Fundi Mchundo
Platinum Member
- Nov 9, 2007
- 12,893
- 11,373
Na mtu mwenye akili timamu atasusia mara ngapi kabla ya kutambua kuwa mwenzake hana nia ya kubadilisha Katiba? Hamtagombea mwaka 2029 kama hapatakuwa na reforms? Na mwaka 2030 kama bado hamna mabadiliko? Hivi mnaamini kuwa CCM wataona aibu kutangaza uchaguzi kwa sababu tu CDM wamesusa?Yaani unataka watu wauawe, wateswe, uchaguzi uchafuliwe mara ngapi ili uone umuhimu wa mabadiliko ya Sheria za uchaguzi na Katiba?
Kama mtu una akili timamu kipi kinakuzuia kutambua kuwa kuanzia mwaka 2019, 2020,2024 uchaguzi uliharibiwa na huo ndiyo utakuwa muendelezo Kwa uchaguzi wa mwaka 2025?
Ni akili za aina gani zinazomfanya mtu kusubiri afanyiwe kosa Kwa zaidi ya mara ya tatu ndipo apambanie haki au utu wake!?
Kwani miaka yote hii ambayo CDM wamekuwa wakigombea walikuwa hawapiganii haki na utu wao? Hamna kitu kinachomtisha bully kama kujua kuwa victim wake ataendelea kupambana nae hata amfanyie nini. Hakainde Hichilema aligombea mara 5 kabla ya kushinda mara ya sita. Alifanyiwa kila aina ya uonevu lakini hakukata tamaa. Nyinyi mara tatu ndio mnataka kufyata mkia. Congress party ya India ilitawala kwa miaka 30 baada ya uhuru wao lakini mwishowe wakatolewa kwenye utawala.
Kushindana na chama kilichotawala toka nchi ipate uhuru sio kazi rahisi. Inahitaji uvumilivu na kuto kata tamaa.
Inaonekana CDM imekata tamaa.
Amandla...
Amandla...