Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Kama Ole atajaribu kumuweka Fred nje katika hali yoyote nitamuona kichaa zaidi.

Naona kwa sasa baada ya ujio wa Bruno nafasi ya kiungo itakuwa na changamoto sana watakapopona Scott na Pogba. Maana hata huyo Mata siku hizi naona anacheza sana na anachangamsha sana timu sasa sijui ndio anaidai namba 10 yake.

Hata matic kawa vizur sana upungufu uliopo 7 na bissaka yule mzur kwa timu za kupak basi kushambulia ni sifur kama wanatafuta sare bissak mzur sana james bado hajawa poa martial mzigo shaw hawez kupiga cross timu nyingi zinazidiwa na liverpool upande wa bek mbili na tatu wale madogo wamechangia
Ushindi mkubwa sana hata ukiwabana wakina salah na roberto firmino wale madogo wanafungua njia sasa ukiangilia bissaka na shaw had dakika ya 88 ndo cross moja inapigwa dalot anakosa goli
 
Not good result, not bad result

Kwa kuangalia midfield iliyocheza, bado naona tumepata matokeo sio mabaya sana

Hayupo Matic, hayupo Tominay, hayupo Pogba. Hao wangekuwepo probably leo Pereira ambaye amecheza chini ya kiwango asingeanza. Nina uhakika tungefanya vizuri zaidi

Leo na siku zote tunazocheza na timu ambazo on paper tunazizidi huwa hatufanyi transition ya haraka ya mashambulizi pindi tunaponyang'anya adui mpira. Na hii ni style isiyomsaidia James kabisa

Martial amejitahidi kupambana lakini mipira mingi aliyopokea alikuwa akilipa mgongo goli la adui hivyo imekuwa ni ngumu sana kufanya jambo lolote

Bruno Fernandes, ambaye amefanya mazoezi jana tu na wenzake amecheza vizuri, sio sana lakini vizuri. Amepiga mashuti golini jambo ambalo tumekuwa tukishindwa kulifanya kwa mechi zetu nyingi. Pia amekuwa akijaribu kupitisha pasi (penetration pass). Kwenye kusaidia ulinzi ametimiza majukumu yake ipasavyo, not a bad debut.

Maguire solid as usual, Lindelof amecheza vizuri, Degea hakuwa bize sana lakini ametimiza majukumu yake, clean sheet kwenye mechi ya pili mfululizo. Inaonesha tunaizidi kuboreka kwenye ulinzi.

Wan Bissaka going forward bado sana, Wan Bissaka akiwa na mpira muda wowote anakosea. Wan Bissaka akikaba huwezi kuwa na wasiwasi. Wan Bissaka ana kazi ya kufanya

Waliobaki wamecheza vizuri. Sijui OGS aliwaza nini kumtoa Pereira na kuingiza Dalot wakati tunatafuta goli, nilidhani atamtoa Bissaka. Kwa mtazamo wangu sub ya Greenwood ilipaswa kuwa ya mapema zaidi, labda dakika ya 70, labda baada tu ya Adama kutoka

Twende kwenye mapumziko ya wiki 2 tukawatazame akina Lukaku wakifanya yao . Wiki mbili bila EPL ni nyingi sana.

Next stop, Stamford Bridge kwa wateja wetu. Ni matumaini Scot, Kirusi na Matic watakuwa wapo tayari.

Sent using Jamii Forums mobile app


Next stop, Stamford Bridge kwa wateja wetu
 
Dah..... Sijui hata nikikueleza utanielewa

Nishawahi kusema kwa mtazamo wangu, Pogba is 65%-75% complete midfielder,

Kwa hiyo ranking ya kiasilimia, sio mchezaji mbaya, ni mzuri, above average

Lakini hiyo haimaanishi kwamba, hakuna midfielders wengine (duniani) ambao ni 70%-80% au to 90%

OGS asingemng'ang'ania summer na tungemuuza na tungenunua mwingine nisingekuwa namuongelea kwenye kikosi chetu leo hii. Lakini kwa sasa ndio yupo kikosini lazima tumtumie, after all midfielder wa hiyo ranking ya 65%-75% sio mbovu kiivyo.

Kiufupi Pogba kama mchezaji, kama yupo tayari kujitoa kwa asilimia zote na akiwa na right attitude ana potential kufika hiyo asilimia 75 kiuchezaji lakini kwa bahati mbaya hana hiyo mentality

Narudia, kwa sasa Pogba ni moja kati ya most creative players tulionao kikosini (nimesema tulionao kikosini, sio duniani) , hivyo kumuweka pembeni akiwa fit ni kujichanganya

Mwisho Pogba ni mchezaji ambaye niseme ni aina wachezaji wenye nyota ya kuwa overhyped, Pogba, Gareth Bale ni aina ya wachezaji wenye majina makubwa kuliko uwezo wao. Pogba ni Kinyume cha wachezaji kama akina Kante, KDB, Firmino & Co.

Ikitokea mtu kashuka kutoka sayari nyingine akatajiwa Pogba anaweza kudhani ni level za akina CR7 au Messi au Hazard kumbe yupo nyuma yao sana kiuwezo
Kumbe unamwelewa pogba na umuhimu wake.... Wacha kumponda sasa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Halafu eti kuna binadamu anamfananisha Martial na Raul Jimenez
Unapata wapi nguvu ya kuandika maneno mengi hivi ili hali timu yako haichukui ubingwa msimu huu?

Unajitesa bure

Fupisha stori:-_

Pereira - BOMU
Martial - Kilaza
James - waruwaru
Bruno - Safi


Sent using Cash Money Wings

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom