Mapadre waanza rasmi kumpigia Magufuli kampeni

Mapadre waanza rasmi kumpigia Magufuli kampeni

Hawa mapadre mliwasifu walivyosema waumini waseme no kwa katiba pendekezwa
 
Dini inapovamia siasa matokeo yake huwa ni machafuko tuu. Kama hilo ndo lengo la uchungaji mliotunikiwa endeleeni kutupeleka huko.
 
kelao

magufuli ni mpango wa mungu,hakuna namna nyingine tanzania inahitaji mtu mwenye kaliba ya magufuli aka kagame wa tanzania
 
Last edited by a moderator:
Mkuki kwa nguruwe! Mmesahau 2010 mapadri walivyompigia debe dk slaa? Hii nchi inaongozwa na kanisa na Kama kanisa limeamua magufuri awe rais hakuna wa kupinga nyie mnasikiliza viongozi wenu wanasema nini na kufata tu, kipindi cha nyuma mliwalaumu waislam kwa kuchanganya dini na siasa ila hata nyie mlikuwa mnachanganya tatizo waislam hawakua wanafiki walisema waziwazi Kama mnavyofanya nyie leo

Mkuu nchi haiongozwi na kanisa, inaongozwa na KITENGO. kama ingekuwa inaongozwa na kanisa Kikwete angekuwa kaokoka/mlokole kitambo.
 
Huyu padre alisema chochote kuhusu ile barua waliowaandikia wakristo kuikataa katiba pendekezwa ya CCM.?
 
Padre huyo nampa tano. Mbona siku zote hamjitokezi kulaani matamko ya jukwaa la wakristo?
 
Ajabu ni Punda kupanda Farasi....mengine siyo ajabu.Padre kumpigia debe magufuli ni jambo la kawaida na pia Waisalmu kudai Mahakama ya Kadhi tulione ni jambo la kawaida.Mchezo uanzie hapo...Mahakama ya Kadhi VS padre na kampeni kwa Magufuli atakayeshinda tumkubali.
 
kelao

najua angemsema slaa ua lowawa msinge pinga kelele,lakini ukweli utabaki kuwa ukweli hakuna wa kumfananisha nae katika vigezo vya urais magufuli
pili kufananisha mchakato uliompata magufuli na ule wa kikwete ni kuonyesha kuwa ndo umeaza kushabikia siasa jana,
 
Last edited by a moderator:
Padre huyo Elimu nzuri lakini bado ni Kilaza... Hajui kuongea kwa mafumbo.. Mle kanisani kuna wafuasi wa namna mbali mbali.. Kwani watu kwenye za ibada si huwa wanafuata Sala na mambo mengine ya kidini, Siasa inaingiaje Kanisani??
Kutojielewa
 
Mie ni mkatoliki tena mseminari lakini niseme tu kuwa Padri huyo ni mpu.mbavu kama alivyokuwa Kilaini mwaka 2005.
 
Huyo Padre achukuliwe hatua stahiki

kwasababu kamuona magufuli anafaa ,angemsema slaa ngeshangilia ,wanafiki nyie,

huyu padre ni miongoni mwa watu wachache ambao wanajua taifa hili linamtaka mtu wa aina gani kwasasa ,hapa sio siasa ni ubora wa mtu na maitajio ya aina ya rais anayetakiwa ,asante mtumishi,
 
Back
Top Bottom