Makapuku Forum

Makapuku Forum

Furahiday; Muziki, Kula, Kunywa na Kufurahika.

Ni siku nzuri katika wiki, wengine huifanya kuwa nusu siku na wingine japo ni siku kama siku nyingine lakini hii ni Furahiday.

Tunafunga kazi, tunafunga ripoti, tunakusanya assignment na kupanga plans za kufanya tunapopumzika. Katika kufanya mipango, nami nina mipango yangu ambayo haiwezi kuwa na sawa na yako. Ila tukikutana hapa mida hii unaujua kabisa mpango ninaouleta hapa, muziki. Na hasa sauti ya gitaa katika muziki.

Kizuri zaidi mdau Sweetiepie kaahidi kuanza kuporomosha nyimbo siku za wikend ikihusisha mwisho wa mwisho wa wiki. Tusubiri.

Jioni hii hebu tubakie hapa hapa Afrika na kuwatizama wapigaji gitaa maarufu wa miziki ya bendi na hata 'binafsi'. Na tunamwangalia gwiji kweli kweli aliyekubalika na wote waongea kiingereza, kifaransa, kiswahili na ligha nyingine nyingi za kiafrika. Huyu ni Francois Luambo Luanzo Makiadi almaarufu Franco.

Kwa tuliokuwa tunakuwa miaka ya 90 tunakumbuka namna nyimbo za gwiji huyu zilivyotawala vituo vya radio nchini. wimbo wa Mario kwa mfano, ulikuwa na sifa kubwa hapa nchini kama ilivyo kwa karibu ukanda wote wa kusini mwa Afrika.

Franco anajulikana pia kwa kuwa na nyimbo ndefu sana, wimbo Kimpa Kisangameni unapanda mwendo kasi toka Masasi kwenda Lindi na ukifika Mnazi Mmmoja ndo kwanza korasi ya kwanza ndo inaishi na wimbo unakorasi zinazofuatana, Kulwa, Dotto na Shija.

Alitoa album zaidi ya 150 na nyimbo alizotunga yeye ziko kama 1000+. Huyu ndiye Franco rafiki wa iliyokuwa Zaire ya Mobutu.

Alifariki mwaka 1989 na serikali ilitangaza siku nne za maombolezo huku kituo cha redio ya taifa kikipiga nyimbo zake asubuhi hadi jioni.

Hapa tumwangalie na wimbo wake Mario, mwingine aliyeimba nanye ni almaarufu Madillu System, lakini kikubwa sikiza alivyokuwa akidonoa gitaa lake kwa mtindo wa Afro-Cuban , kupanda na kushuka kwa tone ya nyuzi.

Wikend Njema Makapuku


Binamu santeee kwa music mzuri
 
Aunt yangu utanikondesha roho hakyanani, kila nikikugoogle naambiwa not richabo, link umekata, pm umesiliba yaani basi tu nikawa nakukumbuka kimoyomoyo. U khali gani wangu?

SN (serious note): Tulikumiss humu, na mimi nilikumiss zaidi
niliwamiss sana binamu nilikua naumwa vipi unaendeleaje mama mchuchu vipi anaendeleaje
 
4/Curtis James Jackson III
7d4dd499f684e7108ae2a940f81948a6.jpg
dcadebd80d30fba9412538ef84fcc37e.jpg
801c59acd497cc7c177e8eba440a8c60.jpg
Nani asiyemfahamu huyu Mswahili?
Anajiita 50 Cent ana umri wa miaka 38
Utotoni alikulia katika umaskini uliotopea ikiwemo kulelewa na bibi yake.
Anewahi kutandikwa risasi lakini akapona.
Ana dili kibao za kuvutia mpunga
Ana utajiri wa USD 240 Milioni
.......
usikute mjumba mkubwa kama huu wanaishi watu watatu tu ndani!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom