Mama Mchungaji. Umegusia Falsafa kabisa ya maisha yangu. Kwa vile nimeshafanikiwa kuacha kunywa pombe sasa bajeti yangu ina nidhamu sana. Lile fungu la 10 mimi hulitumia katika kusaidia wenzangu wenye shida moja kwa moja.
Ukienda huko mahospitalini ndo utaona bahati uliyonayo kwamba ungali na afya. Kuna binadamu huko wana magonjwa sugu na wengine wameshakata tamaa. Wengine ni masikini kabisa na wameshatelekezwa na familia zao. Wako huko mahospitalini wanasubiri kufa. Hawa hata ukimpa elfu moja unamuona anatoa machozi. Ukimpelekea matunda, sabuni, blanketi na hata mafuta ya kujipaka tu anakuona kama malaika. Na cha muhimu zaidi ni maongezi na upendo wa kibinadamu. Kuonyesha kuwa unawajali. Kuwapa matumaini kuwa Mungu bado Anawapenda. Kwamba waweke matumaini katika Yeye Aliyewafia. Kwamba kila kitu kitakuwa sawa.
Ninayo mifano mingi ya watu hawa na kusema kweli ndiyo wamebadilisha mtazamo wangu kuhusu maisha. Kuwasaidia hawa wenye shida kusema kweli ndiyo dini ya kweli.
Halafu mwalimu wangu mmoja hapa alitusisitiza sana kuwa kila siku angalau tufanye tendo moja jema kwa mtu mwingine - random act of kindness. Hii yaweza kuwa maneno ya kutia moyo, kusali pamoja na/au pesa kidogo. Mfano upo kwenye daladala na nyuma yako amekaa bibi kizee. Basi unamlipia nauli kwa siri. Na akifikiwa konda akimwambia bibi wewe nauli yako kuna mtu huko mbele kakulipia. Kitendo kidogo hiki lakini kinaweza kubadilisha siku ya mtu kabisa. Siku moja pale posta mpya kwenye matope mzee mmoja akakatikiwa na kandambili zake. Kwa pembeni pale kulikuwa na machinga anauza open shoes za ngozi. Basi nikamwambia mzee yule achague open shoes za ngozi imara. Alipigwa na butwaa na hakuamini mpaka akaanza kulia. Alichagua viatu imara, mimi nikamlipa yule mmachinga nikaondoka zangu. Ni matendo madogo madogo kama haya yanayotendwa kwa moyo mweupe bila kutegemea malipo wala fadhila ndiyo yanaweza kuuonyesha upendo wa Mungu kwa binadamu wenzetu. Na kupitia kwayo ndiyo tunaweza kupata ridhiko la kweli na thamani halisi ya maisha yetu. Asante sana mama Mchungaji kwa kutukumbusha wajibu huu mtakatifu. Mungu na Atusaidie tupunguze ubinafsi na kiburi cha kibinadamu. Good night!