NUKUU YA LEO
Democracy is beautiful in theory: in practice it is fallacy
Demokrasia ni nzuri katika nadharia, katika vitendo ni Uongo
Haya maneno yaliwahi kutamkwa na mwandishi, mwanasiasa na waziri Mkuu wa 27 wa Italia Bw. Benito Andre mussolini aliezaliwa 29/07/1883 na kufariki 28/04/1945 kwa kupigwa risaasi kijijini Giulino de mezzegra akiwa na mkewe Clara Petacci.
Musollini alikuwa ni kiongozi wa Partio Nazionale Fascista; PNF , chama ambacho kiliweka demokrasia pembeni na kutekeleza sera za kidikteta zilizojulikana kama II Duce.
Mussolini amepigana vita kama vita vya 1 na vya 2 vya Dunia, Vita ya Italia-Ethiopia na Uvamizi wa Itali nchini Albania.
Kiufupi mussolini hakupenda demokrasia hata kidogo na hivyo hakupenda kuwa muongo
Alisema kile alichokiamini yeye..
Lakini katika uhalisia wa ukweli hakuna demokrasia ya kweli..hata wale wanaodai kuwa na demokrasia nchini mwao ni waongo manake kuna vitu vinafanyika havihitaji demokrasia..
Penda usipende kuna vitu vitafanywa na kikundi cha watu wachache bila maamuzi yako.
Kuna mengi kuhusu mussolini lakini nitaweka nyama baadaye..
Morning wakuu.