Naomba wachangiaji tutafute data za hizo pesa toka UN zilivyopotea kwani si busara kumvalia njuga Kasusura kwa wizi wa dola milioni 2 huku mabilioni ya Taifa yakipotea bila jibu la maana.
naona mada imekwenda kwa manji.
Pia Mzee ES nimepunguza credibility yangu kwako mfano umesema kuwa umeongea na mzee wa nchi halafu huyo mzee wa nchi hajui hata idadi ya pesa ambazo zipo kwenye issue sensitive kama ya NSSF? Ina maana kukalia madaraka makubwa ya nchi huku hajui suala la Mengi/Manji na NSSF huyo si mzee wa nchi na wala hastahili kupewa au kuendelea kukalia nafasi hiyo.pia usitegemee data zake kabisa na hao ndio wagomvi wetu tumewapa nchi watuongoze kumbe mbumbu mzungu wa reli.
Suala hili ni kama drama kila siku lipo hata kama mtu uko nje ya nchi. mimi nimeanza kuliona toka toleo la pili la magazeti ya this Day/Kulikoni back to march this year. Na hakuna nakala inayoka kwenye magazeti haya bila issue hii tena yapo on-line
www.ippmedia.com.
Pia Mengi na Manji hawaja-settle nje ya mahakama kama ulivyodai mzee Es kwani suala linasubiri tarehe ya kupangwa kusikilizwa na Manji amedai Billion mia moja.
Mbunge Adam malima yeye hakuhusishwa na Manji kilichotea alikuwa anachangia hoja ya waziri Mohamed Seif khatibu yaani wizara ya habari wakati wa bajeti nadhani ilikuwa mwishoni mwa july. ambapo akasema Mengi amekuwa akijipiga debe kuliko Rais kwenye vyombo vyake vya habari suala hilo ndio likapelekwa kamati ya maadili ya bunge ambapo for the past 3 weeks kikao kinaendelea Dodoma.
Sasa utaona This Day walianza nalo toka machi tena ni second issue. Hapo utaona Mkurugenzi wa NSSF na MALIMA hakuna uhusiano ktk issue hizi mbili.
Binafsi nimeamua kuwa mshiriki humu kwa kushawishiwa na wakata issue kama rafiki yangu Fikiraduni na mada yetu ya Mzumbe, wewe mzee ES nimeona unafagiliwa sana na Tafiti then Jadili. Ila tunapoingia humu tusiweke habari tusiokuwa na uhakika nayo kwani tutakuwa hatuna tofauti na magazeti ya Kasheshe, komesha na akina kaboka mchizi.
Ni bora mtu unyamaze lakini ukija humu uje na dozi kamili na kama unapata habari hizo source ziwe za uhakika. sio lazima mtu achangie tu humu kila siku hata kama habari zenyewe ni nyepesi nyepesi.
Nimelazimika kusema haya kwa heshima niliyompa ES na hata alipoanza kuandika akasema 'WAZEE WANGU HATIMAYE NILIONGEA NA MZEE MMOJA WA NCHI' ikimaanisha utafiti wako umezaa matunda.
Pia kama kuna mtu anadai anatetea maslahi ya nchi na akawa hata hajui kama kuna mabilioni karibu 40 yamepotea kwa jina la Mengi au haijui issue ya NSSF sidhani kama mtu huyo kweli anatetea maslahi ya nchi.
ndio maana nilipoanzisha topic hii nikasema hapa nategemea watu watanifungua macho bado namshukuru Tafiti ingawa naye ame divert mada ila faida tumepata kama kuona Press release ila amesahau naye kuna kesi ya DR. mahalu na Mengi(This day).
ADMINISTRATOR- kuna issue mbili tofauti (1) kesi ya Manji na mengi kuhusiana na This day na kulikoni. na (2) wizi wa mabilioni ya UN kwa ajili ya Watanzania wenye ukimwi pesa hizo zimepotea kiajabu na zilitiwa kupitia jina la Mengi hapa Manji hahusiki hata kidogo mimi nauliza issue hii, kwani mengi hakuletewa pesa kama yeye bali kaletewa kwa ajili ya Taifa hapa ndio naomba tusaidiane wenye data za uhakika.
Mwisho mzee Es inabidi ukiwa na mchango ufanyie utafiti maana tunakutegemea sana humu,kuna mawili matatu ulinitia mashaka nyuma. mfano kwenye mada ya Mkurugenzi wa usalama wa Taifa ulisema kuwa kuna nyumba ilinunuliwa mwaka 1960 kama nyumba ya ubalozi. ukipiga hesabu fupi tu. utagundua mwaka 1960 hata uhuru hatujapata.
Pia kuna mada ya Mbowe na CCM ukasema wewe unamjua sana Mbowe na watu wengine wawili uliwataja lakini ukaja kusema gazeti la Tanzania Daima linamilikiwa na Mtandao! wakati mtu haitaji kumjua Mbowe ili kujua kama ni mkurugenzi wa gazeti la Tanzania Daima.
Naomba sana msamaha kama nimuvuruga lakini lengo forum iwe inajadili vitu kwa kina, hatutaki kuja kuitwa Wazee wa NYEPESI NYEPESI mliopo nje ya nchi akina Firaduni ulizeni kwa jamaa zenu waliopo hapa kwa bimkubwa(bongo) nini maana ya nyepesi nyepesi