Lakini cha ajabu ni kuwa, sasa yuko kwenye harakati za chini kwa chini kuidhoofisha CHADEMA chini ya uongozi mpya wa Tundu Lissu na wenzake...
Ukimya wake ktk wakati huu ambapo chama unachodai kuwa alikijenga kwa jasho na damu, kinapitia ktk wakati mgumu wa mashambulizi kutoka pande zote; i.e CCM na serikalI yao pamoja na taasisi zake kama polisi, TISS, Msajili wa vyama vya siasa, mahakama na kutoka ndani ya chama chenyewe kwa waliokuwa chawa wake wakati wa uchaguzi wakisaidiwa na CCM kumtaka aendelee ni uthibitisho wa wazi sana kuwa, yuko kwenye harakati za kumdhoofisha mwenzake (Tundu Lissu) ionekane hawezi kuongoza chama kama alivyokaa yeye miaka 22 asijue kuwa isingekuwa kina Lissu hawahawa, asingekaa muda mrefu hivyo...
Mimi badala ya kumheshimu, nimemdharau kabisa na namuona kama mtu mwenye ego na ubinafsi. Na hii ni udhihirisho kuwa, alijenga chama ambacho yeye na baadhi wenzake walikigeuza kama mradi wa kisiasa kufanyia deal zao za kifedha kutoka kwa CCM na serikali yao...
Kuona kuwa kitega uchumi chao sasa kiko chini ya viongozi wengine tena waadilifu wasiojihusisha na bishara za kisiasa kwa CCM na wanausafisha uchafu waliouficha miaka mingi ndani ya chama, inawauma na kuibua vita mpya dhidi ya uongozi mpya kwa msaada wa waliokuwa wanafanya nao biashara ya kisiasa yaani CCM na serikali yao ovu...