Ngurumo
Hivi hata kabla ya kuanza kujibu hoja humu ulianza kuwasaka wachangiaji wa hii JF ili uwafahamu maana yake ni nini hasa? Unaogopa kitu gani kusema bila kuwachunguza wachangiaji? Hii inaonyesha jinsi ulivyo filisika kimawazo i.e. unaangalia nani kasema nini badala ya hoja iliyotolewa. Inaonyesha jinsi ambavyo bado una safari ndefu katika masomo yako kama ni kweli na uelewa wako.
Unaongelea elimu, tulikuwa na Mkwawa, Kinjekitile, Mirambo, Chaburuma etc. waliweza kuongoza makabila tofauti na kutufikisha katika fani tofauti tofauti. Mfano Mkwawa aliweza kuwapiga Wajerumani na kuweza kuwakomesha katika vita yao ya kwanza, na walilifahamu hili, bila shaka uliona jinsi walivyojizatiti mara ya pili. Kuna kitu kinaitwa elimu dunia, sio lazima ukae darasani tu kuwa na elimu.
Vile vile hakuna sheria ya whistle blowers Tanzania unataka wale wanaoleta nyeti za viongozi (mfano wakubwa wao wa kazi) wawafahamu, you must be joking! Where is the freedom of speech? Una maanisha kama mtu hakusoma kutokana na definition yako asichangie? Mbona hao waliosoma ndio wametufikisha hapa! (PANAPONUKA) Sasa hiyo elimu ina maana gani kama kila siku mnaimba kwa kutegemea kura kwa wasiosoma lakini kwenye mawazo hamuwataki.
Tunafahamu waandishi wengi wanatumiwa na wale wanaowawekea kitoweo mezani, huwezi kukata mkono unaokulisha hivyo huandika yale ambayo hayako mioyoni mwao bali ya vikaragosi wao kwa hiyo hubadilika na kuwa vibaraka.
Ngurumo kukata mzizi wa fitna wapo ambao watafungua forum kwa wale wanaopenda kutumia majina halisi n.k. ni uchaguzi. Usije hapa na kutuletea longolongo ambalo halina maslahi kwa Taifa. Kama umekwazwa jibu hoja na weka ukweli, waswahili husema kwenye uongo ukweli hujitenga.
Ngugu yangu DUA,
Mbona hoja yangu ilikuwa wazi?
Nimesoma maandishi yako na nimegundua kwamba:
Unaogopa kufahamika na unadhani wanaojitahidi kukufahamu wamefilisika. Binafsi nimejieleza kwamba I am curious. kama unadhani curiosity hiyo haipaswi kunifikisha katika kutaka kujua watu ninaowasiliana nao, basi fikiri upya. Lakini una haki ya kuwa na maoni yako. Sitayaingilia.
Nionavyo mimi, na ninavyoelewa, ukiwafahamu watu unaojadiliana nao mjadala unanoga. Kule kuwajua kuna-
shape hata lugha unayotumia. Unachagua maneno yanayolingana na ujumbe unaokusudia kufikisha, unaoshahabiana na upeo wa
calibre ya wanaokusikiliza au kukusoma. Hii ni sehemu ya etiquette za mawasiliano. Kama nimekosea kukufahamu, ndugu yangu niwie radhi. Maana naona nimegusa nyongo yako! Pole! Ila sasa napata shida. Nitafanyaje ili nisikufahamu baada ya kuwa nimekufahamu? Changamoto hiyo!
Hata hivyo, nimegundua kwamba wewe nami tunakubaliana katika mambo mengi ya msingi uliyojadili kuhusu identity, elimu, na waandishi kutumiwa. Tunachotofautiana ni approach.
Kwa mfano, mimi sikuubeza usomi wa mtu yeyote. Nilichosisitiza ni kwamba kuna watu katika forum hii wanadhani wamesoma sana, wana upeo kuliko wenzao, kiasi cha kubeza wengine. Nikahoji kwamba hata mimi nikiwachunguza hao wanaobeza wenzao, sioni usomi katika maandishi yao. Usiwe na shaka. Naelewa vema tofauti kati ya elimu na usomi; ujuzi na vyeti. Huu pia ni mjadala mwingine unaoweza kujitegemea. Lakini kwa sababu nimeshakufahamu, usihofu; kama kuna hoja tutajadiliana tu. Hatuna sababu ya kurushiana maneno. Tujadiliane.
Nimefarijika na kauli mbiu yako ya
Dua la Kuku Halimpati Mwewe, ambayo ni sehemu ya jina lako la kalamu kwenye forum hapa. Wakati ningependa ukumbuke hoja ya msingi iliyonifanya niingie kwenye forum hii, si vibaya nikukuhakikishia kwamba sitakasirika kwa sababu ya ukali wa kauli zako. Hayo nakutana nayo sana sehemu nyingi. Binadamu hatufanani na hatulingani. Na kama wewe ni kuku, basi mimi ni mwewe! Nina hakika dua lako halitanipata!
Siku nyingine, Dua,
punguza hasira, jenga hoja kama unavyosisitiza.
Nimemsoma pia Mzee ES.
Amenishauri kwamba nikitukanwa nami nijibu kiroho mbaya! Namhakikishia kwamba sitajibu matusi bali hoja kama zitakuwapo, na kama zitakuwa zinahitaji kujadiliwa nami pia.
Kwamba kuna mambo mengi sisi watu wa
media tumeshindwa kuyafanya, nakubali. Yapo. Tunayajua. Na tunajitahidi kujikosoa. Usisahau kuwa nasi ni binadamu kama wewe na mwingine. Tunakosea, tena sana. Jambo muhimu ni kutambua kwamba tunakosea, tukayarekebisha na kusonga mbele tukiwa watu wapya, kuliko kuyang'ang'ania au kuyakana.
Kwamba ni jambo la kipuuzi mtu kuuma mkono unaomlisha (kama alivyodokeza Dua), kila mmoja wetu anajua. Na ndiyo maana tumekuwa tukielezana kuwa walioajiriwa na serikali kufanya kazi ya serikali waifanye kweli kweli, watumikie mikataba yao, maana tunawalipa mishahara na posho; na wasitulaumu tunapokata kuwaunga mkono au kuwasaidia. Wao wamo katika chombo chenye nguvu na mabavu; sisi wengine tutabaki kuwa midomo na masikio ya raia wanyonge wasio na kauli. Ila tunakumbusha kuwa katika kufanya hiyo, watofautishe maslahi ya umma na ya watawala. Na wakizingatia ethics za kazi yao, hakuna litakaloharibika.
Hata sasa kama unasoma habari za nyumbani nadhani umeona malumbano yanajitokeza katika media hizo hiyo. Ni harakati ambazo labda zinatusaidia kuliweka taifa letu katika ramani mpya ya utawala.
Pamoja na hayo yote, nadhani ujumbe uliokusudiwa umefika. Waliochukia approach yangu, poleni na samahani. Nadhani sasa mmeshaanza kutabasamu ili muweze kuenmdelea kujenga hoja ( au kukata issue kama anavyosema Mzee ES.) Kwa kuwa nanyi ni watu wazima kama mimi, nadhani mnaelewa. Ndio ukubwa wenyewe huo!