Mbowe vs Chifupa + CHADEMA vs Family Business

Mbowe vs Chifupa + CHADEMA vs Family Business

Status
Not open for further replies.
Wacha,
Alijiunga na BOT alipomaliza National Service. Nadhani it was 1981 or 1982. Na wakati huo Gavana alikuwa Nyirabu.

Kama ni homeboy wangu or whatever, that is not the issue. Facts still stand as facts. Baada ya Benki ndiyo akaingia kwenye shughuli za Baba yake pale Mbowes.
 
Invicible,
Good question. What may be important to Chinga may be upupu to others.
 
Jasusi

Thanks, but do you know what position he had?
 
Unajua jamaa wa CHADEMA wanapokuja humu kuwalaumu wenzao about honsty nadhani they should have started by wao kuwa honest na watu then we can take it from there

By the way its not illegal kwa wao kuwa karibu na conservatives but this doesnt mean that the room for questions is closed
 
Aljazeera;10187
Hivi leo hii ni nani anaweza kutuambia zile dola milioni ishirini alizopewa kikwete na Iran (source BBC) zilitumikaje kuwasaidia wagombea wengine mnaweza kutuambia. Tutenganishe misaada au michango binafsi na ili ya chama.



Can you post a link of this BBC story?
 
Jamani ninaomba kuelewa, hivi Freeman anapata hela toka conservative party au ile Charity ya Tony Blair?
 
of course habari hiyo ni classified na naona CHADEMA wanavyokuwa kimya ndivyo hii issue inavokuwa blown out pf proportion

I can imagine chinga takuja na nini humu lakini hii sio thread ya shutma lakini itabidi hiii issue iwekwe wazi ili wapiga kura nao wajue kuwa isije kuwa yale yale ya kuuza nchi kwa waingereza mara ya tatu
 
Wacha,
I am not sure. But I think it was managerial.
 
DrWHO,
Tanzania today is in a political/leadership crisis. Sijui kuongelea uhusiano wa Chadema na Conservative wa Uingereza itasaidia nini. Tumepata rais kwa njia za rushwa na hongo.

Money from Iran, money from Tanzanite one, money from Rostum, hivi havizungumziwi. Chadema is a small party and the Conservatives are a party in the wilderness. So may be they have something in common in that they are both outsiders. Kuna ubaya gani for one to help the other?

Does that mean Chadema will swallow the policies of the Conservatives? That is a question only Chadema can answer and I cannot speak for them.
 
Chinga,
Duuh, bado tuu mshikaji...
Mbona umekuwa mzito na mada yako mwenyewe hasa pale unapouliza..Mbowe na Chifupa nani zaidi?

Labda nikwambie kitu gani kinatushinda kujibu hata sisi tusiokuwa na upande!...hayo mengine ya Helikopta nadhni walengwa ni Chadema kwa hiyo watayajibu wenyewe - Freeman na Myinka na hata mimi ningependa sana kuelewa.

Tatizo linalotusumbua wengi hapa ni swali lenyewe kwani leo hii ukiniuliza Sunday Manara na Nyambui nani alikuwa zaidi itakuwa ngumu kwangu pamoja na kwamba wote hawa walikuwa wanamichezo (sports) bora. Huwezi kupima Uzito wa Sukari na Chunvi kutafuta zaidi kipi hali unachotaka kutumia ni ktk upikaji wa chai...Jibu lake ni rahisi na tunashindwa kuelewa kwa nini unazidi kuuliza wewe mpika chai!

Pili, Uzito wa mzani siku zote hupimwa kwa makusudio, mathlan utaipima sukari ktk mzani na upande wa pili utaweka jiwe la uzito uliokusudiwa. Malengo ya upimaji ni kupata sukari yenye uzito tulio -TEMEGEA. Hapa nashindwa kuelewa kama huyo Chifupa ni jiwe!
 
Hello Watu

Nafikiri Sijui Kama Katika Ina Sehemu Yoyote Inayokataza Chama Cha Siasa Kisipate Pesa Kutoka Nje Ya Nchi Hii Haijawekwa Wazi Kama Basi Kupata Pesa Kutoka Nje Ni Makosa Kwa Mbowe Mbona Kikwete Alipata Pesa Toka Arabuni Wakati Wa Kampeni Na Ameshawapa Mbuga Za Wanyama Sasa Hivi Anataka Kuwakatia Wilaya Moja ? Hii Hatuiulizi Kwa Sababi Kikwete Ni Handsome Chaguo La Wengi Au Sio ?

Kama Wanapewa Pesa Inabidi Ijulikane Na Waweke Wazi Uhusiano Wao Nao Ijulikane , Kama Mbowe Alienda Usa Katika Mkutano Na Rep -- Juzi Hapa Jk Nae Alienda Kuongea Na Bush Kuhusu Siasa Za Kenya Lazima Kutakuwa Na Kitu Hapo Kimejificha Mimi Sikijua Ila Ni Hiyo Mchangu Wangu Tu

Kwaherini Kwa Sasa
 
Hello Watu

Nafikiri Sijui Kama Katika Ina Sehemu Yoyote Inayokataza Chama Cha Siasa Kisipate Pesa Kutoka Nje Ya Nchi Hii Haijawekwa Wazi Kama Basi Kupata Pesa Kutoka Nje Ni Makosa Kwa Mbowe Mbona Kikwete Alipata Pesa Toka Arabuni Wakati Wa Kampeni Na Ameshawapa Mbuga Za Wanyama Sasa Hivi Anataka Kuwakatia Wilaya Moja ? Hii Hatuiulizi Kwa Sababi Kikwete Ni Handsome Chaguo La Wengi Au Sio ?

Kama Wanapewa Pesa Inabidi Ijulikane Na Waweke Wazi Uhusiano Wao Nao Ijulikane , Kama Mbowe Alienda Usa Katika Mkutano Na Rep -- Juzi Hapa Jk Nae Alienda Kuongea Na Bush Kuhusu Siasa Za Kenya Lazima Kutakuwa Na Kitu Hapo Kimejificha Mimi Sikijua Ila Ni Hiyo Mchangu Wangu Tu

Kwaherini Kwa Sasa



La hasha lakini naona Chadema wamekuwa wakilifisha hili lisionekane sasa iweje wao wanalalmika kuwa chama tawala wanaongoza kwa politics za rushwa nk huku wao hawataki kuonyesha mfano wa kuwa TRANSPARENT katika mambo yao sasa tofauti ni nini?

Pili hakuna ubaya wowote kwa wao kuwa na uhusiana na chama chochote kwa sababu sio dhambi ila tu waje clean katika hili then tuendelee kufanya coparative kati yao na kuangalia kama ndoa hii inamnufaisha nani zaidi


Hiii hoja yako kuwa JK alienda kuongea na Bush kuhusu siasa za Kenya ni another CHEAP SHOT ambayo naamini umeitoa kwenye nation media ambao tulishwajibu,ikulu iliwajibu na white house nao waliclarify sasa sielewi unasema nini labda ungefafanua zaidi hili la conservatives
 
Chinga

unajua nilipojaribu kutoa hoja ya masasi nilimaanisha upeo wa watu wa masasi, katika kujadili mambo. Sikuona point kubwa ya kujadili hapo.

Nimesoma Comments ya Mkandara kidogo nimefurahi sana maana alielekea ktk kitu nilichokiona ktk mada hii. Mimi nailinganisha na hile picha fulani ambayo huwa iko ktk ukurasa wa mwisho wa gazeti la Mtanzania(samahani sana ukiangalia mwisho kabisa huwa kuna catuni fulani pale chini sijui kama mpaka sasa bado huwa ipo). Huwa inajaribu kutoa mitazamo ya mtindo huu.

Ndio maana umeona watu wengi wameshindwa hata kuelewa kinachoendela, wamepata kigugumizi ktk kutoa majibu. Wanajaribu kujenga picha hawaipati.
 
Kakindo master.
ina maana Mzee Mkapa uelewa wake mdogo? umetumia kigezo gani kuona sisi watu wa Masasi huoni wetu wa kuchambua mambo ni mdogo? naona sio busara kutuambia hivyo.

mkandara.
uelewa wa swali langu kila mtu ana upeo wake wa kulielewa swali. kama vile wewe unaweza kupima katika mzani wa sukari na chumvi au jiwe n.k

ndio hata majibu ya mtihani watu hutofautiana hata kama wamesoma pamoja.

MBOWE aliahidi kujibu kila hoja itakayojitokeza humu labda aone haina maana,lakini anawajibu wa kujibu ndio maana nimekuwa nikirudia maswali yangu kwani sijajibiwa na chadema au Mbowe, na yeye alituasa tusiwe waoga na kila kitu tuulize tu, na hata majina yetu tusifiche huo ni usia wa mzee Mbowe, mimi nimetumia demokrasia hiyo tuliyopewa na mheshimiwa.

Pia kama unafuatilia vyema kule kwenye Tamko la chadema niliombwa na mwanachadema Mikael nianzishe thread yangu nimefanya.

Mkandara sio lazima mada lazima wewe uchangie ndio iwe na maana kwako, mie kuna mada nyingi sijachangia haina maana hazina maana na wewe sio kigezo cha mada kuwa ina maana au laa.

Mkandara huwajahi kuona wachezaji wetu wa mpira wakijifananisha na wachezaji wa timu za Arsenal, barcelona n.k utaona mchezaji anaitwa Omar Hussein lakini mashabiki wake wanamwita Kevin keegan au Razak Yusuf akaitwa careca kuna Remmy Ongara kuitwa Bob Marley kuna dada zetu wasanii akina SINTA wanajiita Jenifer Lopez, watu wamefikia kusema usalama wa Taifa Tanzania ni zaidi ya marekani au Israel, sikuona bwana mkandara kuhojia vigezo vya mizani gani imetumika ?

Naona maneno yako Mkandara hayana ukweli, toka nimepost thread hii utaona imesomwa na watu wengi sana na imechangiwa na watu wengi sana ktk muda mfupi, hata jambo forum imepata members wengi wapya kuja kutoa hoja kama akina Nyanza, kakindo just to mention a few, Mkandara tizama wasomaji wanakimbilia elfu mbili ndani ya siku tatu tu.

Kichuguu

DR.Who ameomba source ya story iliyosemwa toka BBC hicho ulicholeta ni story za mtikila na hiyo issue labda nikusaidie iliandikwa na Mzanzibar mmoja aliyekuwa akiandikia africa analysis na JK alimfungulia mashitaka na hatimaye gazeti lilimfukuza kazi huyo mwandishi kwani habari ilikuwa haina ukweli wowote, Na ilikuwa wiki mbili kabla ya kwenda Dodoma na magazeti yote yaliandika hiyo story including Tanzania Daima likiweka kichwa cha habari 'Kikwete kulishitaki jarida'
 
Naona maneno yako Mkandara hayana ukweli, toka nimepost thread hii utaona imesomwa na watu wengi sana na imechangiwa na watu wengi sana ktk muda mfupi, hata jambo forum imepata members wengi wapya kuja kutoa hoja kama akina Nyanza, kakindo just to mention a few, Mkandara tizama wasomaji wanakimbilia elfu mbili ndani ya siku tatu tu.

It is the quantity that counts.
 
CHADEMA ni mwanachama wa umoja wa vyama vya kidemokrasia duniani kwa kimombo Internationla Democrats Union (IDU). Miongoni mwa wanachama wa vyama hivyo ni vyama vya Repulican na Conservatives of US and UK respectively. Vyama vingine wanachama ni pamoja na Moderat-chama kinachotawaka Sweden, Hoyre - Chama cha upinzani Norway, NPP-Ghana chama tawala, DP-Kenya na vyama vingine kadhaa.

Hapo ndipo uhusiano kat ya CHADEMA na Conservative unapokuja. Ni vyama vya mrengo mmoja, vinavyoamini katika Soko Huru, Uhuru wa mtu binafsi kumiliki mali (The right to own Property) na utawala wa sheria.

Kama ilivyo kwa CCM kuwa ni mwanachama wa Socialist International pamoja na Labour cha UK, SPD cha Ujerumani na Socialist Party cha Ufaransa na vile vile CUF kuwa ni mwanachama wa Liberal INternational pamoja na UK Liberals, UDF Malawi, MDC Zimbabwe ndivyo ilivyo kwa CHADEMA.

Si kweli kuwa CHADEMA imekuwa kimya katika mahusiano haya. CHADEMA imekuwa wazi sana, ziara za viongozi wa vyama hivi Tanzania zimekuwa zikitangazwa wazi wazi na hata Freeman Mbowe anaposafiri kuwa katika mikutano mbalimbali ya vyama hivi inatangazwa. CHADEMA haina cha kuficha katika hili kwani ni lazima vyama viwe na mahusiano na vyama vya nje ya Tanzania.

Kwa taarifa tu ni kuwa Mbowe kwa sasa ni Katibu Mkuu wa tawi la IDU Afrika nzima na Tanzania ndio makao makuu ya Democrats Union of Afrika (DUA).

Chama cha Conservative hakiipi CHADEMA fedha kama watu wengi wanavyodhani. Na pia CHADEMA haijapokea hata senti moja kutoka chama cha Republican. Matumizi ya Kampeni za CHADEMA katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2005 yaliwekwa wazi kabisa katika magazeti.

CCM nao waseme walitumia kiasi gani katika kampeni na walipata wapi fedha za kampeni ...................maweeeeeeeeee
 
Chinga,
Tunakuja kwa wingi ktk mada hii kwa sababu mada hii ni sawa na magazeti ya Udaku ama vipindi vya TV kama vile Entertainment Tonight!...Hii ni burudani na shukran sana.

Isipokuwa unataka kuchanganya sasa hizi mada mbili. Ile nyingine ndiyo yenye maswali yako kwa Chadema na Freeman lakini hii umetuwekea sisi tupime Freeman na Chifupa. Hawa hawako ligi moja wala hawachezi mchezo mmoja.

Kuhusu Upimaji wa vijana wetu na wachezaji wa nje kama Arsenal, nadhani hapa bado hujaipata picha. hawa vijana wanamichezo (sportsman) wanacheza mpira wa miguu sawa na ule unaochezwa na Arsenal. Hawa vijana wanajiita majina hayo sii wachezaji wa Tennis.

Malengo ya kipimo cha Freeman ambaye namwita -sukari, ni ktk kuunga kiti cha RAIS! (Chai).. sasa hapo lazima tuweke uzito wa jiwe la ujazo wa kiti hicho. Hii ndio maana yangu ktk upimaji wa Sukari na jiwe. Lakini tunapoweka Chifupa kuwa jiwe la kupimia hali Chifupa ni Chunvi -Mbunge na sijui waziri wa kuteuliwa nashindwa kuelewa malengo ya upimaji huu wakati tunachotaka kujenga ni mapishi ya Chai.

Kisha bibi huyu ni mcheza Tennis hali Freeman anacheza Football...Ndio maana muda wote nashindwa kuelewa malengo ya upimaji wa elimu ya Sunday Manara na Nyambui hali tunachotafuta ni ujuzi na uwezo wa mcheza football.

Kweli kabisa Watu tunatofautiana kuelewa. Yawezekana wewe umeweka Sukari kila upande wa mzani na kupima uzito bila malengo halisi.
 
chinga,
sijui kama utanielewa ila nitajaribu kukuelewesha, katika mawasiliano kuta kitu kinaitwa "protocals". ili watu au vitu viwili viweze kuwasiliana na kuelewena lazima kuwepo na protocals, protocals ni kanuni na sheria za kurahisisha mawasiliano,

mfano lugha tunayotumia humu ndani ni moja ya protocals, wote tunatumia lugha ya kiswahili na kunawakati tunatumia lugha ya kiingereza kwa asumptions kuwa wengi wanailewa,
kama kuna mtu angekuja hapa ndani na kuanza kuzungumza kichina au kihindi sidhani kama tungekuwa na mawasiliano.

sasa kanuni hizo za mawasiliano haziishi tu kwenye lugha, manaweza kuwa mnatumia lugha moja lakini bado mkawa hamuelewani kwasababu bado kuna kanuni nyingine hazijafuatwa,
mfano freeman mbowe ni mwenyekiti wa chama,kwa mtazamo wangu unapotaka kuwasiliana na mtu kama huyo lazima ujitahidi kufuata protocals hizo,mojawapo ikiwa ni kumheshimu yeye na wadhifa wake, siamini kama amekimbia maswali bali hajakuelewa kutokana na lugha unayoitumia, nafikiri ungekuwa makini katika kufuata hizo kanuni za mawasiliano angekuwa ameshatoa majibu.

mfano unao wewe unapotaka kwenda kuwasiliana na mzazi wako lazima utumie lugha ya heshima ili muweze kuelewana.

pili kwa wale wanaodai kuwa viongozi wa chadema wamekosea kutumia majina yao kwenye forum hii natofautiana nao,

kwa mtazamo wangu hii ilikuwa ni nafasi muhimu kujadili mambo mengi ya msingi ikiwa ni pamoja na hayo mnayo hoji kama ya uhusiano wa chadema na conservative na mambo ya hellocpter na sera ya majimbo.
tungepata majibu kutoka kwa mwenyekiti mwenyewe wa chadema ambaye ndie muhusika mkuu.

tatizo ninaloliona hapa ni hilo la immotional incompetence kama linavyojadiliwa kwenye ile topic ya waafrika ndivyo walivyo?

watu wengi wanafikiri hii forum inasomwa na watanzania pekee,hawajui kuwa kuna watu wa mataifa mengine wanasoma humu kama wakenya, waganda, warwanda...
mfano kunasiku nilikuta mke wa professor mbilinyi(mzungu) ameweka post yake mahali fualani.
sasa wageni hawa wanapokuja kusoma humu na kuona mitazamo ya watanzania na jinsi tunavyojenga hoja ni wazi kuwa tunajiabisha.

kuna sehemu zimetengwa kwa ajili ya mambo kama haya ya udaku, manaweza kwenda kule mkaweka hizi post zote na waopenda kujadili mambo haya watawafuata huko, ila kutuletea hapa ni wazi tunajionyesha jisni tusivyo serious na mambo muhimu katika nchi yetu.

naomba kutoa hoja.
 
Chinga

Katika post ya ukurasa wa saba nilitoa mfano, ningeweza kutoa kijiji kingine chochote/sehemu nyingine yoyote iliyo na watu wa kawaida kabisa. Nilitegemea ungeweza kuelewa kirahisi.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom