Makapuku Forum

Makapuku Forum

e7097c36e82740e4fa958b9c27e22789.jpg
3253f6305a911f7951644c31439f3538.jpg

Neno
"Dikteta" wamelipachika Wamarekani tu....namfahamu zaidi Bikteta Ceorge W Bush
........
Kweli hakuna haki hapa duniani. Leo nchi yote imeparaganyika. Na bado wakafanya lile lile kwa Gaddafi. Jamaa wala hawajifunzi kutokana na makosa yao. Hata hayo mafuta waliyokuwa wanayatafuta hawajaweza kuyapata. Wameishia kuharibu nchi na kuua mamilioni ya watu bure.
40bc1a2d54d3a19bff55620552f720bd.jpg
 
NUKUU YA LEO

Democracy is beautiful in theory: in practice it is fallacy

Demokrasia ni nzuri katika nadharia, katika vitendo ni Uongo

362b0125f1ba9a740a97042fb0b0eb40.jpg

Haya maneno yaliwahi kutamkwa na mwandishi, mwanasiasa na waziri Mkuu wa 27 wa Italia Bw. Benito Andre mussolini aliezaliwa 29/07/1883 na kufariki 28/04/1945 kwa kupigwa risaasi kijijini Giulino de mezzegra akiwa na mkewe Clara Petacci.

Musollini alikuwa ni kiongozi wa Partio Nazionale Fascista; PNF , chama ambacho kiliweka demokrasia pembeni na kutekeleza sera za kidikteta zilizojulikana kama II Duce.

Mussolini amepigana vita kama vita vya 1 na vya 2 vya Dunia, Vita ya Italia-Ethiopia na Uvamizi wa Itali nchini Albania.

Kiufupi mussolini hakupenda demokrasia hata kidogo na hivyo hakupenda kuwa muongo

Alisema kile alichokiamini yeye..

Lakini katika uhalisia wa ukweli hakuna demokrasia ya kweli..hata wale wanaodai kuwa na demokrasia nchini mwao ni waongo manake kuna vitu vinafanyika havihitaji demokrasia..

Penda usipende kuna vitu vitafanywa na kikundi cha watu wachache bila maamuzi yako.

064949a6396b35b885086d1ebde90cd5.jpg
1ebd5b6274d5a011bf7dedbdd8d26e53.jpg

d4d6c664d073e6d4ccc31791926418a8.jpg

Kuna mengi kuhusu mussolini lakini nitaweka nyama baadaye..

Morning wakuu.
Ila "madikteta" mara nyingi huwa na mwisho mbaya sana kihistoria na vinginevyo sijui kwa nini. Kuna documentary moja hapa ya Hitler na jinsi alivyomtumia huyu jamaa kivita ilinishangaza sana.
 
Ndio yeye mkuu
KK is also an intellectual. Nilihudhuria warsha yake moja na nilifurahishwa sana na uwezo wake wa kujenga hoja mpaka maprofesa wakawa wanamshangaa. First generation ya viongozi wa Afrika ambayo haitasahaulika. Angalau walikuwa na idea walichotaka kufanya na japo hawakufanikiwa lakini angalau walijaribu na malengo yao na falsafa zao za kitaifa zilikuwa wazi. Siyo kama sasa hata haijulikani kinachoendelea...
 
Tongotongo la Asubuhi
c150ac590e0b0179e747b9a848a4d814.jpg

Mwaka 2010 katika hospitali moja huko London Uingerrza wsnandoa Wa Kinigeria walibahatoka kupata mtoto "mweupe" mwenye macho ya blue na ngozi nyeupe km wazungu
Wanandoa hao wote ni Waafrika weusi
Ingekuwa Bongo lingeibuka timbwili mpaka basi
Asubuhi njema
.............
Hapo talaka ingehusika
 
List ya nchi 5 zilizotumia fedha nyingi kwa ajili ya majeshi 2016
China-Parade.jpg

Inaelezwa kuwa sifa ya nchi yoyote ni uwezo wa Jeshi lake katika kujilinda na kupambana kwa ajili ya wananchi ambapo tumekuwa tukishuhudia gharama inayotumika kuhakikisha Idara hiyo inaimarika kwa kulipa mishahara minono na kununua vifaa vya kisasa.

Kwa mujibu wa Taasisi ya Kimataifa ya Utafiti wa Amani ya Stockholm ‘SIPRI’ zimetajwa nchi 5 zinazotumia fedha nyingi zaidi kwa ajili ya Jeshi hadi kufikia 2016 zikiongozwa na Marekani.

SIPRI imesema kuwa matumizi ya dunia katika majeshi yaliongezeka hadi Dollar 1.7 trillion mwaka 2016 ambapo Marekani inasalia kinara kwa kutumia fedha nyingi kwenye jeshi mwaka 2016 ambapo matumizi yameongezeka kwa 1.7% kuifanya ifikishe Dollar 611 billion.

China ilitumia Dollar 215 billion na kuifanya kukamata katika nafasi ya pili huku Urusi ikikamata nafasi ya tatu ikitumia Dollar 69.2 billion. Saudi Arabia inakamata nafasi ya nne ikitumia Dollar 63.7 billion na India katika nafasi ya tano ikitumia Dollar 55.9 billion.

Capture-13.png
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom