WE HAVE TO BE RUTHLESS,HII YA KUSEMA UNITED WAY UNITED WAY HAIWEZI KUTUPELEKA POPOTE..Fergie alikuwa genious.
✓Ole kila anapopata golden chance anaipoteza kizembe tu kwa kushindwa kuwa na game plan nzuri na tactics nzuri za kuipatia timu matokeo pale yanapohitajika kuliko wakati wowote..kwenye miaka yake hii miwili na nusu UTD ilibidi awe amebeba trophy yoyote..it is simple as that.
✓Benchi letu pia ni kama halimsaidii Ole huyu ambaye ni mchache wa mipango..McKenna na Carrick ni kama hawana lolote..Carrick anashangaa tu kama mgeni asiyejua lugha kwenye nchi ya watu.
✓Ni ngumu sana kuamini kuwa kocha sub-standard anaweza kukupatia timu bora barani ulaya kwani hata akipewa wachezaji wakali wengi bado atashindwa kutamba.
=========
Embu tukiangalie kikosi chetu
=========
Kama tukiwa Ruthless enough,yafuatayo inabidi yafanyike.
1.Lazima tutafute Holding Midfielder mmoja mzuri ambaye atafanya kazi ya kina Fred +McTominay..Hawa wawili kwa kweli technical ability yao ipo chini sana sana..Tunataka mtu anayeweza kukamata dimba kisawasawa kwenye kila kitu..kukaba,kutoa pass zenye macho,kudribble n.k.
2.CB combination yetu bado ni ya hovyo..Lindelof bado sana..tunahitaji kitasa cha kukaa na Maguire..Bailly kuongezewa mkataba mwingine sikuelewa kabisa..mtu ni spana mkononi 3yrs za nini tena?..huu ndo upuuzi wetu.
3.Tumesajili watoto kibao..yes,maybe kwa ajili ya matumizi ya baadae,lakini kwa sasa tunahitaji kutafuta straika na RW..Mtu kama Kane na Sancho kwenye hizo position.
°°°°Tunahitaji kufanya final touches ili kuweza kupambana ulaya ila pia ubora wa kocha wetu unatia mashaka°°°°Mimi binafsi naona hawezi kutupeleka zaidi ya hapa..We have to be ruthless°°°Chelsea wako hivyo ndo maana hawakai muda mrefu bila la kunyanyua kwapa and it seems pia wana wataalamu wa ufundi wazuri sana,mfano kwa sasa timu yao ile ikipata straika kama Kane au Haalland haitakamatika kabisa.