Mbowe vs Chifupa + CHADEMA vs Family Business

Mbowe vs Chifupa + CHADEMA vs Family Business

Status
Not open for further replies.
Mimi nasubiri kwa hamu ufafanuzi wa Special Seat...maana hapo ndipo palipobakia kwa mimi kutofautisha kama Chadema ni NGO au Chama cha watanzania wote.
 
Mbowe bado ataendelea kuwa zaidi maana kachaguliwa na wananchi na Chifupa kachaguliwa na raisi kutokana na uwanawake wake nikiwa na maana angekuwa mwanaume asingechaguliwa.na suala la ukodishaji unabaki palepale hata kama hao wanaokukodisha magari wanakuchaji hivyo basi unaibiwa we nenda ktk kampuni za ujenzi na uone ni jinsi gani wanavyokodisha
 
Mwanasiasa,
Issue zipo tunasubiri kwanza majibu ya zile za mwanzo.
1. Majimbo.
2. ndoa ya Chadema na Conservative.
3. Chadema kuwa ni chama cha familia.
4. Chadema ktk Ukabila na Udini.

Mimi nadhani haya maswala manne yanatosha kabisa kwa kuanza na ikiwa Chadema wanakubali mapungufu haya na kuyafanyia kazi itakuwa jambo zuri zaidi kwa sababu Chadema kitakuwa chama cha kwanza Tanzania kuweza kufanya mabadiliko ya sera zake kupitia kwa wananchi. Laa sivyo, tupeni sababu na maelezo yenu kisha nasi tutawapa mchango wetu.

Sisi sote binadamu tunachojaribu kutengeneza hapa ni hoja ambazo zinawakera wananchi walio wengi. hao CCM, TLP, CUF na wengineo hawana mpango wa kumsikiliza mwananchi isipokuwa wao ni watunzi wa Dira, sheria, mifumo, sera kwa ajili yetu. Sisis ni wasafiri tu hatuna sauti ya kusema tunataka kwenda wapi.

Naamini kabisa sababu ya Freeman kuingia hapa ni kutaka kujua sisi wananchi tunataka kwenda wapi?...Dira ya kitaifa na sio sisi kupanda bus lake na kwenda atakako yeye. hii ni dalili nzuri sana tofauti na CCM ama vyama vinginevyo.
 
Mkandara,

Safi, Chadema walikosea Chinga alipouliza wao wakaanza kulalamika, ilitakiwa wajibu wanayoona yana maana, hata mimi niliuliza kuhusu majimbo sikujibiwa, hii ikatufanya tumuone Chinga amewazidi.
Mnyika amehaidi kuja na majibu tusubiri

FD
 
well and detail answers by mnyika ,this is a good tradition of making clarfications as to clear the air, you know when lies are continuesly repeatedly finally it will sound like truth.

we would be happy if any politician or whoever alleged here make efforts to come out clean.
 
Mkandara, swali lako la 3 na 4 nilijitahidi kulifafanua katika post ya CHADEMA ni family business. Nafikiri bado ipo humu. Mnyika ameahidi kuteremka na data kwa ajili ya swali la 1 na 2.

Baada ya hapo, tutaangalia sasa wapi pa kurekebisha na kwenda mbele. Ngoja niitafute ile topic halafu ni-paste some posts
 
Bob Mkandara,

Maswali hayo ni lovely, na super na hasa Chadema kuwa ni famly business hilo bado I am trubled nalo, unlesss kama kuna maelezo zaidi!
 
Mwanasiasaa,
Alivyosema Mzee Es ndio ukweli unaotuweka bado wengi hapa. family business na Ukabila na Udini bado kabisa hamjatupa la straight bila ktuyumbisha na hizo siasa!

Tunachotaka kujua ni KWELI ama Sii kweli?.. Sio kweli basi tupate maelezo yanayohusu hali halisi ya Chadema leo hii!

Nakumbuka kama Chinga aliuliza kuhusu Freeman kuzaa nje!.. Hilo halikuwa tatizo letu isipokuwa kama familia hiyo waliingizwa Chadema na kupewa madaraka ya JUU!

Hapa kidogo tuna utata wa kuelewa. nakumbuka ulitumia mifano ya CCM lakini binafsi sidhani kama kujisafisha kwa Chadema kutafuatia tu baada ya usafi wa CCM.

Wengi wetu tumechoka na CCM, na sasa tunatazama mwanga uko wapi? Kwa hatua za kuchechemea, simba aliyejeruhiwa huwa mbaya sana kuliko yule mwindaji.

CCM wanaweza kuwarudi haraka sana na sikudanganyi ndugu yangu -watu wanasubiri NABII atokee CCM... hilo kwanza fahamu na usafi wenu hapa utatusaidia sana kuweza kuvutwa kabla hawa simba wenda kimya hawajaamka.
 
Mkandara: Nilieleza katika majibu yangu awali kuwa katika wajumbe wa kamati kuu zaidi ya 30, wanaotoka katika mikoa ya kilimanjaro, Manyara na Arusha ni 7 ambao ni sawa na 23.3%.Hii haifanyi chama kuwa cha kikanda. Nikaeleza pia kuwa katika wajumbe hawa, wenye undugu ni wanne (Freeman na Mtei; na Ndesamburo na Grace). Pia moja ya wabunge ni mtoto wa Ndesamburo ambaye ni Lucy. Hili pia kwa maoni yangu halihalishi hiki chama kuitwa cha familia.

Nikaeleza pia kuwa katika wenyeviti watatu tangu CHADEMA ianze, moja alitoka Shinyanga na wawili wametoka Kilimanjaro. Hili nalo halitoshi kukiita chama ni cha kifamilia.

Hoja yangu ya kulinganisha na CCM ilitokana na matokeo ya utafiti wa bwana Tafiti. Kwa aina ya utafiti aliyoufanya bwana Utafiti, matokeo yake yasingekamalika bila kufanya ulinganisho na vyama vingi kwa sababu utafiti wake uliangukia katika kundi la utafiti linganishi.

Inawezekana wenzangu wakaja na majibu ya kushawishi zaidi.
 
Ukabila na ukanda upo.

mwaka huu MBOWE alipeleka wenyeviti wake watatu London kuwapongeza kwa ushindi na kati hayo watatu wote ni wachaga na wanatoka Kilimanjaro,
cha kujiuliza hakukuwa ma mwenyekiti toka Mara au Kigoma au Mpanda ambako nako kulipatikana viti.

Mnyika kuwa consultant nalo ni kituko kwangu, kweli form six anaweza kuwa consultant? hiyo labda Chadema lakini katika medani ya kitaifa na kimataifa consultant huwa na elimu ya kutosha na si form six.

Firaduni na Kichuguu mlikuwa mnawalalamikia DR.Warioba, DR.Nchimbi,na Kamala kuwa na udokta na hili la Mnyika mnaunga mkono form six kuwa consultant,
mngezingatia humu wanasoma watoto walioko shuleni wanaweza kupata feeling kuwa hakuna haja ya kusoma zaidi ili kuwa consultant kwani wameona Fikiraduni akikubali Form six ni consultant.

Mnyika.

inawezekana Chadema wakakuita consultant sio mbaya ila katika medani ya kitaifa huna cheo hicho ni sawa na professor maji marefu au profesor kejeli wa bagamoyo kujiita professor.
 
Somehow mtalii is right.

Swali la kujiuliza ni "What's a Consultant?",
Je mtu anae-enda ku-consult (kuomba ushauri) mtu mwingine je ni Consultant?

Tujuavyo wengi wetu ni kuwa, ili uwe Consultant is that one has to be an expert to advice professionally and/or technically.

Je does kuwa msomi make or would make somebody a consultant? (from mtalii theory), the Answer to this is NO,
kwa sababu sio wote waliosoma ktk level anayotaka mtalii wanaweza kuwa washauri (Consultants) effectively.
A knowledge can also be acquired from uzoefu i.e. experience (those with smart brains) na si lazima kuwe na a formal training.

Je ni vigezo gani vya ku-consider kuwa fulani ni consultant?, je Prof Maji Marefu, Prof Vulata et al walikuwa ma-Consultant? na Msomi wetu Dr Nchimbi et al waweza kuitwa Consultants?

Je Mnyika ni Consultant or alikuwa Consultant?
Kutokana na maelezo hapo juu malizia mwenyewe.............
 
Ogah,

Nooo bob, Ukisoma maelezo ya Mnyika swala hili ni wazi kabisa...
Alisema:-
Wakati nikiwa consultant wa mradi wa kuwajengea uwezo wabunge nilikuwa nalipwa dola 100 kwa siku.

Sasa ni jukumu la huyu Mtalii kutuambia hiyo kuwajengea uwezo wabunge inahitaji fani gani ya elimu ktk hizo Masters au Phd!...
 
By the way kule HULL jana ndio walimaliza courseworks na ratiba ya exams January imeshatolewa
 
Yes Mkandara, na tumsibiri mtalii atuambie

Mzee Es
Good question mzee! Pengine hapo Mnyika atueleze vizuri.
 
Wajameni, Chifupa na Mbowe wanaonewa bure katika mjadala huu. Wanaowajadili wote wanatumia magazeti na mtandao wa kompyuta kuwajua. Watu hawa ni tofauti kama mbingu na dunia. Ukitaka kuwajua, kutana nao. Waulize swali lolote, na sikiliza majibu ya kila mmoja. Hapa tunadanganyana!
 
Mzee K,

Hapa hatudanganyani, hayo magazeti unayoyasema ndiyo yametufanya tuwe hapa baada ya kununuliwa na mtandao, unajua sometimes kama huna hoja ni vyema kunyamaza,

yaani una maana kwamba mwenyekiti wa chama cha Chadema, na mgombea urais mwaka 2005, na mbunge wa zamani wa bunge la taifa letu, anakuja kuingia kwenye kudanganyana?

Wanasema ukinyamaza kimya, huenda watu wakaamini una busara kuliko kutoa pumba, yaani mzee wangu bila kukuficha uliyosema hapo juu ndiyo hapa tunaita NONESENSE!
 
Ninaposoma maandishi ya Mukandara, navutiwa kuendelea. Anajadili issues. Na hata anapojadili watu anawaunganisha na issues. Sitaki kuhoji elimu yake, lakini naona anajitofautisha na wengine wetu humu...

KATIKA tafutatafuta, nimekutana na tovuti ya CHADEMA. Nimeisoma na kugundua inajibu baadhi ya maswali tunayoulizana hapa. Kwa mfano sera ya majimbo. Ione hapa. www.chadema.net
 
Watu wenye elimu nzito, mpaka kuwaelewa wenye elimu nzito wenzao wanatafuta nini kwenye forum za kudanganyana?

Hivi elimu tunayotishiwa nayo bongo kila kukicha anayo nani? Mbona nji yetu haiendi kokote? Miaka 44 ya uhuru bado hatuna umeme, lakini tunaimbiwa elimu weeeeeee, jamani mimi siiitaki hiyo elimu!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom