Shule ya English Medium imegoma kumuhamisha mwanangu. Hatiani kukosa mtihani wa darasa la nne

Fateema

Member
Feb 8, 2024
13
41
Mimi ni single mother umri wangu ni miaka 34. Kwa ufupi Nina watoto wawili wa kiume wa kwanza ana miaka tisa wa pili ana miaka saba. Huyu kwanza yupo darasa la 4 na wa pili yupo darasa la 3. Kilicho nifanya nilete ujumbe huu hapa Jamii Forums ni kitendo cha dhulma kinacho taka kufanywa na shule ya English Medium dhidi ya watoto wangu.

Ni hivi baada ya kuachana na baba wa watoto wangu niliwapeleka wanangu kwa bibi yao Mwanza.

Wakati nawapeleka Mwanza mkubwa alikuwa kafikisha umri wa kuingia darasa la kwanza na mdogo alikuwa na umri wa kuingia chekechea.

Walipo fika mwanza nikawapeleka kwenye shule moja ya English Medium. Mwalimu wa shule hiyo ambae alikuwa jirani yangu ndio alie nishawishi niwapeleke watoto wangu kwenye shule hiyo kwa sababu alisema walikuwa na utaratibu mzuri wa malipo na walikuwa wanachukua hata shilingi elfu hamsini kwa mwezi au themanini.

Niliona inanifaa kwa sababu iliendana na kipato changu. Baba wa watoto pia alikuwa ana toa sapoti ya ada. Kweli nilienda nikalipa hela watoto wakasajiliwa wanapewa na prem number wakaanza kusoma. Pesa nililipa kwa huyu mwalimu kwa sababu aliniambia pesa niwe nalipa kwake yeye anaziwasilisha kwa uongozi kwa sababu walikuwa wanapewa commission na shule kwa kila mwanafunzi watakae mpeleka shuleni. Sikuwa Mimi tu pia kuna baadhi ya wazazi walikuwa wanalipa kwa utaratibu huo. Niliwaacha watoto kwa bibi yao nikarudi zangu Dar kuendelea na shughuli zangu. Nikiwa naendelea na utaratibu huo huo wa kulipa kupitia kwa huyo mwalimu ambae alikuwa anawaandikia watoto risiti wanaziwasilisha kwa bibi yao. Wakati mwingine anasema alikuwa anawaandikia maelezo ya kawaida kwamba wamelipa ada na kwamba ataziwasilisha hela kwa uongozi kisha atapewa risiti na shule atawapatia watoto wazipeleke kwa bibi yao.

Fast forward mwaka jana mwezi wa saba wakati wa likizo nilipiga simu kwa huyo madam kwamba ninataka kuwahamisha watoto wangu kuwaleta Dar anisaidie kuongea na uongozi tupate prem numbers za watoto. Madam akaniambia analishughulikia but akaniambia kwa wakati huo wa likizo watoto wanatakiwa kuwa shuleni hivyo ninatakiwa kulipa shilingi elfu themanini ambayo kama ilivyo kuwa siku zote alitaka niilipe kupitia simu yake. Lakini Mimi nilimwambia Nina wachukua watoto waje Dar ili niwe nao kwa ukaribu zaidi. Akasema sawa atashughulikia suala la uhamisho. Siku iliyo fuata nikampigia sikumpata nikaona nimtume mdogo wangu aende kuchukua namba za mwalimu mkuu wa shule.

Nilipo ongea na mwalimu mkuu wa shule cha kushangaza akasema huyo madam sio mwalimu wa hapo kwa zaidi ya miezi miwili na kwamba amewaliza wazazi wengi ambao walikuwa wanampa pesa yeye. Nikauliza sasa kuhusu haki za watoto wangu vipi kwa sababu ninataka kuwahamisha ma huyo mwalimu alikuwa mwajiriwa wao wanatusaidia vipi sisi wazazi tulio muamini na kumlipa pesa zetu?

Pili nikamwambia atazame kama watoto wamesajiliwa kwa sababu nilimpa shilingi laki moja na elfu sitini kama gharama za usajili kwa kila mtoto.

Niliogopa sana nilihisi huenda hata hiyo shule yenyewe haina usajili.

Mkuu akasema wacha atazame kuhusu status ya wanafunzi hao pamoja na rekodi zao za ada.

Kuhusu status ya usajili akasema watoto wote wana prem numbers ingawa gharama za kuwasajili pia nilipigwa.

Kuhusu ada nikaambiwa nadaiwa shilingi milioni moja na laki 2 kwa sababu tangu watoto waanze kusoma kwenye shule hiyo hawajawahi lipa hata senti tano.

Nikajiuliza how comes mnasema watoto hawajawahi lipa hata senfi wakati hadi matokeo ya watoto yapo nyumbani.

Walifanya vipi mitihani bila kulipa hata senti 5?

Walipata vipi prem numbers kama hawajawahi kulipa hata senti tano?

Nilifadhaika sana na nilianza kukosa imani na hiyo shule kabisa.

Niliwaagiza watoto wangu Dar then nika watafutia shule ya kawaida ya kiswahili. Nili ichagua shule hii kwa sababu ipo karibu na mahali ninapo ishi lakini pili sina uwezo wa kulipa kwenye shule za English Medium kwa sababu ya kupanda kwa gharama za maisha na uwezo wangu kifedha kushuka na sapoti ya baba watoto imekuwa ndogo.

Kingine nilikosa kabisa imani na shule za English Mediums hasa hizi zinazo Anza Anza zenye wanafunzi wachache. Bado nilikuwa na kidonda kibichi kutoka kwa shule hiyo waliyo soma watoto wangu.

Nilipata nafasi kwenye shule ya kiswahili huku nikipambana kuomba shule waliyo kuwa wanasoma wawahamishe wanangu kwenye mfumo wawatoe kwenye shule yao wawahamishie kwenye shule hii mpya. Lakini cha ajabu muda wote wamekuwa wakinipiga danadana wanadai niwalipe pesa ambayo kiufupi hawanidai.

Sasa hivi darasa la nne wapo kwenye usajili wa mitihani ya taifa huyu mwanangu jina lake bado linasoma kwenye shule aliyo toka.

Walimu wanasema asipo hamishwa ndani ya deadline maana yake ni kwamba atatakiwa kwenda kufanya mtihani kwenye shule ile ile ambayo ni ya kiingereza au atatakiwa kurudia shule na kama akirudia basi prem number yake itaendelea kusoma juu yani itaonekana yupo darasa la 5 wakati yupo darasa la 4 yani kiufupi ndoto za mwanangu kitaaluma ndio zinakuwa zimeishia hapo. Sasa Mimi naomba msaada wa mamlaka zinazo husika zinisaidie ili mtoto wangu apewe haki yake ya kufanya mtihani wake wa darasa la 4 ambayo inataka kupokwa na wamiliki wa shule aliyo toka bila justification yoyote. Sheria na taratibu za elimu ya Tanzania zina kataza mtoto kunyimwa haki ya kufanya mtihani kwa sababu yoyote ile inayo husiana na fedha. Uongozi wa hiyo shule ya English Medium unataka kuvunja sheria hii kwa kumkosesha mwanangu haki yake ya kufanya mitihani ya darasa la nne kwa sababu ya deni hewa. Mtoto wangu ameshinda analia siku nzima ya leo anauliza sasa mama itakuwaje..

Naomba msaada tafadhali. Namba za huyo mwalimu alie kuwa anachukua ada zipo namba za mkurugenzi wa shule zipo namba za mkuu wa shule zipo na risiti zote ambazo zilikuwa zinaandikwa kwamba mwanangu amelipa ada pia zipo kwa bibi wa watoto. Nipo tayari kuziwasilisha risiti hizo mbele ya uongozi wa shule kama zikihitajika ila kwa sasa ninacho hitaji ni mtoto wangu apewe haki yake ya kufanya mtihani wake wa darasa la nne.

Uwepo wa namba za huyo mwalimu alie kuwa anachukua hela zangu pamoja na as wazazi wengine utarahisisha kukamatwa kwa huyo mwalimu ili alipe hizo pesa alizo Chukua. Niliwaambia uongozi wa shule wanisaidie huyo mwalimu akamatwe lakini wamekuwa wanapiga danadana kana kwamba wana mkingia kifua au wana ogopa kuchafua taswira ya shule yao.

Naomba msaada pia huyu madamu akamatwealipe hizo hela alizo Kula lakini wakati zoezi la kumtafuta na kumuweka ndani huyu madamu linaendelea naomba watoto wangu wapewe haki yao ya uhamisho.

Serikali waki hitaji ni disclose taarifa za hiyo shule pamoja na majina ya huyo madam wanae sema amekimbia na hela pamoja na majina ya uongozi nipo tayari kufanya hivyo.

Yericko Nyerere

Mh.
Dkt. Gwajima D
 
Mimi ni single mother umri wangu ni miaka 34. Kwa ufupi Nina watoto wawili wa kiume wa kwanza ana miaka tisa wa pili ana miaka saba. Huyu kwanza yupo darasa la 4 na wa pili yupo darasa la 3. Kilicho nifanya nilete ujumbe huu hapa Jamii Forums ni kitendo cha dhulma kinacho taka kufanywa na shule ya English Medium dhidi ya watoto wangu.

Ni hivi baada ya kuachana na baba wa watoto wangu niliwapeleka wanangu kwa bibi yao Mwanza.

Wakati nawapeleka Mwanza mkubwa alikuwa kafikisha umri wa kuingia darasa la kwanza na mdogo alikuwa na umri wa kuingia chekechea.

Walipo fika mwanza nikawapeleka kwenye shule moja ya English Medium. Mwalimu wa shule hiyo ambae alikuwa jirani yangu ndio alie nishawishi niwapeleke watoto wangu kwenye shule hiyo kwa sababu alisema walikuwa na utaratibu mzuri wa malipo na walikuwa wanachukua hata shilingi elfu hamsini kwa mwezi au themanini.

Niliona inanifaa kwa sababu iliendana na kipato changu. Baba wa watoto pia alikuwa ana toa sapoti ya ada. Kweli nilienda nikalipa hela watoto wakasajiliwa wanapewa na prem number wakaanza kusoma. Pesa nililipa kwa huyu mwalimu kwa sababu aliniambia pesa niwe nalipa kwake yeye anaziwasilisha kwa uongozi kwa sababu walikuwa wanapewa commission na shule kwa kila mwanafunzi watakae mpeleka shuleni. Sikuwa Mimi tu pia kuna baadhi ya wazazi walikuwa wanalipa kwa utaratibu huo. Niliwaacha watoto kwa bibi yao nikarudi zangu Dar kuendelea na shughuli zangu. Nikiwa naendelea na utaratibu huo huo wa kulipa kupitia kwa huyo mwalimu ambae alikuwa anawaandikia watoto risiti wanaziwasilisha kwa bibi yao. Wakati mwingine anasema alikuwa anawaandikia maelezo ya kawaida kwamba wamelipa ada na kwamba ataziwasilisha hela kwa uongozi kisha atapewa risiti na shule atawapatia watoto wazipeleke kwa bibi yao.

Fast forward mwaka jana mwezi wa saba wakati wa likizo nilipiga simu kwa huyo madam kwamba ninataka kuwahamisha watoto wangu kuwaleta Dar anisaidie kuongea na uongozi tupate prem numbers za watoto. Madam akaniambia analishughulikia but akaniambia kwa wakati huo wa likizo watoto wanatakiwa kuwa shuleni hivyo ninatakiwa kulipa shilingi elfu themanini ambayo kama ilivyo kuwa siku zote alitaka niilipe kupitia simu yake. Lakini Mimi nilimwambia Nina wachukua watoto waje Dar ili niwe nao kwa ukaribu zaidi. Akasema sawa atashughulikia suala la uhamisho. Siku iliyo fuata nikampigia sikumpata nikaona nimtume mdogo wangu aende kuchukua namba za mwalimu mkuu wa shule.

Nilipo ongea na mwalimu mkuu wa shule cha kushangaza akasema huyo madam sio mwalimu wa hapo kwa zaidi ya miezi miwili na kwamba amewaliza wazazi wengi ambao walikuwa wanampa pesa yeye. Nikauliza sasa kuhusu haki za watoto wangu vipi kwa sababu ninataka kuwahamisha ma huyo mwalimu alikuwa mwajiriwa wao wanatusaidia vipi sisi wazazi tulio muamini na kumlipa pesa zetu?

Pili nikamwambia atazame kama watoto wamesajiliwa kwa sababu nilimpa shilingi laki moja na elfu sitini kama gharama za usajili kwa kila mtoto.

Niliogopa sana nilihisi huenda hata hiyo shule yenyewe haina usajili.

Mkuu akasema wacha atazame kuhusu status ya wanafunzi hao pamoja na rekodi zao za ada.

Kuhusu status ya usajili akasema watoto wote wana prem numbers ingawa gharama za kuwasajili pia nilipigwa.

Kuhusu ada nikaambiwa nadaiwa shilingi milioni moja na laki 2 kwa sababu tangu watoto waanze kusoma kwenye shule hiyo hawajawahi lipa hata senti tano.

Nikajiuliza how comes mnasema watoto hawajawahi lipa hata senfi wakati hadi matokeo ya watoto yapo nyumbani.

Walifanya vipi mitihani bila kulipa hata senti 5?

Walipata vipi prem numbers kama hawajawahi kulipa hata senti tano?

Nilifadhaika sana na nilianza kukosa imani na hiyo shule kabisa.

Niliwaagiza watoto wangu Dar then nika watafutia shule ya kawaida ya kiswahili. Nili ichagua shule hii kwa sababu ipo karibu na mahali ninapo ishi lakini pili sina uwezo wa kulipa kwenye shule za English Medium kwa sababu ya kupanda kwa gharama za maisha na uwezo wangu kifedha kushuka na sapoti ya baba watoto imekuwa ndogo.

Kingine nilikosa kabisa imani na shule za English Mediums hasa hizi zinazo Anza Anza zenye wanafunzi wachache. Bado nilikuwa na kidonda kibichi kutoka kwa shule hiyo waliyo soma watoto wangu.

Nilipata nafasi kwenye shule ya kiswahili huku nikipambana kuomba shule waliyo kuwa wanasoma wawahamishe wanangu kwenye mfumo wawatoe kwenye shule yao wawahamishie kwenye shule hii mpya. Lakini cha ajabu muda wote wamekuwa wakinipiga danadana wanadai niwalipe pesa ambayo kiufupi hawanidai.

Sasa hivi darasa la nne wapo kwenye usajili wa mitihani ya taifa huyu mwanangu jina lake bado linasoma kwenye shule aliyo toka.

Walimu wanasema asipo hamishwa ndani ya deadline maana yake ni kwamba atatakiwa kwenda kufanya mtihani kwenye shule ile ile ambayo ni ya kiingereza au atatakiwa kurudia shule na kama akirudia basi prem number yake itaendelea kusoma juu yani itaonekana yupo darasa la 5 wakati yupo darasa la 4 yani kiufupi ndoto za mwanangu kitaaluma ndio zinakuwa zimeishia hapo. Sasa Mimi naomba msaada wa mamlaka zinazo husika zinisaidie ili mtoto wangu apewe haki yake ya kufanya mtihani wake wa darasa la 4 ambayo inataka kupokwa na wamiliki wa shule aliyo toka bila justification yoyote. Sheria na taratibu za elimu ya Tanzania zina kataza mtoto kunyimwa haki ya kufanya mtihani kwa sababu yoyote ile inayo husiana na fedha. Uongozi wa hiyo shule ya English Medium unataka kuvunja sheria hii kwa kumkosesha mwanangu haki yake ya kufanya mitihani ya darasa la nne kwa sababu ya deni hewa. Mtoto wangu ameshinda analia siku nzima ya leo anauliza sasa mama itakuwaje..

Naomba msaada tafadhali. Namba za huyo mwalimu alie kuwa anachukua ada zipo namba za mkurugenzi wa shule zipo namba za mkuu wa shule zipo na risiti zote ambazo zilikuwa zinaandikwa kwamba mwanangu amelipa ada pia zipo kwa bibi wa watoto. Nipo tayari kuziwasilisha risiti hizo mbele ya uongozi wa shule kama zikihitajika ila kwa sasa ninacho hitaji ni mtoto wangu apewe haki yake ya kufanya mtihani wake wa darasa la nne.

Uwepo wa namba za huyo mwalimu alie kuwa anachukua hela zangu pamoja na as wazazi wengine utarahisisha kukamatwa kwa huyo mwalimu ili alipe hizo pesa alizo Chukua. Niliwaambia uongozi wa shule wanisaidie huyo mwalimu akamatwe lakini wamekuwa wanapiga danadana kana kwamba wana mkingia kifua au wana ogopa kuchafua taswira ya shule yao.

Naomba msaada pia huyu madamu akamatwealipe hizo hela alizo Kula lakini wakati zoezi la kumtafuta na kumuweka ndani huyu madamu linaendelea naomba watoto wangu wapewe haki yao ya uhamisho.

Serikali waki hitaji ni disclose taarifa za hiyo shule pamoja na majina ya huyo madam wanae sema amekimbia na hela pamoja na majina ya uongozi nipo tayari kufanya hivyo.

Yericko Nyerere

Mh.
Dkt. Gwajima D

Pole sana dada kwa changamoto. Kuna baadhi ya vitu unaweza ukaviboresha zaidi hapo mbeleni, hasa kutuma pesa ukiamini unafanyiwa kazi. Nimeona watu wanatuma mamilioni ya pesa kwenda shambani, wakati hata shamba hawajawahi liona. Boresha hilo. Vitu vingine fuatilia mwenyewe physically. Delegation nayo ina mipaka. Naamini uliowa tag watakusaidia.
 
Pole sana dada kwa changamoto. Kuna baadhi ya vitu unaweza ukaviboresha zaidi hapo mbeleni, hasa kutuma pesa ukiamini unafanyiwa kazi. Nimeona watu wanatuma mamilioni ya pesa kwenda shambani, wakati hata shamba hawajawahi liona. Boresha hilo. Vitu vingine fuatilia mwenyewe physically. Delegation nayo ina mipaka. Naamini uliowa tag watakusaidia.
Ameen
 
Msiwe mnapeleka watoto wenu kwenye shule hizo za English Mediums ni ubabaishaji mtupu
Nadhani hiyo statement iko generalized, kuna english mediums zinafanya vizuri sana. Tatizo watu wengine hawajui kuchagua, akisikia shule, basi ni kupeleka tu watoto. Haijalishi shule ni ya binafsi, serikali, mchepuo wa kiswahili, kiingereza au kimataifa, ni lazima ujue kufanya chaguzi.
 
Ulikua unampa mtu hela ya ada mkononi kwani shule haina bank account ? Hizi za kayumba tu zina account una contribute kupitia account ya shule, andaa risit za malipo uliyofanya kupitia bank ili u prove kuwa hudaiwi ila kama ulikua unatuma hela kwa mpesa tena kwenda kwenye namba binafsi ya mwalimu tu itakusumbua sana.

Inabidi umalizie ada ili umuamishe mtoto wako shule haina njia nyingine ya kudai haki yake tofauti na kuzuia uhamisho wa mtoto wako.

Tusiwaamini sana watu hata mimi kuna mambo yananitesa kwa kuamini watu haraka.
 
Mimi ni single mother umri wangu ni miaka 34. Kwa ufupi Nina watoto wawili wa kiume wa kwanza ana miaka tisa wa pili ana miaka saba. Huyu kwanza yupo darasa la 4 na wa pili yupo darasa la 3. Kilicho nifanya nilete ujumbe huu hapa Jamii Forums ni kitendo cha dhulma kinacho taka kufanywa na shule ya English Medium dhidi ya watoto wangu.

Ni hivi baada ya kuachana na baba wa watoto wangu niliwapeleka wanangu kwa bibi yao Mwanza.

Wakati nawapeleka Mwanza mkubwa alikuwa kafikisha umri wa kuingia darasa la kwanza na mdogo alikuwa na umri wa kuingia chekechea.

Walipo fika mwanza nikawapeleka kwenye shule moja ya English Medium. Mwalimu wa shule hiyo ambae alikuwa jirani yangu ndio alie nishawishi niwapeleke watoto wangu kwenye shule hiyo kwa sababu alisema walikuwa na utaratibu mzuri wa malipo na walikuwa wanachukua hata shilingi elfu hamsini kwa mwezi au themanini.

Niliona inanifaa kwa sababu iliendana na kipato changu. Baba wa watoto pia alikuwa ana toa sapoti ya ada. Kweli nilienda nikalipa hela watoto wakasajiliwa wanapewa na prem number wakaanza kusoma. Pesa nililipa kwa huyu mwalimu kwa sababu aliniambia pesa niwe nalipa kwake yeye anaziwasilisha kwa uongozi kwa sababu walikuwa wanapewa commission na shule kwa kila mwanafunzi watakae mpeleka shuleni. Sikuwa Mimi tu pia kuna baadhi ya wazazi walikuwa wanalipa kwa utaratibu huo. Niliwaacha watoto kwa bibi yao nikarudi zangu Dar kuendelea na shughuli zangu. Nikiwa naendelea na utaratibu huo huo wa kulipa kupitia kwa huyo mwalimu ambae alikuwa anawaandikia watoto risiti wanaziwasilisha kwa bibi yao. Wakati mwingine anasema alikuwa anawaandikia maelezo ya kawaida kwamba wamelipa ada na kwamba ataziwasilisha hela kwa uongozi kisha atapewa risiti na shule atawapatia watoto wazipeleke kwa bibi yao.

Fast forward mwaka jana mwezi wa saba wakati wa likizo nilipiga simu kwa huyo madam kwamba ninataka kuwahamisha watoto wangu kuwaleta Dar anisaidie kuongea na uongozi tupate prem numbers za watoto. Madam akaniambia analishughulikia but akaniambia kwa wakati huo wa likizo watoto wanatakiwa kuwa shuleni hivyo ninatakiwa kulipa shilingi elfu themanini ambayo kama ilivyo kuwa siku zote alitaka niilipe kupitia simu yake. Lakini Mimi nilimwambia Nina wachukua watoto waje Dar ili niwe nao kwa ukaribu zaidi. Akasema sawa atashughulikia suala la uhamisho. Siku iliyo fuata nikampigia sikumpata nikaona nimtume mdogo wangu aende kuchukua namba za mwalimu mkuu wa shule.

Nilipo ongea na mwalimu mkuu wa shule cha kushangaza akasema huyo madam sio mwalimu wa hapo kwa zaidi ya miezi miwili na kwamba amewaliza wazazi wengi ambao walikuwa wanampa pesa yeye. Nikauliza sasa kuhusu haki za watoto wangu vipi kwa sababu ninataka kuwahamisha ma huyo mwalimu alikuwa mwajiriwa wao wanatusaidia vipi sisi wazazi tulio muamini na kumlipa pesa zetu?

Pili nikamwambia atazame kama watoto wamesajiliwa kwa sababu nilimpa shilingi laki moja na elfu sitini kama gharama za usajili kwa kila mtoto.

Niliogopa sana nilihisi huenda hata hiyo shule yenyewe haina usajili.

Mkuu akasema wacha atazame kuhusu status ya wanafunzi hao pamoja na rekodi zao za ada.

Kuhusu status ya usajili akasema watoto wote wana prem numbers ingawa gharama za kuwasajili pia nilipigwa.

Kuhusu ada nikaambiwa nadaiwa shilingi milioni moja na laki 2 kwa sababu tangu watoto waanze kusoma kwenye shule hiyo hawajawahi lipa hata senti tano.

Nikajiuliza how comes mnasema watoto hawajawahi lipa hata senfi wakati hadi matokeo ya watoto yapo nyumbani.

Walifanya vipi mitihani bila kulipa hata senti 5?

Walipata vipi prem numbers kama hawajawahi kulipa hata senti tano?

Nilifadhaika sana na nilianza kukosa imani na hiyo shule kabisa.

Niliwaagiza watoto wangu Dar then nika watafutia shule ya kawaida ya kiswahili. Nili ichagua shule hii kwa sababu ipo karibu na mahali ninapo ishi lakini pili sina uwezo wa kulipa kwenye shule za English Medium kwa sababu ya kupanda kwa gharama za maisha na uwezo wangu kifedha kushuka na sapoti ya baba watoto imekuwa ndogo.

Kingine nilikosa kabisa imani na shule za English Mediums hasa hizi zinazo Anza Anza zenye wanafunzi wachache. Bado nilikuwa na kidonda kibichi kutoka kwa shule hiyo waliyo soma watoto wangu.

Nilipata nafasi kwenye shule ya kiswahili huku nikipambana kuomba shule waliyo kuwa wanasoma wawahamishe wanangu kwenye mfumo wawatoe kwenye shule yao wawahamishie kwenye shule hii mpya. Lakini cha ajabu muda wote wamekuwa wakinipiga danadana wanadai niwalipe pesa ambayo kiufupi hawanidai.

Sasa hivi darasa la nne wapo kwenye usajili wa mitihani ya taifa huyu mwanangu jina lake bado linasoma kwenye shule aliyo toka.

Walimu wanasema asipo hamishwa ndani ya deadline maana yake ni kwamba atatakiwa kwenda kufanya mtihani kwenye shule ile ile ambayo ni ya kiingereza au atatakiwa kurudia shule na kama akirudia basi prem number yake itaendelea kusoma juu yani itaonekana yupo darasa la 5 wakati yupo darasa la 4 yani kiufupi ndoto za mwanangu kitaaluma ndio zinakuwa zimeishia hapo. Sasa Mimi naomba msaada wa mamlaka zinazo husika zinisaidie ili mtoto wangu apewe haki yake ya kufanya mtihani wake wa darasa la 4 ambayo inataka kupokwa na wamiliki wa shule aliyo toka bila justification yoyote. Sheria na taratibu za elimu ya Tanzania zina kataza mtoto kunyimwa haki ya kufanya mtihani kwa sababu yoyote ile inayo husiana na fedha. Uongozi wa hiyo shule ya English Medium unataka kuvunja sheria hii kwa kumkosesha mwanangu haki yake ya kufanya mitihani ya darasa la nne kwa sababu ya deni hewa. Mtoto wangu ameshinda analia siku nzima ya leo anauliza sasa mama itakuwaje..

Naomba msaada tafadhali. Namba za huyo mwalimu alie kuwa anachukua ada zipo namba za mkurugenzi wa shule zipo namba za mkuu wa shule zipo na risiti zote ambazo zilikuwa zinaandikwa kwamba mwanangu amelipa ada pia zipo kwa bibi wa watoto. Nipo tayari kuziwasilisha risiti hizo mbele ya uongozi wa shule kama zikihitajika ila kwa sasa ninacho hitaji ni mtoto wangu apewe haki yake ya kufanya mtihani wake wa darasa la nne.

Uwepo wa namba za huyo mwalimu alie kuwa anachukua hela zangu pamoja na as wazazi wengine utarahisisha kukamatwa kwa huyo mwalimu ili alipe hizo pesa alizo Chukua. Niliwaambia uongozi wa shule wanisaidie huyo mwalimu akamatwe lakini wamekuwa wanapiga danadana kana kwamba wana mkingia kifua au wana ogopa kuchafua taswira ya shule yao.

Naomba msaada pia huyu madamu akamatwealipe hizo hela alizo Kula lakini wakati zoezi la kumtafuta na kumuweka ndani huyu madamu linaendelea naomba watoto wangu wapewe haki yao ya uhamisho.

Serikali waki hitaji ni disclose taarifa za hiyo shule pamoja na majina ya huyo madam wanae sema amekimbia na hela pamoja na majina ya uongozi nipo tayari kufanya hivyo.

Yericko Nyerere

Mh.
Dkt. Gwajima D
Lipa ada ya watu ndo uwahamishe watoto. Utaratibu wa kulipa ada kote unajulikana, unalipa kwa control number au account ya benki au kwa Cashier na unachukua risiti. kama wewe ulikuwa unatuma kwa shosti yako hiyo ni hela yenu ya matanuzi wewe na shost yako. Kalipe ada ya watu upate uhamisho wa watoto.
 
Back
Top Bottom