BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,377
- 8,121
Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya itaanza kusikiliza maombi ya kupinga mkataba uwekezaji wa bandari kati ya Serikali ya Tanzania na Dubai kupitia Kampuni DP World baada ya kupokea majibu ya Serikali.
Katika maombi hayo ya kikatiba, waleta maombi wanaitaka Serikali kuieleza mahakama sababu za kile wanachodai kuwa ni kusaini mkataba pasipo ushirikishwaji wa wananchi.
Shauri hilo litaanza kusikilizwa Julai 20, 2023, ikiwa leo Jumatatu limefikishwa kwa mara ya kwanza mbele ya Jaji Mfawidhi wa mahakama hiyo, Dastan Ngunguru likiwasilishwa na mawakili wa utetezi, Boniface Mwabukusi na Philipo Mwakilima dhidi ya wateja wao wanne waliopeleka malalamiko hayo.
Waliopeleka malalamiko hayo ni Alphonce Lusako, Raphael Ngonde, Emmanuel Chengula na Frank Nyalusi.
Mwanasheria wa Serikali, Hangi Chang'a ameeleza mahakamani hapo kuwa walipokea nyaraka za shauri hilo Juni 26, 2023 na kupata siku 21 kulipitia na kujibu.
Amesema kuwa tangu Juni 26 mwaka huu shauri hilo lilipofikishwa mahakamani, walitakiwa kujibu ndani ya siku 21 ambapo kwa sasa zimesalia siku 17 watakuwa wamejibu kwa ajili ya hatua za kuanza kusikiliza kesi hiyo ili kutenda haki.
Wakili wa utetezi, Boniface Mwabukusi akishirikiana na Philipo Mwakilima wameitaka mahakama kuharakisha majibu ya maombi hayo ya kikatiba kwani tayari wamesajiri maombi madogo ya dharura na wanasubiri maelekezo ya mahakama hiyo.
Amesema kuwa kesi hiyo ni ya kikatiba ambayo wanaitaka Serikali kuieleza mahakama sababu za kile wanachodai kusaini mkataba pasipo ushirikishwaji wa wananchi na kusababisha sintofahamu kwa Watanzania wazalendo.
Awali, Jaji Mfawidhi wa mahakama hiyo, Dastan Ndunguru baada ya kusikiliza pande zote ameshauri upande Serikali kujibu maombi hayo kwa umakini mkubwa kwani kesi hiyo ni ya kikatiba na msingi ambayo itasikilizwa na majaji watatu.
Aidha Jaji Ndunguru ameahirisha kesi hiyo mpaka Julai 20, 2023 ambapo itaanza kusikilizwa mfululizo baada ya upande wa mashtaka kuwasilisha majibu ya maombi mbele ya mahakama hiyo.
MWANANCHI
Katika maombi hayo ya kikatiba, waleta maombi wanaitaka Serikali kuieleza mahakama sababu za kile wanachodai kuwa ni kusaini mkataba pasipo ushirikishwaji wa wananchi.
Shauri hilo litaanza kusikilizwa Julai 20, 2023, ikiwa leo Jumatatu limefikishwa kwa mara ya kwanza mbele ya Jaji Mfawidhi wa mahakama hiyo, Dastan Ngunguru likiwasilishwa na mawakili wa utetezi, Boniface Mwabukusi na Philipo Mwakilima dhidi ya wateja wao wanne waliopeleka malalamiko hayo.
Waliopeleka malalamiko hayo ni Alphonce Lusako, Raphael Ngonde, Emmanuel Chengula na Frank Nyalusi.
Mwanasheria wa Serikali, Hangi Chang'a ameeleza mahakamani hapo kuwa walipokea nyaraka za shauri hilo Juni 26, 2023 na kupata siku 21 kulipitia na kujibu.
Amesema kuwa tangu Juni 26 mwaka huu shauri hilo lilipofikishwa mahakamani, walitakiwa kujibu ndani ya siku 21 ambapo kwa sasa zimesalia siku 17 watakuwa wamejibu kwa ajili ya hatua za kuanza kusikiliza kesi hiyo ili kutenda haki.
Wakili wa utetezi, Boniface Mwabukusi akishirikiana na Philipo Mwakilima wameitaka mahakama kuharakisha majibu ya maombi hayo ya kikatiba kwani tayari wamesajiri maombi madogo ya dharura na wanasubiri maelekezo ya mahakama hiyo.
Amesema kuwa kesi hiyo ni ya kikatiba ambayo wanaitaka Serikali kuieleza mahakama sababu za kile wanachodai kusaini mkataba pasipo ushirikishwaji wa wananchi na kusababisha sintofahamu kwa Watanzania wazalendo.
Awali, Jaji Mfawidhi wa mahakama hiyo, Dastan Ndunguru baada ya kusikiliza pande zote ameshauri upande Serikali kujibu maombi hayo kwa umakini mkubwa kwani kesi hiyo ni ya kikatiba na msingi ambayo itasikilizwa na majaji watatu.
Aidha Jaji Ndunguru ameahirisha kesi hiyo mpaka Julai 20, 2023 ambapo itaanza kusikilizwa mfululizo baada ya upande wa mashtaka kuwasilisha majibu ya maombi mbele ya mahakama hiyo.
MWANANCHI