back
Top Bottom