Matokeo ya Uchaguzi mdogo Igunga (matokeo ya awali)

Matokeo ya Uchaguzi mdogo Igunga (matokeo ya awali)

Status
Not open for further replies.
Taarifa ya Novatusi Makunga juu ya ile taarifa ya awali haikua sahihi juu ya matokeo haikua sahihi kabisa,alikosea
 
hakuna matokea ya kata,matokeo ya vituo tu ndio yametoka na chadema wanaongoza,kwa mjibu wa msimamizi halijaingia saduku lolote makao makuu,kuna matokeo ya kata moja tu na hawajasema nani anaongoza.
 
Haya, ninachokiona hapa matokeo katika vituo kadhaa vya mjini Igunga yanaonyesha CHADEMA inaongoza na hali ni shwari sasa ila viongozi wengi wa CCM wameondoka hapa mjini igunga kila ukupita mitaani sasa ni CHADEMA mwendo mdundo. Mjini ndio kuna wapiga kura wengi hapa Igunga.

CCM wamekimbia mji hoteli waliyofikia vigogo ipo kimya. Kwa sasa nasubiri vituo vya vijijini.


Other updates:

06:00 PM Misururu ya vijana imeonekana mida ya jionijioni, yawezekana idadi ya waliopiga kura ikaongezeka.

mpaka hapo ccm wanongoza kwa kura 1285 kwa mujibu wa takwimu ulizoleta asante kwa kutujuza
 
Ufoo Saro anasema DED amesema atatangaza matokeo kuanzia saa tisa to saa kumi hapa nahisi Magamba wanataka kucheza rafu hawa mijizi

roho yangu ina firaha ajabu, tumewakamatia pabaya sana hawa wezi
 
Kwani lazima wote tuwe chama cha magwanda ndio tuonekane wajanja??ni demokrasia gani mnayoililia kama mtatulazimisha wote tuwe magwanda?JF ni ya wote, si mangwanda tu, kila mtu ana uhuru wake mkuu. Au una maumoivu ya kushindwa Igunga???
U r laggard 'wait and see' ndo nyie mloliwa DECI
 
Poor analysis
Wagombea wote wa CDM na CCM wakristo na hamna muislam!
Mmmh, sina uhakika kama kwenye post yangu ya msingi nimeongelea habari ya mgombea kuwa muislamu au mkristo, bali nimeongelea habari ya BAKWATA kuwazuia waumini wake kuipigia kura CHADEMA, na habari ya kwamba asilimia kubwa ya wakazi wa Igunga ni waislamu
 
Kwa kifupi chadema wameshinda kwa mujibu wa data za ITV na star TV, nashangaa tbc wameuchuna hawasemi kitu
 
Matokeo ya awali yamewapa hamasa wana Mwanza,hapa wamama,wadada,wababa,wazeee ni pipoz pawaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa

wapoze. Waambie washushe munkari, tutashangilia when the time is right.
 
Kuendana na matokeo mengi, inaonekana CUF wako ICU wanapumulia Oxygen. Natumanini ile ndoa yao na CCM imekula kwao !
 
hakuna matokea ya kata,matokeo ya vituo tu ndio yametoka na chadema wanaongoza,kwa mjibu wa msimamizi halijaingia saduku lolote makao makuu,kuna matokeo ya kata moja tu na hawajasema nani anaongoza.

kuwa mpole acha hasira kaka
 
ITV: Hali ya hewa sio nzuri, mvua inanyesha. Hii imesababisha utoaji wa matokeo kudorora. Labda kuanzia saa tisa au kumi alfajiri ndio kazi ya kuhesabu itakamilika.
Ndio mwanzo wa kuchakachua hapo.
 
bado sana idadi ya kura hazijajulimshwa kwa kiasi cha kutosha.

Pole sana, kile chama chako ulichojaribu kuanzisha kilikufa kifo cha kusikitisha, kilifia tumboni kabla hakijaiona dunia. Bora ubaki kushabikia magwanda!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom