Mengi vs Manji: Ukweli ni upi?

Bwana tafiti
naheshimu sana mawazo yako ila naku hakikishia kwamba hapa hakuna kitu na Warioba hatafika mbali . Umesha chukua side lakini ujue Mengi is not saving Watanzania kwa habari bali anatangaza mtandao.Kazi kwako na mimi yangu macho tuone mtakako ishia .
 
mimi nadhani na wewe bwana Mugishagwe umeshachukua side kwa vile ''mengi is not saving watanzania bali anatangaza mtandao'' huu ni msimamo very clear kuwa na wewe unakerwa na tabia za mengi.

Naomba ufafanue unaposema Warioba hafiki popote, do you know something we don't? huyu ni jaji na mwanasheria maarufu mjini amekwenda mahakamani kuomba haki itendeke, unataka kusema warioba anajisumbua kwa vile Mengi ''hashtakiki'' au Warioba ni zoba hivyo anajipotezea muda kuwa mengi analindwa?

Mimi nilidhani tungengoja tuone wamefikia wapi katika kesi ili kujua mambo yakoje,nashukuru umechangia kistaarabu as always unlike others...

Please fafanua ndugu yangu..
 
Warioba si Zoba kabisa na aa haki ya kuomba Mahakama impe haki . Pia Mengi simpendi maan anatumia vibaya vyombo vyake lakini kwa issue ya warioba na Manji .

Ila Kweli Wariona kashitaki Kulikoni na Magazeti ya This Day ama ni mimi sijaelewa ? Kama ni kweli basi tungoje tutaona sooooooooooooote . Mzee Es mwamshe huyu tafiti naona hajafanya utafiti wake .
 
Tafiti,
Kitu ambacho waandishi wetu wanapaswa kuzingatia, hasa katika hizi makala za investigative reporting, ni kuhakikisha kuwa wana wanasheria ambao wanaweza kuwasaidia kuhakikisha kuwa ripoti zao ni sue-proof. Kama wana uhakika wa kile wanachoandika, then well and good, and they must be prepared to prove it. Nakumbuka Jaji Warioba alitahadharisha wakati ile ripoti ilipotoka kuwa wasimhusishe na hiyo kampuni ama sivyo ata -sue. They kept quiet. So unless they know something we do not know!
 
Jasusi sitaku kusema sana ila kuna moto mbele na mnaweza msijue maamuzi ya Mahakama mwisho wa siku . Kazi kubwa hiii wazee.
 
Sasa Mugishagwe maelezo yako na yangu yana tofauti gani? kiasi nihitaji kuamshwa! Mugishagwe take time to read my submission na za kwako utaona tunaongea almost lugha moja...nadhani usikurupuke kupinga kabla hujajua hoja hasa ni ipi...au na wewe una msimamo kuwa chochote mtu fulani akisema ni cha kupingwa?!

tuwe na mijadala constructive...

Mzee Jasusi

Naona umekata points hapo, ni kweli kabisa hoja yako nadhani waandishi wanahitaji kuwa na wanasheria ili kuwaguide zaidi.

Kwenye uandishi hapa UK media lawyers ni kama editors vile nao wana power ya kuapprove stories na kutaka ziwe edited ili kuondokana na legal consequences.
 
Kama mtu anataka kuwaset up mbona ni jambo rahisi... I'll bet you this.. wakienda mahakamani documents zote walizo nazo TD zitagundulika kuwa ni fake na hapo ndipo watakapojikuta "wanakombwa"....
 
tafiti
Futa usemi wako wa kusema msimamo wa kukupinga .Hapana sina muda mchafu wa kukupinga kama umesema point . Sijakupinga ila nimepiga kelele uamke .Mzee Mwanakijii umesema jambo zuri wacha uone .Hapa sasa mchezo unakuja kuwa mzuri .Kumbua Wariona alionya na sasa akawa ignored is the outcome ya kwenda Mahakamani. Why they did ignore his warning ? Wana uhakika kiasi gani ? Je hawakujua kama jamaa ni Mwanasheria maarufu na waziri mkuu mstaafu? Ngomba mbele .Again tafiti hupingwi ila umeamshwa .
 
Mugishagwe nadhani unamiss pointi hivi maneno yako, ya mwanakijiji na ya kwangu yana tofauti gani, sote tuna maoni kuwa mengi yupo hatarini.

Nahitaji kuamshwa kivipi wakati kama ni kuamka kuwa na msimamo kama wako basi na wewe umelala halikadhalika unahitaji kuamka, take trouble kuanza kusoma hii thread from my initial contribution ndio utaelewa!
 
kwa maoni yangu kama ni mengi kuwa hatarini si kweli kwa kuwa mwisho wa siku ni jina tu limektumika kuwa anaown magazet yale lakini ukweli wacha tungoje pale mbele ya jaji kama warioba kaamu kwenda mbele za haki.
 
Kwakweli ninajaribu kuuelewa huu mjadla bado, but nitasema kitu kimoja kuwa Mengi ndiye anaye-control all politics zinazoandikwa kwenye magazeti yake, hilo sina ubishi nalo,

isipokuwa bado sijaulelewa mjadala vizuri.
 
tafiti then jadili said:
For the last few months tumekuwa tukiona magazeti ya bwana Mengi yakichukua a dramatic twist katika story zake:

1. Amekuwa akimuandama sana Yusuph Manji kwa kurudia stori hiyo hiyo kupitia gazeti la THIS DAY akidai ni crook business man ambae ana shaddy deals na mamlaka kadhaa.

2. Amekuwa akiiandama sana taasisi ya NSSF kwa kuwa na the same story kila siku tangu gazeti lilipoanza akizungumzia kitu kimoja tu cha ubungo plaza akidai limenunuliwa na NSSF kimakosa.

3. Ameiandama sana hii kampuni ya madini inayodaiwa kuwa na link na ccm

Sasa kumekuwepo na malalamiko mengi kuwa amekuwa akitumia vyombo vyake vya habari kujijengea himaya ya kuogofya watendaji wa serikali huku wengine wakidai ana misuse his media outlets to serve his personal benefits.

Mimi binafsi nikiangalia naona alianza vizuri na vyombo vyake ila siku za karibuni kuna changes nyingi katika operations zake manake sawa mfanyabiashara haanzishi mavyombo mengi kama yale bila kuwa na personal benefits lakini anakwenda to the extreme kwa sasa.

Hii ni kesi ya tatu kuisikia ambayo Bwana Mengi ameshitakiwa manake ya kwanza ni ile ya YUSUPH MANJI anaedai bilioni moja na pesa nyingine kadhaa, ya pili ni ile ya mhariri wa daily news mkumbwa Ally ambae nae ameshitaki kwa kudai kukashifiwa na sasa hii kwa hiyo unaona kama wote wakifanikiwa mengi kwisha!

Wakati umefika sasa vyombo vya habari indeed owners wawe restricted to some sort of commitment kucover vitu vyenye national interests zaidi kuliko kuserve personal interest za owner.

Same old songs...unacholalamika ni magazeti ya Mengi kuandika tuhuma dhidi ya vigogo au ungependa yaandike habari nyingine zaidi ya tuhuma hizo?Kwanini usifanye utafiti kabla hujakurupuka kutetea?Of course,kila chobo cha habari kinatekeleza policies zilizowekwa na owner wa chombo hicho,lakini kwa hili la Mengi na Manji kuna maswali kadhaa ambayo magazeti hayo yametusaidia tu kutujibia.Je wakati unakimbilia kuyalaumu magazeti hayo,umeshafanya utafiti wowote kuthibitisha kuwa dili ya NSSF Plaza haikuwa na walakini kama yanavyodai magazeti ya Mengi?

How far sure are you kwamba magazeti hayo yana-cover stories za personal interests za Mengi na sio kutumikia jamii?Je habari za rushwa kwako sio za national interest?Najua,akisifiwa kiongozi ndio unajiskia raha.Well,kusifia kiongozi sio dhambi pindi akifanya vizuri,lakini akikosea lazima alaumiwe pia.

Tafiti...try to live up to your name ie TAFITI THEN JADILI.Kumbuka,NO RESEARCH NO RIGHT TO SPEAK.Kwa kuwa hujawasilisha uthibitisho wowote kuwa magazeti ya Mengi hayatumikii maslahi ya Taifa bali maslahi binafsi ya mfanyabiashara huyo,huna haki ya kutoa tuhuma zako.Kesi ziko mahakamani,huko ndiko ukweli utajulikana.

Hate him or love him,kwa sie tulio huku tuliko tunaishukuru IPP kwa kutu-keep informed about what's happening back home.Ukilinganisha ippmedia.com/thisday.co.tz/darhotwire.com na websites like uhuru.info au dailynews-tsn.com utaelewa ninachokisema.

Tatizo lako wewe ni kwamba unapenda sana kuona nchi yetu inatafunwa na hutaki kuskia watu wakilalamika au kuhoji ulaji huo.Pengine wewe si Mtanzania maana tuna Banyamulenge kadhaa nchini mwetu ambao wamejipenyeza kutumia mgongo wa wanamtandao.Hawa hawana uchungu na nchi yetu,na siku zote wanahangaika kuttetea ulaji.
 
Mlalahoi,

Tatizo la wa TZ wengi akishawemo serikalini basi hata serikali ifanye nini basi anashindwa kulikemea. hii ni kwasababu wengi na hata yeye ni walaji. Nimelishuhudia kwenye forum nyingi tu na nyingine za wazi kama Tanzanet. Mkubwa hawezi kuchangia tofauti na serikali hata serikali imekosea. Ni sawa, ki maadili, nakubali. Lakini hata huku tunakotumia majina feki?! Ebo! nyie vipi?

Kuna akina BANDORA wengi mzee tafiti "anaweza" kuwa mmoja wao!

I lavu zisi foramu!

FD
 
Fikiraduni,

Hiyo ni kweli kabisa, unajua kwa waTz mkubwa hajambi (mtaniwia radhi kwa neno hilo). Ndio maana hata elimu hazitusaidii, mtu anaPhD lakini mamuzi anayofanya ni ya kilumpeni, why? hataki kupingana na wakuu maana atahaharibu kula yake, ubinafsi mtupu!
 
tafiti then jadili said:
Sasa Mugishagwe maelezo yako na yangu yana tofauti gani? kiasi nihitaji kuamshwa! Mugishagwe take time to read my submission na za kwako utaona tunaongea almost lugha moja...nadhani usikurupuke kupinga kabla hujajua hoja hasa ni ipi...au na wewe una msimamo kuwa chochote mtu fulani akisema ni cha kupingwa?!

tuwe na mijadala constructive...

Mzee Jasusi

Naona umekata points hapo, ni kweli kabisa hoja yako nadhani waandishi wanahitaji kuwa na wanasheria ili kuwaguide zaidi.

Kwenye uandishi hapa UK media lawyers ni kama editors vile nao wana power ya kuapprove stories na kutaka ziwe edited ili kuondokana na legal consequences.

Yaani kumbe uko UK halafu unapiga kelele eti "magazeti yanayotumikia personal interests" yafungiwe?Hivi News of The World,The Sun,SKY na vyombo vingine vya News International Co,vinamtumikia Ruppert Mordoch au the British society?

Na usitake kudanganya watu kuwa media lawyers ndio wanao-aprove nini kiandikwe na nini kisiandikwe katika magazeti ya hapa UK,sema most editors are well versed with the media law that they tend to think twice before approving a story for publication.And that in itself doesnt necessarily mean they always get the stories right eg in the Tommy Sheridan vs News of The World case.Kama media lawyers ndio wangekuwa wana-approve story basi Piers Morgan asingeingia mkenge na picha za "British soldiers doing an abu ghraib kind of turture in Iraq",a scandal that led him to be sacked form the Daily Mirror.

Ukitaka kujua zaidi try to get in touch with Prof Eric Barendt,a professor of Media Law at the Uni College of London (e-mail:e.barendt@ucl.ac.uk).
 
fikiraduni said:
Mlalahoi,

Tatizo la wa TZ wengi akishawemo serikalini basi hata serikali ifanye nini basi anashindwa kulikemea. hii ni kwasababu wengi na hata yeye ni walaji. Nimelishuhudia kwenye forum nyingi tu na nyingine za wazi kama Tanzanet. Mkubwa hawezi kuchangia tofauti na serikali hata serikali imekosea. Ni sawa, ki maadili, nakubali. Lakini hata huku tunakotumia majina feki?! Ebo! nyie vipi?

Kuna akina BANDORA wengi mzee tafiti "anaweza" kuwa mmoja wao!

I lavu zisi foramu!

FD

Naafikiana nawe kabisa.Lakini nahisi huyu TAFITI THEN JADILI ni kibaraka tu wa hao anaowatetea,na inawezekana kabisa kuwa huo utetezi anaotoa katika kila jambo linalohusu ulaji ni kazi yake ya full-time,yaani ndio inayomwezesha kupeleka mkono kinywani.Sijaona her single article in which she criticise maovu yanayotokea kila kukicha huko nyumbani but kila kiongozi akizungumziwa au kuhusishwa na skandali,yeye ndio wa kwanza kutetea.Pengine anajipendekeza apewe nafasi ya Msemaji wa Serikali,pengine analipa fedhila kwa mtu flani,au labda ni mzembe wa kufikiri tu.
 
Mimi ningependa kuungana na wale wanaosema kuwa editors wa haya magazeti ndio accountable na sio owners,when it comes to what has been printed.Mfano,mwaka jana wakati wa vuguvugu la kutafuta mgombea wa CCM gazeti la Mwananchi lilitoa picha ya Salim Ahmed Salim amepose na Sultan wa Zanzibar in the 60's.Ile picha lengo lake lilikuwa ni kuonyesha Salim ni Hizbu,hivyo asingefaa kuwa rais wa Tanzania.Hayo magazeti yanamilikiwa na gazeti la Nation la Kenya,ambalo linamilikiwa na Aga Khan.Huko nyuma,Salim alishalishtaki Nation la Kenya,na alilipwa kitu kama dola laki nane hivi.Picha yake na Sultan ilikuja kugundulika kuwa ni computer generated,matokeo yake Nation walimfukuza yule editor wa Mwananchi,na kuomba msamaha kwa Salim.

Sasa labda nae Mengi badala ya kuingia gharama kutoa matangazo kwenye magazeti kuwa hana ugomvi na Manji na kuwa yeye ni mmiliki tu wa magazeti,lakini ni msomaji kama wengine, angejiweka sawa na kuchukua hatua kama hizo za Nation pale inapoonekana kuwa ukweli ulipotoshwa ili kuondoa hio dhana kuwa habari hizo zinaandikwa kwa kumnufaisha yeye binafsi na biashara zake.
Lakini kwa mwendo huo,kinachonishangaza mimi ni hichi,kama hii forum ingekuwa gazeti,na watu tungeweza kuandika tunavyoandika humu,tungewacha? Mbona watu humu wanalalamika kuhusu rushwa za viongozi,lakini pale inapoandikwa kwenye magazeti haohao ndio wanakuwa wa kwanza kusema kuwa huyo aliyeandika ana sababu zake binafsi,sisi humu sababu zetu ni nini? Uchungu wa taifa letu au envy kwa sababu hao viongozi wanajipatia njia rahisi za kutajirika,na kama hata sisi tungekuwa kwenye nafasi tungefanya hivyohivyo? Kama Warioba na Manji wanamshtaki Mengi kwa sababu walizozitoa,si wana-exercise rights zao kama hayo magazeti yalivyojaribu ku-exercise rights zake kwa kuandika habari ambazo mhariri aliona zinafaa kuchapishwa,mahakama itaamua ni nani mwenye makosa.
 
