Mbowe na tafakuri zake...

Mbowe na tafakuri zake...

Wataalamu wa Logic tusaidiane kulitafakari hili.


Unajua mtu ukigubikwa na chuki au ubinafsi wa kupindukia ni vigumu kuona mazuri ya kile unachokichukia, hata yakiwa wazi. Sentence yako Mugongo inaonyesha hawa wawili ni complementaries.....fallacy(unless evidence is provided).

Mzee Es
Heshima yako mkuu. Mugongo ni mtoa hoja mwenye akili sana......ila lengo lake linaonekana lina kasoro....na hapo ndipo unapoonekana udhaifu wa akili yake(unbalanced). Mimi naamini kabisa wewe mzee Es waweza kumrekebisha ili aweke vitu constructively; maana anakukubali. Labda unapenda vitu vyake kwa sababu anaisaidia CCM (ha...ha...ha).
Mimi binafsi nilishamshambulia kwa matusi; na wala sisikitiki kwa hilo. He will learn slowly.
 
Nimewasikia wakuu, ninasema kwamba cha muhimu hapa ni kuheshimiana, matusi na kejeli, havitusaidii kitu, zaidi ya kuwafukuza wana-forum muhimu. Today I regret, kwamba tumepoteza wana-forum wengi imara kwa sababu ya matusi na lugha mbovu,

Watu kama Tafit, walikuwa ni moja ya dhaahabu ya hii forum, Kulikoni, Flemming, Msemakweli, Mafuti, Sizzla, Babu Ubwete, na wengineo ambao walikuwa imara na wasiotaka mchezo na ishu, sasa ungetegemea kuwa tumejifunza, NO! here wa are attacking the man, kwa sababu hatutaki mawazo yake, lakini serikali ikiyakemea magazeti ya Tanzania Daima, up in arms we are, OOH serikali haifai! Uhuru wa speech imekuwaje? Here we are doing exactly, tusichotaka kutoka kwa serikali, ndio maana ninasema viongozi wetu ni wasaniii, lakini sio zaidi ya sisi wananchi.

Huyu mtu Mugongox2, amekosa nini? angalau Mzee Yebox2 amemjibu kwa heshima, lakini wengine sielewi yaani matusi na kejeli tuuuu, ameuliza uwezo wa Freeman kiuongozi, kitu ambacho kinafanyika hapa kila siku kwa viongozi wa CCM, na upinzani pia, sasa matusi ya nini? Kitu gani mnachokificha na kukilinda kuhusu Freeman kwamba akiguswa tuu, inakuwa matusi, vitisho, na kwamba sisi wengine wote tuna wivu, lakini the fun thing ni kwamba hizi kejeli huwa hazi-apply kwenye upande wenu, it is kind of sad kwa mtu yoyote mwenye akili timamu, akiingia hapa na our behavior!

I mean muacheni kijana aweke vitu vyake, hoja hujibiwa kwa hoja wazee, na again ninampa kudos, kijana Mugongox2, unajua ni kijana mdogo sana, endleea na kuweka vitu vyako usiwe na wasi maana kelel za mlango huwa haizuiii mtu kulala ndani, I mean Mzee Invicible, heshima mbele mkuu, lakini mimi ninaheshimu mawazo ya mtu yoyote hapa bila ya kujali kama ni CCM, ni jana tu nimempongeza Mzee Ngurumo, kwa kuiweka serikali sawa katika article yake moja niliikiuta kwenye gazeti la bongo, on uhuru wa speech, inayowaita viongozi wetu wakuu wa CCM, Boys 11 Men, I mean perfect article, ninaheshimu sana msimamo, na ndio maana ninamheshimu huyu kijana maana msimamo wake ni strong na hayumbi, kuna watu kama Mkandara na Mwanasiasa( sometimes), ambao nao pia huwa hawayumbi na hasa Bob, kuna DR.WHO, na wengine wengi humu, lakini tunaenda wapi na hii tabia, ambayo inatufanya tupoteze wajumbe kila siku?

Mzee Mugongo keep it up, the good works, na wana-forum wengine pia tuendelee kukata ishu kiroho mbaya, hakuna kulala hapa!

