Morning too papaaGoodmorning family
1992 - Thibaut Courtois anazaliwa.
Kipa namba 1 wa Chelsea na timu ya taifa ya Ubelgiji.
1981 - Mwanamuziki mashuhuri wa Regge na Mwanaharakati kutoka Jamaica, Robert Nesta ' Bob ' Marley anafariki Dunia.
Mmoja kati ya watu maarufu katika karne ya 20.
Alifariki kutokana na kansa. Aliacha watoto 13 kutoka kwa mama watatu.
Alizikwa kitaifa siku 10 baadae huko Kingston, Jamaica.
Alifariki akiwa na miaka 36, na kuwa mmoja kati ya watu maarufu kufariki kabla ya kufikisha miaka 50.
Pamoja na kwamba leo ni miaka 36 toka afariki lakini bado amebakia kuwa maarufu utadhani amefariki mwaka jana.
Morning shemelaGoodmorning family
Mwenyewe banaa
Haya basi nimebwaga manyanga. Ye yote tu atafaa ila mtafutie kwanza Shedede. Ukimalizana naye basi ndo uanze kumhangaikia Msukuma wako mbishi...![]()

1996 - Nnamdi Azikiwe anafariki Dunia.
Ni Rais wa kwanza wa Nigeria.
Kwa heshina yake, kuna mtaa hapa Dar Es Salaam umepewa jina lake kama kumuenzi, mtaa wa Azikiwe.
Yuko vizuri. Nilijaribu kujifunza kupiga gitaa. Aisee ni gumu balaa hata wiki sikumaliza nikasarenda...
Sijajua chanzo hasa ni nini?![]()
![]()
Ni bahati mbaya au hujuma?
......
Ishi na watu kwa wema utafurahia muziki
Najua tumekuwa na wakti mzuri na tunapoenda kuimaliza Jumatano hii basi kama kawaida Makapuku nawakaribisha katika ka-kipengele haka ka ala za muziki na hasa tukijikita katika udonoaji na wadonoaji wa gitaa.
Kwa wapenzi wa muziki wa dansi miaka 20 nyuma, na wanaofuatilia miziki ya bakulutu, bendi ya Maquis Original ni bendi yenye umaarufu mkubwa hapa nchini ikiundwa na wanamuziki wengi toka Kongo na mmoja wao ni mpiga gitaa maarufu Dekula Kahanga almaarufu Vumbi. Mitindo kama Zembwela na Sendema haiwezi kukutoka kiurahisi.
Sikiza vibao cha Ngalula, Mayanga, Makumbele, Karubandika na vingine vingi katika mitindo ya Sendemaa na Zembwela. Gitaa utakalosikia linamuongoza muimbaji awe ni Tshimanga Assossa au Kasaloo basi ni la nguli Dekula Kahanga.
Bado yupo na anafanya muziki wake nchini Sweden akiwa na band yake ya Dekula Band.
Hapa nakuwekea baadhi ya nyimbo alizoweza kuzicharaza na kuzifanya zikavutia zaidi.
FYI: Upigaji wake mzuri umechangiwa zaidi na kufuatisha mipigo ya Nguza Viking (yupo jela sasa akitumikia adhabu ya maisha gerezani)
Dekula anaamini katika kuishi vizuri na watu, kwani huwezi kujua maisha yatakupeleka wapi.
hapa najiuliza nikuache na Ngalula au nitupie clip ya YouTube ambayo anacharaza baadhi ya nyimbo zake, isiwe ishu, nakuacha na zote mbili, suala la kukumalizia MB zako mpenzi msomaji liko nje ya uwezo wangu (joke)

AmenHakuna kitu kinacholeta faraja na furaha kama kusaidia wahitaji hata kama huna kitu,kushare kidogo ulichonacho na wale ambao hawana kabisa imagine unaenda hospital kumtembelea ndugu yako amelazwa mnajikuta mko 20 mmezunguka kitanda ,lakini next bed kuna mtu kapata referal kuja muhimbili hana ndugu hebu sogea tumia muda nae,ongea nae mpe kidogo ulichonacho aaah huwezi amini utakuwa unatafuta safari a kutembelea watu wa aina hii na hutapungukiwa,nauli,cha kuwapa hata neno la kuwatia moyo .hata majumbani wapo wengi wanahitaji faraja ,kutiwa moyo,kusikilizwa pata muda wa kuwaona watu hawa wapo wengi sana Mungu atutie nguvu
Nehemia 8
10b....furaha ya BWANA ni nguvu zenu.
Haleuiya![]()
![]()
MATENDO YA MITUME 20
35.Katika mambo yote nimewaonyesha ya kuwa kwa kushika kazi hivi imewapasa kuwasaidia wanyonge,na kuyakumbuka maneno ya Bwana Yesu ,jinsi alivyosema mwenyewe. Ni heri kutoa kuliko kupokea
Atakuwa amemshusha Manyau mtaa wa sita!!!Matokeo ya mechi zilizochezwa jana
England EPL
Arsenal ana matumaini ya kucheza UCL![]()
Safi za wewe?
Pamoja mkuuAsante mkuu Mussolin5 kwa historia ubarikiwe.