Mapadre waanza rasmi kumpigia Magufuli kampeni

Mapadre waanza rasmi kumpigia Magufuli kampeni

Kuna waraka ulitoka jukwaa la wakristo kipindi cha mchakato wa Katiba mpya kuelekea kwenye upigaji wa kura ya maoni ingawa haukufanikiwa(upigaji kura) waraka ule uliwataka waumini wakristo kupiga kura ya hapana kwa katiba Pendekezwa wengi wenu humu mlishangilia sana.

Cardinal Pengo alijitokeza akasema yeye hakubaliani na ule waraka na hasa kwenye kuwaambia waumini wapige kura ya hapana yeye alitaka wananchi waachwe waamue kwa utashi wao wenyewe kama wanapiga kura ya ndio au hapana badala ya watu wengi kumuunga mkono wengi walionekana kumshambulia kwa kila aina ya matusi wakimhusisha na UCCM Sasa leo kaibuka tena Padri kasema kile kile alichokuwa anakikataa Cardinal Pengo na kwa sababu wengi wenu hakijawafurahisha mnaanza kumlushia matusi Padre wa watu mnasahau kwamba Pengo aliliona hili mapema na nyinyi mkampuuza kubalini tu yaishe kama mlifurahia kuambiwa mpige kura ya hapana kwenye katiba mpya kwa nini leo mkasirike kuambiwa mmpigie kura ya Ndio ndugu JPM
 
Ili suala karibu makanisa yote ya kiroma yametangaza hivyo. Hata dsm makanisa mengi baada ya kuhubiri dini leo wamegeuka kumhubiri magufuli. Wanatuchanganya cc waamini.

Huu ni mpango kutoka Vatican kuhakikisha ni mkristo mkatoliki tu anayetawala Tanzania kama sio muislamu. Alianza Pengo kumuengua lowasa kwa kudai kwamba tusimchague mtu tajiri kwenda ikulu. Sasa mapadre wakatoliki wanaendeleza sera ileile kwa kumpigia debe magufuli kwa sababu tu ni mkatoliki bila kuangalia athari ambazo taifa letu litazipata kama CCM ikiendelea kuwepo madarakani. Mungu atunusuru kwani hawa jamaa wako tayari kumwaga damu ili kukidhi matakwa yao ya kidunia kama yaliyotokea Rwanda na Burundi walipoingilia kati mchakato wa kisiasa na kusababisha mauaji ya kimbari.
 
Mkuu kinachofanyika sio issue ya uDINI ni uCCM cz hawa viongozi wa hizi IMANI wanaamini wakiwapigia Debe wakichaguliwa watakuwa wanawakumbuka Kwani Kikwete alieitwa Chaguo la MUNGU Methodius Kilaini kwani. kikwete alikuwa Mkristo acheni kuwaza namna hiyo

sio udini ccm inapanga hivyo, baada ya miaka 10 atakuja muislam na lazima awe shia yaani BAKWATA na wakatoliki hawatagombea maana wanajua hilo-JKhakupata upinzani kutoka katoliki ni kina mwandosia monrovian muslims wenzie
 
Kuna Askofu mmoja alisema wasiompenda Lowasa wale malimao. Oia kuna mwingine aliwahi kusema Lowasa asipokuwa Rais auawe. Pia wapo akina Kilaini, Niwemungizi na wengine kibao. Mbona hamkupiga kelele?
 
Cha kushangaza hapa
Sijui tukimchagua Slaa sio mkatolic? hawa watu wako very biased. Yani humu watu duu yani unafikiria mpaka unaona kweli tunasafari
 
if you can't find what's good in Magufuli try to find what's wrong in you.
 
Kwa hiyo JK alipokuwa anaongoza kumchinjia EL Lowassa baharini alikuwa amepewa maagizo na kanisa?