Zanaki,

Kuongezea Daily Nation wanamiliki 60% RA and Balozi Ruhinda wanamiliki 20% kila mmoja.
Kabla hao watu wawili ndio walikuwa wanamiliki 60%.

Unaweza kuendelea kupembua..

FD
 
Ndiyooooooooooooooooooooo wana kunyumba leo mmenikuna na kunichinginya kabisa .Walahi pale pale kwenye Bombi moja leo haya ndiyo maneno .tafiti si mtafiti wa maana bali mjenga majina ya watu .Hata hakuweza kuona kwamba Mugisha alikuwa anampinga na kumuonea huruma kwamba kama ni kweli ni mtetezi wa serikali basi angalijua nani ana own Kulikoni na This day lakini ni mgeni huyu hana ajualo.Mengi angaliweza kufanya kama hao jamaa wa daily nation lakini kashitakiwa na yeye kama owner hawezi kumfukuza kazi . Juu ya yote haya Warioba ataweza kuibuka kidedea kweli ama kaanza moto ambao ataibika nao ????????Ndiyo swali langu
 
Ukweli wa mambo ni kwamba hamna cha Warioba wala Mengi.

Hii kesi itazimika kama mvua ya vuli. Wanaweza wasimpende Mengi na magazeti yake lakini ukweli utabakia pale pale siku zote.

Halafu kitu wanachosahau ni kwamba This Day na Kulikoni hayamilikiwi asilimia 100 na Mengi, ndiyo maana hayachapishwi na Guardian Printers kama Nipashe na mengineyo. Pia ndiyo maana hutaona habari za jinsi ya Kulikoni na This Day kwenye magazeti yake.

Kwa wale wenye kumbukumbu zuri mtakumbuka kuwa Africa Media, kampuni inayochapisha This Day na Kulikoni ilitangaza Bodi ya Wadhamini na Wakurugenzi mwezi wa tano, na mengi ni mmojawapo wa wadhamini.

Tukirudi kwenye Kesi ya Warioba au ile ya Manji, nadhani wahusika wanasahau kuwa This day na Kulikoni walitumia makaratasi waliyopata kutoka BRELA (Business Registration and Licensing Agency). Makaratasi hayo ni pamoja na MEMART (Memorandum of Understanding and Articles of Association). Kwenye MEMART kuna kila kitu kuanzia number of shares, capital, directors and ownership, na Mwanasheria aliyetumika kusajili Kampuni.
Wewe binafsi pia unaweza kwenda kwenye ofisi zao na kutoa TZS 1000 na utapata access ya kupitia Registrar Directory.

Hapa hamna cha kusema eti kisa Warioba na Mwanasheria, jaji mkongwe basi apate free ticket ya kutokuandikwa. Mimi nakuakishieni yeye mwenyewe kimya kimya ataondoa hiyo kesi au utasikia ikitajwa mwaka 2008.

Tatizo watu wengi wanafikiri Mengi naye anaingia kichwa kichwa au hana wanasheria wanaomshauri. This guy has been there and he know what he is doing and the consequences. Ana timu ya mawakili wazawa na wasio wazawa.

tusubiri tuone, siyo ajabu hata hamna kesi iliyofunguliwa bali ni maneno ya magazeti tu, kwani tunafahamu tabia ya magazeti yetu, yanashindwa kutofautisha nia na dhamira ya kushita au kufungua kesi na kitendo cha kufungua kesi yenyewe.
 

Similar Discussions

3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom