Mashindano ya 'U-Miss' Yamezidi. Michezo Mingine Tumeisahau?...Twisted Priority?

---kuna makala nimekutana nayo kwenye gazeti la Mwananchi, maudhui yanafanana fanana na thread hii.... nainukuhu:

Posted Date::6/14/2008
Makala: Miss vitogoji ...ukicheza na Nyani utavuna mabua

Na Phillip Nkini


KAMA unazungumzia sekta inayotoa ajira kwa vijana ususani wasichana basi uwezi kuiweka kando mashindano ya Miss Tanzania ambayo tangu kuanzishwa kwake upya yamebadilisha maisha washiriki wengi.

Mashindano haya kwa Tanzania yamejijengea umaarufu siku za hivi karibuni kutokana na watu wengi kuanza kuyafuatilia kutokana na washiriki wake kuanza kutofutwa kuanzia vitogoji.

Mashindano haya yamekuwa na msisimko mkubwa sana kwenye jamii nzima na kila baada ya muda yamekuwa yakibadilisha mwelekeo mara kwa mara na kuongeza msisimko.

Kumeibuka mashindano mengi huku vigezo vikitofautiana kwa mtazamo na vigezo vya awali na mwisho wa mashindano husika.

Mashindano ya Miss Tanzania kama yalivyo mashindano mengine yana vigezo vyake ambavyo hutumika kwa ajili ya usimamizi mzima wa mashindano kwa ujumla.

Moja ya vigezo ambavyo vinatumika ili mrembo aruhusiwe kushiriki mashindano haya ni kwanza asiwe ameolewa, (yaani hana Mume), mwenye umri kuanzia miaka 18 hadi 24 na hasiwe na mtoto.

Nasema haya kwa kuwa nataka nikulete kwenye hoja yangu kuwa uandaaji wa mashindano haya kuanzia huku chini ngazi ya vitongoji ni mbovu na ndio maana mara nyingi tumekuwa hatufanyi vizuri kwenye mashidano kimataifa.

Ni hali ya hatari kwa sasa kama msichana ni mwembamba na mrembo akiwa anakatiza katika mitaa ya jiji la Dar es Salaam kuzongwa na kufuatwa na wimbi la Mawakala wanaoadaa mashindano haya ngazi ya vitongoji.

Mawakala hawa wamekuwa hata wakiacha shughuli zao nyingine na kupanda dala dala moja hadi nyingine huku wakimfuata msichana mmoja ambaye wamemuona anafaa kwa ajili ya shindano lao.

Imetokea mara nyingi kuona kuwa mmoja wa rafiki wa mtu anampigia mwezake ambaye anaanda mashidano haya na kumwambia njoo sehemu fulani uongee na mrembo mmoja ambaye yupo jirani yangu kwenye hoteli fulani nimekaa.

Au wakati mwingine utakuta mrembo ameshiriki vitogoji furani ameshindwa ana rusiwa kushiriki sehemu nyingine bila ya kipingamizi.

Baadhi ya wasichana wanaosoma shule za katikati ya jiji wamekuwa pia ni waathirika wakubwa wa kukimbizwa huku na mara anapokataa kutii amri hii huanza kusumbuliwa kwa maombi ya muda mrefu.

Hoja yangu hapa ni kwamba je vigezo hivyo vinatumika kwa ajili ya maandalizi haya wana juaje kama msichana huyu anakidhi vigezo vinavyotakiwa ili kushiriki ngazi ya Taifa?

Je unapomwangalia msichana unajua kuwa msichana huyu ameolewa au la unajua kama ana miaka zaidi ya 24 au je vyeti huonyeshwa kwa nani na lini kama mtu huyu ni mdogo au mkubwa.

Kwanini kusiwe na misingi dhabiti najua hakuna sehemu yeyote ambayo vyeti vyao vinaonyeshwe ana umri gani au ameolewa au vipi.

Kigezo kikubwa hapa ni kwamba kuna ubovu mkubwa sana kwenye utaratibu wa kuanzia mwanzo wa mashindano haya hadi mwisho kutokana na kutokuwa na mpangilio maalum.

Ni nani anayejua kuwa huyu anayepewa nafasi ya kuwa wakala sehemu moja au nyingine anaweza kupata washiriki wakutosha na wenye vigezo.

Pointi ya msingi inayotumika ni kwamba nani amewahi kuomba nafasi ya kufanya onyesho lake sehemu fulani na akapewa nafasi hiyo kwa kipindi kile.

Mashindano haya hapa nchini yamekuwa hayana faida kubwa baada ya mara nyingi washindi wa nchi hii kushindwa kufurukuta nje ya nchi ambapo wanakuta na na warembo waliopata maandalizi na vigezo vya juu.

Itakuwa kawaida kila mara kuona mshindi wa kwanza ngazi ya Taifa kupatikana jiji Dar es salaam kwa sababu wako karibu na mashindano hayo yanapofanyika kitaifa.

Lini waandaji wataweza kuwa kuna umuhimu wa kufanya mashindano haya kwenye ngazi ya Taifa mikoani ili kutoa semina kabambe na huku nao wajue kuwa kuna haja ya kujipanga na kupata semina ya vigezo husika ili waache kulalamika kila mara kuwa washidi wanatoka Dar es salaam.

Nafikiri ni muda muafaka sasa kabla mawakala hawa hawajapewa nafasi ya kuandaa mashidano katika kitongoji fulani basi wapewe kwanza kazi ya kutafuta wajumbe kabla ya kuanza mchakato huu mzima nikiwa na maana wapate kwanza angalau warembo kumi ambao wataangaliwa vigezo vyao ndio wapewe nafasi ya kuandaa tuone kama kuna hata mmoja atagombania hivi vitongoji.

Kwa sasa imekuwa ni kawaida kwa asilimia kubwa ya kitongoji kukuta kina warembo watatu zikiwa zimebaki siku tano tarehe ya mashindano yake kufanyika na hao wenyewe kuna siku wanakuja wawili na siku nyingine mmoja na wakati mwingine unakuta hata mwandaaji mwenyewe hayupo, je ni kweli kuwa tutapata mrembo mwenye vigezo vya kuwa mrembo wa Miss World.?

Kwa mtindo huu wa ubabaishaji tutaishia kuangalia warembo wakiangaika jukwaani na siku ya mwisho tutabaki tukisema kuwa mrembo wetu amekwenda Ulaya kutalii je msingi tuliweka? wapi alileta cheti kuwa amemaliza kidato cha nne au anauwezo wa kuzungumza kiingereza au tulimfundisha wapi ya kwamba akienda kule nje asizungumze kiingereza kwa kuwa hajua na azumgumze kiswahili na watu watamwelewa.

Mara kwa mara tumekuwa tunafika sehemu ya kulaumu kuhusu mashindano haya bila kuwa na vigezo vya Msingi ni dhahiri kuwa huku nyuma kumeoza na tupatengeneze kwanza ndio tupate nguvu za baadae kuongea.

Ni muda sasa wa kutafuta vyeti vya kuzaliwa vya washiriki kufundishana mchakato mzima wa kuwapata hawa warembo na kuweka kigezo cha elimu ili kulisaidia Taifa letu na warembo wenyewe ili waache kupoteza muda kwa ajili ya shilingi laki mbili za mshindi.

Tuwaheshimu warembo wetu kwa kuwa ni watu wakubwa na wenye hadhi yao na wanahitaji heshima kubwa si kama inavyofanyika sasa tujaribu kufungua macho yetu na kuangalia kwanza tatizo liko wapi ili tuweze kwenda mbele na si kurudia yale yale kila siku.
Source link: http://mwananchi.co.tz/newsre.asp?id=6198

SteveD.
 
Tangu mashindano ya kumtafuta Miss Tanzania yaanze tena mwaka takriban miaka kumi na tano iliyopita, Tanzania imekuwa haikosi mwakilishi ama kwenye Miss World, Miss Universe au mashindano mengine ya aina aina hiyo ngazi ya dunia. Ingawa wakati mwingine dada zetu huwa hafurukuti huko, wengi wao huwa wananyanyua vichwa vyao kwenye uloingo huo wa kimataifa ambapo ama wanafikia kati ya 20 bora au 10 bora au 5 bora kati ya warembo wa dunia nzima !!!, (Amanda wetu ni kati ya warembo ishirini bora wa dunia nzima yenye watu takriban bilion 7 !!!, siyo kidogo hiyo).

Ukiangalia kwa kina, mashindano hayo ya Miss Tanzania ambayo huanzia ngazi ya kitongoji hadi ngazi ya taifa huwa yanafadhiliwa na sekta binafsi kwa asilimia mia kwa mia.

Swali langu ni kwamba, kama tumefanikiwa kutumia sekta bionafsi kuendeleza vipaji vya urembo, kwa nini sekta hiyo isjikite pia kwenye vipaji vya michezo? Kuna michezo mingi sana ambayo sielewi kwa nini Tanzania tusiwe na wawakilishi; hebu angalia michezo kama ifuatavyo:

(a) kutupa Mkuki
(b) kutupa mshale
(c) kuendesha baiskeli
(c) kuogelea
(d) kucheza mpira wa majini (water polo)
(e) kutupa jiwe (tufe)
(f) Kuruka juu
(g) kuruka chini
(h) kuruka kwa upondo
(i) Volley ball
(j) basketball
(k) ....
nk....

Baadhi ya michezo hiyo ni asili yetu na tusingekuwa na ugumu wa kuwafundisha vijana wetu kwa vile iko kwenye damu yao tayari kama vile mbio ndefu zilivyo kwenye damu ya wakikuyu.

Wadau mnasemaje? Nashauri tuwe na kampeini ya kusensitize hii sekta binafsi inyanue michezo mingine pia tusiwe tunategemea urembo, ngumi, na mpira wa miguu tu.
 
kichunguu, nafikiri inabidi tutafute kiini kwanza cha kwa nini sekta binafsi imefanikiwa kwenye mambo ya urembo tu?

is it because urembo una gharama ndogo, na hawahitaji kuwa envolved kwa muda mrefu na warembo hao?
is it because urembo sio talent, ni maumbile tu, na sekta binafsi haipotezi pesa nyingi kwa ajili ya kutrain kwa muda mrefu?
is it because mabosi wengi wa sekta binafsi wanavutiwa personally na urembo wa wanawake ?
au sekta binafsi imejikita zaidi kwenye urembo tu kwa sababu wamepelekewa iyo offer in a plate na wao hawahitaji kutumia kitu chengine chochote zaidi ya pesa zao?
 
mtazamo wangu ni kuwa sekta binafsi ianze, halafu serikali irregulate tu.
Misaada, udhamini, utaratibu utafutwe na huyo mwenye mapenzi
Wenye kuandaa mashindano ya urembo, wafanye kama biashara. Wasitegemee ruzuku.
Wafanye marketing kupata wachezaji hodari.
Wafanye investment kwenye vijana, majeshi, na makabila yenye vipaji maalum.
Wasiwe kama sasa hivi wako kama hawana sera maalum ya kuendeleza mchezo wao.
Mfano mzuri ni Tennis, inapanda na kupandishwa na WAPENZI wake, na waloshawishiwa baada ya kuona uzuri wake. Si matatizo yake.
Watushawishi kuupenda mchezo na kuuchangia kwa kuona uzuri wake.
kwa sasa wanatushawishi kama vile ni kazi ya kizalendo.
Wabadili strategy.
tiketi ya kuingia mashindano ya umiss ni ghali sana, lakini watu wanaingia, netiboli ni bure lakini watu hawaendi, ni strategy tu. sio kulia na kuombaomba.
Angalia mashindano ya baiskeli sasa yanaanza kupanda chati, kwa sasa ni ishu kubwa sana pale mwanza, vipaji vinaonekana na vyombo vya habari vinayapa umuhimu sasa.
inatakiwa mtu/kampuni ifanye hiyo kama biashara au investment.
 
jamani naendelea kupata mawenge wenge kuna nini kinaendelea hapa, hili si ni jukwaa la thiatha?
 
Kichuguu Kwani Sekta Binafsi Imeshikwa Mikono?....u-miss Mashindano Ya Uchi, Na Watu Wengi Ni Sexidism...hawa Mashindano Hayana Mpango...

Kama Watu Tupo Serious, Tuwe Na Program Za Udhamini Wa Mambo Ya Elimu, From Elimu Kila Mtu Ataweza Kusimama Kwa Miguu Yake!!!
TUSIKIE WALE WAKALI WANAFUNZI WAKALI MASHULENI, WAKIENZIWE NA WALE WALIOCHINI/VILAZA WAKIWEKEWA MKAKATI WA KUINULIWA KIMASOMO NA SI KUWATELEKEZA
 
Hizo politics za umiss zikiingizwa kwnye michezo mingine itawezekana kweli?
Anyway, hii thread sijui inatafuta nini kwenye siasa?!?
 
jamani naendelea kupata mawenge wenge kuna nini kinaendelea hapa, hili si ni jukwaa la thiatha?

Hizo politics za umiss zikiingizwa kwnye michezo mingine itawezekana kweli?
Anyway, hii thread sijui inatafuta nini kwenye siasa?!?



Pole sana kwa kutokutambua kuwa sera za uendeleazaji michezo ni sehemu ya siasa. Kuna tofauti kubwa kati ya kujadili matokeo ya mechi za vilabu fulani, na kujadili sera za uendelezaji wa michezo nchini; ndiyo maana mkataba wa Maximo unasimamiwa na Ikulu.

Kichuguu Kwani Sekta Binafsi Imeshikwa Mikono?....u-miss Mashindano Ya Uchi, Na Watu Wengi Ni Sexidism...hawa Mashindano Hayana Mpango...

Kama Watu Tupo Serious, Tuwe Na Program Za Udhamini Wa Mambo Ya Elimu, From Elimu Kila Mtu Ataweza Kusimama Kwa Miguu Yake!!!
TUSIKIE WALE WAKALI WANAFUNZI WAKALI MASHULENI, WAKIENZIWE NA WALE WALIOCHINI/VILAZA WAKIWEKEWA MKAKATI WA KUINULIWA KIMASOMO NA SI KUWATELEKEZA

Ni kweli uendelezaji wa elimu mashuleni ni jambo muhimu sana ambapo sekta binafsi ingepromote kwa kuwazawadia vizuri wanaofnya vizuri, lakini vile vile itabidi uwe makini na statement hiyo kwani elimu vile vile inajumuisha na mambo kama muziki na michezo. BTW, ninafahamu kuwa makampuni kadhaa yamekuwa yanawazawadia vijana wanaofanya vizuri katika masomo yao; nakumbuka enzi zangu nilipokuwa Chuo nami niliwahi kujipatia shilingi mia mbili kutoka UFI kama zawadi.

Point ninayosisitiza hapa ni kuwa sekta binafsi ina wajibu mkubwa katika jamii. Tanzania iko chini sana kimichezo duniani. Ukiangalia timu tutakayopeleka kwenye Olimpiki kutakuwa na wapigana ngumi na wakimbiaji tu wakiongozana na maofisa wa michezo lukuki. Kuna michezo mingine mingi sana ambako tungeweza kuwakilishwa kwa ufanisi lakini hatufanyi hivyo, na ninaaona uwezekano mdogo sana kwa serikali kuiendeleza kutokana na historia yetu ilivyo. Najua Sekta binafsi haikushikwa mikono lakini labda inahitajika sensitization effort fulani ili wanyooshe mikono yao. Unajua wakati taifa stars ilipotoka sare, sekta binafsi ilimwaga fedha nyingi sana kwa vile kufanya hivyo ilikuwa pia ni namna ya kujitangaza kutokana na ukweli kuwa wananchi wanapenda sana soka. Kama wananchi wakionyesha kupenda michezo mingine pia, utaona sekta binafsi inaingilia; kinachotakiwa ni namna ya kuanza.
 
Pole sana kwa kutokutambua kuwa sera za uendeleazaji michezo ni sehemu ya siasa. Kuna tofauti kubwa kati ya kujadili matokeo ya mechi za vilabu fulani, na kujadili sera za uendelezaji wa michezo nchini; ndiyo maana mkataba wa Maximo unasimamiwa na Ikulu.



Ni kweli uendelezaji wa elimu mashuleni ni jambo muhimu sana ambapo sekta binafsi ingepromote kwa kuwazawadia vizuri wanaofnya vizuri, lakini vile vile itabidi uwe makini na statement hiyo kwani elimu vile vile inajumuisha na mambo kama muziki na michezo. BTW, ninafahamu kuwa makampuni kadhaa yamekuwa yanawazawadia vijana wanaofanya vizuri katika masomo yao; nakumbuka enzi zangu nilipokuwa Chuo nami niliwahi kujipatia shilingi mia mbili kutoka UFI kama zawadi.

Point ninayosisitiza hapa ni kuwa sekta binafsi ina wajibu mkubwa katika jamii. Tanzania iko chini sana kimichezo duniani. Ukiangalia timu tutakayopeleka kwenye Olimpiki kutakuwa na wapigana ngumi na wakimbiaji tu wakiongozana na maofisa wa michezo lukuki. Kuna michezo mingine mingi sana ambako tungeweza kuwakilishwa kwa ufanisi lakini hatufanyi hivyo, na ninaaona uwezekano mdogo sana kwa serikali kuiendeleza kutokana na historia yetu ilivyo. Najua Sekta binafsi haikushikwa mikono lakini labda inahitajika sensitization effort fulani ili wanyooshe mikono yao. Unajua wakati taifa stars ilipotoka sare, sekta binafsi ilimwaga fedha nyingi sana kwa vile kufanya hivyo ilikuwa pia ni namna ya kujitangaza kutokana na ukweli kuwa wananchi wanapenda sana soka. Kama wananchi wakionyesha kupenda michezo mingine pia, utaona sekta binafsi inaingilia; kinachotakiwa ni namna ya kuanza.
asante kwa kutupa ilmu siye tusiyeelewa, hivi bajeti ya wizara inayohusu masuala hayo inasomwa lini?
 
Mwalimu Kichuguu,

Tatizo la Tanzania kushindwa kung'ara katika mambo ya Michezo na Utamaduni ni kwa kuwa tunayaona kama hayana msingi, hayawezi kuwa vianzio vya kuleta pesa au kuinua Uchumi.

Hii inatokana na msukumo wa jamii na siasa kuona kuwa "Talanta: za maana ni kuwa zile za kisomi pekee, Udaktari, Uwakili, Uhandisi, Uhasibu na zingine nyingi ambazozinapewa vyeti na kupewa kazi.

Wenzetu na hasa nchi tajiri kama Marekani, Uingereza, Ujerumani, Japan na hata Urusi, Michezo na Utamaduni vimepewa nafasi sawa kuheshimiwa na jamii kama Uhandisi.

Ikiwa sisi tunadharau hata taaluma kama Uandishi, Ualimu, Utabibu na Uuguzi, Uhunzi, Ukulima, Ufugaji, Useremala na kuziona ni kazi "alosto" za walioshindwa kwenda Chuo na kupata Shahada na kutembea kifua mbele, ni vipi tutaanza kuona kuwa Michezo na Utamaduni ni vitu vya heshima na si Burudani kuangalia wasio na "kisomo" wakiehuka kutupa starehe?

Hili ndio tatizo na si ajabu ni mtazamo huo huo ulimfanya Mungai afute michezo ya UMISETA kwa kuona kuwa Michezo na Utamaduni haina faida katika jamii au kuwa katika mitaala ya kufundisha mashuleni.

Kama Taifa tukibadilisha mtizamo wetu katika kuangalia ni kazi gani eti ina thamani na kuthamini kila kazi na kila sehemu ya mtu kuwa ni muhimu katika maisha na mjumuiko wetu kama jamii, basi tunaweza kuanza hata kuleta mabadiliko ambayo tunalilia kila siku kupitia Siasa na kupigia debe kwa kuwa tunaona hayo machache ni muhimu.

Kila kitu ni Muhimu, Machinga ni Sehemu muhimu, hata Changuduoa pamoja na kuwa si halali na sawa, bado ni sehemu muhimu na wanapaswa kuheshimiwa. Utingo, Dereva Teksi, wazoa takataka, Shoe shine, wachuuzi sokoni, kuli bandarini, mwendehsa mkokoteni,fundi Baiskeli na wengine wengi wana nafasi sawa katika jamii na wanahitaji kupewa heshima na kuthaminiwa kazi zao kama Mbunge, Daktari au Waziri.

Tuna nafasi kubwa kubadilisha mtazamo huo duni kuona kuwa ni Urembo tuu, ambao unaweza kuwa unaleta mafanikio. Lakini hata kwenye mashindano ya Urembo, ushabiki mkubwa unatokana na Ukware na Ujogoo, kuona kuwa hawa "warembo" watapatikanaje na kuwa "asusa" za wenye pesa?

Ukiangalia kina Lundenga wakianza mchakato hata wa Miss Manzese, mpaka wabunge na vigogo (wenye pesa) huingia na kuchangia, kwa kuwa wote ni washindani kutafuta mabinti wa kuwatongoza.

Lakini ukiwaambia timu ya mpira wa vikapu inahitaji michango wanunue mipira mipya, wale wale wachache watatokea, hawatakunywa kwa kutosha na kufanya fund raising!

Binafsi ningependelea kurudishwa kwa elimu ya michezo, muziki na utamaduni kuanzia shule za msingi. Na hii si kwa kipindi cha break time pekee, bali liwe ni somo maalum, kipindi ambacho watoto wetu wataanza kujifunza mambo mengine mengi yanayozunguka ulimwengu wao na kuwapa fursa ya kujijenga vyema na kuwa na option nyingi huko baadaye.

Mfano, kama shule ikifundisha watoto Muziki, wakajifunza zumari, zeze, vinubi, tarumbeta na hata kusoma Muziki (music notes) je hatuoni kuwa tutakuwa tumechemsha upeo wao na kuwaongezea maarifa?

Maigizo, ngoma na Michezo vikifundishwa kama vipindi maalum, hatuoni kuwa tutaanza kujenga Taifa lenye kuthamini Utamaduni na elimu ya michezo itawafya watoto wetu waanze kujijenga kimiili na kuwa washindani bora hata katika masomo kwa kutumia misingi wanayojifunza wanaponyoosha viungo au wanapokimbia?

Tuna nafasi kubwa sana kubadilisha mtazamo wetu kama jamii na hivyo kuongeza kwa upana mkubwa sekta mpya ambazo zinaweza kuwa chimbuko la ajira na kupunguza kero kuwa hakuna ajira.

Watakaoanza hayo mapinduzi ya fikra kuthamini niliyoyataja ni sisi tunaojiita "Wasomi"!
 
Reverend,

Asante sana kwa kuliangalia hili kwa kina namna hiyo. Umenigusa sana ulipoweka bayana kuwa watu wetu hawajui kama michezo ni kazi. Sasa hivi nimemaliza kusoma post ya bwana mtsimbe kuhus Tanzania Professionals, inaelekea kabisa kuwa hiyo TPN inachukulia kuwa Professionals ni hao hao, wahandisi, wanasheria, Madaktari, wahasibu n.k.

Ni vizuri niongezee uzito kwenye maneno yako tena kuwa michezo inatoa ajira nzuri sana hasa kwa nchi yetu ambayo haina waajiri wengi. Tukumbuke tena kuwa akina Nyambui na Bayi wako katika nafasi walizo nazo kwa sababu ya michezo. Sasa hivi tunamsubiri kijana wetu hashim naye ang'are kwenye NBA kwa sababu ya michezo.

Bahati mbaya sana watu wetu hawalijui jambo hili, ndiyo maana ninataka kulipigia kelele kusudi tuamke.
 
inabidi kubadilika kweli kama jamii, tupanue wigo na kufikiria katika nyanja mbalimbali, la muhimu ni kujenga kizazi kisichoogopa kujaribu na ushindani pia, mwl kichuguu umenipa kitu cha kufikiria na kweli kwa haraka haraka mambo uliyogusia nimeona na mimi nipo kwenye kundi hilo la watu wanaochukulia michezo na utamaduni siyo ajira inayoeleweka, katika kufikiria huko nimegundua makuzi niliyopata ndio yamenijenga katika fikra hizo, asante tena kwa changamoto yako.
 
Hongera kwa WASHINDI wa Miss Tanzania 2008!!

Nafikiri huu ni wakati mwafaka wa kuliangalia hili swala la uandaaji wa mashindano haya na mengineyo yafananayo na haya kiundani zaidi.

Industry hii ni muhimu iwe regulated mapema iwezekanavyo, otherwise tutatahamaki na kukuta kila kampuni yenye hela za kuchezea ina endesha mashindano ya u-miss kwa vigezo vyake yenyewe. Na vigezo vingine vitakuwa kwa madhara ya mabinti wetu warembo wa Kitanzania.

SteveD.
 
Tatizo ni vipaumbele vyetu viko wapi...kama watu wako tayari kudhamini mamilioni kwenye mashindano ya umiss lakini hawadhamini ujenzi wa angalau jengo moja la shule au zahanati kwenye mji ambao hayo mashindano yanafanyika then kuna tatizo.

Its all about business promotion.Unadhani promotion itakayovuta watu wengi na wenye fedha zao ni pale utakapodhamini ujenzi wa vyoo ambavyo wao tayari wanavyo au pale utakapo promote u-miss?? nadhani tuangalie kwa mtizamo huo pia.
Labda tuangalie ni vipi through Corporate Social Reponsibilities tutaweza kuyachagiza makampuni yadhamini hayo mambo yenye kipaumbele kwa wanajamii/taifa kama usafi wa mazingira, ujenzi na matumizi ya vyoo n.k na in a sustainable manner.

Its all about putting your money where your mouth is.. or is it putting your mouth where your money is....??
 
Its all about business promotion.Unadhani promotion itakayovuta watu wengi na wenye fedha zao ni pale utakapodhamini ujenzi wa vyoo ambavyo wao tayari wanavyo au pale utakapo promote u-miss?? nadhani tuangalie kwa mtizamo huo pia.
Labda tuangalie ni vipi through Corporate Social Reponsibilities tutaweza kuyachagiza makampuni yadhamini hayo mambo yenye kipaumbele kwa wanajamii/taifa kama usafi wa mazingira, ujenzi na matumizi ya vyoo n.k na in a sustainable manner.

Its all about putting your money where your mouth is.. or is it putting your mouth where your money is....??[/
QUOTE]

Ni kweli its business promotion na its difficult to find someone willing to put his/her money where they wont reap.If you contribute in social affairs in anyway you don't expect to gain but if you throw your money in miss tz...or anything of that sort there is a way of getting more than you have given.

In my opinion, they put their money where their mouth already is
 
twisted ni washabiki, washiriki na wanahabari, na hao ni wachache tu, waandishi wanatudanganya ili kutuchota tufikiri ni ishu ya kitaifa SI KWELI.
 
kipaumbele cha nani?
Waandaaji, wadhamini, washabiki, washiriki, au waandishi?
manake
waandaaji: ndio kazi yao lazima waifanye kwa bidii, na bidii yao inatokana na imani kuwa kuna soko la starehe hiyo, wanawapa mashabiki kitu wanataka.

wadhamini: hawana kosa, wanadhamini mambo mengi tu, hili ni mojawapo tu, tena la muda mfupi, tofauti na udhamini mwingine ambao kwa mwaka unachukua zaidi ya miezi michache ambayo mamiss kuanzia vitongojini wanaanza kuandaliwa hadi miss tanzania anapatikana, pia lengo la mdhamini huwa ni kusambaza jina lake hivyo naona wadhamini wanajitahidi kuuza majina yao, wako staight, not twisted.

washabiki: kama uko kwenye kundi la washabiki, jiulize maadili uliyofundishwa yakoje, ni vizuri kushabikia wasichana walio nusu uchi? kama hakuna neno huko utokako basi endelea, ila kama sivyo wewe uko twisted. pamoja na wale wote wanaopenda na kushabikia huu mtindo. kwa kusoma, kununua, na kulipa viingilio, wajiulize. Lakini najua sio wengi sana kama ambavyo wanahabari wangependa tuamini.

Washiriki? hapo sina la kusema, ila najua baadhi wanafuatwa na wanarubuniwa kushiriki, kama akili kichwani hakuna basi, suzuki grand unaiona kama njia pekee ya kutokea kimaisha.

Wahahabari: kama kawaida wanatumia fani yao kuuza na magazeti. wamezoe kutwist habari ili wauze, hawajali madhara ya habari ile kwa wasomaji.

Hawa ndio mimi naona wako TWISTED zaidi kuliko wote wengine, wanataka tuamini kuwa ni jambo kubwa sana linatokea kumbe ni STAREHE YA AJABU AJABU TU YA KIKUNDI CHA WATU WACHACHE WANAOPENDA KUANGALIA WASICHANA.
 
...Tuna nafasi kubwa kubadilisha mtazamo huo duni kuona kuwa ni Urembo tuu, ambao unaweza kuwa unaleta mafanikio. Lakini hata kwenye mashindano ya Urembo, ushabiki mkubwa unatokana na Ukware na Ujogoo, kuona kuwa hawa "warembo" watapatikanaje na kuwa "asusa" za wenye pesa?

Ukiangalia kina Lundenga wakianza mchakato hata wa Miss Manzese, mpaka wabunge na vigogo (wenye pesa) huingia na kuchangia, kwa kuwa wote ni washindani kutafuta mabinti wa kuwatongoza.

...Rev. Kishoka huo msumari ulioupigilia na hapo ulipapigilia ndipo haswaaa!!! ...hata nikiongeza neno langu itakuwa naliharibu tu 'jeneza'!

Ubarikiwe!
 
Miss E.A ’09 kuondoka na Range Rover Vogue

MSHINDI wa kinyang’anyiro cha kumsaka mrembo wa Afrika Mashariki ataondoka na gari aina ya Range Rover Vogue Sport, lenye thamani ya zaidi ya sh mil. 120, kinyang’anyiro kitakachofanyika Desemba 18 mwaka huu jijini Dar es Salaam.


......

.
Mashindano ya Miss East Africa 2008 yalifanyika nchini Burundi, ambapo Claudia Niyonzima, aliibuka mshindi wa mashindano hayo na kuzawadiwa gari la kisasa aina ya Lexus RX 300, lenye thamani ya zaidi ya sh mil. 40.


http://www.freemedia.co.tz/daima/habari.php?id=5492

What's goin on with Miafika aisee? kuna kazi sana wakati wenzetu wanashindanisha vijana kwenye teknolojia sisi tunatoa gari la mamilioni kwa mtu kuonyesha nyeti zake hadharani.....
 
Back
Top Bottom