Ndugu Chinga kama nilivyokuahidi kurudi na majibu yangu hoja kwa hoja, nafanya hivyo. Majibu yangu yatatumia marejeo yalipo kwenye Taasisi za Serikali ikiwemo, Tume ya Uchaguzi, Kitengo cha Nyaraka za Wafanyakazi wa Serikali (kipo nyuma ya UNICEF), nk. Bado nasubiri nyaraka za NECTA na
Hoja 1: Public CV
Website ya Bunge la Jamhuri ya Muungano, ni sehemu ya mwisho kabisa kutafuta wasifu wa wabunge kwani kuna historia ya siku nyingi kuhusu ukweli wa record zilizopo. Ukitaka kuona hili basi jaribu kuangalia CV ya Mbunge mwingine ye yote halafu ulinganishe na ukweli halisi. Kwa harakaharaka unaweza kuanzia na wabunge wenye majina makubwa hapa Bongo na hata viongozi wa vyama.
kama unataka kuona CV halisi na timilifu basi nenda tume ya Uchaguzi utapewa kama una sababu zitakazowaridhisha. Miaka ya nyuma niliwahi kuwasiliana na wanaosimamia hiyo website Datavision kuhusu info za aliyekuwa mbunge wangu kwani yeye binafsi alipinga kuwa na shahada ya Kilimo iliyokuwa imeonesha kwenye website infact alikuwa mafunzo ya miezi mitatu ya bwana shamba Uholanzi, lakini wakasema hizo habari walipewa na wafanyakazi wa bunge.
Mfano: hiyo CV uliyotuletea inasema High School bila kusema jina la Shule, ukiendelea kusoma nyingine utaona watu wamepewa Shahada kibao bila kusema wamepata wapi na mwaka gani.
Kwa hilo tu linatosha kusema, website ya Bunge letu siyo chanzo kizuri cha habari, na kuna makosa mengi mno kiasi kwamba tunaweza kusema ni vigumu kutumia cv za hawa wahusika kuwachambua.
Hoja 2: Elimu
(a)Si wote wana elimu ya kidato cha sita. Hapa siongelei mambo ya kufaulu au kushindwa. Kuendana na record kutoka source nilizotaja hapo mwanzo ni kwamba Freeman Mbowe ana Stashahada ya Elimu. Mpaka sasa hivi sijafanikiwa kupata majibu kamili kutoka NECTA kama Mbowe alisomea hiyo stashahada baada ya Form Four au Form six, kwani wale wa miaka ya nyuma mtakumbuka kwenda kusomea ualimu uliweza kufanya baada ya kidato cha nne au cha sita. Pia kwa sasa siwezi kutaja shule na chuo alichosomea kwani sijathibitisha kutoka kwa mamla husika au shule.
Nadhani Mbowe mwenyewe ndiye anaweza kuondoa utata huu wakati tunasubiri NECTA watumwagie vitu.
b) Huwezi kulinganisha uelewa wa Mbowe na Chifupa, hata mtu mwenye akili makini hawezi kumlinganisha mtu aliyewahi kuajiriwa na Bank na mtu ambaye hakuweza kuajiri na vyombo vya Uandishi wa habari pamoja na Diploma yake uandishi wa habari (sijui kutoka chuo gani). Ijapokuwa ni fani tofauti lakini ukijaribu kulinganisha sidhani kuna mlinganyo.
c) Kuhusu mbowe kusomea shahada mbili kutoka vyuo tofauti hilo siyo swala geni hata kidogo. Usilinganishe Tanzania ambako mtu huwezi kufanya shada mbili kutoka vyuo tofauti, mfano Open University na Mlimani. Binafsi nikiwa nafanya shahada yangu nje, nilikuwa nafanya vyuo viwili tofauti katika miji tofauti, kuna kitu kinaitwa "interdisciplinary studies". hapa vyuo vina makubaliano na vyuo vingine ili kusimamia program ambazo hazipo chuoni kwao, lakini ni sehemu ya degree ya mwanafunzi. mfano mimi nilipata degree kutoka UK na Canada wakati muda wote nilikuwa kwenye chuo kimoja isipokuwa mara chache kama kwenye defense ya thesis.
d) Pia kumbuka Mbowe hasomi program za kawaida ambazo mimi na wewe tunaweza kusoma, tumeambiwa program zimetengenzwa mahsusi kwa ajili yake. Kwa hiyo course load inaweza kuwa tofauti kabisa na course work ya wanafunzi wa kawaida.
d)Kuhusu kutajwa Hull tu nadhani, kwenye gazeti habari ilisema rpogram moja imetengenezwa kwa kushirikisha vyuo vya Uingereza, japani na Marekani, haikusema kuwa atasomea kwenye vyuo vitatu. Naomba mwenye hile habari kwenye archieve zake aiweke tena hapa.
>>Nadhani Mbowe pia anaweza kujitokeza kuclarify mambo zaidi
e)Ndugu yangu nani alikuambia elimu inategema umri. Nyerere (rip) aliwahi kusema elimu haina mwisho wakati anaanzisha Elimu ya Watu wazima. Kama watu wangefuata umri kwenda shule basi tusingekuwa na maprofesa kwani hamna mtu anayepata huo uprofesa kwa sababu ana umri mdogo bali wanazotea bila kujali alianza akiwa na mwaka mmoja au hamsini.
Pia mtu mwenye majukumu ya kisiasa kama mbowe au kiongozi mwingine hawezi kufuata syllabus ya kawaida, pita dunia nzima na utaona huu ukweli.
Yaani wewe badala ya kumshauri Chifupa hata angalau ajiunge na open University tena wamtengenezee program maalum kwa ajili yake (kuenddana na habari za kimtandao hana sifa za kujiunga na University kama kweli alipata Division 0 kidato cha sita).
3. Siasa
Umesema
(b) Hakuna loloote kubwa katika miaka mitano ya ubunge
wa Mbowe.
Ndugu yangu basi sasa unanipa wasiwasi hata kuamini kama unafahamu unachosema. Hebu jaribu tu kupitia hansard za bunge halafu urudie kusoma hoja yako hapo juu. Angalia maswali na hoja zake akiwa bungeni, kuanzia mgawanyo wa madaraka, pesa za Serikali, ujenzi na matumizi mabaya fedha.
Pili, nadhani upo bongo, naomba tu ufanye trip angalau ya siku moja tu kutembelea jimbo la hai halafu uone ndani ya miaka mitano alifanya nini kuanzia maswala ya maji, miundo mbinu, viwanja. jaribu kufikiria kwa nini Serikali iliamua kugawa jimbo la hai mara mbili, hii ilikuwa kudhoofisha upinzani kwani walidhani Mbowe angegombea lakini hakugombea. Watu wa hai walitokwa na machozi kwa kitendo chake cha kutokugombea tena.
Ndugu yangu hapa ni sawa na mtu kusema Wibroad Slaa hajaleta maendeleo Karatu.
(c) Chifupa kaingia siasa kwa initiatives zake. Mbowe kavutwa kurithi kiti cha Mkwewe.
Holy cow: inaoneka hujui historia ya siasi Tanzania au unakataa kukubali jambo usilolijua. kwa upande wa Chifupa sijui nianzie wapi. Lakini la Mbowe kwa kweli hufahamu historia yake. Mbowe siasa hakuanza leo, tizama historia kuanzia babake na ikiwezekana waulize wanaomfahamu wakuambie. Naomba nikuulize hivi Mtei kaachia uongozi wa Chadema lini na Mbowe kachukua lini, je enzi ya mtei kuna mtu alikuwa anamfahamu Mbowe. hata kwenye uchagzui wao mkuu hamna aliyetarajia angechukua uenyekiti wa chama kwani kulikuwepo na wagombea wengine na kama nakumbuka vizuri aliwapita wenzake kwa kura chache sana
Kuhusu Helikopta:
Pitia ripoti ya matumizi ya Uchaguzi wa chadema.
Tatizo lako kubwa na kwamba unatumia habari ya kwenye Guardian 08/12/2005 aliyotoa David Mgasi na Lucy Mdemu baada ya kuhama Chadema na kuhamia CCM. Walisema CHADEMA walipewa bilioni tatu na Conservative Party ya Uingereza lakini walipoambiwa watoe vielelezo walisema email haifanyi kazi.
Ijapokuwa sijui gharama halisi ya helikopta, ninachoweza kusema ni kwamba gharama kubwa zililipiwa na Mbowe mwenyewe kutoka kwenye michango aliyopewa na marafiki siyo kwa ajili ya chama bali kwa ajili yake binafsi, kama baadhi yetu tulivyomchangia Mnyika. Chadema tofauti na CCM kwenye Uchaguzi uliopita hatukuwa na ruzuku kubwa kama CCM, ndiyo maana uliona wagombea wakigharamia baadhi ya mambo peke yako kama kuweka mafuta kwenye magari yao baada ya kupewa magari na chama.
Hivi leo hii ni nani anaweza kutuambia zile dola milioni ishirini alizopewa kikwete na Iran (source BBC) zilitumikaje kuwasaidia wagombea wengine mnaweza kutuambia. Tutenganishe misaada au michango binafsi na ili ya chama.
naomba niishie hapa kwa leo.
Hoja 1: Public CV
Website ya Bunge la Jamhuri ya Muungano, ni sehemu ya mwisho kabisa kutafuta wasifu wa wabunge kwani kuna historia ya siku nyingi kuhusu ukweli wa record zilizopo. Ukitaka kuona hili basi jaribu kuangalia CV ya Mbunge mwingine ye yote halafu ulinganishe na ukweli halisi. Kwa harakaharaka unaweza kuanzia na wabunge wenye majina makubwa hapa Bongo na hata viongozi wa vyama.
kama unataka kuona CV halisi na timilifu basi nenda tume ya Uchaguzi utapewa kama una sababu zitakazowaridhisha. Miaka ya nyuma niliwahi kuwasiliana na wanaosimamia hiyo website Datavision kuhusu info za aliyekuwa mbunge wangu kwani yeye binafsi alipinga kuwa na shahada ya Kilimo iliyokuwa imeonesha kwenye website infact alikuwa mafunzo ya miezi mitatu ya bwana shamba Uholanzi, lakini wakasema hizo habari walipewa na wafanyakazi wa bunge.
Mfano: hiyo CV uliyotuletea inasema High School bila kusema jina la Shule, ukiendelea kusoma nyingine utaona watu wamepewa Shahada kibao bila kusema wamepata wapi na mwaka gani.
Kwa hilo tu linatosha kusema, website ya Bunge letu siyo chanzo kizuri cha habari, na kuna makosa mengi mno kiasi kwamba tunaweza kusema ni vigumu kutumia cv za hawa wahusika kuwachambua.
Hoja 2: Elimu
(a)Si wote wana elimu ya kidato cha sita. Hapa siongelei mambo ya kufaulu au kushindwa. Kuendana na record kutoka source nilizotaja hapo mwanzo ni kwamba Freeman Mbowe ana Stashahada ya Elimu. Mpaka sasa hivi sijafanikiwa kupata majibu kamili kutoka NECTA kama Mbowe alisomea hiyo stashahada baada ya Form Four au Form six, kwani wale wa miaka ya nyuma mtakumbuka kwenda kusomea ualimu uliweza kufanya baada ya kidato cha nne au cha sita. Pia kwa sasa siwezi kutaja shule na chuo alichosomea kwani sijathibitisha kutoka kwa mamla husika au shule.
Nadhani Mbowe mwenyewe ndiye anaweza kuondoa utata huu wakati tunasubiri NECTA watumwagie vitu.
b) Huwezi kulinganisha uelewa wa Mbowe na Chifupa, hata mtu mwenye akili makini hawezi kumlinganisha mtu aliyewahi kuajiriwa na Bank na mtu ambaye hakuweza kuajiri na vyombo vya Uandishi wa habari pamoja na Diploma yake uandishi wa habari (sijui kutoka chuo gani). Ijapokuwa ni fani tofauti lakini ukijaribu kulinganisha sidhani kuna mlinganyo.
c) Kuhusu mbowe kusomea shahada mbili kutoka vyuo tofauti hilo siyo swala geni hata kidogo. Usilinganishe Tanzania ambako mtu huwezi kufanya shada mbili kutoka vyuo tofauti, mfano Open University na Mlimani. Binafsi nikiwa nafanya shahada yangu nje, nilikuwa nafanya vyuo viwili tofauti katika miji tofauti, kuna kitu kinaitwa "interdisciplinary studies". hapa vyuo vina makubaliano na vyuo vingine ili kusimamia program ambazo hazipo chuoni kwao, lakini ni sehemu ya degree ya mwanafunzi. mfano mimi nilipata degree kutoka UK na Canada wakati muda wote nilikuwa kwenye chuo kimoja isipokuwa mara chache kama kwenye defense ya thesis.
d) Pia kumbuka Mbowe hasomi program za kawaida ambazo mimi na wewe tunaweza kusoma, tumeambiwa program zimetengenzwa mahsusi kwa ajili yake. Kwa hiyo course load inaweza kuwa tofauti kabisa na course work ya wanafunzi wa kawaida.
d)Kuhusu kutajwa Hull tu nadhani, kwenye gazeti habari ilisema rpogram moja imetengenezwa kwa kushirikisha vyuo vya Uingereza, japani na Marekani, haikusema kuwa atasomea kwenye vyuo vitatu. Naomba mwenye hile habari kwenye archieve zake aiweke tena hapa.
>>Nadhani Mbowe pia anaweza kujitokeza kuclarify mambo zaidi
e)Ndugu yangu nani alikuambia elimu inategema umri. Nyerere (rip) aliwahi kusema elimu haina mwisho wakati anaanzisha Elimu ya Watu wazima. Kama watu wangefuata umri kwenda shule basi tusingekuwa na maprofesa kwani hamna mtu anayepata huo uprofesa kwa sababu ana umri mdogo bali wanazotea bila kujali alianza akiwa na mwaka mmoja au hamsini.
Pia mtu mwenye majukumu ya kisiasa kama mbowe au kiongozi mwingine hawezi kufuata syllabus ya kawaida, pita dunia nzima na utaona huu ukweli.
Yaani wewe badala ya kumshauri Chifupa hata angalau ajiunge na open University tena wamtengenezee program maalum kwa ajili yake (kuenddana na habari za kimtandao hana sifa za kujiunga na University kama kweli alipata Division 0 kidato cha sita).
3. Siasa
Umesema
(b) Hakuna loloote kubwa katika miaka mitano ya ubunge
wa Mbowe.
Ndugu yangu basi sasa unanipa wasiwasi hata kuamini kama unafahamu unachosema. Hebu jaribu tu kupitia hansard za bunge halafu urudie kusoma hoja yako hapo juu. Angalia maswali na hoja zake akiwa bungeni, kuanzia mgawanyo wa madaraka, pesa za Serikali, ujenzi na matumizi mabaya fedha.
Pili, nadhani upo bongo, naomba tu ufanye trip angalau ya siku moja tu kutembelea jimbo la hai halafu uone ndani ya miaka mitano alifanya nini kuanzia maswala ya maji, miundo mbinu, viwanja. jaribu kufikiria kwa nini Serikali iliamua kugawa jimbo la hai mara mbili, hii ilikuwa kudhoofisha upinzani kwani walidhani Mbowe angegombea lakini hakugombea. Watu wa hai walitokwa na machozi kwa kitendo chake cha kutokugombea tena.
Ndugu yangu hapa ni sawa na mtu kusema Wibroad Slaa hajaleta maendeleo Karatu.
(c) Chifupa kaingia siasa kwa initiatives zake. Mbowe kavutwa kurithi kiti cha Mkwewe.
Holy cow: inaoneka hujui historia ya siasi Tanzania au unakataa kukubali jambo usilolijua. kwa upande wa Chifupa sijui nianzie wapi. Lakini la Mbowe kwa kweli hufahamu historia yake. Mbowe siasa hakuanza leo, tizama historia kuanzia babake na ikiwezekana waulize wanaomfahamu wakuambie. Naomba nikuulize hivi Mtei kaachia uongozi wa Chadema lini na Mbowe kachukua lini, je enzi ya mtei kuna mtu alikuwa anamfahamu Mbowe. hata kwenye uchagzui wao mkuu hamna aliyetarajia angechukua uenyekiti wa chama kwani kulikuwepo na wagombea wengine na kama nakumbuka vizuri aliwapita wenzake kwa kura chache sana
Kuhusu Helikopta:
Pitia ripoti ya matumizi ya Uchaguzi wa chadema.
Tatizo lako kubwa na kwamba unatumia habari ya kwenye Guardian 08/12/2005 aliyotoa David Mgasi na Lucy Mdemu baada ya kuhama Chadema na kuhamia CCM. Walisema CHADEMA walipewa bilioni tatu na Conservative Party ya Uingereza lakini walipoambiwa watoe vielelezo walisema email haifanyi kazi.
Ijapokuwa sijui gharama halisi ya helikopta, ninachoweza kusema ni kwamba gharama kubwa zililipiwa na Mbowe mwenyewe kutoka kwenye michango aliyopewa na marafiki siyo kwa ajili ya chama bali kwa ajili yake binafsi, kama baadhi yetu tulivyomchangia Mnyika. Chadema tofauti na CCM kwenye Uchaguzi uliopita hatukuwa na ruzuku kubwa kama CCM, ndiyo maana uliona wagombea wakigharamia baadhi ya mambo peke yako kama kuweka mafuta kwenye magari yao baada ya kupewa magari na chama.
Hivi leo hii ni nani anaweza kutuambia zile dola milioni ishirini alizopewa kikwete na Iran (source BBC) zilitumikaje kuwasaidia wagombea wengine mnaweza kutuambia. Tutenganishe misaada au michango binafsi na ili ya chama.
naomba niishie hapa kwa leo.