Hiyo inajulikana toka anaingia ndio maana utakumbuka sister mmoja mkatoliki alimvisha taji na kanisa lilimpigia debe na hakuna mkatoliki aliyejitokeza kwa nia hasa ya kutaka urais. alikuwapo mwandosya morovian salim na kina kigoda.Inajulikana ni agano kuu
 
Hiyo inajulikana toka anaingia ndio maana utakumbuka sister mmoja mkatoliki alimvisha taji na kanisa lilimpigia debe na hakuna mkatoliki aliyejitokeza kwa nia hasa ya kutaka urais. alikuwapo mwandosya morovian salim na kina kigoda.Inajulikana ni agano kuu

Kwa hiyo Slaa siku hizi sio mkatoliki alivyoacha upadre akahama na ukatoliki pia?
 
Kuna waraka ulitoka jukwaa la wakristo kipindi cha mchakato wa Katiba mpya kuelekea kwenye upigaji wa kura ya maoni ingawa haukufanikiwa(upigaji kura) waraka ule uliwataka waumini wakristo kupiga kura ya hapana kwa katiba Pendekezwa wengi wenu humu mlishangilia sana.

Cardinal Pengo alijitokeza akasema yeye hakubaliani na ule waraka na hasa kwenye kuwaambia waumini wapige kura ya hapana yeye alitaka wananchi waachwe waamue kwa utashi wao wenyewe kama wanapiga kura ya ndio au hapana badala ya watu wengi kumuunga mkono wengi walionekana kumshambulia kwa kila aina ya matusi wakimhusisha na UCCM Sasa leo kaibuka tena Padri kasema kile kile alichokuwa anakikataa Cardinal Pengo na kwa sababu wengi wenu hakijawafurahisha mnaanza kumlushia matusi Padre wa watu mnasahau kwamba Pengo aliliona hili mapema na nyinyi mkampuuza kubalini tu yaishe kama mlifurahia kuambiwa mpige kura ya hapana kwenye katiba mpya kwa nini leo mkasirike kuambiwa mmpigie kura ya Ndio ndugu JPM

Haya mambo ya kumtayarisha Magufuli kuwa Rais hayakuanza juzi. Yalishapangwa mda mrefu tuu ndio maana Magufuli alipewa nguvu ya kuwatunia misuli mawaziri wenzake katika maamuzi yanayokingana, kupewa ndege ya Serikali kwa ajili ya mazishi ya mwanae, n.k.

Hivyo Pengo akiwa kama Kiongozi wa kanisa la katoliki lazima alihusishwa kwenye mpango mzima mapema bila ya mapadre wengine kujua nini kinachoendelea. Ndio maana alipoona mapadre wenzake wanalivalia njuga lile suala dhidi ya Serikali akaja na mtazamo tofauti dhidi ya wenzake kwani alishajua kwamba Rais anayeandaliwa ni Magufuli hivyo maslahi ya wakatoliki yatazingatiwa tu chini ya Urais wa Magufuli.
 
Huu ni mpango kutoka Vatican kuhakikisha ni mkristo mkatoliki tu anayetawala Tanzania kama sio muislamu. Alianza Pengo kumuengua lowasa kwa kudai kwamba tusimchague mtu tajiri kwenda ikulu. Sasa mapadre wakatoliki wanaendeleza sera ileile kwa kumpigia debe magufuli kwa sababu tu ni mkatoliki bila kuangalia athari ambazo taifa letu litazipata kama CCM ikiendelea kuwepo madarakani. Mungu atunusuru kwani hawa jamaa wako tayari kumwaga damu ili kukidhi matakwa yao ya kidunia kama yaliyotokea Rwanda na Burundi walipoingilia kati mchakato wa kisiasa na kusababisha mauaji ya kimbari.
Acha maneno ya ki uchochezi wewe. Unaotaota maneno yako tu unayaandika. Waliomchagua magufuli ni pamoja na mzee mwinyi,karume,kikwete nk ambao ni waislam. Kwa nini wasimchague january au bilal nk ambao ni waislam wenzao kama kulikua na factor ya udini. Kama huna point nyamaza,haudaiwi
 
Hiyo inajulikana toka anaingia ndio maana utakumbuka sister mmoja mkatoliki alimvisha taji na kanisa lilimpigia debe na hakuna mkatoliki aliyejitokeza kwa nia hasa ya kutaka urais. alikuwapo mwandosya morovian salim na kina kigoda.Inajulikana ni agano kuu

Huu lazima utakuwa ni mpango ambao ulisimikwa na Nyerere chini ya kipindi cha Mkapa kwamba kanisa katoliki liwe na mwakilishi kwenye "KITENGO" cha kuchagua na kuwaanda marais wajao ili kuhakikisha maslahi ya marais waliotanguli na kanisa katoliki yanazingatiwa. Na kuna uwezekano mkubwa sana kwamba marais wastaafu sasa hivi wanatapokezana watu wao wa kuwa marais wajao ili kulinda maslahi yao binafsi na ya familia zao. Kwa mfano kwa sababu kwa sasa ni zamu ya mkristo basi jukumu la kumwandaa rais wa wakati huu lilikuwa chini ya Mkapa. Ndio maana sishangai kuona Pinda kapigwa chini kwa sababu kila mtu anafahamu kwamba Magufuli ni chaguo bora kwa Mkapa kwa ajili ya kulinda maslahi yake kwani Magufuli nyota yake iliwashwa na Mkapa mwenyewe. Na sintashangaa chaguo la rais atakayekuja baada ya Magufuli ikawa zamu ya Kikwete kuweka mtu wake muislamu. Na hapa naona maandalizi yameshaanza kupitia Januari Makamba. Tutaona support na exposure atakayopewa January katika kipindi cha Magufuli kama, mungu apishie mbali, CCM ikishinda ili kujenga jina lake kuelekea Uchaguzi wa 2025.
 
Acha maneno ya ki uchochezi wewe. Unaotaota maneno yako tu unayaandika. Waliomchagua magufuli ni pamoja na mzee mwinyi,karume,kikwete nk ambao ni waislam. Kwa nini wasimchague january au bilal nk ambao ni waislam wenzao kama kulikua na factor ya udini. Kama huna point nyamaza,haudaiwi

Hayo wanayozungumza huko mapadre makanisani sio maneno ya uchochezi kuwabagua watanzania wote wenye haki ya kiupigiwa kura na kumwacha Magufuli tu peke yake?
 
Wewe kama mseminari maliza kwanza shule ndo ujilinganishe na kaka yako. Kuna distance kubwa kati ya padre na seminarist kwahiyo chunga sana, huwezi kujua kesho huyu padre anaweza kuletwa shuleni kwenu akaja kukufundisha "moral theology"
Mimi ni ex- seminarian, lakini hata hivyo mafundisho ya kanisa kuhusu kutenganisha dini na siasa pamoja na mafundisho ya Ecummenism hayahitaji uwe umesoma falsafa na teolojia kuyaelewa. Haya yanafundishwa ktk elementary level na yanaweza kueleweka kirahisi kwa mwamini(muumini) yeyote ambaye anaamini ktk imani na misingi ya kikatoliki achilia mbali yule anayeamini ktk binadamu (kiongozi) mmoja mmoja.
 
Mimi ni ex- seminarian, lakini hata hivyo mafundisho ya kanisa kuhusu kutenganisha dini na siasa pamoja na mafundisho ya Ecummenism hayahitaji uwe umesoma falsafa na teolojia kuyaelewa. Haya yanafundishwa ktk elementary level na yanaweza kueleweka kirahisi kwa mwamini(muumini) yeyote ambaye anaamini ktk imani na misingi ya kikatoliki achilia mbali yule anayeamini ktk binadamu (kiongozi) mmoja mmoja.

Kwahiyo unakubali kwamba Padre kusema kuwa Magufuli anafaa kuwa rais hakukosea? Na kama unaongelea imani, Imani ni object hata biblia inasema imani ni UHAKIKA wa mambo yatarajiwayo, sasa tafuta kosa la Padre kuusema uhakika (imani) wake mbele ya waamini.

Kutenganisha Dini na siasa ni vugumu sana na haitawezekana maana vyote vinamhusu binadamu huyu ambaye pia kwa asili anaviishi vyote. Kilichofanyika ni kuweka utaratibu kwamba dini na siasa vifanywe katika taratibu tofauti. Lakini ukitafuta maana ya DINI utakuta pia siasa imo. Kwahiyo ndugu yangu padre anaposema kesho (jumatatu) mkajiandishe kwenye BVR anatimiza wajibu wa na matakwa ya dini. Wabbilah tawfiq
 
haa haa alikuwa anampigia kampeni mwanakondoo wake... chezea ukatoliki wewe..
 
Katika kile kinachoonyesha viongozi wa dini kuingilia mambo ya siasa, padre Mbano akihubiri ktk Ibada ya leo j2 kwenye Kanisa kuu Katoliki Songea Mjini amesema ujio wa Magufuli ndio jembe haswa lililokuwa linasubiriwa.

Akaendelea kusema kuwa anawaomba radhi wapinzani safari hii waachane na urais wamwachie Magufuli aweke mambo sawa. kaendelea kusema, 'wapinzani tutawapa ubunge, lkn urais Magufuli anatosha' hapa kulikuwa na minong'ono kanisani. Najiuliza ni mapadre hawa hawa na maaskofu mwaka 2005 walisema JK ni chaguo la Mungu lkn sote ni mashahidi wa kilichotokea. Kwa nini wasiwaachie wananchi waamue wenyewe?

Kwa ushawishi walio nao mapadre kwa waumini wao wapinzani wasipokemea haya basi wasahau urais 2015. Pia hawa mapadre wana elimu kubwa sana lkn wanashindwa kutambua kuwa wale waumini wanaowahubiria kuwa ni wafuasi wa vyama mbali mbali..

huyo padre atakuwa wa kishetani anayehubiri siasa kanisani
 
Katika kile kinachoonyesha viongozi wa dini kuingilia mambo ya siasa, padre Mbano akihubiri ktk Ibada ya leo j2 kwenye Kanisa kuu Katoliki Songea Mjini amesema ujio wa Magufuli ndio jembe haswa lililokuwa linasubiriwa.

Akaendelea kusema kuwa anawaomba radhi wapinzani safari hii waachane na urais wamwachie Magufuli aweke mambo sawa. kaendelea kusema, 'wapinzani tutawapa ubunge, lkn urais Magufuli anatosha' hapa kulikuwa na minong'ono kanisani. Najiuliza ni mapadre hawa hawa na maaskofu mwaka 2005 walisema JK ni chaguo la Mungu lkn sote ni mashahidi wa kilichotokea. Kwa nini wasiwaachie wananchi waamue wenyewe?

Kwa ushawishi walio nao mapadre kwa waumini wao wapinzani wasipokemea haya basi wasahau urais 2015. Pia hawa mapadre wana elimu kubwa sana lkn wanashindwa kutambua kuwa wale waumini wanaowahubiria kuwa ni wafuasi wa vyama mbali mbali..
Sitaki kuamini kuwa padre wa katoliki anaweza katika maubiri akayaema hayo kama ulivyo andika. Ninafikiri unataka kuwachongnisha tunkwa wananchi. Najua kumekuwa na mtazamo wa kuwa kanisa lilimuunga mkono silaa uchaguzi uliopita, yawezekana sasa mnaanza kuwachochea ili wafarakane.
 
Kila mtu ana haki na uhuru wa kutoa maoni yake-hayo ni maoni ya Padre Mbando amesema Magufuli anatosha Urais 2015-2025.
Na wewe kama una maoni yako useme hadhalani,usisubiri kupinga maoni ya mtu mwingine

Mimi naona hakatazwi kutoa mawazo yake,yuko huru kabisa nadhani kinachowakwaza watu kutumia madhabahu kumpigia mtu kampeni
 
Back
Top Bottom