Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Sio kweli mkuu naomba Greenwood usimuweke hilo kundi kabisa, sio mchoyo na hapotezi mpira hovyo.

Had sasa ana goli moja tu mkuu hapo timu inapigania ubingwa na hao ndio washambuliaji wetu

Rashford goli 7 martial 2 greenwood 1 umeona hapo palipo na ugumu walau wangekuwa na goli 5 kila mmoja au 6 sasa bruno asipokuwa vizur tunatoka kapa
 
Tupo unbeaten Away zaidi ya mwaka, na hata kupoteza Msimu huu Ukitoa mwanzo wa ligi ambapo tulikuwa Hatuna fitness, tupo unbeaten mechi 12 sasa hivi toka November 2020, mechi zipi ndogo ambazo tumepoteza? Hata draw msimu huu ni against timu kubwa, ndogo zote tumezifunga.
Na pia tuna possibly worst home record
 
Mkuu unamtetea huyu? Hapa si kajikabisha mwenyewe hii counter haina tofauti na ile ya rooney,ronaldo na park dhidi ya arsenal kwa juu yake kuna had pogba ambae angapiga pass pia kwa cavan
View attachment 1681047
Rashford mpuuzi sana, mchoyo sana wa pasi, ujue sifa zishamlewesha huyu mpuuzi, awe anatazama video za rooney zitamfunza kitu
 
JamiiForums345638302.jpg
 
Mkuu unamtetea huyu? Hapa si kajikabisha mwenyewe hii counter haina tofauti na ile ya rooney,ronaldo na park dhidi ya arsenal kwa juu yake kuna had pogba ambae angepiga pass pia kwa cavan
View attachment 1681047
Amuangalie cavani hapo analalamika wkt huyo fala bado anao mpira.

Tatizo la trashford ni kujiona tayari keshakuwa world class wkt bado sn.
 
Bruno Fernandes alikuwa amechoka sana na probably anahitaji kupumzika walau 3 consecutive games au apunguziwe dakika za kucheza.
Bruno Fernandes bado hajaonyesha dalili za kuchoka kimwili ila aina ya uchezaji wake ndio unawafanya mashabiki wawe na imani ya kwamba huenda jamaa ameshachoka na anahitaji mapumziko japo ya mechi mbili, binafsi naamini hata kama itatokezea bruno amepewa mapumziko ya mechi tano mfululizo bado nina imani atarudi na aina ile ile ya uchezaji wake tuliouzowea.

kwanza bruno amenyimwa skills na uimara ndio maana hana uwezo wa kukaa na mpira akiwa kwenye presha ya adui na utofauti wake dhidi ya KDB unaanzia hapo licha ya kwamba wote ni risk takers (KDB hana skills kama iniesta lakini bado ana uwezo wa kuddrible dhidi ya mchezaji mmoja hadi wawili akiwa kwenye presha kubwa).

Ukitaka kumdhibiti bruno apply pressing kwake kama walivyofanya arsenal, liverpool na manchester city. Ukitaka bruno akuadhibu ruhusu gape kati ya mstari wako wa ulinzi na kiungo na wakati huo huo umeruhusu space kubwa ya wachezaji wa timu pinzani (hapo utaombea rashford na martial wapoteze nafasi kisenge huku wakisingizia uimara wa kipa)

bruno ni mchezaji ambaye hathamini possession (careless in possession) ila kwa kuwa amejificha kwenye kivuli cha risk takers imefikia hatua hata benchi la ufundi linaimbishwa wimbo huu na tatizo hili nakumbuka lilizungumzwa hata na scouts wa timu kabla ya usajili wake kughairishwa kwenye dirisha kubwa la usajili uliopita (accuracy pass takwimu zake ni mwendo wa 75%). Muda wote anapokuwa na mpira yeye anawaza attempts ndio maana baadhi ya nyakati hufanya maamuzi yasiovumilika kwa jicho la kawaida (hili tatizo linatatulika kama atasimamiwa na makocha au timu zinazoamini possession mfano guardiola, fc barcelona na hata louis van gaal na man utd yake)

mfano baadhi ya nyakati anaweza kupiga through ball akiwa eneo letu akiamini mchezaji wetu anaweza kukimbia eneo husika, muda mwengine anaweza kupiga pasi eneo ambalo limetawaliwa na walinzi wa timu pinzani akiamini pasi hiyo inaweza kuvuka lines ya safu ya ulinzi, huku akisahau ya kwamba kumbe ana uwezo wa kupiga pasi ya kawaida kwa mchezaji mwenzake aliyekaribu na kuifanya timu imiliki mpira na hatimaye kutengeneza mikimbio ya hatari (lakini hii itategemea na aina ya wachezaji waliomzunguka, mfano hawa kina mc'tominay, henderson, fred, fernandinho si waumini wa progressive pass ndio maana huenda hawa KDB na bruno muda mwingi huwaza kupiga mpira mbele wakiamini wataweza kutengeneza nafasi kuliko square pass)
=======================
 
uchezaji wetu wa tahadhari uliopitiliza nao ni kikwazo kikubwa sana kwa timu yetu kudominate game kwa dakika 5-10, kama tunahitaji kuzicontrol hizi mechi kubwa kama wafanyavyo liverpool au man city tunahitaji kuwa na utulivu wa kiuchezaji and organised time with the ball.

Binafsi naunga mkono mbinu alizokwenda nazo Ole dhidi ya liverpool bila ya kusahau fikra na heshima na taadhima kubwa dhidi ya adui yetu. Kuna baadhi ya makocha na timu zao huwa hawana heshima dhidi ya wapinzani wao na inapotokezea wamedhalilishwa kimatokeo ndipo mashabiki wao huanza kumyooshea kidole mlengwa fulani.

naambatanisha na mifano
  • mechi ya liverpool dhidi ya atletico madrid: kuanzia wachezaji, benchi la ufundi hadi mashabiki hawakuwaheshimu atletico madrid baada ya kumalizika kwa dakika 90 pale vicente calderon, wachezaji wengine walifika hatua ya kusema mutakuja anfield na huko tutawafunza adabu kama mabwana zenu barcelona(hapa nimetumia uswahili). kilichotokezea ni kulaumiwa kipa namba mbili
  • barcelona dhidi ya liverpool + bacelona dhidi ya AS ROMA: (mechi zote mbili barcelona hawakuonyesha heshima dhidi ya maadui zao ndio maana wakakumbana na comeback ya aibu)
kuna watu walitaka Ole aende Anfield akiwa uchi wa mnyama na ikitokezea dhahama waje wamnyooshee kidole huku wakimkumbusha baada ya mechi:
  • wewe Ole unakwenda uchi anfield huku ukijisahaulisha takwimu za liverpool za kutofungwa pale anfield kwa takribani misimu mitatu, kwa wachezaji gani ulionao hata ukacheze total football na wazee wa higher line defensive?
  • wewe Ole unakwenda uchi anfield huku ukijisahaulisha takwimu za liverpool za kutokushindwa kufunga goli pale anfield kwa takribani misimu miwili, kwa walinzi gani ulionao hata ukacheze uchi na utatu mtakatifu wa klopp?
nimesema hapo juu tahadhari na uoga dhidi ya adui yako ni muhimu lakini kama mwalimu unahitaji kuyasoma mazingira au tension ya huyo adui yako unayepambana naye. kwa mfano kipindi cha kwanza takribani wachezaji wetu wote walishindwa kuidhibiti pressing ya liverpool na matokeo yake tukawa tunalose possession na mipira ovyo mara kwa mara, lakini kadri dakika zilivyokuwa zikisogea kuelekea kipindi cha pili tulishuhudia baadhi ya wachezaji wakirudisha utulivu na hatimaye tukaanza kubypassing pressing ya liverpool na kwa hapa nimpe heshima yake scott mctominay kwa kurudi mchezoni kwa haraka zaidi kuliko mchezaji mwengine yeyote.

mpaka dakika ya 70 wapinzani wetu walishakata moto(hawakuwa na nguvu ya kutengeneza nafasi yeyote ya hatari ndani ya boksi letu), kilichonikera ni kuendelea kuushuhudia uoga na tahadhari iliopitiliza dhidi yao, wachezaji wetu wakiongozwa na scott, pogba, shaw na hata fred walishafanikiwa kuivunja pressing ya liverpool kwani tulishuhudia mara kwa mara wakivunja central line ya majogoo ila kilichokuwa kinakosekana ni muunganiko wa pale mbele.

ningelikuwa Ole ningelimtoa scott/ fred ndipo nikamuingiza edison cavani.
hii ndio substitution pekee iliohitajika, baada ya hapo ningeliangalia zaidi mwenendo wa rashford na martial.​
====================
  1. tunamuhitaji zaidi jack grealish ili tuwe na 4-4-2 inayonymbulika hadi 4-2-2-2 ya hatari, tunachokikosa kwa bruno na pogba tutakipata kutoka kwake na huu utakuwa ni usajili bora zaidi​
  2. uoga na tahadhari zipunguzwe, Darmian aliandika vizuri sana hapo juzi akinasihi benchi la ufundi litafute njia sahihi ya kiuchezaji baada double pivot ili kuongeza ukali wa safu ya ushambuliaji​
 
Bruno Fernandes bado hajaonyesha dalili za kuchoka kimwili ila aina ya uchezaji wake ndio unawafanya mashabiki wawe na imani ya kwamba huenda jamaa ameshachoka na anahitaji mapumziko japo ya mechi mbili, binafsi naamini hata kama itatokezea bruno amepewa mapumziko ya mechi tano mfululizo bado nina imani atarudi na aina ile ile ya uchezaji wake tuliouzowea.

kwanza bruno amenyimwa skills na uimara ndio maana hana uwezo wa kukaa na mpira akiwa kwenye presha ya adui na utofauti wake dhidi ya KDB unaanzia hapo licha ya kwamba wote ni risk takers (KDB hana skills kama iniesta lakini bado ana uwezo wa kuddrible dhidi ya mchezaji mmoja hadi wawili akiwa kwenye presha kubwa).

Ukitaka kumdhibiti bruno apply pressing kwake kama walivyofanya arsenal, liverpool na manchester city. Ukitaka bruno akuadhibu ruhusu gape kati ya mstari wako wa ulinzi na kiungo na wakati huo huo umeruhusu space kubwa ya wachezaji wa timu pinzani (hapo utaombea rashford na martial wapoteze nafasi kisenge huku wakisingizia uimara wa kipa)

bruno ni mchezaji ambaye hathamini possession (careless in possession) ila kwa kuwa amejificha kwenye kivuli cha risk takers imefikia hatua hata benchi la ufundi linaimbishwa wimbo huu na tatizo hili nakumbuka lilizungumzwa hata na scouts wa timu kabla ya usajili wake kughairishwa kwenye dirisha kubwa la usajili uliopita (accuracy pass takwimu zake ni mwendo wa 75%). Muda wote anapokuwa na mpira yeye anawaza attempts ndio maana baadhi ya nyakati hufanya maamuzi yasiovumilika kwa jicho la kawaida (hili tatizo linatatulika kama atasimamiwa na makocha au timu zinazoamini possession mfano guardiola, fc barcelona na hata louis van gaal na man utd yake)

mfano baadhi ya nyakati anaweza kupiga through ball akiwa eneo letu akiamini mchezaji wetu anaweza kukimbia eneo husika, muda mwengine anaweza kupiga pasi eneo ambalo limetawaliwa na walinzi wa timu pinzani akiamini pasi hiyo inaweza kuvuka lines ya safu ya ulinzi, huku akisahau ya kwamba kumbe ana uwezo wa kupiga pasi ya kawaida kwa mchezaji mwenzake aliyekaribu na kuifanya timu imiliki mpira na hatimaye kutengeneza mikimbio ya hatari (lakini hii itategemea na aina ya wachezaji waliomzunguka, mfano hawa kina mc'tominay, henderson, fred, fernandinho si waumini wa progressive pass ndio maana huenda hawa KDB na bruno muda mwingi huwaza kupiga mpira mbele wakiamini wataweza kutengeneza nafasi kuliko square pass)
=======================
Hili ni wachache wanaoliona..

There are many things that Bruno must improve ili kweli tumuimbe vizuri..
 
uchezaji wetu wa tahadhari uliopitiliza nao ni kikwazo kikubwa sana kwa timu yetu kudominate game kwa dakika 5-10, kama tunahitaji kuzicontrol hizi mechi kubwa kama wafanyavyo liverpool au man city tunahitaji kuwa na utulivu wa kiuchezaji and organised time with the ball.

Binafsi naunga mkono mbinu alizokwenda nazo Ole dhidi ya liverpool bila ya kusahau fikra na heshima na taadhima kubwa dhidi ya adui yetu. Kuna baadhi ya makocha na timu zao huwa hawana heshima dhidi ya wapinzani wao na inapotokezea wamedhalilishwa kimatokeo ndipo mashabiki wao huanza kumyooshea kidole mlengwa fulani.

naambatanisha na mifano
  • mechi ya liverpool dhidi ya atletico madrid: kuanzia wachezaji, benchi la ufundi hadi mashabiki hawakuwaheshimu atletico madrid baada ya kumalizika kwa dakika 90 pale vicente calderon, wachezaji wengine walifika hatua ya kusema mutakuja anfield na huko tutawafunza adabu kama mabwana zenu barcelona(hapa nimetumia uswahili). kilichotokezea ni kulaumiwa kipa namba mbili
  • barcelona dhidi ya liverpool + bacelona dhidi ya AS ROMA: (mechi zote mbili barcelona hawakuonyesha heshima dhidi ya maadui zao ndio maana wakakumbana na comeback ya aibu)
kuna watu walitaka Ole aende Anfield akiwa uchi wa mnyama na ikitokezea dhahama waje wamnyooshee kidole huku wakimkumbusha baada ya mechi:
  • wewe Ole unakwenda uchi anfield huku ukijisahaulisha takwimu za liverpool za kutofungwa pale anfield kwa takribani misimu mitatu, kwa wachezaji gani ulionao hata ukacheze total football na wazee wa higher line defensive?
  • wewe Ole unakwenda uchi anfield huku ukijisahaulisha takwimu za liverpool za kutokushindwa kufunga goli pale anfield kwa takribani misimu miwili, kwa walinzi gani ulionao hata ukacheze uchi na utatu mtakatifu wa klopp?
nimesema hapo juu tahadhari na uoga dhidi ya adui yako ni muhimu lakini kama mwalimu unahitaji kuyasoma mazingira au tension ya huyo adui yako unayepambana naye. kwa mfano kipindi cha kwanza takribani wachezaji wetu wote walishindwa kuidhibiti pressing ya liverpool na matokeo yake tukawa tunalose possession na mipira ovyo mara kwa mara, lakini kadri dakika zilivyokuwa zikisogea kuelekea kipindi cha pili tulishuhudia baadhi ya wachezaji wakirudisha utulivu na hatimaye tukaanza kubypassing pressing ya liverpool na kwa hapa nimpe heshima yake scott mctominay kwa kurudi mchezoni kwa haraka zaidi kuliko mchezaji mwengine yeyote.

mpaka dakika ya 70 wapinzani wetu walishakata moto(hawakuwa na nguvu ya kutengeneza nafasi yeyote ya hatari ndani ya boksi letu), kilichonikera ni kuendelea kuushuhudia uoga na tahadhari iliopitiliza dhidi yao, wachezaji wetu wakiongozwa na scott, pogba, shaw na hata fred walishafanikiwa kuivunja pressing ya liverpool kwani tulishuhudia mara kwa mara wakivunja central line ya majogoo ila kilichokuwa kinakosekana ni muunganiko wa pale mbele.

ningelikuwa Ole ningelimtoa scott/ fred ndipo nikamuingiza edison cavani.
hii ndio substitution pekee iliohitajika, baada ya hapo ningeliangalia zaidi mwenendo wa rashford na martial.​
====================
  1. tunamuhitaji zaidi jack grealish ili tuwe na 4-4-2 inayonymbulika hadi 4-2-2-2 ya hatari, tunachokikosa kwa bruno na pogba tutakipata kutoka kwake na huu utakuwa ni usajili bora zaidi​
  2. uoga na tahadhari zipunguzwe, Darmian aliandika vizuri sana hapo juzi akinasihi benchi la ufundi litafute njia sahihi ya kiuchezaji baada double pivot ili kuongeza ukali wa safu ya ushambuliaji​
Amaizing..

Mimi mwenyewe niliwaza hivi..baada ya Liverpool kukata moto kwenye dakika ya 70 hivi nilitaka Fred atoke aingie Cavani..Martial,Rashford na Cavani mbele pale tungeweza kupata goli kabisa..

Game zote za Big six tumecheza kwa tahadhari sana huku mbele tukiwa na nguvu ndogo..no wonder hatujashinda hata moja..

✓United 0 vs Arsenal 1

✓United 0 vs City 0

✓United 0 vs Chelsea 0

✓Liverpool 0 vs United 0
 
Back
Top Bottom