Deogratius n
JF-Expert Member
- Jan 10, 2015
- 1,193
- 254
Ili suala karibu makanisa yote ya kiroma yametangaza hivyo. Hata dsm makanisa mengi baada ya kuhubiri dini leo wamegeuka kumhubiri magufuli. Wanatuchanganya cc waamini.
Nikiwa kama Mkatoliki,siwezi kushawishiwa na Kiongozi wangu wa Kanisa kwamba nimchague fulani na fulani hafai,nitachagua kwa utashi wangu Mungu alionijaalia kwa kusikiliza na kuchambua sera zao na kuchanganya na zangu..haya mambo ya viongozi wa imani kuingilia ingilia siasa kwa matamko yao waamini wenzangu na waTanzania kwa ujumla tusishawishiwe nao siku ya uchaguzi ikifika vote kwa mwenye sera nzuri unaeona atatuletea maendeleo kama taifa.
anayepinga kuwa Magufuli kwa hali tuliyonayo sio chagua sahihi basi
1, ana matatizo ya akili
2,hajui taifa hili linamtaka mtu wa aina gani
3,inawezekana ni mkimbizi humu tz
4, siasa za makundi, vyama,ukabila ndo zinamfanya kipofu
5, miemuko ya siasa inamfanya kupoteza wererdi wa kujua wapi na nani anaweza kutupeleka tunapotaka kwenda,
Tatizo la mapdre hawa ni wao kujiona wamesoma na wanajua zaidi kuliko sisi waamini wao!! Hili ndilo kosa kubwa wanalofanya. Humo kanisani kuna watu wengi tu tena sana wanaowazidi Elimu na uelewa, kinachotupeleka pale ni kutimiza imani yetu lakini si kutulisha mambo ambayo hayakutupeleka pale, kama wanataka kuzungumza siasa wasubiri mikutano ya hadhara nao watoe yao ya moyoni na kanisani au msikitini ambako kila mtu ana chama chake. Wakiendekeza mambo haya kuelekea uchaguzi mkuu sadaka zitapungusio wote wapo wengine kama huyu padre wenye jicho la pekee na kutusaidia sisi tunaoendekeza miemuko ya siasa chafu na kupoteza weredi wa kujua kiongozi bora,
Je yule aliye acha upadri na kukimbilia tamaa ya Mwili?
.... huyo padre alaaniwe
Bavicha huwa wasahalifu kabisa...Siasa ni vurugu mechi hasa wakizivamia mahayawani.
Pengo aliposema viongozi wa dini hawana mamlaka ya kuwaamulia waumini wao juu ya kupiga kura ya NDIO/HAPANA kwa katiba pendekezwa alitukanwa na Gwajima na woote mkamuunga mkono Gwajima eti Viongozi wa dini wanapaswa kuwaongoza waumini wao hasa kwenye mambo yanayohusu mstakabali wao.(au mmesahau?)
Nashangaa hamueleweki hata mnachokisimamia au kwa kuwa hajamtaja mnayemshabikia?
Msipende kusikia mnachokitaka tu hii ndiyo demokrasia.
Wewe mtoa mada ndo mchawi,kama kimetokea kwako nyumbani wewe na mkeo,munayaongea nae padre wenu mnamfuata mnamtonya Usirudie hivi na hivi. Hata wewe ukikosana na mkeo unaongea nae taratibu na mnapata suluhisho sasa wewe unamwaga mtama kwenye kuku na hatujui kama ni ukweli.Watu kama nyie msio na common sense ni hatari sana katika jamii.Heri kufungiwa jiwe na kutupwa baharini.
Haya kayasema hadharani mkuu, tena mbele ya waamini wasio pungua elfu moja.. Ni ktk kanisa kuu la mt. mathias mulumba kalemba Songea Mjini.. Mapema leo asubuhi.
Katika kile kinachoonyesha viongozi wa dini kuingilia mambo ya siasa, padre Mbano akihubiri ktk Ibada ya leo j2 kwenye Kanisa kuu Katoliki Songea Mjini amesema ujio wa Magufuli ndio jembe haswa lililokuwa linasubiriwa.
Akaendelea kusema kuwa anawaomba radhi wapinzani safari hii waachane na urais wamwachie Magufuli aweke mambo sawa. kaendelea kusema, 'wapinzani tutawapa ubunge, lkn urais Magufuli anatosha' hapa kulikuwa na minong'ono kanisani. Najiuliza ni mapadre hawa hawa na maaskofu mwaka 2005 walisema JK ni chaguo la Mungu lkn sote ni mashahidi wa kilichotokea. Kwa nini wasiwaachie wananchi waamue wenyewe?
Kwa ushawishi walio nao mapadre kwa waumini wao wapinzani wasipokemea haya basi wasahau urais 2015. Pia hawa mapadre wana elimu kubwa sana lkn wanashindwa kutambua kuwa wale waumini wanaowahubiria kuwa ni wafuasi wa vyama mbali mbali..