Kitila Mkumbo
JF-Expert Member
- Feb 25, 2006
- 3,354
- 1,943
Tafiti: Pole ndugu yangu, mimi sitoki kaskazini ng'o. Nitafute vizuri hujanipata bado.
Naam, nilikuwa najua sana hayo mahusiano kati ya Philemon, Grace na Lucy. Hao watu wote nimefanya nao kampeni mwaka jana, nisingeacha kujua jambo lililo wazi kiasi hiki! Hii haijawahi kunipa shida hata kidogo. Nitafafanua baadaye, kwa sasa ngoja nimalizane na wewe kwanza katika utafiti wako.
Japokuwa unakimbia hii forum kwa kudai kuwa adm amekuuzi, kabla hujakimbia lazima nimalizie majibu yangu katika utafiti wako kama ifuatavyo.
Utafiti mzuri wa aina yako ungefanya pia comparative analysis. Kwa mfano hali ikoje katika vyama vingine angalau viwili vitatu kabla ya ku-draw such bold conclusions. Kwa mfano, kwa kutumia idadi ya watu uliotumia wewe hao viongozi sita. Tukifanya hivyo hivyo katika uongozi wa CCM wa sasa utakuta kwamba katika viongozi sita wa juu yaani Mwenyekiti, Makamu wawili, Katibu Mkuu na Manaibu Makatibu wakuu wawili (total six)-utakuta kwamba 4 kati ya hawa wote ni waislamu, hii ni sawa na 66.7%, Je hii inatosha kusema kuwa CCM ina mwelekeo wa kidini yaani kiislamu? Bila shaka jibu unalo. Tukiangalia uongozi uliopita chini ya Mkapa, utakuta kwamba katika viongozi wa juu wa CCM(6), wanne kati ya hawa walikuwa ni wakristo ambayo ni sawa na 66.7%. je tuseme kuwa hiki chama kila mwenyeketi anapokuwa dini fulani basi kinakuwa na mwelekeo wa dini hiyo? Nafikri jibu pia unalo.
Maoni yangu ni kuwa tuwe makini sana katika kutumia takwimu. Wakati mwingine takwimu zikitafsiriwa vibaya zinapotosha mno. Ukiwa na viongozi wawili na moja ni muislamu na mwingine mkristo, unaweza kabisa ukasema asilimia 50% katika hiki chama ni wakristu au waislamu kadri unavyotaka! Kimahesabu upo sawa kabisa, lakini kimantiki unaweza ukawa mbali kabisa na ukweli.
Huyo chinga mimi sioni cha ku-argue naye tena!
Naam, nilikuwa najua sana hayo mahusiano kati ya Philemon, Grace na Lucy. Hao watu wote nimefanya nao kampeni mwaka jana, nisingeacha kujua jambo lililo wazi kiasi hiki! Hii haijawahi kunipa shida hata kidogo. Nitafafanua baadaye, kwa sasa ngoja nimalizane na wewe kwanza katika utafiti wako.
Japokuwa unakimbia hii forum kwa kudai kuwa adm amekuuzi, kabla hujakimbia lazima nimalizie majibu yangu katika utafiti wako kama ifuatavyo.
Utafiti mzuri wa aina yako ungefanya pia comparative analysis. Kwa mfano hali ikoje katika vyama vingine angalau viwili vitatu kabla ya ku-draw such bold conclusions. Kwa mfano, kwa kutumia idadi ya watu uliotumia wewe hao viongozi sita. Tukifanya hivyo hivyo katika uongozi wa CCM wa sasa utakuta kwamba katika viongozi sita wa juu yaani Mwenyekiti, Makamu wawili, Katibu Mkuu na Manaibu Makatibu wakuu wawili (total six)-utakuta kwamba 4 kati ya hawa wote ni waislamu, hii ni sawa na 66.7%, Je hii inatosha kusema kuwa CCM ina mwelekeo wa kidini yaani kiislamu? Bila shaka jibu unalo. Tukiangalia uongozi uliopita chini ya Mkapa, utakuta kwamba katika viongozi wa juu wa CCM(6), wanne kati ya hawa walikuwa ni wakristo ambayo ni sawa na 66.7%. je tuseme kuwa hiki chama kila mwenyeketi anapokuwa dini fulani basi kinakuwa na mwelekeo wa dini hiyo? Nafikri jibu pia unalo.
Maoni yangu ni kuwa tuwe makini sana katika kutumia takwimu. Wakati mwingine takwimu zikitafsiriwa vibaya zinapotosha mno. Ukiwa na viongozi wawili na moja ni muislamu na mwingine mkristo, unaweza kabisa ukasema asilimia 50% katika hiki chama ni wakristu au waislamu kadri unavyotaka! Kimahesabu upo sawa kabisa, lakini kimantiki unaweza ukawa mbali kabisa na ukweli.
Huyo chinga mimi sioni cha ku-argue naye tena!