John Mnyika
JF-Expert Member
- Jun 16, 2006
- 713
- 1,249
Kwa mtu anayemfahamu Mengi na biashara zake ukweli uko wazi kwamba kwa kipindi cha 1995 mpaka 2005 amekuwa kinyume kabisa na upinzani nchini. Vyombo vya habari vya Mengi particularly ITV vina nguvu sana-kama angeunga mkono CHADEMA mambo yangekuwa tofauti sana. Lakini ilikuwa kinyume chake.
CHADEMA bado haijaamua mgombea urais wake, kusema kwamba Mengi ni mgombea wa CHADEMA wakati hata sio mwanachama ni kutokututendea haki.
Baadhi mmeunganisha msimamo wa CHADEMA kuhusu pesa za NSSF ama shutuma za ndesamburo na Mengi na uchaga. Huku nako ni kutukosea haki na kuhamisha mjadala wa msingi. CHADEMA tumesimamia mambo mengi ya kitaifa na tunaendelea kuyasimamia. Wakati tunapinga ununuzi wa ndege ya rais sikusikia mtu akisema anayepingwa ni Mramba Mchaga. Wakati tunapinga ununuzi wa RADA haya hayajitokeza. Wakati tunamshambulia Lowasa kuhusu Richmond sijasikia yoyote hapa akisema kwamba huo ni UKASKAZINI.
Bottomline, hapa kuna watu wanataka kututoa kwenye kujadili masuala ya vyanzo(source issues)- kwenye suala la NSSF/PSPF-suala la msingi ni je, bilioni 83 za michango ya walipakodi ziliwekezwa vizuri au zilizochotwa kutokana na ufisadi? NSSF/PSPF/Manji nk wanawajibu wa kujibu?
Ndesamburo ameweka bayana madai ya rushwa na amesema chanzo ni nini, Mengi na Lowasa. Lowasa ni kiongozi wa umma, hajajitokeza kujibu. Rais amesema serikali haitajibu. Kuna nini hapa kinafichwa? Hili ni suala hapa! Tulijadili na kuhoji
Ya Mengi na Manji tuwaachie wenyewe wameshapelekana mahakamani kwa tuhuma za kukashifiana. Tusiingilie uhuru wa mahakama.
Lakini haya matumizi ya pesa za walipa kodi na tuhuma za rushwa; ni ya kwetu haya, tuyajadili kweli kweli...
CHADEMA si chama cha wachaga: rejea tamko rasmi la chama kuhusu suala hili http://www.chadema.net/tamko/2007/mwanri.php
Kwa hiyo mtanzania yoyote ana haki ya kuwa ndoto ya kugombea urais kupitia CHADEMA 2010: awe msukuma, awe mhaya, awe mchaga, awe mjita:wote karibuni ili mradi tu uendani na misingi ya falsafa ya nguvu ya umma http://www.chadema.net/nyaraka/falsafa.php na itikadi ya mrengo wa kati http://www.chadema.net/nyaraka/itikadi.php
JJ
CHADEMA bado haijaamua mgombea urais wake, kusema kwamba Mengi ni mgombea wa CHADEMA wakati hata sio mwanachama ni kutokututendea haki.
Baadhi mmeunganisha msimamo wa CHADEMA kuhusu pesa za NSSF ama shutuma za ndesamburo na Mengi na uchaga. Huku nako ni kutukosea haki na kuhamisha mjadala wa msingi. CHADEMA tumesimamia mambo mengi ya kitaifa na tunaendelea kuyasimamia. Wakati tunapinga ununuzi wa ndege ya rais sikusikia mtu akisema anayepingwa ni Mramba Mchaga. Wakati tunapinga ununuzi wa RADA haya hayajitokeza. Wakati tunamshambulia Lowasa kuhusu Richmond sijasikia yoyote hapa akisema kwamba huo ni UKASKAZINI.
Bottomline, hapa kuna watu wanataka kututoa kwenye kujadili masuala ya vyanzo(source issues)- kwenye suala la NSSF/PSPF-suala la msingi ni je, bilioni 83 za michango ya walipakodi ziliwekezwa vizuri au zilizochotwa kutokana na ufisadi? NSSF/PSPF/Manji nk wanawajibu wa kujibu?
Ndesamburo ameweka bayana madai ya rushwa na amesema chanzo ni nini, Mengi na Lowasa. Lowasa ni kiongozi wa umma, hajajitokeza kujibu. Rais amesema serikali haitajibu. Kuna nini hapa kinafichwa? Hili ni suala hapa! Tulijadili na kuhoji
Ya Mengi na Manji tuwaachie wenyewe wameshapelekana mahakamani kwa tuhuma za kukashifiana. Tusiingilie uhuru wa mahakama.
Lakini haya matumizi ya pesa za walipa kodi na tuhuma za rushwa; ni ya kwetu haya, tuyajadili kweli kweli...
CHADEMA si chama cha wachaga: rejea tamko rasmi la chama kuhusu suala hili http://www.chadema.net/tamko/2007/mwanri.php
Kwa hiyo mtanzania yoyote ana haki ya kuwa ndoto ya kugombea urais kupitia CHADEMA 2010: awe msukuma, awe mhaya, awe mchaga, awe mjita:wote karibuni ili mradi tu uendani na misingi ya falsafa ya nguvu ya umma http://www.chadema.net/nyaraka/falsafa.php na itikadi ya mrengo wa kati http://www.chadema.net/nyaraka/itikadi.php
JJ