Hapa watayasema yote, kesi inayosema upendeleo wa ITV kumwonyesha Mengi zaidi, ati Mke wa Mwizi Prof. Mahalu anakwenda kutoa ushahidi, KUMBUKA huya mama anashare ya 20million ktk mradi wa BOT kusafisha dhahabu! hizo ni fedha alizoiba mumewe akiwa balozi Italia!
Haya sasa Masilingi, ambaye kama sikosei ndo alikuwa na bifu na Mengi ktk uuzaji wa Kilimanjaro hoteli! hapa Mengi amekwisha!
.............................
:U Can't Change The Nature:
******************************************************
Warioba atoa ushahidi kesi ya Mengi bungeni
Na Shadrack Sagati
WAZIRI Mkuu Mstaafu, Jaji Joseph Warioba, jana alikuwa miongoni mwa watu waliotoa maelezo mbele ya kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge katika shauri ambalo Mwenyekiti Mtendaji wa IPP, Reginald Mengi, anamlalamkia Mbunge wa Mkuranga, Adam Kighoma Malima.
Mwingine ambaye jana alifika mbele ya kamati hiyo ni Vulfrida Grace Mahalu[/U], ambaye ni mke wa aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Italia, Profesa Costa Mahalu. Vulfrida alitoa ushahidi wake baada ya Jaji Warioba.
Warioba aliwasili katika eneo la ofisi za Bunge saa 3.45 na akapokelewa na Adamu Malima na akaongozana naye hadi kwenye ukumbi wa bodi, ambako kikao hicho kilikuwa kinafanyika.Hakuna mjumbe ambaye alikuwa tayari kueleza walichomhoji Warioba ambaye ni mmoja wa wanasheria wanaoheshimika nchini. Warioba alihojiwa hadi saa 5.40. Baada ya kumaliza Warioba ndipo alipoitwa mke wa Balozi Mahalu ambaye naye haikujulikana ni maelezo yapi alienda kuyatoa lakini kama Warioba alionekana kuwa karibu zaidi na Malima kabla ya kuingia kwenye ukumbi wa mahojiano.
Wengine ambao wameshafika mbele ya kamati hiyo ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii, Ramadhan Dau pamoja na Maalim Ally Basaleh. Wengine ni Mkurugenzi wa ITV/Radio One, Joyce Mhavile, Adam Malima na Mengi mwenyewe.Mwenyekiti wa kamati hiyo, Juma Suleiman N'hunga ambaye ni mbunge wa Dole hadi jana hakuwa tayari kuzungumzia mahojiano ya mashahidi hao. Pia haikufahamika aina ya ushahidi ambao wanahitaji kutoka kwa Warioba na kwa mke wa Mahalu.
Chanzo cha malalamiko hayo kinatokana na Mengi kumwandikia Spika wa Bunge, Samwel Sitta akimlalamikia Malima kuwa alimzushia uongo bungeni wakati akichangia hotuba ya bajeti ya Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo.
Akizungumza bungeni Agosti 2, Malima alikilalamikia kituo cha televisheni ya ITV kuwa kinatumia dakika 10 za taarifa zake za habari kumwonyesha mmiliki wake huku kikitoa dakika moja na nusu kwa habari zinazowahusu viongozi wa nchi ambao ni Rais na Waziri Mkuu.
Malima katika kuthibitisha kauli yake, alitoa mfano wa ziara ya wanafunzi wa shule kutoka Zanzibar waliotembelea kiwanda cha Coca Cola kampuni tanzu ya IPP kuwa walipewa muda wa dakika 10 katika tarifa ya habari ya ITV.
Mbunge huyo pia alitoa mfano mwingine kile alichodai matumizi mabaya ya televisheni ni pale ambapo Mengi alikuwa akizungumza na watoto wa Madrasa kuwa kituo chake kilitumia dakika 10 za taarifa ya habari kuonyesha tukio hilo.
Madai hayo yalionekana kumkera Mengi ambaye hata kabla ya kupeleka malalamiko yake kwa Spika, alijibu madai hayo kwa kutoa matangazo kwenye vyombo vya habari kueleza kile alichodai ni ukweli wa mambo.
Katika utetezi wake, Mengi alitoa mfano kuwa wakati Waziri Wkuu, Edward Lowassa, alipozungumzia njaa mjini Dodoma, Februari 19, mwaka huu alipewa muda wa dakika 2.38 na sio dakika moja aliyodai Malima.
Mfano mwingine ni wa Aprili 22 wakati watoto wa Zanzibar walipotembelea kiwanda cha Coca Cola ambao alidai kuwa mazungumzo yake na watoto hao yalikuwa dakika 1.12, wakati Mei 25 alipozungumza na watoto wa Madrasa alitumia dakika 2.29 na sio dakika 10 zilizodaiwa na Malima.
Wajumbe wengine katika kamati hiyo ni Mbunge wa Moshi mjini, Philemon Ndesamburo, Mbunge wa Chalinze, Ramadhan Maneno, Mbunge wa Iramba, Magharibi, Juma Killimbah, Mbunge wa Igalula, Tatu Ntimizi, Mbunge wa Kisarawe, Athuman Janguo, Mbunge wa Muleba Kusini, Wilson Masilingi na Christopher ole Sendeka wa Simanjiro