Makapuku Forum

Makapuku Forum

Ishi na watu kwa wema utafurahia muziki

Najua tumekuwa na wakti mzuri na tunapoenda kuimaliza Jumatano hii basi kama kawaida Makapuku nawakaribisha katika ka-kipengele haka ka ala za muziki na hasa tukijikita katika udonoaji na wadonoaji wa gitaa.

Kwa wapenzi wa muziki wa dansi miaka 20 nyuma, na wanaofuatilia miziki ya bakulutu, bendi ya Maquis Original ni bendi yenye umaarufu mkubwa hapa nchini ikiundwa na wanamuziki wengi toka Kongo na mmoja wao ni mpiga gitaa maarufu Dekula Kahanga almaarufu Vumbi. Mitindo kama Zembwela na Sendema haiwezi kukutoka kiurahisi.

Sikiza vibao cha Ngalula, Mayanga, Makumbele, Karubandika na vingine vingi katika mitindo ya Sendemaa na Zembwela. Gitaa utakalosikia linamuongoza muimbaji awe ni Tshimanga Assossa au Kasaloo basi ni la nguli Dekula Kahanga.

Bado yupo na anafanya muziki wake nchini Sweden akiwa na band yake ya Dekula Band.

Hapa nakuwekea baadhi ya nyimbo alizoweza kuzicharaza na kuzifanya zikavutia zaidi.

FYI: Upigaji wake mzuri umechangiwa zaidi na kufuatisha mipigo ya Nguza Viking (yupo jela sasa akitumikia adhabu ya maisha gerezani)

Dekula anaamini katika kuishi vizuri na watu, kwani huwezi kujua maisha yatakupeleka wapi.

hapa najiuliza nikuache na Ngalula au nitupie clip ya YouTube ambayo anacharaza baadhi ya nyimbo zake, isiwe ishu, nakuacha na zote mbili, suala la kukumalizia MB zako mpenzi msomaji liko nje ya uwezo wangu (joke)





Asante Obe mimi kwangu hii yapili haifunguki ya kwanza nimechezaaaaaa nimekumbuka mbali sana hahaha
 
Haya basi nimebwaga manyanga. Ye yote tu atafaa ila mtafutie kwanza Shedede. Ukimalizana naye basi ndo uanze kumhangaikia Msukuma wako mbishi...
fbf4c672b2fd77177ad967bffcc52e6f.jpg
Huo ni mwili wake kweli mbona kama kajazwa jazwa as a toy?
 
Ishi na watu kwa wema utafurahia muziki

Najua tumekuwa na wakti mzuri na tunapoenda kuimaliza Jumatano hii basi kama kawaida Makapuku nawakaribisha katika ka-kipengele haka ka ala za muziki na hasa tukijikita katika udonoaji na wadonoaji wa gitaa.

Kwa wapenzi wa muziki wa dansi miaka 20 nyuma, na wanaofuatilia miziki ya bakulutu, bendi ya Maquis Original ni bendi yenye umaarufu mkubwa hapa nchini ikiundwa na wanamuziki wengi toka Kongo na mmoja wao ni mpiga gitaa maarufu Dekula Kahanga almaarufu Vumbi. Mitindo kama Zembwela na Sendema haiwezi kukutoka kiurahisi.

Sikiza vibao cha Ngalula, Mayanga, Makumbele, Karubandika na vingine vingi katika mitindo ya Sendemaa na Zembwela. Gitaa utakalosikia linamuongoza muimbaji awe ni Tshimanga Assossa au Kasaloo basi ni la nguli Dekula Kahanga.

Bado yupo na anafanya muziki wake nchini Sweden akiwa na band yake ya Dekula Band.

Hapa nakuwekea baadhi ya nyimbo alizoweza kuzicharaza na kuzifanya zikavutia zaidi.

FYI: Upigaji wake mzuri umechangiwa zaidi na kufuatisha mipigo ya Nguza Viking (yupo jela sasa akitumikia adhabu ya maisha gerezani)

Dekula anaamini katika kuishi vizuri na watu, kwani huwezi kujua maisha yatakupeleka wapi.

hapa najiuliza nikuache na Ngalula au nitupie clip ya YouTube ambayo anacharaza baadhi ya nyimbo zake, isiwe ishu, nakuacha na zote mbili, suala la kukumalizia MB zako mpenzi msomaji liko nje ya uwezo wangu (joke)






Video ya pili mkuu iko cracked
7711db2b953a3136019a0a53e10617c4.jpg
 
  • Thanks
Reactions: Obe
Hakuna kitu kinacholeta faraja na furaha kama kusaidia wahitaji hata kama huna kitu,kushare kidogo ulichonacho na wale ambao hawana kabisa imagine unaenda hospital kumtembelea ndugu yako amelazwa mnajikuta mko 20 mmezunguka kitanda ,lakini next bed kuna mtu kapata referal kuja muhimbili hana ndugu hebu sogea tumia muda nae,ongea nae mpe kidogo ulichonacho aaah huwezi amini utakuwa unatafuta safari a kutembelea watu wa aina hii na hutapungukiwa,nauli,cha kuwapa hata neno la kuwatia moyo .hata majumbani wapo wengi wanahitaji faraja ,kutiwa moyo,kusikilizwa pata muda wa kuwaona watu hawa wapo wengi sana Mungu atutie nguvu

Nehemia 8

10b....furaha ya BWANA ni nguvu zenu.

Haleuiya

MATENDO YA MITUME 20

35.Katika mambo yote nimewaonyesha ya kuwa kwa kushika kazi hivi imewapasa kuwasaidia wanyonge,na kuyakumbuka maneno ya Bwana Yesu ,jinsi alivyosema mwenyewe. Ni heri kutoa kuliko kupokea
Mama Mchungaji. Umegusia Falsafa kabisa ya maisha yangu. Kwa vile nimeshafanikiwa kuacha kunywa pombe sasa bajeti yangu ina nidhamu sana. Lile fungu la 10 mimi hulitumia katika kusaidia wenzangu wenye shida moja kwa moja.

Ukienda huko mahospitalini ndo utaona bahati uliyonayo kwamba ungali na afya. Kuna binadamu huko wana magonjwa sugu na wengine wameshakata tamaa. Wengine ni masikini kabisa na wameshatelekezwa na familia zao. Wako huko mahospitalini wanasubiri kufa. Hawa hata ukimpa elfu moja unamuona anatoa machozi. Ukimpelekea matunda, sabuni, blanketi na hata mafuta ya kujipaka tu anakuona kama malaika. Na cha muhimu zaidi ni maongezi na upendo wa kibinadamu. Kuonyesha kuwa unawajali. Kuwapa matumaini kuwa Mungu bado Anawapenda. Kwamba waweke matumaini katika Yeye Aliyewafia. Kwamba kila kitu kitakuwa sawa.

Ninayo mifano mingi ya watu hawa na kusema kweli ndiyo wamebadilisha mtazamo wangu kuhusu maisha. Kuwasaidia hawa wenye shida kusema kweli ndiyo dini ya kweli.

Halafu mwalimu wangu mmoja hapa alitusisitiza sana kuwa kila siku angalau tufanye tendo moja jema kwa mtu mwingine - random act of kindness. Hii yaweza kuwa maneno ya kutia moyo, kusali pamoja na/au pesa kidogo. Mfano upo kwenye daladala na nyuma yako amekaa bibi kizee. Basi unamlipia nauli kwa siri. Na akifikiwa konda akimwambia bibi wewe nauli yako kuna mtu huko mbele kakulipia. Kitendo kidogo hiki lakini kinaweza kubadilisha siku ya mtu kabisa. Siku moja pale posta mpya kwenye matope mzee mmoja akakatikiwa na kandambili zake. Kwa pembeni pale kulikuwa na machinga anauza open shoes za ngozi. Basi nikamwambia mzee yule achague open shoes za ngozi imara. Alipigwa na butwaa na hakuamini mpaka akaanza kulia. Alichagua viatu imara, mimi nikamlipa yule mmachinga nikaondoka zangu. Ni matendo madogo madogo kama haya yanayotendwa kwa moyo mweupe bila kutegemea malipo wala fadhila ndiyo yanaweza kuuonyesha upendo wa Mungu kwa binadamu wenzetu. Na kupitia kwayo ndiyo tunaweza kupata ridhiko la kweli na thamani halisi ya maisha yetu. Asante sana mama Mchungaji kwa kutukumbusha wajibu huu mtakatifu. Mungu na Atusaidie tupunguze ubinafsi na kiburi cha kibinadamu. Good night!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom