Mbowe vs Chifupa + CHADEMA vs Family Business

Mbowe vs Chifupa + CHADEMA vs Family Business

Status
Not open for further replies.
Wapendwa,

Bwana Forum nimekuja kujibu nimekuta umechanganya mahindi, mchele, mtama nk kwa kuwa zote tu zi nafaka. Umenichanganya. Lakini nimeona radhi yako. Nashukuru. Hivyo nitachangia hapa hapa. Hivi hivi kwa kuwa sehemu kubwa ya hoja zilizoshwa nazikumbuka.

Chinga nashukuru kwa pole ya msiba wa kwanza. Ulikuwa ni wa kaka yake na Akwilombe kwa hiyo unastahili kumpa pole zaidi yeye. Jana nilitumia tena sehemu ya muda kwenye msiba mwingine. Katibu wa CHADEMA mburahati jimbo la Ubungo alifariki(Mungu amlaze mahali pema).


Sasa nanza kujibu rasmi hoja mbalimbali zilizoelekezwa kwangu. Michango imekuwa mingi sana kwa hiyo nitajibu kwa ujumla zile hoja ambazo hazijatolewa ufafanuzi. Na kama kuna zingine nitaziruka wahusika waniambie nizijibu.

Nianze na kukumbusha hoja zilizoleta maswali kuhusu elimu yangu: Moja ni mjadala ya kuwa Tanzania kuna udini na kwamba wakristu wanapendelewa zaidi na kwamba kutokana na kupendelewa huko mimi nilipendelewa kupata division 1.7 kidato cha nne nikiwa na A tisa na kwamba kidato cha sita kwa kuwa sikusoma shule ya kanisa nikapata division 3.17(tatu ya mwisho).

Pili, niliweka tamko la CHADEMA kuhusu uchaguzi wa EALA, mara ikaja hoja kuwa CHADEMA haiwezi kutoa tamko kuhusu suala la nasaba katika kushika nafasi za uongozi kwa kuwa na yenyewe ina utamaduni huo. Kabla hata jibu halijatoka mjadala ukabadilika Chinga akaingiza tena hoja ya kwamba nimepata division 3 ya mwisho kidato cha tatu pindi nilipofafanua hili akaendelea kusisitiza kuwa nina division 3 na akaingiza hoja nyingine kuhusu kuchelewa kwangu kumaliza shahada yangu chuo kikuu cha DSM. Huu ndio muktadha wa mjadala mzima kuhusu elimu yangu.

Maneno makali makali yalitumiwa katika mjadala mengi yanakaribia matusi kwangu lakini sioni busara kuyajibu hayo badala yake nitajadili masuala yaliyojitokeza.

Ila nirejee tena kauli yangu ya mara kwa maratujadili masuala sio masihara!.....kwa upande mwingine tunaotumia majina ya kalamu tuheshimu wajibu wetu.nia ya kutumia jina la kalamu ni kuweza kusema ukweli bila hofu ya kutambulika kutokana na sababu mbalimbali na si kutumia fursa hiyo kutukana. Ni suala la ubinadamu tu.

Baadhi wamesema kuzuka kwa hoja ya udini ni suala dogo. Mimi naamini ni suala kubwa sana. Na kuna suala kubwa zaidi ya hilo, UBAGUZI. Tanzania kuna ubaguzi unaochemka chini kwa chini. Its a volcano, and perhaps a time bomb.

Binafsi kabla ya kuingia kwenye uchaguzi mwaka jana nilipata nafasi ya kusoma kitabu cha Mauaji ya Mwembechai kilichopigwa marufuku. Na kumbuka Mwembechai kama eneo lina taathira kuwa katika siasa za Ubungo hususani Makurumla na Mburahati. Lakini niliacha kabisa kuizungumzia hii ajenda.

Kwa kuwa nilijua sensitivity yake hususani wakati wa uchaguzi. Lakini sasa ni wakati mwafaka wa kuyajadili haya. Mimi ni msomaji wa kila wiki wa magazeti yenye mrengo wa kidini ya kislamu the likes of Al Nour, Nasaha, Alhudaa. Na magezeti ya kikristu the likes of Msemakweli, Nyakati, Kiongozi, Tumaini letu na mengineyo.

There is a volcano boiling. Infact, it seems to be a global phenomenon-the conflict between western and eastern civilization that is fought through various fronts including religious. Nisingependa kulijadili hili hapa,nisije nikaendelea kutoka nje ya mstari!
 
1. Lakini wote mliohusisha matokeo yangu ya kidato cha nne na suala hili la udini kwamba nilipendelewa mmetumia wrong indicator. Na nasema hizi kwa sababu tatu: Mosi, ninahistoria ya kufanya vizuri sana katika masomo yangu kabla hata ya kwenda seminarini.

Kwa hiyo labda mnijibu, niliposhika nafasi ya kwanza mkoa wa DSM na kuchaguliwa kwenda shule ya vipaji maalumu ilboru, nilipendelewa na kanisa?Mkumbuke shule ya msingi mbuyuni niliposoma haikuwa shule ya kanisa! Pili, kati ya wanafunzi wote wa Maua seminari niliomaliza nao kwa nini ni mimi tu waliamua ‘kunipendelea' kunipa division 1.7. Why me?.

Tatu, nilipofika Tambaza na kuendelea kushika nafasi ya kwanza darasani napo palikuwa na mkono wa kanisa?. Nadhani ni vyema aliyetoa na mliounga mkono hoja hii mkakiri kwamba mlitumia mfano ambao sio sahihi!.

2. Narudia tena; sijapata division 3 pointi 17 kidato cha tano. Nilipata division 2 pointi 12. Niliposema awali Chinga amekuja tena na kusema nimedanganya. Sijui una nia gani ndugu yangu.

Utamaduni wa Forum hii ni kuwa mtu akiteleza na kutoa fact kimakosa anaomba radhi. Sasa wewe unaendelea kusimamia hoja isiyo kweli. Katika hali kama hii siwezi kuita kwamba ulikosea bali naamini uliamua kudanganya kwa makusudi. Naomba kwa mara ya pili, toa ushahidi ama kiri kwamba ulikosea.

Nimemaliza Tambaza 2001 hivyo matokeo yangu ni rahisi tu kuonekana baraza.Go and check Chinga, acha ubishi usio wa lazima. Kama kuna mtu anataka kujua kwamba kwanini nilipata A saba O-level, na kuendelea kushika nafasi ya kwanza Tambaza lakini Mtihani wa Mwisho nilipata daraja la pili niko tayari kujibu.

3. Ni kweli nimechelewa kumaliza shahada yangu ya utawala wa biashara(BBA) chuo kikuu cha DSM. Niwaombe radhi wote mnanionitakia mema. Najua suala hili linawaumiza sana. Suala hili lina muumiza zaidi mama yangu. Na hivi karibuni limekuwa sababu mojawapo ya mpenzi wangu ‘kuniacha '. Kwa hiyo nakiri kuwa ni changamoto. But time kills, time heals, Time tells. Niwaeleze tu context, si kwa nia ya kujitetea or justifying, ila kwa nia ya kuweka kumbukumbu sahihi.

Mzee Es, ni kweli ulilizungumza hili BCStimes. Na nikakujibu very boldly. Nilikuwa najua ninachokisema. Nimeshamaliza miaka mitatu ya kwanza kwa hiyo bado mwaka mmoja ambao una semester mbili. Moja ya darasani pamoja na mitihani, moja ni nje ya darasa bila mitihani(project work). So wakati ule nilikuwa naingia kwenye uchaguzi then mara baada ya uchaguzi ningefanya mitihani.

Lakini si kila ambacho unapanga wakati wote kinakuwa kama ulivyopanga, baada ya kifo cha Mzee Jumbe(RIP), uchaguzi ulisogezwa mbele na kuingilia mitihani-so I had two option- Ama kuacha kampeni na kujiandaa kwa ajili ya mitihani na kufanya mitihani au kuendelea na kampeni na kuahirisha masomo. Kupanga ni kuchagua. By then tayari watu wa Ubungo walikuwa na hamasa kubwa na tayari kuna wengi waliokuwa wameathika kwa namna moja au nyingine kutokana na kuniunga mkono. Sikutaka kujipendelea mwenyewe na kufanya usaliti. I had to swallow a difficult pill.

Nikawasilisha barua ya kuahirisha mwaka. Sasa nasuburi semester zangu ambazo sijafanya nirudi masomoni pamoja na kufanya viporo vya mitihani. Kwa hiyo toka Januari nimekuwa huru pindi nitakapokamilisha taratibu nitarajea. ( I hope hakutakuwa na siasa katika taaluma!). Ila nawashukuru wote kwa kuwa concerned. It's a valid concern. Mwanasiasa,umesema kweli kwamba nimewapa fursa wapinzani wangu ya kunishambulia.

Nakubaliana nawe. Lakini ni mashambulizi ya muda. Kwa upande mwingine, hata lisingekuwepo hili wangesema mengine, mashambulizi ni kitu cha kawaida kwa wanaoamini siasa za kimakaveli( mimi siamini katika the prince, naamini katika the new prince ya Dick Morris). Niliwasoma wote hawa kabla ya kuingia siasa. Visome vyote utajua ninachomaanisha. Soma pia kitabu cha Ashcroft-Dirty times, dirty politics utajua ninachokisema.

4. Swali linaloweza kuzuka ambalo ki msingi niliwahi kudokeza huko nyuma kwamba ilikuwa ni moja ya sababu kwa nini mama yangu ina particular alikataa kata kata nisigombee mwaka 2005 ni ‘kwa nini usisubiri kabisa ukamaliza ndio ukaingia siasa na kugombea?'. Narudia tena jibu nililomjibu-nilimwambia wakati huo nikiwa na miaka 24- ‘Nia ninayo, sababu ninazo, uwezo ni nao. Kwa nini nisubiri. Hivi kama kila mzazi akimwambia mwanae asiingie upinzani mtoto wa nani atakuwa upinzani. 2005 kuna uchaguzi, nataka ni-make a point kwamba vijana ama viongozi wa kizazi kipya tunaweza.

Nimewahimiza vijana walionizidi umri kugombea naona wengi wanaogopa. Nitawaonyesha kama inawezekana halafu chaguzi zijazo watajitokeza wengi zaidi. Sitaweza kutoa mfano huu vizuri kama nikisubiri mpaka mwaka 2010 ambapo nitakuwa na miaka 30. Najua hofu yako ni kuwa CCM watanifanya nisimalize masomo. Remember, nitakuwa na miaka 26 baada ya kumaliza uchaguzi. Nina muda bado wa kutosha wa kurekebisha historia.

Na wakifanya hivi watakuwa wametengeneza missile. Hii ndiyo maana ya struggle. Lazima kuna kafara kidogo. La muhimu ni kuhakikisha tu haiwi kafara kabisa ambayo hupoteza nguvu ya mapambano. Inawezekana. Wakati utathibitisha'. Inawezekana kuna majibu nimeyaruka katikati lakini hiyo ndiyo context! Samahinini wote mnaonipenda kama msimamo wangu unatazama zaidi umma na kusahau maisha binafsi. Mkitafakari kwa makini maneno yangu mtaona nimezingatia yote mawili.

5. Kuna mengi yamepotoshwa in between. Kwamba nashauriwa vibaya, infact mngesema najishauri vibaya kwa kuwa kila anayenizunguka ikiwemo ndani ya CHADEMA wanamsimamo kama wenu. Infact watu kama Eric Ongara huwa wananitukana kabisa katika hili. Kwa hiyo kama ni ushauri mbaya then najishauri mwenyewe vibaya.

Na ikizidi sana nawaruhusu kuniita ‘HAAMBILIKI'. Napokea ushauri wenu na kuufanyia kazi lakini nami pia najua ninachokitaka. Imesemwa kuwa posho za safari za CHADEMA ndio zinanipumbaza. Inachekesha!. Yoyote anayenifahamu hawezi kusema kauli kama hii. Uliyetoa hoja hii jua kwamba nasafiri zaidi ndani na nje ya nchi kwa shughuli zangu za nje ya chama zaidi ya za kichama.

Na ukweli ni kuwa financial napoteza kupindukia kwa kufanya kazi za CHADEMA. Both real(in terms of giving out) and opportunity(in terms of time) costs. Unayetoa hoja hii hebu pitia kidogo CV yangu. Nikupe mfano mdogo tu, wakati nikiwa consultant wa mradi wa kuwajengea uwezo wabunge nilikuwa nalipwa dola 100 kwa siku. Hii kufuru ukilinganisha na mshahara wa mwalimu wa Tanzania kwa mwezi. Siku hizi nimepunguza idadi ya siku za kazi zangu zingine kwa ajili ya chama.

Ni majitoleo ya kutosha. Niliamua kujitolea mwaka huu kwa ajili ya CHADEMA, mwakani pia nitajitolea kwa ajili ya chama. Nia nikujenga systems hususani ya vijana!(ili hata ukipunguza nguvu wawepo wengine wa kuendeleza). Halafu nitakwenda kujiendeleza zaidi kielimu. Nimejitolea kujenga chama mbadala Tanzania. Katika Maslow Hierarchy of needs mimi nimeshapita level ya basic needs. Siasa hainilishi wala kunivisha!.

6. Kwamba mimi na CHADEMA hatutoi kipaumbele kwa elimu. Another kichekesho!. Aliyesema hoja hii asome sera ya elimu ya CHADEMA. CHADEMA ni zaidi ya Mbowe na Mnyika, CHADEMA ni asasi ya watu wengi.

Infact siku moja nilipata shock mwaka jana mtu aliponiambia kwamba CHADEMA ni chama cha wasomi, makamu mwenyekiti katibu mkuu wote ni madaktari wa kusomea sio udaktari wa heshima na akanitupia lawama kwa nini mmnamuacha Profesa Baregu asimamie masuala ya kisera wakati kwa usomi wake wananchi hawatamwelewa.

Hili nitalijadili wakati najadili uhusioano wa CHADEMA na conservative. Umewahi kujadili elimu ya wabunge wa viti maalumu wa CHADEMA kwa uwiano na kulinganisha na vyama vingine?. Nilisoma gazeti la mtanzania nikashangaa katika habari yake yake kuu kaburu alipojitoa sababu kuu iliyotolewa ni kwamba CHADEMA inakumbatia vijana wasomi.

Natambua umuhimu wa elimu. Yoyote anayetaka kujua msimamo wangu kuhusu elimu asome mada yangu niliyoandika nikiwa kidato cha sita na kuiwasilisha kwenye warsha ya wabunge Dodoma(Towards a more functional education in Tanzania). Knowledge is power.

When I said education makes a wise wiser and a fool more foolish Kikwete wakati huo akiwa waziri wa mambo ya nchi za nje alisimama kupongeza ingawa alinilaumu kwa kuingiza issue ya Michael Sikupya kwenye mada yangu, Mwanri wakati huo akiwa Mbunge wa siha yeye alisifia approach ya ukombozi wa fikra.

Cheti ni muhimu lakini elimu ni zaidi ya cheti! That's is why as an emerging enterpreneur my first investment is in education in one of the district that is backward in this important sector. Anyway, yapo mambo mengi. Niache kwa sasa kuhusu CHADEMA na elimu yangu unless kama kuna maswali.

Nataka sasa kuingia kwenye suala la CHADEMA na conservative, then nitakuja suala la allegation za ukabila katika viti maalumu CHADEMA, then nitajadili allegation the CHADEMA kuwa ni business family, suala la helikopta, uhusiano wa CHADEMA na conservative then on and on mpaka nitakapo exhaust masuala yote!

Lakini kwa upande mwingine-nilishangaa kabisa mmeacha kujadili masuala mengi ya msingi katika lile tamko la EALA(tembelea www.chadema.net, tazama pia katuni ya wiki icheke!). Naomba kila mmoja alipitie tena, tunapaswa kutazama zaidi maslahi mapana ya kitafa….

Coming soon………


Natabaruku.


JJ
 
Safi sana kijana Mnyika,

Niliwahi kuandika kuwa Chinga hajakosea lolote kuuliza lolote, mnatakiwa mje na hoja zenu kama hizi nasi tuchambue

FD
 
Well put Mnyika. Cha kuzingatia katika siasa ni kuhahakisha unazima unnecessary loop holes kwa wapinzani wako. Najua kuwa hawatakosa sababu za kukushambulia, lakini ni muhimu kuziba ile mianya iliyo ya wazi kabisa. Kwa hiyo hilo la elimu yako ni mwanya usio na ulazima hasa kwa kuzingatia uwezo wako.

Hili la elimu sasa linatosha, huna sababu ya kuendelea kujitetea. Wewe piga shule sisi tusikie tu baadaye kuwa umeshavaa gauni lako pale mlimani.

Endelea kutoa shule katika maeneo mengine. Ukiendelea na kujenga hoja hivi najua ndugu zangu Chinga, Dr WHO na Tafiti watarudi maana wameshakimbia baada ya merging ya mada.
 
JJ Safi, kazi nzuri hii. Maaliza shule uwe na busara zaidi pamoja ya kuwa nakubali unafanya kazi ya kitume.

Kwa bahati mbaya majibu yako yamekuja wakati ambapo chinga amekwisha aga.
 
EO,

Simshangai Chinga, nilijua atawika kwa wiki zisizozidi 3 au nne. Kama kaondoka ni vema. Alikosea maeneo mengi lakini wengine tumenyamaza kimya kuona mbio zake zitaishia wapi.

Duh, Mnyika umeandika mwenyewe au una mtu anakuandikia? Mengi kweli. Kama uliyoandika ni kweli toka rohoni, basi nakubali kuna kujitolea kabla ya kupata ufanisi.

Siasa zinahitaji watu kama wewe. Wanaoongea uwongo ili kupata kula (si kura) wanakuwa wanatufanya wengine tuone siasa ni ulingo wa wasanii. Nice job bro, keep it up. Nakupa shavu mtu wangu!

Ila babake kamua shule si unajua mambo si mambo UDSM? Pakizingua wewe fanya mawasiliano na watu wa hapa naamini hawatakutupa watakusaidia kupata vyuo mbadala.

Keep it up bro! Nasubiri aingie kiongozi wa CUF, TLP au CCM. Ningependa aje mwanamageuzi halisi mzee wa NCCR. Napenda sana kuona hoja zake hapa. Hapajui? Hakuna watu wa NCCR? Au ndo kusema internet mzozo wakati wa mgawo wa umeme? Najua maswali na hoja nyingine za hapa wengine wataweza kuzivunja keyboards kwa jazba na hasira baada ya kukumbana na kina Chingaz kwani yataka moyo kujibu hoja flani. Nilitarajia Mnyika aje na ma2c lakini haikuwa hivo!

Adios, naandika kwanza juzuu juu ya mafanikio ya JK katika mwaka mmoja.

BrB
 
Well done JJ. Well said all the best. When you get time please return to answer other questions regarding Ukabila ndani ya Chadema, Viti Maalum etc.
 
Mzee JJ,

Heshima yako mkuu! Nimeona vitu vyako ila ninahitaji muda kidogo kuvi-diggest halafu tutarudi kuendelea na somo.
 
JJ Mnyika,

Sijui hata niseme kitu gani!....
Inasikitisha tu kuona watu walikuvalia njuga elimu yako hali watu hawa hawa sijawasikia wakiuliza elimu ya mwinyi, Mkapa na hata JK na alipata division gani na hizo point!

I mean, Kuna maswala muhimu sana kwetu kuliko Elimu yako kwa sababu sidhani kama wewe na Elimu yako ndiye utatuvuta sisi kuingia ama kuchagua Chadema. Labda nakosea lakini sioni kabisa uhusiano wa Elimu yako na sisi kuweza kuielewa Chadema.

CCM hawana jipya siasa zao zinajulikana na hawawezi kabisa kuingia humu kwa hiyo jaribu kujibu maswala yake uliyoyaacha.. Please hayo ndio muhimu zaidi.
 
Hongera Sana Mnyika.

Ujasiri Wa Kuja Kujibu Hoja Kwenye Hii Forum Ila Raha Imepungua Naweza Kusema Paka Akiondoka Panya Hutawala Rafiki Yako Chinga Alikusubiri Kwa Muda Uje Ameondoka Na Wewe Umekuja Yote Kheri.

Nilikuwa Msomaji Tu Nimeona Kuna Kitu Sijui Unaweza Kukifafanua? Katika Maelekezo Yako Umesema Ulikuwa Consultant Ukilipwa Dola Mia Kwa Siku, Naamini Consultant Anatakiwa Mtu Mwenye Elimu Ya Kutosha Huwa Phd Na Masters Sana Au Professional Qualifications Like A.c.c.a, Kwako Ulikuwa Ukitumia Elimu Ipi Ya Kukupa Hadhi Ya Kuwa Consultant?

Nimefuatilia Mjadala Inaonekana Una Elimu Kidato Cha Sita, Hapo Fafanua Vizuri Siamini Kidato Cha Sita Anaweza Kuwa Consultant, Na Hata Kama Ulipewa Hiyo Kazi Basi Kimakosa Au Uliipata Kiupendeleo,

Unajua Unaweza Kukaa Na Watu Kwa Upeo Wao Wakakupachika Cheo Hata Haunacho Utaona Mtu Anaitwa Professor Huku Si Professor Kuna Watu Wamejipachika Au Kupachikwa Udokta Huku Hawana Sifa Hizo Huenda Waliokupa Uconsultant Walikuwa Na Nia Kama Hizo Juu.

Kulipwa Dola Mia Kwa Siku Hata Milioni Kwa Siku Hakuifanyi Elimu Iwe Haina Thamani,unaweza Kuuza Barafu Na Ukapata Milion Kwa Siku Na Kuna Daktari Analipwa Laki Mbili Kwa Mwezi Katika Mizani Ya Ufanisi Bado Daktari Au Mwalimu Anakuwa Juu Zaidi.

Umesema Basic Needs Umeshapita Lakini Kwa Mtazamo Wangu Basic Needs Ina Jumuisha Elimu Inayoendana Na Wakati Nadhani Kutokuwa Na Digrii Kwa Kiasi Fulani Hujapita Basic Needs, Chukulia Uko Wewe Na Vijana Ulikuwa Nao Shuleni Mwenzako Anasema Nimemaliza Mba Yangu Mzumbe Na Sasa Niko Sehemu Fulani Na Mwingine Anasema Namalizia Cpa Yangu Baada Ya Kumaliza B.com Udsm, Wewe Utasema Nini? Utaona Hau Fit Katika Kikao Hicho.

Umesema Kuna Sera Nzuri Ya Elimu Chadema Kumbuka Sera Nzuri Isiyoambatana Na Vitendo Haina Mantiki Sana, Kuna Watu Wanatembea Na Project Write Up Nzuri Sana Za Ngo Au Taasisi Mbalimbali Kuomba Funds Lakini Uhalisia Wa Hizo Project Ni Tofauti Na Vitendo Vya Hizo Taasisi.

Kuhusu Kidato Cha Sita Ungesema Umepata Nini Kama Unavyoweka O-level Una A Tisa Kila Somo, Vipi Kidato Cha Sita Naona Kama Imekuwa Siri Na Inaleta Utata Kidogo?

Mengine Yote Umefanya Vizuri Na Tuletee Zaidi.
 
Guys, vipi lakini?
Mtalii, tafadhali haya ya elimu ya JJ yanatosha. Hii sio tena ushauri ila kumchambua mtu uchi wake mwisho akibakia uchi mnazidi kumcheka yeye.

Ebu tuambieni nyie Elimu zenu kabla ya kumchambua mtu mwingine na mmeweza kuzitumia vipi hizo Elimu zenu. Kumbukeni tu Elimu sio muhimu kwa mtu mmoja ama mwanasiasa pekee, Elimu ni muhimu kwa kila mmoja wetu.

Mpya, hakuna zaidi ya kuwa tunazidi kujigonga wenyewe. Ebu tazama maelezo yako hapo juu umesema hivi:-
Kuna Sera Nzuri Ya Elimu Chadema Kumbuka Sera Nzuri Isiyoambatana Na Vitendo Haina Mantiki Sana, Kuna Watu Wanatembea Na Project Write Up Nzuri Sana Za Ngo Au Taasisi Mbalimbali Kuomba Funds Lakini Uhalisia Wa Hizo Project Ni Tofauti Na Vitendo Vya Hizo Taasisi.
Ikiwa unayaona mapungufu ktk Project written up, basi ndivyo kabisa inavyokuwa ktk Elimu.

Wapo wenye vyeti vizito sana na bado wanashindwa ktk vitendo vya hizo taasisi....(tumeyaona toka CCM) na kama kweli Elimu peke yake ingekuwa hoja kubwa zaidi ktk utendaji kazi basi pasingekuwepo na Interviews... Ukionyesha cheti nitolee umepita! na rais wetu sijuji angekuwa nani yule mwenye digrii saba sijui tisa!

Consultant sii lazima awe na Phd... Haya ni maradhi ya waafrika sisi ambao tukisikia Phd basi huyu ndiye anafaa. Haya maneno labda Afrika lakini navyoelewa mimi wapo ma- consultant kibao ambao hawana Phd isipokuwa experience zao na vipaji vimeweza kuwapa nafasi hiyo.

Mtalii Ulaya kuna watu wana Phd ktk injinia ama Udaktari lakini wanafanya kazi kama madereva wa mabus ama taxi!...wengine wanauza Juice na barafu. kwa hiyo muuza barafu sii lazima awe hana elimu wapo wenye elimu.

Je, utapanda taxi za hawa jamaa kwa sababu wana elimu?... nadhani jibu litakuwa hapana! kwa sababu Elimu ni bora kwa kila binadamu sio kwa sababu ya ajira (kazi). Kifupi, wapo wauza barafu wenye Phd na wanazitengeneza fedha vizuri.
Come on guys the guy kajieleza vya kutosha mnataka aanze kuwaeleza jinsi gani kaajiriwa kwa kulipwa $100 kwa siku?... damn mnakwenda mbali sana tena nje ya topic!

Sorry! tunaanza kuchemsha sasa maana kilichobaki mtaanza hata ku - question uume wake.
 
Samahani Mtalii,

Kama umewahi kufanya kazi ktk consultancy firm (kama nifanyavyo mimi) utagundua umekosea au umeteleza kidogo. Nikiwa kama consultant siwezi kwenda Library au field kukusanya raw data, always kuna vijana watakwenda kunitafutia reference mbalimbali, ukiona ninakwenda mwenyewe basi ujue hiyo kazi ni very sensitive, mimi nina compile au ku review na kupresent. Angalia hata kwenye research institutions hali ni hiyo hiyo. Kama JJ amekosea kujijumuisha kwenye hiyo consultancy sijui, ila kama alikuwemo kwenye team ya kufanya consultancy ya kazi fulani, sioni kosa lake kusema alikuwa consultant.

PHD tunazo za kumwaga serikalini ndugu yangu, profesa wa kumwaga nieleze Richmond zinatoka wapi? si unataka consultancy ifanywe na PHD ma MBA nieleze IPTL zinatoka wapi? mikataba ya madini inatoka wapi?, soma vizuri au rudia Mnyika alivyoelezea elimu, inaweza kukufanya mjinga zaidi au mwerevu zaidi.

Naomba fanya kidogo homework kabla ya kujibu.

Asante

FD
 
FD
Mie huwa sielewi hivi watu kama Mtalii huwa wnachukulia maana ya Elimu ni nini? Mtu kuwa consultant inabidi awe na Elimu gani? Who is a consultant? Mtalii labda unge-define unachukuliaje consultancy na Education levels.

Mie ninge-doubt kama Mnyika angeenda kufanya consultancy ya Medicine while he is taking BBA; it is time we know what we write.
 