Wazee tukate ishu tuache usaniii!
 
This is my earlier posting:

Kuna mambo mawili ya msingi:

1. Ngurumo ni mwajiriwa wa Mama Mbowe na mtoto wa Mbowe (Gazeti la Tanzania Daima, linamilikuwa na kampuni ya Free Media, ambayo wakurugenzi wake ni mke na mtoto wa Freeman Mbowe)

2. Ngurumo anasomeshwa na "mwajiri" wake huko Uingereza;

3. Ngurumo alishiriki kikamilifu kwenye kampeni ya Urais wa Mbowe;

Conclusion: Huwezi kumtaja Ngurumo bila kumtaja Mbowe and vice versa. Kwahiyo, Bwana Ngurumo you are going to have to deal with it. Acha wadau tuendeleze makamuzi.

This is Ngurumo's message "quoting" my posting:

Quote:
Originally Posted by mugongo mugongo
Kuna mambo mawili ya msingi:

Conclusion: Huwezi kumtaja Ngurumo bila kumtaja Mbowe and vice versa...
Wataalamu wa Logic tusaidiane kulitafakari hili
.

Unajua mtu kama Ngurumo, ambaye distortions is part of his life, sometimes anakosa soni kabisa. Of course, a message iliyakatwa kipande is illogical! Even Mbowe would tell you that (without you telling him, of course)

Mzee ES,

Tuko pamoja! Cha msingi ni kwamba hypocrisy yao sasa inaonekana wazi. Demokrasia inaanzia pale unapovumilia mawazo tofauti na ya kwako. Hawa jamaa nawajua vizuri na nime-reserve vitu vizito zaidi kadri mijadala unavyoenda. La msingi ni kuendelea kuheshimiana. Faraja yangu ni kwamba nimewachokoza panapouma: ukweli.
 
This is my earlier posting:



This is Ngurumo's message "quoting" my posting:



Unajua mtu kama Ngurumo, ambaye distortions is part of his life, sometimes anakosa soni kabisa. Of course, a message iliyakatwa kipande is illogical! Even Mbowe would tell you that (without you telling him, of course)

Mzee ES,

Tuko pamoja! Cha msingi ni kwamba hypocrisy yao sasa inaonekana wazi. Demokrasia inaanzia pale unapovumilia mawazo tofauti na ya kwako. Hawa jamaa nawajua vizuri na nime-reserve vitu vizito zaidi kadri mijadala unavyoenda. La msingi ni kuendelea kuheshimiana. Faraja yangu ni kwamba nimewachokoza panapouma: ukweli.

Ha....ha....haaa....Someone who is not somebody anyway feels the nerves!
 
Mbowe: Uchumi wetu wapaa kwenda kuzimu
Zitto Naibu Katibu Mkuu Chadema

na Tamali Vullu

MWENYEKITI wa Taifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, ameeleza kushangazwa kwake na kauli ya Waziri Mkuu, Edward Lowassa, ya hivi karibuni kuhusu mwenendo wa uchumi hapa nchini.
Mbowe aliyekuwa akifungua kikao cha siku mbili cha Kamati Kuu ya Chadema jijini Dar es Salaam jana, alisema hali ya uchumi imeendelea kuwa mbaya kinyume cha maneno hayo ya Lowassa.

Akitoa mfano alisema, makali ya kodi zilizoongezwa katika bajeti ya mwaka huu kwa wananchi ni ushahidi wa namna mwelekeo wa uchumi unavyozidi kuwakandamiza wananchi wa kawaida.

“Waziri Mkuu anasema uchumi wa nchi unapaa, sisi tunasema hata kama unapaa, basi unapaa kuzimu. Bajeti ya mwaka huu ni maumivu makubwa kwa Watanzania walio wengi. Kama mtu alikuwa mgonjwa, sasa atakuwa mahututi. Bajeti haina huruma, haithamini Watanzania, bali inathamini matakwa ya viongozi.

“Serikali ya Rais Kikwete inalazimika kuongeza kodi za bidhaa mbalimbali, ili kufikia malengo kutokana na ahadi nyingi walizotoa wakati wa kampeni,” alisema Mbowe.

Alisema pamoja na bajeti hiyo kuwa mwiba kwa Watanzania walio wengi, Waziri Mkuu na Waziri wa Fedha, Zakia Meghji, wamekuwa wakiitetea mpaka kufikia hatua ya kuwapuuza watu waliokuwa wakiikosoa, wakiwemo baadhi ya wabunge na waandishi wa habari.

Hata hivyo, alisema baada ya mwezi mmoja, bei ya mafuta ilipanda tofauti na alivyoahidi Waziri Meghji kuwa mafuta ya dizeli na petroli hayatapanda bei.

“Leo mwezi mmoja umepita, nilifanya ziara katika mikoa mbalimbali nchini, nimeshuhudua jinsi bei ya mafuta ilivyopanda… Serikali ya Jakaya Kikwete inacheza na maisha ya Watanzania, gharama za maisha zimepanda na serikali haina meno ya kudhibiti bei ya mafuta,” alisema Mbowe.

Mbali ya hilo, Mbowe alisema ni jambo lisiloingia akilini kuona serikali ikipandisha kima cha chini cha mshahara wa watumishi wake kwa sh 9,000, kiwango ambacho ni kidogo kuliko yalivyo mahitaji halisi ya kimaisha na serikali hiyo hiyo ikadai eti uchumi unapaa.

Mbali ya hayo, Mbowe alisema katika kikao hicho cha kamati kuu, wanatarajia kujadili hali ya siasa nchini na leo mchana tamko rasmi linatarajiwa kutolewa kuhusu mkutano huo.

Alisema katika kikao hicho, wajumbe watajadili utendaji wa uongozi wa Rais Kikwete katika kipindi cha miezi sita iliyopita na kisha kutoa tamko kuhusu suala hilo leo.

Hata hivyo, Mbowe alibainisha kuwa, uongozi wa Rais Kikwete unalipeleka taifa pabaya na inashangaza kuona kuwa Waziri Mkuu, anatoa kauli akisema kuwa uchumi wa nchi unapaa.

Mwenyekiti huyo alisema pia kikao hicho kitajadili mwenendo wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, jinsi linavyotumika kuzima haki za Watanzania.

Alisema wabunge wa kambi ya upinzani wamekuwa wakijitahidi kutetea wananchi kwa kutoa ushauri kwa serikali kuhusu masuala mbalimbali kwa maslahi ya Watanzania.

“Wapinzani hawako kwa ajili ya kuibomoa serikali, lakini wameshuhudia jinsi wabunge wa chama tawala wanavyokuwa wakiingiza ushabiki wa kisiasa katika kuzima masuala ya msingi.

“…Tunawaambia Watanzania haya ndiyo matunda ya kuchagua wabunge wengi wa chama kimoja,” alisema Mbowe.

Alisema sambamba na masuala hayo, pia watajadili suala la ukaguzi wa hesabu za Benki ya Tanzania (BoT) ya mwaka 2005/06.

Habari ambazo gazeti hili lilizipata kutoka ndani ya kikao hicho zinaeleza kuwa, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zubeir Zitto, aliteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho kujaza nafasi iliyoachwa wazi na Shaibu Akwilombe aliyetangaza kuachia nafasi hiyo hivi karibuni.

Taarifa za uhakika kutoka ndani ya chama hicho zinaeleza kuwa, jina la Zitto, mmoja wa wabunge vijana machachari, lilipendekezwa na Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Lindi, Juma Lichonyo na likaungwa mkono na Mwenyekiti mstaafu wa chama hicho, Bob Makani.

Habari zaidi zinaeleza kuwa, Zitto aliungwa mkono na wajumbe wote 28 waliopiga kura.
 
Kimepita kitambo Mwenyekiti wa Chama cha Kidemokrasia (Chadema)hajasikika kwa makala zake zile maarufu kama "Tafakuri ya Mbowe".

JF ikiwa ni jungu kuu lisilo kosa ukoko nawasilisha rasmi kwenu wadau kuulizia kulikoni Mwenyekiti mbona kimya?
 
Kimepita kitambo Mwenyekiti wa Chama cha Kidemokrasia (Chadema)hajasikika kwa makala zake zile maarufu kama "Tafakuri ya Mbowe".

JF ikiwa ni jungu kuu lisilo kosa ukoko nawasilisha rasmi kwenu wadau kuulizia kulikoni Mwenyekiti mbona kimya?


Sasa hivi tunatafakuri wenyewe sasa hii mikataba ma mauza uza mengine, ni kama mwalimu anatoa introduction ya somo kisha mnaendelea kujifunza wenyewe.....LOL

Lakini pia ni muhimu kutambua kuwa kila jambo an wakati wake, ule ulikuwa wakati wake na sasa tuna mambo mengine mengi tu na nadhani hata yeye pia anayo mengi kichwani mwake, ndo maana kuna delegeation ya mambo mengine, sidhani kama alimaanisha kuandika tafakuri kwa muda wote...sijui muda gani, was there a time limit?
 
Mbowe yuko busy, kadandia boti la Dr. Slaa na Zitto, wasije wakamzidi kete.

Wapenzi wake wanaami Mbowe naye eti anaweza kuwa rais. I ngelikuwa huku majuu vijana wangeshaanza kuchangamkia post yake, lakini kwa nyumbani haiwezekani maana bila resources sio rahisi kuwang'oa wazee hata kama wanajikongoja.
 
They work as a team, curretly they have put Zitto and Dr. Slaa in front!!!

Don't you know that?
 
Kuna taarifa alikuwa anaandikiwa sasa sijui mwandishi wake kagoma au vipi.

Just being curious....
 
Kuna taarifa alikuwa anaandikiwa sasa sijui mwandishi wake kagoma au vipi.

Just being curious....
I knew you were up to something, LOL, lakini ni vigumu kuamini, maadamu umesikia, hata JK juzi si nasikia huko AR kachelewa kuanza ratiba vile hotuba ilikuwa haijakamilika kuandikwa, unakumbuka mkuu? Kwa hiyo hapo hakuna jipya hata kama alikuwa anaandikiwa,
 
I knew you were up to something, LOL, lakini ni vigumu kuamini, maadamu umesikia, hata JK juzi si nasikia huko AR kachelewa kuanza ratiba vile hotuba ilikuwa haijakamilika kuandikwa, unakumbuka mkuu? Kwa hiyo hapo hakuna jipya hata kama alikuwa anaandikiwa,

Hey yamekuwa haya!
 
nakulilia,
una maana kile kinachoweza kuwa kinamla adui yako chaweza kuwa ndicho kinachomtafuna rafiki yako...
 
hata mie sijamsikia mbowe muda sasa, na zitto ! Mbowe upo wapi ? rudi JF tuchanganye maakuli hapa.
 
Masatu
JF Senior Expert Member Join Date: Mon Jan 2007
--------------------------------------------------------------------------------

Kuna taarifa alikuwa anaandikiwa sasa sijui mwandishi wake kagoma au vipi.


Mkuu Masatu,

Heshima mbele mkuu, hivi kweli huyu juu ni wewe au nimekosea mkuu, maana haingiii akilini kabisa kuwa ni wewe mkuu, kuna mtu ana-pass word yako nini?
 
Wakuu,

Hivi majina ya wale wasaidizi wa Mbowe waliopelekwa kusoma Hull
University kabla ye yeye, je kuna mtu anaweza kuyapeperusha hapa tena?

Hivi wao ni waandishi wa habari? Nataka kulinganisha na majina niliyoyaona sehemu.

Inabidi kupata the dataz za uhakika kabla ya kujenga hoja.
 
Wakuu,

Hivi majina ya wale wasaidizi wa Mbowe waliopelekwa kusoma Hull
University kabla ye yeye, je kuna mtu anaweza kuyapeperusha hapa tena?

Hivi wao ni waandishi wa habari? Nataka kulinganisha na majina niliyoyaona sehemu.

Inabidi kupata the dataz za uhakika kabla ya kujenga hoja.


Moja ni mwandishi wa habari tena ana blogu give me few minutes.
 
Back
Top Bottom