Tangu siku inaanza nilikuwa sina amani kwa kuamini leo tutadhalilishwa na vijana wa pep,nikajiaminisha kuwa vyovyote matokeo yatakavyokuwa nitaridhika kutokana na tofauti ya ubora wetu na city. Lakini baada ya matokeo nimeumia zaidi kwa kutambua kuwa bado tuna safari ndefu sana kufikia kuchukua ubingwa wa ligi kuu achilia mbali kucheza fainali ya ligi ya mabingwa.
Matokeo hayajanihuzunisha sana kama ambavyo tumekuwa wanyonge mbele ya city ukizingatia uwekezaji wetu na wao hatukupaswa kuwa na tofauti kubwa sana aidha kiuchezaji au mtizamo tunaoingia nao dimbani. Ni dhahiri tangu upangaji wa vikosi vilivyoanza mou hakutegemea pointi 3 kwa city bali alihitaji droo kwanza na point 3 zije kama ziada flani hivi. Angalia mid field yetu ilivyokuwa nzito kutembeza mipira kwenda mbele. Kwa mechi tatu zilizopita tumeshuhudia umuhimu wa mata katika kuichangamsha timu kwa mipira ya kwenda mbele,lakini hofu ya mou imemzidi akamweka huyu mtu nje hadi pale alipoona yuko nyuma kimatokeo.
Kama ambavyo wengi tumeona na kuamini kuwa kukosekana kwa pogba kumechangia matokeo mabaya lakini binafsi sikubaliani na sababu hiyo kwa asilimia nyingi sana. Pogba anakuwa mzuri timu inaposhambulia Ila kwa mpira wa city unahitaji kiungo anayeshambulia na kukaba kwa haraka,na sio pogba anayejivuta vile. Kwa mawazo yangu ili kukabiliana na city yenye wachezaji wanyumbulifu tulihitaji viungo ambao ni attack minded ili kuwatia hofu city wasije wengi langoni kwetu hasa beki zao. Angalia long range alizokuwa anafanya fernandinho kisa tu hakuna mtu wa kumbughudhi. Kama mou alikuwa ni wa kujifunza,Wolverhampton walituonyesha jinsi ya kucheza na city,kupishana. Najua hapa watu watasema hatuna wachezaji wenye ubora wa kupishana na city,he wolves wana kikosi kizuri kuliko united?
Kwa game ya leo,city ni bora kwa mchezaji mmoja mmoja na kimbinu pia walituzidi. Mbali na martial sijaona mchezaji yeyote wa united ambaye anaweza walau kumtoka beki mmoja wa city wakiwa 1x1 ila city wanawatoka wachezaji wa united kirahisi sana. Leo hii no aibu na dhihaka kubwa sana kumuona Felipe Anderson anaichezea westham,Madison anaichezea Leicester, Richarlson anakipoga Everton, wakati sisi tuna lingaard kama namba 10 wetu. Tuna shida katika soko la usajili kama ambavyo mkuu
Damushin amekuwa akidai. Saa nyingine huwa najiuliza mou huwa anawafundisha nini hawa wachezaji wetu pale carrington maana mbinu yetu kubwa ya magoli imekuwa ni mipira iliyokufa zaidi. Set up ya mashambulizi imekuwa ni dhaifu mno tena ni hadi adui atuchokoze. Kwa sasa pale EPL hakuna timu tunayoizidi kucheza mpira mzuri kati ya timu zote 19 maana hata Leicester wanaugusa mwingi kuliko sisi.
Nimalizie kwa kusema kwamba kwa mwenendo huu mwakani tujiandae kucheza Europa ligi na nangojea kukutana na akina BATE Borisov ,spartak Moscow na wenzake.
Mniwie radhi wakuu maana nimeandika kwa hasira kidogo maana sioni tumaini kwa hii timu kufikia hapa.
GGMU