IO,

Jamaa mtalii kweli, lakini alikotalii hakuangalia kilichompeleka kutalii. Nina wasiwasi kama hajapata mwongozaji wa watalii atadumbukia shimoni...

Angalia:

John Mnyika said:
...Nianze na kukumbusha hoja zilizoleta maswali kuhusu elimu yangu: Moja ni mjadala ya kuwa Tanzania kuna udini na kwamba wakristu wanapendelewa zaidi na kwamba kutokana na kupendelewa huko mimi nilipendelewa kupata division 1.7 kidato cha nne nikiwa na A tisa na kwamba kidato cha sita kwa kuwa sikusoma shule ya kanisa nikapata division 3.17(tatu ya mwisho). ....Narudia tena; sijapata division 3 pointi 17 kidato cha tano. Nilipata division 2 pointi 12

mtalii said:
Kuhusu Kidato Cha Sita Ungesema Umepata Nini Kama Unavyoweka O-level Una A Tisa Kila Somo, Vipi Kidato Cha Sita Naona Kama Imekuwa Siri Na Inaleta Utata Kidogo?

Hapo unaweza kujua mtu anasoma haraka bila kurudia kabla ya kujibu. Simlaumu mtalii, utalii wake unahitaji mwongozaji. Usikonde mtalii, swali lako lilijibiwa lakini huenda hukusoma vema. Doubts zako ziko wapi zaidi? Hatutaki Mnyika arudierudie kuhusu elimu kwani ameongea kwenye threads nyingi na tungependa agusie mengine zaidi.

CUF, CCM, NCCR, UMD, PPT Maendeleo, TLP, NRA, etc wako wapi???

Makubwa!
 
IO,

Problem hasa ya watanganyika wengi ndio hiyo, wamekariri sana kuhusu Elimu, na hawa watu wamejaa serikalini, utakuta serikali inamsomesha administrator wa ofisini PHD, jamani Phd ya nini kwa mtawala?!!!!! au mimi siwezi kufikiria? kama anayo Phd well and gud lakini kumtoa ofisini kwenda kusomea Phd kwa hela yetu hiyo siungi mkono, Peleka Medicine doctors wakabobee na Phd, peleka Engineers wakabobee, peleka wataalamu wa kilimo wakabobee, lakini ya kupeleka siasa, wasanii na walifanya biashara, HELL NO! ninakataa.

Kuna sehemu nimesoma kuwa kuna uhusiano mkubwa kati ya watu walioenda shule sana (PHD) kushindwa ku perform kazini. Of course serikali ya Tanzania ni live example ya hiyo, usishangae.
Mtalii, karibu sana lakini achana na mawazo ya kiserikali kiserikali ya Tanzania humu, think kama unafanya kazi kwenye serikali ya Malaysia au Singapore kidogo.

FD
 
wOrM,

Nadhani TLP, si unamjua Mrema? ahah ahahahah kwa kuongezea mwishoni Mnyika akasema kapata Div 2 ya point 12 kama nakumbuka vyema. Ila Mtalii bado anauliza kapata div gani na point ngapi?! kaazi kweli kweli

FD
 
Wazee

JJ maelezo yako safi, ila naomba usiwe unaingia mtini kwa muda mrefu kunapokuwa na hoja inayokuhusu kwasababu it sends a wrong message. All in all, mwelekeo wako kielimu ni mzuri, ongeza bidii umalize hiyo digrii ili upate muda zaidi kwenye politics!
 
Sikumbuki nani aliongelea ufeki wa utendaji kazi wa watu wenye PH.D huko nyuma. Nilitaka kuongezea kuwa mimi ni mmoja wa wanaoamani kuwa digrii za Ph.D ni specialized kiasi kuwa si za kila mtu ila wachache tu katika jamii.

Wale wanaojilazimisha kuzipata nje ya imani hiyo huwa baadaye zinakuja kuwaumbua kama ambavyo tuonavyo pale serikali Tanzania ambao kuna MaPh.D mengi yasikuwa na specialization zozote.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom