Makapuku Forum

Makapuku Forum

Ujuee nimeshangaaa kuona unaukana ukoo wetu wakati kwenye ukoo mim na Obe binamu ndo afwadhwariiii ....wewe kibokoooo unakombaaa kuanziaa mama mpka bibi mtu


...ha hahaha, unakumbuka kipindi kile ulipomsaidia asishikwe na sungusungu wa soko? Alimuumiza sana yule dada muuza karanga kwenye choo cha soko
 
Ikiwa kama lengo lako ni kusimama katika maisha itakuwa haina maana kukaa chini eti kwa kuhofia maneno ya watu au kuchekwa. Fahamu kuwa sio kila kitu unachokifanya kinatakiwa kiridhiwe na watu wote duniani hapana, kuna vyengine lazima vitapingwa tu hata kama unachokifanya kitakuwa na maana kiasi gani. Kupingwa katika maisha ni jambo ambalo halikwepeki hata kama utafanya wema na uzuri kiasi gani. Wengi wetu tumekuwa tunafuta ndoto zetu kwenye akili zetu kwa kuhofia maneno ya watu na vicheko vya watu. Kuna usemi unasema"Mapambano yoyote huwa hayana matokeo mwanzoni bali matokeo huwa mwishoni" Sasa itakuwa ni jambo la ajabu sana wewe kutaka katokeo mazuri mwanzoni mwamwapambano kabla ya kufika mwisho. Katika maisha unatakiwa kufahamu kuwa sio kila anguko la kiuchumi kwako ni mateso hapana, bali kuna maanguko mengine yanatokea kwako kwasababu maalumu na lengo maalumu. Muhimu na kinachotakiwa kufanywa ni wewe kuanza kurasa mpya kutokana na pale ulipodondoka punde tu utajiona umesimama sawa sawa. Unapoiyanza safari ya mafanikio basi tambua kuwa kuna mengi yatajitokeza katikati ya safari na hata mwisho wa safari. Ustahamilivu na kuishi kwenye adhima yako ndio kitu pekee kitakachokufanya umalize safari yako vyema ukiwa na matunda ya safari. Wazo kubwa lenye kutisha kwa wanaokuzunguka moyoni mwako lifanye kuwa dogo na weka matumaini kuwa litafanikiwa hata kama unaona kufanikiwa kwake kutachukuwa muda mrefu. TAFAKARI KWA KINA Maisha ni ustahamilivu
 
Hatakiwi kuvumilia mwanamke juu ya madhira na mahudhi ya mwanaume mshenzi ambae hajali familia yake wala hana mapenzi na mke wake. Kuwa mwanaume ni hadhi kubwa pia ni ujemadari wa hali ya juu sio rahisi kama wengi tunavyofikiria. Mwanaume anatakiwa awe na busara,heshima na ukereketwa wa dhati na familia yake wakati wote. Mwanaume ambae hana heshima wala huruma na familia yake huyo hana hadhi ya kuitwa mwanaume kamili. Tafsiri ya mwanaume inatakiwa ivae uhalisia wa hakika kwa kujituma na kijiumiza ilimladi tu familia yako ipate ahuweni ya maisha. Ulevi siku zote huwa unampa mtu tafsiri mbaya kwa Mungu na hata kwa watu wanaomzunguka. Maisha ya kuitesa familia na njaa na kutokuwapa mahitaji yao muhimu kwa kuthamini pole na uzinzi huu ni ujinga ngazi ya Phd. Mwanaume timamu na mwenye seli hai za kiume kamwe hawezi kufanya unyanyasaji na ukatili kiasi hichi. Yani unadiriki kumtukana mke wako na watoto wako kwasababu ya kuendekeza ulevi na marafiki wanaokubomoa fikra zako. Watoto wanahitaji mahitaji muhimu ya shule na ya kimaisha, lakini kutokana na uzwazwa wako hela unawanunulia marafiki pombe wakati huku familia yako inaumia kwa mateso yanayotokana na mkono wako. Mke hana nguo nzuri wala mpya, na si kuwa uwezo wa kumnunulia huna hapana, ila wenye haki ya kununuliwa na wewe ni wahudumu wa bar na sehemu za kujiuza. Inasikitisha sana kuona kuna familia zina wanaume wa aina hii. Ila kumbuka mateso yako unayowapiyitishia familia yako leo, kesho yatarudi mikononi mwako. TAFAKARI KWA KINA Mwanaume ni hekima sio kujaza mwili na vyuma
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom