Malalamiko kwa Shule Binafsi: Wizara ya Elimu na Tamisemi waliangalie na kulitolea muongozo

mcfm40

JF-Expert Member
Nov 2, 2010
4,452
3,150
Tunaomba serikali na hasa Wizara ya Elimu na ike ya Tamisemi waliangalie sana hili na kulitolea muongozo mapema.

Malalamiko yenyewe ni kwamba kumekuwa na utaratibu kwa shule za binafsi hasa zile za English Medium kuzuia wanafunzi wa madarasa ya mitihani kwenda likizo hasa ya mwezi wa sita.

Inajulikana kwamba utaratibu wa likizo upo duniani kote kwa binadamu wote wanaofanya kazi wakiwepo wanafunzi. Na hili linafanyika baada tafiti kuonesha kwamba binadamu hawawezi kufanya kazi mfululizo bila kupumzika kwani hilo linaadhiri ufanisi wao katika kazi.

Sasa inashangaza kuona shule hizi za msingi za binafsi zinawanyima wanafunzi wa darasa la nne na la sita kwenda mapumziko ya mwezi mmoja eti kisa wanawaandaa kwa mitihani ijayo.

Hawa ni watoto wadogo, wanasoma mfulilizo bila kupumzika kisa mitihani kweli hili ni sawa? Kaka na dada zao wa Form Two na Form Four wana mitihani mwishoni mwa mwaka huu lakini wapo likizo. Sasa iweje hawa wa form two na darasa la sita? Ni nini hasa so special kwa hawa wanafunzi wa English Medium schools.

Je, ni kweli kwamba muda uliopo hautoshi kuwaandaa hawa watoto kufanya vizuri kwenye mitihani yao?

Hao watalaam wa elimu na wanasaikolojia waliopendekeza utaratibu huo na ukakubalika pengi walikosea?

Isitoshe, kwa sasa kuna waraka wa serikali unaokataza shule za serikali kutofunga shule au kuongeza muda wa masomo kwa wanafunzi bila ruhusa ya mkurugenzi/serikali. Tena yamewekwa masharti na mambo ya kuzingatia kama shule itataka kutumia muda wa mapumziko wa wanafunzi kufundisha.

Je, Shule hizi za private hazifungwi na taratibu na secular hizo za serikali? Wanaruhusiwa kufanya mambo wanavyoona tu wao? Kiholela.

Tunaomba serikali na bunge waliangalie hili na liwekewe utaratibu mzuri kwa sababu linaleta usumbufu mkubwa kwa wazazi na kunyima haki ya watoto kupumzika "from daily routines za shule!"
 
Umelazimishwa kumpeleka mwanao private na wakati kuna elimu bila ada mkuu anatakuwa anafunga mara 4 kwa mwaka?
 
Watanzania jueni kwamba Elimu kwenye taasisi binafsi ni biashara hivyo kama biashara zingine lazima wafanye vizuri kuvutia wateja ( kufaulisha).

Wasipofanya jitihada za kufaulisha ikiwemo kuondoa likizo kwa madarasa ya mitihani na wengine wakifanya hivyo ni dhahiri watakosa soko.

Kama unaona wewe ni ngumu kwenda nayo muombee ruhusa mwanao asihudhurie au mpeleke shule ya serikali.

Note

Pamoja na mambo mengine wizara ya Elimu HAIRUHUSU KABISA wanafunzi kubaki shule au kuendelea kusoma kipindi cha likizo.
 
Watanzania jueni kwamba Elimu kwenye taasisi binafsi ni biashara hivyo kama biashara zingine lazima wafanye vizuri kuvutia wateja ( kufaulisha).

Wasipofanya jitihada za kufaulisha ikiwemo kuondoa likizo kwa madarasa ya mitihani na wengine wakifanya hivyo ni dhahiri watakosa soko.

Kama unaona wewe ni ngumu kwenda nayo muombee ruhusa mwanao asihudhurie au mpeleke shule ya serikali.

Note

Pamoja na mambo mengine wizara ya Elimu HAIRUHUSU KABISA wanafunzi kubaki shule au kuendelea kusoma kipindi cha likizo.

Nimekusoma: Elimu kwenye taasisi binafsi ni biashara! Hii ndio hoja yangu haswa. Hawa wafanya biashara wanapaswa wawe regulated kama biashara nyingine. Kutaka sifa kwao kusiwe kigezo cha kuwatesa watoto kwa kuwa overload. Hii nchi sio shamba la bibi kwamba yeyote anayewrza kujifanyia atakavyo bila kufuata miongozo iliyowekwa.

Nashukuru umesisitiza hapo mwishoni kwamba hawa wanavunja kanuni na raratibu za wizara!

Swala la kupeleka watoto shule za serikali kama naona private hakufai ni hoja ya ajabu kidogo. Hiki kihoja hakina tofauti na kipindi kile mtu analalamika mshahara mdogo mwendazake anajibu kama mshahara mdogo acha kazi! Is this the way to go? Kwamba huna haki ya kulalamika kwenye jambo unaloona halipo sawa? Hakuna uhusiano wa moja kwa moja kati ya kubakisha watoto shuleni mwezi wa sita na ufaulu wao! Kama upo ni very insignificant! Kana upo naomba huo utafiti unaoonesha hilo!

Nimenote kwamba waalimu wengi wa private wamevamia huu uzi kuupinga kwacsababu zilizo wazi!
 
Lasaba wana mtihani September,wakiwa nyumbani likizo,wakifungua July watakuwa na miezi 2 tu.

Au tatizo lako ni kuwa shule nyingine zinachajisha hela kwa huo mwezi mmoja wa sita?
 
Sidhani kama wanaenda shule fulltime.

Wa kwangu wanaenda saa1 mpaka saa 8, wakibaki nyumbani vurugu sana bora wakipata muda walau masaa kadhaa shuleni akirudi masaa yaliyobaki yanatosha kucheza.
 
Nakubaliana na Mtoa hoja..Watoto wanasona vizuri na waalimu wako vizuri kwa nini wa tunawamis Watoto wetu eti tu mna-wasupplimate wafaulu vuzuri. Serikali or rather Bunge wekeni swala hili sawa. Thanks Mzazi Ninayeumizwa na utaratibu huo.
 
Lasaba wana mtihani September,wakiwa nyumbani likizo,wakifungua July watakuwa na miezi 2 tu.

Au tatizo lako ni kuwa shule nyingine zinachajisha hela kwa huo mwezi mmoja wa sita?

Wala hawachaji chochote. Mimi lalamiko langu ni kunyimwa kubreak kutoka nazingira ya shule. Basi uwe ni utaratibu kwamba madarasa ya mitihani hawapaswi kufunga! Lakini kwangu mimi sidhani kama kuna chochote kukubwa cha ziada wanapata kinachohalisha kuwanyima mapumziko. Homework na revision zingwatosha kabisa! Pia muda wa masomo ukitumika vizuri hakuna sababu ya watoto kusoma kwa mfululizo.

Hawa bado ni watoto sio wanafunzi wa sekondari. Hawahitaji kushindiliwa mambo mengi kiasi hicho kwaxsababu tu shule inashindana na nyingine kibiashara! Watoto wanaishia kukaririshwa maswali ya mitihani bila maarifa yoyote ya kile wanachosoma. Ni bahati mbaya wazazi wengi hawalionin hili wanabbaki tu kushangilia kutumiwa na wafanya biashara hawa kujinufaisha kwa kutesa watoto wetu!
 
Nakubaliana na Mtoa hoja..Watoto wanasona vizuri na waalimu wako vizuri kwa nini wa tunawamis Watoto wetu eti tu mna-wasupplimate wafaulu vuzuri. Serikali or rather Bunge wekeni swala hili sawa. Thanks Mzazi Ninayeumizwa na utaratibu huo.
Nashukuru tupo wachache tunaoelewa ubaya wa jambo hili!
 
Wala hawachaji chochote. Mimi lalamiko langu ni kunyimwa kubreak kutoka nazingira ya shule. Basi uwe ni utaratibu kwamba madarasa ya mitihani hawapaswi kufunga! Lakini kwangu mimi sidhani kama kuna chochote kukubwa cha ziada wanapata kinachohalisha kuwanyima mapumziko. Homework na revision zingwatosha kabisa! Pia muda wa masomo ukitumika vizuri hakuna sababu ya watoto kusoma kwa mfululizo.

Hawa bado ni watoto sio wanafunzi wa sekondari. Hawahitaji kushindiliwa mambo mengi kiasi hicho kwaxsababu tu shule inashindana na nyingine kibiashara! Watoto wanaishia kukaririshwa maswali ya mitihani bila maarifa yoyote ya kile wanachosoma. Ni bahati mbaya wazazi wengi hawalionin hili wanabbaki tu kushangilia kutumiwa na wafanya biashara hawa kujinufaisha kwa kutesa watoto wetu!
Watapumzika baada ya mitihani kuanzia Sept-Dec mkuu tulia dawa ipenye
 
Back
Top Bottom