Mbowe apewe heshima yake anayostahili!!

Mbowe apewe heshima yake anayostahili!!

Shida ilianza kwa akina LEMA kusambaza taarifa nyingi za uongo na kumchafua MBOWE!!!

Ikiwa MBOWE ataongea ni TATIZO
Ikiwa MBOWE atakaa kimya ni TATIZO

Sasa Bora ajikalie kimya.....
Padri Kitima au Askofu Mwamakula siyo wanasiasa wenye vyeo.

Mtu anatakiwa awe mwanasiasa au awe na cheo cha kisiasa kukemea maovu???
 
Ivi mwaka flan mkoa wa iringa ..wilaya ya kilolo kata ya ILOLE ukumbi wa bwana DUMA ulikuja kutoa semina pale ya chadema au warsha ni nan ali sponsor ile event maaana na mm nilikula wali ule ...samahan lkn bwana ALLEN
David Mfugwa alinialika na wanachama wenyewe ndiyo walifadhili pambano.

Tangu mwaka ule (2019) sijarudi tena Ilole!
 
Shida MBOWE kila atakachoongea watoto wa 2005 watamuona amepotoka, hivyo Bora aendelee kukaa kimya
Siasa za visasi havitaisaidia Chadema.Jana Katibu wa Chadema wa Mkoa wa Kilimanjaro Bazil Lema amesimamishwa eti kwa kuandaa mkutano wa wanachadema wanaotaka kuhama chama.
Kwa mujibu wa Lema kikao cha kumsimamisha kingefanywa na kamati ya maadili ya Kanda kwa mujibu wa katiba..Anadai hakuna kikao kilichofanyika na amearifiwa kwa barua tu bila kuitwa.Tuhuma ni kwamba kuna mtu aliripoti kwamba ameambiwa Bazil Lema anaandaa mkutano.
Akihojiwa na Moshi FM Bazil Lema amedai chama kimekuwa kinaendeshwa kwa matamko na sio Katiba.
 
Wanaomdharau Mbowe ukiwauliza Lissu alikuwa chama gani kipindi hicho, unaambulia matusi.
Wanachama wa CHADEMA wanahitaji kujua historia ya chama chako vizuri waache mihemko.
Yaani wamejaa hasira visasi na kuropoka kama mwenyekiti wao.Hawajui chochote zaidi ya kuzuia uchaguzi,mahakamani wameshindwa kufika ni kwenye uchaguzi watazuia.!! Eti waandamane siku ya uchaguzi kama mahakamani wanavunjwa miguu kwenye uchaguzi si ndio watavunjwa shingo.Haya mambo yalihitaji hekima
 
1. Alipopigwa risasi Lissu Mbowe alikuwa mstari wa mbele kuhakikisha kuwa hapelekwi Muhimbili.
2. Mbowe alikaa rumande na wakina Esther Matiko. Alipofungwa jela, alikataa kutoka mpaka wale wote waliofungwa nae walipotolewa jela kwa dhamana.
3. Alienda Mwanza kuungana na wenzake wakati anajua wazi kuwa atatiwa ndani na uwezekano wa kupigwa ulikuwepo.
4. Alikaa ndani kwa takriban miezi minane. Alipoachiwa alikubali mualiko wa Samia kwenda Ikulu, ambako chimbuko likawa mada ya maridhiano.
5. Kutokana na hayo maridhiano wanachama wa CDM waliokuwa nje waliweza kurudi, mikutano ya hadhara na zaidi ya yote mamia ya wanachama na wafuasi wa CDM waliweza kuachiwa kutoka rumande na jela.
6. Alipopigwa Lissu Mbeya, Mbowe alienda kuungana nae. Matokeo yakawa ya yeye kukamatwa na kurudishwa Dar.
7. Aliitisha maandamano ya kupinga mauaji na kupotea kwa watanzania ikiwa pamoja na wanachama wa Chadema. Lissu alizuiwa nyumbani kwake. Lema akakamatwa airport. Mnyika akajifungia kwa maista. Sijui Heche alikuwa wapi. Mbowe hakulala nyumbani siku ya maandamano kwa sababu alijua watamzuia kutoka. Akaibuka sehemu ya kuanzia maandamano akiwa yeye na binti yake. Mashujaa wafia Chadema hawakuonekana hata mtu mmoja.
8. Alitoa shilingi zaidi ya milioni 250 kufanikisha mkutano mkuu wa chama. Alihakikisha kuwa uchaguzi mkuu unakuwa wa haki na uwazi. Haku endorse mtu katika uchaguzi huo tofauti na mshindani wake ambae aliendorse watu kama aliyekuwa mgombea wa uenyekiti wa Bawacha.
9. Mara baada ya uchaguzi alimpongeza aliyeshinda akajiondokea.

Baada ya uchaguzi tumeshuhudia wale waliokuwa Team Lissu wakiendeleza mapambano dhidi ya Mbowe. Wanawake wa Bawacha walioenda kumsalimia baada ya uchaguzi walionyeshwa wazi wazi kuwa uongozi wa sasa hawakufurahia kitendo chao. Sigrada alimsifia Mbowe mbele ya Lissu, matokeo yakawa ni kichapo. Lissu akamsimanga Aida hadharani.
Yote hayo bado mnataka Mbowe akajipendekeze kwa wakina Heche?

Wanacho sahau keyboard warriors ni kuwa Mbowe alijijengea heshima kubwa na kuna watu wengi hawafurahi wanapoona anavyodhalilishwa na kuvunjiwa heshima. Watu kama G55 ni lazima wanaumia wanapo shuhudia yote hayo. Lakini kila kitu kina mwisho wake.

Amandla...
Team Lisu hata uwaeleze mazuri ya Mbowe kwa kuweka speaker maskioni mwao hawawezi kukuelewe wamemezeshwa shetani wa ubishi.Hawaamini aliyejenga chama kwa sehemu kubwa ni Mbowe.Mbowe amejenga vijana na watu wengi kisiasa.Nileteeni mmoja tu ambae ametengenezwa na Lisu niwape zawadi.Zaidi ya hawa waropokaji aliotengeneza,na wako kwenye mitandao tu,wala mtaani huwaoni.
 
unajisumbua tu mkuu. BINAADAMU HAWANA SHUKURANI.

Suala la kutukanwa na kudhalilishwa Mbowe limenifanya nipoteze Imani na CHADEMA
Shukrani tunazo hata kwa sisimizi,hata kwa wanaotudhulumu huwa tunawashukuru kwa kila zuri wafanyalo na kuwalaumu ili wajirekebishe pale pasipo sawa.
 
i wameshindwa kufika ni kwenye uchaguzi watazuia.!! l
Kuzuia uchaguzi siyo hoja ya uongozi wa sasa ni hoja tangu mwaka 2023. Kila mwanachadema anatakiwa kuwaza njia gani sahihi ya kuzuia uchaguzi itumike!

No Reforms No Election!
 
Team Lisu hata uwaeleze mazuri ya Mbowe kwa kuweka speaker maskioni mwao hawawezi kukuelewe wamemezeshwa shetani wa ubishi.Hawaamini aliyejenga chama kwa sehemu kubwa ni Mbowe.Mbowe amejenga vijana na watu wengi kisiasa.Nileteeni mmoja tu ambae ametengenezwa na Lisu niwape zawadi.Zaidi ya hawa waropokaji aliotengeneza,na wako kwenye mitandao tu,wala mtaani huwaoni.
Ndio maana nawaita cult. Mpaka leo hawajaambiwa namna watakavyo hakikisha uchaguzi haufanyiki lakini wanataka kila mtu aimbe NRNE! Hilo swali hata mimi najiuliza. Hata katika fani yake hamna aliyejitokeza kusema kuwa Lissu amemjenga. Wakati huo huo watu kama Heche wanamshukuru Mbowe kwa kuwajenga na kuwafikisha walipo sasa. Watu wa ajabu sana.

Amandla...
 
Yapo mengi yamegundulika ya Mbowe kama yakiwekwa hadharani hata wanaomshabikia watamtema mate na yeye ameshajua kuwa yamejulikana ndiyo maana kwa sasa ana keep low profile ana aibu nyingi yakimwagwa atakimbia hata nchi hii.
 
Mbowe ni mjanjamjanja hivi. Angestahili heshima angekuwa wa kwanza kuwakemea wachumia tumbo kina Mrema. Kuwasapoti Ginga 55 kumemmaliza kabisa!
 
Yapo mengi yamegundulika ya Mbowe kama yakiwekwa hadharani hata wanaomshabikia watamtema mate na yeye ameshajua kuwa yamejulikana ndiyo maana kwa sasa ana keep low profile ana aibu nyingi yakimwagwa atakimbia hata nchi hii.

anahusishwa na vifo CHADEMA
 
Ndio maana nawaita cult. Mpaka leo hawajaambiwa namna watakavyo hakikisha uchaguzi haufanyiki lakini wanataka kila mtu aimbe NRNE! Hilo swali hata mimi najiuliza. Hata katika fani yake hamna aliyejitokeza kusema kuwa Lissu amemjenga. Wakati huo huo watu kama Heche wanamshukuru Mbowe kwa kuwajenga na kuwafikisha walipo sasa. Watu wa ajabu sana.

Amandla...
Ni mbinafsi na hajawahi kutengeneza yeyote zaidi ya kundi la kumtukana mtangulizi wake.Hapo umeongeza hata kwenye fani yake hamna.
 
Ndio maana nawaita cult. Mpaka leo hawajaambiwa namna watakavyo hakikisha uchaguzi haufanyiki lakini wanataka kila mtu aimbe NRNE! Hilo swali hata mimi najiuliza. Hata katika fani yake hamna aliyejitokeza kusema kuwa Lissu amemjenga. Wakati huo huo watu kama Heche wanamshukuru Mbowe kwa kuwajenga na kuwafikisha walipo sasa. Watu wa ajabu sana.

Amandla...
Una sound kama CCM.

Binafsi najua kabisa hawawezi kuzuia uchaguzi.

Lakini pamoja na kuwa hawana effect na ni harmless, unadhani kwanini Lissu anashitakiwa kwa uhaini na watu wanapigwa kila siku kwa kwenda mahakamani tu.

Lakini pia, kwanini ushiriki kitu ambacho unajua kabisa hutapata chochote.

Mlishiriki serikali za mitaa, mlipata nini??
 
Ni mbinafsi na hajawahi kutengeneza yeyote zaidi ya kundi la kumtukana mtangulizi wake.Hapo umeongeza hata kwenye fani yake hamna.
Hapa umemshambulia Lissu kibinafsi (Personal attack). Kutengeneza watu kukoje na wewe hebu toa mfano wa watu unaojua wewe kuwa walitengenezwa na walitengenezwaje?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom