Makapuku Forum

Makapuku Forum

1/Andre Romelle Young
bfe00a6ac2aca64b192cf9d20ca1c24a.jpg
1d90aca69f620db62c7a061783b69cc1.jpg
bb80c029189e7f6cec64fa5ed15fa7f6.jpg
Huyu jamaa huko kwa Trump nu kama Mkubwa Fella wasanii kibao wamepitia kwake
Ni prodyuza abayefahamika kwa jina la Dr Dre jamaa kweli ni daktari wa muziki
Ana umri wa miaka 49
Anamiliki studio na vitega uchumi kibao
Ana utajiri wa USD 790 Milioni
.
.
.
.
.
.
.Shukrani kwa mliosapoti mada
Tukutane Jumatatu
Mwisho
..............
Ubarikiwe
 
10/Dwayne Michael Carter Jr
8e30dd29d888e6986b37d5f9e20f8386.jpg
5ff73d5f07da0b5492c2d091c29504a8.jpg
59f223b0df92ed07e2a4507d2bcc3890.jpg
Ana umri wa miaka 31
Anajulikana zaidi km Lil Wayne hakuna mtu anayefuatilia muziki wa mamtoni asiyemfahamu
Anaingiza mkwanja mrefu kutokana na kazi yake ya usanii pia anajishughulisha na biashara mbalimbali mfano mavazi n.k
Anajadiriwa kuwa na utajoli wa USD 100 milioni
.....
duuh! hili lijamaa lipo kwenye kumi bora
salute kwa wayne
 
Bandiko zuri changamshi as usual. Wengi hudhani kwamba Mamou pengine ndiyo wimbo wake bora kabisa kisanaa. Vocals zake na Madilu wakijibizana zinaweza kukutia simanzi na kukusisimua hata kama hujui kinachoimbwa. Mwanafunzi mmoja wa Musicology alikuwa anadai hivyo katika tasnifu yake ya Masters katika Chuo Kikuu kimoja huko Ujerumani. Nilishindwa kufuatilia hoja zake za kitaalamu kwa sababu sijui cho chote kuhusu taaluma ya muziki.
 
Furahiday; Muziki, Kula, Kunywa na Kufurahika.

Ni siku nzuri katika wiki, wengine huifanya kuwa nusu siku na wingine japo ni siku kama siku nyingine lakini hii ni Furahiday.

Tunafunga kazi, tunafunga ripoti, tunakusanya assignment na kupanga plans za kufanya tunapopumzika. Katika kufanya mipango, nami nina mipango yangu ambayo haiwezi kuwa na sawa na yako. Ila tukikutana hapa mida hii unaujua kabisa mpango ninaouleta hapa, muziki. Na hasa sauti ya gitaa katika muziki.

Kizuri zaidi mdau Sweetiepie kaahidi kuanza kuporomosha nyimbo siku za wikend ikihusisha mwisho wa mwisho wa wiki. Tusubiri.

Jioni hii hebu tubakie hapa hapa Afrika na kuwatizama wapigaji gitaa maarufu wa miziki ya bendi na hata 'binafsi'. Na tunamwangalia gwiji kweli kweli aliyekubalika na wote waongea kiingereza, kifaransa, kiswahili na ligha nyingine nyingi za kiafrika. Huyu ni Francois Luambo Luanzo Makiadi almaarufu Franco.

Kwa tuliokuwa tunakuwa miaka ya 90 tunakumbuka namna nyimbo za gwiji huyu zilivyotawala vituo vya radio nchini. wimbo wa Mario kwa mfano, ulikuwa na sifa kubwa hapa nchini kama ilivyo kwa karibu ukanda wote wa kusini mwa Afrika.

Franco anajulikana pia kwa kuwa na nyimbo ndefu sana, wimbo Kimpa Kisangameni unapanda mwendo kasi toka Masasi kwenda Lindi na ukifika Mnazi Mmmoja ndo kwanza korasi ya kwanza ndo inaishi na wimbo unakorasi zinazofuatana, Kulwa, Dotto na Shija.

Alitoa album zaidi ya 150 na nyimbo alizotunga yeye ziko kama 1000+. Huyu ndiye Franco rafiki wa iliyokuwa Zaire ya Mobutu.

Alifariki mwaka 1989 na serikali ilitangaza siku nne za maombolezo huku kituo cha redio ya taifa kikipiga nyimbo zake asubuhi hadi jioni.

Hapa tumwangalie na wimbo wake Mario, mwingine aliyeimba nanye ni almaarufu Madillu System, lakini kikubwa sikiza alivyokuwa akidonoa gitaa lake kwa mtindo wa Afro-Cuban , kupanda na kushuka kwa tone ya nyuzi.

Wikend Njema Makapuku


Asante Obe
 
Namkubali sana huyu Mzee japo sijafanikiwa kuishi zama zake. Kuna kibao chake aliimba kwa Kiswahili na Sam Mangwana pia nakikubali mno.


Mdau, wimbo huo ulikuwa na utabaki kuwa mzuri wakati wote. Sauti ya Mangwana na gitaa la Franco yalilandana sana....
"'muongo na mlozi ni watu wa kuchomwa.....Franco.....ukipata taabu omba kwa Mungu..."

Hii hapa clip ya YouTube wimbo huo unaitwa Toujours OK (For Ever)

 
zipo hapo kwa udhamini wako

kuhusu isha naona kashapata yule aliyekuwa akimtafuta kule tulipomkuta

tangu anipe cha mbavu sijamuona mpk leo na sio kawaida yake ilikuwa haipiti wiki lazima aje kusalimia, labda yupo kwenye fungate
hahahhh atakua amempata aliyekua anamtafuta
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom