Makapuku Forum

Makapuku Forum

1981 - Mwanamuziki mashuhuri wa Regge na Mwanaharakati kutoka Jamaica, Robert Nesta ' Bob ' Marley anafariki Dunia.

Mmoja kati ya watu maarufu katika karne ya 20.

Alifariki kutokana na kansa. Aliacha watoto 13 kutoka kwa mama watatu.

Alizikwa kitaifa siku 10 baadae huko Kingston, Jamaica.

Alifariki akiwa na miaka 36, na kuwa mmoja kati ya watu maarufu kufariki kabla ya kufikisha miaka 50.

Pamoja na kwamba leo ni miaka 36 toka afariki lakini bado amebakia kuwa maarufu utadhani amefariki mwaka jana.
 
1960 - Huko Argentina: Makachero wanne wa Shirika la Upelelezi la Mossad la nchini Israel wanamkamata Luteni Kanali Adolf Eichman wa Jeshi la Nazi la Kijerumani aliyekuwa anaishi mafichoni huku akitumia jina la Ricardo Klement.

Adolf Eichman ni mmoja ua makamanda katika jeshi la Nazi la Hitler lililohusika na Mauaji ya Maelfu ya Wayahudi.

Eichman alienda kunyongwa kama hukumu baada ya kupatikana na hatia.
99fea8ffc5f048201d84207e5e6a54f9.jpg
7d2a5624ee932fcd89a7ebc74775811f.jpg
79a375a3793dd7216d3a4ca486bf12e4.jpg

Bora hata Joseph Goebbels akiamua kujiua baada ya kuzingirwa kuliko kuaibishwa na kutundikwa kama paka
...
..
 
1984 - Andres Iniesta anazaliwa.

Kiungo mshambuliaji Barcelona na timu ya taifa ya Spain.

Mmoja kati ya viungo bora kabisa kuwahi kutokea katika uso wa Dunia. Kombinesheni yake na Xavi Hernandez ilikuwa ya kusisimua na iliyowaacha wapinzani wasijue wamkabe yupi wamuache yupi.

Ni mfungaji wa goli pekee lililoipa Spain kombe la Dunia mwaka 2010 pale Afrika ya Kusini.

Ni mmoja kati ya wachezaji wachache duniani ambao wameshinda kila kombe kwa ngazi ya vilabi na timu ya taifa.
HBD Andres Iniesta
 
1989 - Giovani Dos Santos anazaliwa.

Winga wa zamani wa Barcelona, Toylttenham, Villareal ambaye kwa sasa anachezea LA Galaxy na timu ya taifa ya Mexico.

Mmoja kati ya wachezaji wenye vipaji maridhawa kutoka Akademi ya La Masia ya Barcelona.

Mpaka leo wachambuzi wa soka wanashindwa kujua ni kwanini Dos Santos alipotea kwenye soka mapema sana licha ya kipaji cha hali ya juu alichobarikiwa.
HBD Giavon Dos Santos
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom