THE DOM
Sehemu Ya 18
Mtunzi..... MoonBoy
Simu No. +255714419487 WhatsApp
Instagram....
Ilipoishia Jana →↓↓↓↓←
SON OF PRESIDENT GU
sikiliza we kaka, usitake kutuingiza majaribuni,... Sisi hatumjui huyo mtu"
Sasa sahi akakumbuka alimuulizaga jina yule dada siku ileee,
"enheeee, huyo mdada anaitwa sauda"
Sasa waliposikia jina la sauda, wenyewe walisikitika sana tena sana.
"we leah?? Sauda si yule mgeni wenu cha uvivu"
"ndio yeye, na siku anayo ongelea huyu kaka ndio siku ya kwanza sauda anaingia kazini"
Sasa huyu huyu leah ndio alikuwa anaishi na sauda, je atamjuaje kama huyu ndio aliokuwa anaishi nae
"pole sana kaka yangu kwa nitakayokwambia kuhusu huyo mdada unaemtafuta"
Aliongea leah huku akisikitika sana
"kwani kafanya nini???... Kaacha kazi ya kujiuza au??"
"bora hata angeacha kazi na kubaki mjini.. Lakini sasa, pole mwaya kaka, kama ni huyo umemkosa"
"we leah??... Usimwambie ukweli bwana hata sisi ni wanawake tunahitaji wanaume..... We kaka, huyo mtu unaemtafuta kagongwa na gari juzi kafariki na sasa hivi yupo mochwariiiiiii, hapa tunatafuta pesa tumsafirishe.... Wewe kama vipi twende ukanitumie, mimi pia ni msumbufu kama yeye, mana unaonekana unapenda wasumbufu sana"
"ati unasemaje we dada??... Sauda amefariki dunia"
"sasa unashangaa nini?, ina mana hujui kifo wewe?"
ENDELEA.........
Kawaida ya wadada wanaojiuza ni moja tu, hua ukipita mitaa yao wao huona kuwamba umefuata miili yao, hivyo unaweza kupatwa na hasira za bure uje kumjeruhi mtoto wa watu,.. Sahi alikuja danguro hapa almaarufu kama shivaz, ili kupata angalau fununu kuhusu dom, mana yeye ni mpelelezi hivyo hata akikuangalia kwa macho tu anaweza kukuhisi kuwa una jambo unalotaka kulisema,
Sahi akiwa katikati ya wasichana watano wazuri waliokuwa wakihitaji mwanaume, lakini kwa bahati mbaya sahi hakufuata swala hilo, hivyo kila anachokiuliza anajibiwa tofauti
Sasa unashangaa nini??, ina mana hujui kifo wewe?"
Aliongea dada mmoja ambaye ni mmoja kati ya hao machangudoa, lakini kabla sahi hajatamka neno, ghafla Leah akasema
"weee nisha, kumwambia mqenzio kafa sio vizuri, kwa mfano ni wewe afu unasikia unaambiwa umekufa ungejiskiaje... Acha hizo bwana nisha"
Aliongea Leah baada ya nisha kuongea uongo juu ya kifo cha sauda,
"aahhh, unajua leah sio kosa langu, hata sisi ni wanawake tunahitaji mwanaume, iweje umuelekeze alipo sauda, yaani akafanywe yule sisi tuachwe? Kwani hatutaki hizo pesa"
"ni sawa nisha, lakini sio kwa kumtakia mwenzio mabaya....... Sikiliza we kaka, huyo mtu unaemtafuta, karudi kijijini, maisha ya kujiuza yamemshinda"
Sahi kusikia tu kuwa mtu huyo karudi kijijini, alikata tamaa ya kuipata dom, mana huyo ndio anaemhisi kuwa ndio kachukuwa dom
"sikiliza wewe dada leah, mi naona tuachie hapo tu mana matumaini ya kumpata hakuna... Nashukuruni sana kwa msaada wenu"
Sahi aliwaambia hivyo wadada hao huku akirudisha mguu nyuma ili kuondoka,
"kaka si unichukie basi"
Aliongea dada aitwaye nisha, eti achukuliwe na sahi aende akatafunwe,
"Kiukweli mimi ni mtu hadhi yangu, ukikijua cheo changu, hutotamani hata kulala na mimi... Nyote ni wasichana wazuri sana cha kuwashauri tafuteni mitaji muachane na hizo kazi, mkumbuke kuwa mtazeeka, na mkisha zeeka hamuwezi kuifanya hio kazi tena, sasa kama hujajichumia sidhani kama utaweza kuishi mjini tena"
Sahi aliongea kweli kila mtu aliingiwa na maneno hayo lakini kwao haikuwa na jinsi mana ni ukosefu wa ajira Tanzania hivyo hawana budi kuifanya kazi hiyo
Sasa baada ya sahi kuongea hivyo, ndio wakaamini kweli huyu mtu hakuwa akihitaji mwanamke kwa ajili ya mapenzi
"samahani kaka etu, kwani ulikuwa unamtakia nini"
Aliuliza nisha yule yule aliokuwa kimbelembele wa kutaka ngono zembe...
"Kiukweli, sina uhakika na hili, ila siku ya kwanza kufanya mapenzi na yule dada, siku ile kuna kifaa nilikipoteza, lakini sikua nimekagua begi langu, hivyo jana ndio nikaligundua hilo na kuwaza nije nijaribu hata kumuuliza yule dada,.. Lakini sasa hayupo Nitafanyaje"
Masikini ya mungu sahi aliongea kwa uchungu sana mana anajua dom ndio imeshapotea hivyo... Sasa baada ya sahi kuingea hivyo, nisha akadakia juu kwa juu
"leah, au ni kile kidude alichokuja nacho siku ile"
"labada itakiwa ndio hicho"
Sasa sahi kusikia kuwa kuna kidude alikuja nacho, ikabidi atoe simu yake na kuwaonyesha
"hicho kidude ni kama hiki"
Sahi aliwaonyesha pocha kupitia simu yake,
"ndio"
"ndio"
"ndio.... Tena nikamwambia aende akakiuze ili tupate pesa ya kula, Kiukweli hakurudi nacho kile kidude, tena akatuomba nauli tukampa arudi zake kijijini mana anatuletea jam tu"
Sahi alipandwa na kichaa kuskia hicho kidude kweli alikuwa nacho,
"nani anajua kijijini kwao"
Wote wakamnyooshea kidole Leah
"huyu hapa huyu, mana ndie aliemleta"
"eti dada, unapajua kwao vizuri"
Sahi alimuuliza leah ambaye ni mkuu wa kikosi hicho cha watu kama saba hivi, ila sasa wamepungua kwasababu sauda hayupo, ila hapa wapo watano na mmoja wa sita haijulikani alipo
"ni kweli napajua, mana ni kijiji kimoja na mimi"
Aliongea leah mschana mzuri aliobarikiwa kila ina ya uzuri wake, yaani umbo lake Mashalaah, sura yake Mashalaah.. Kifua chake Mashalaah, rangi yake ya maji ya kunde, ndio iliomfanya akawa mzuri kupitiliza, ila sasa kazi yake tu ndio chafu, yaani leah hata usiwe rijali lakini huezi kosa kumtamani, yaani ni bonge la toto wacha mchezo,... Alibarikiwa kupewa kalio mtoto wa kike, figa analo... Lakini kakosa mume, kakosa kazi ya maana... Serikali yetu hii bwana, inapoteza warembo, na pia sio leah tu karibia wote ni wazuri tena hua wanazidiana kwa vitu tofauti tofauti...
"tafadhali sana dada yangu, naomba unipeleke hapo kesho Please dada yangu"
Sahi alitamani hata kupiga magoti ili dada huyo akubali,...
"leah, mpeleke tu kaka wa watu"
Waliongea wale rafiki zake, huku leah akitamani kweli kumpeleka,... Machangudoa walikuwa wengi sana eneo hilo, yaani kila kikundi kinatamani sahi aponywe na kile kikundi kingine cha akina leah mana wanakaa kikundi kikundi, kwasababu kuna mijidume MoonVisioner.Blog.Com ngine inachukuaga wote wakamshike shike tu..
"sawa, nioo tayari kufanya hivyo... Lakini mimi sina nauli afu kwao ni huko tanga ndani ndani huko wanakuita magoma"
Aliongea leah tena kwa upole
"kuhusu nauli, kula, kuvaa, kulala, kila kitu niachie mimi... Kikubwa ukubali kunipeleka"
"basi nimekubali kukupeleka... Kesho njoo geto kwetu twende mana sisi mchana tupo nyumbani tu"
"hapana, yaani tunakwenda sasa hivi, yaani hata kukuacha hapa naona nitakupoteza na wewe"
Sahi aliongea hivyo huku akitoa waleti mfukoni na kutoa kiasi cha laki nne na kuwapa akina nisha laki moja moja kila mmoja, mana walikuwa watano pamoja na leah sasa kwakuwa leah anaondoka hivyo wapewe hao wanne kwanza...
"jamani, tunakwenda kulala hoteli gani"
Aliuliza leah huku akitamani naye apewe pesa,
"usijali mama utakwenda tu"
Sahi aliongea kwa furaha kubwa sana huku leah akisema tena
"mbona mi hunipi"
"wewe malipo yako ni tofauti na hawa, endapo kazi utakapoimaliza"
"mmmhh sawa, sasa hata ya matumizi sipati"
"sasa kula kwangu kulala kwangu, kuvaa kwangu shida yako nini dada leah"
"ok poa"
Leah alikubaliana na sahi... Huku wakiwaaga akina nisha, lakini nisha hakuacha kumtumia rafiki yake meseji,
"LEAH KIPENZI CHETU, KAMA KUTAKUWA NA TATIZO TUJULISHE... MANA WANAUME HAWAAMINI NDUGU YANGU... KUWA MAKINI SANA"
nisha alimtumia leah meseji hio, wakati huo leah ndio anapanda gari la sahi, kisha haoo
Wakiwa njiani, Leah ndio anaifungua ile meseji kisha akamjibu
"USIJALI NISHA NITAKUWA MAKINI, ILA NAWASIHI MSIGOMBANE, AFU PIA SIONI HAJA LEO YA KUWEPO HAPO, MUMESHAPATA PESA BORA MUONDOKE TU HAPO... KALALENI TU"
Leah anawapenda sana rafiki zake, na anawajua hawaishi kugombana pindi wanapoulizana vipatao walivyoingiza kwa siku fulani....
Leah kwa mawazo yake anajua anapelekwa hotelini, lakini alishangaa kaletwa Ostabei kwenye jengo la kifahari, yaani leah alibaki kushika mdomo kwa jengo lilivyo zuri na la kifahari hajawahi hata kuingia, yaani licha ya kuishi, hata kuingia kwa kuomba maji katika majengo kama hayo hajawahi...
"hapa ndio wapi kaka"
Leah aliuliza,... Machangudoa ni watu wenye hekima kwa wachache sema kazi yao ndio inawafanya kuwa wabaya...
"hapa ni nyumbani"
Sahi alijibu kwa ufupi, lakini leah hakuridhika na jibu hilo
"ni nyumbani kwako"
"ndio"
Leah kashangaa sana kusikia ni nyumbani kwake,... Afu kijana mwenyewe ni mdogo sana, hafananii na jengo hilo,...
"mkeo akiniona je"
Aliuliza leah
"sina mke"
"jumba lote hili unaishi peke yako"
"ndio"
"kwanini usioe na una maisha mazuri hivi"
"nitamuoa nani na wanawake wenyewe ndio nyie mliojikita kwenye kazi hizo..... Uliona wapi mwanaume akaoa changudoa"
Leah alijiskia vibaya kwa maneno hayo, mana pamoja na uzuri wake wote kuolewa kwake ni bahati sana, tena ataolewa na mwanaume ambae hamjui,.. Leah alitamani hata asishuke katika gari kwa aibu ya maneno ya sahi,... Lakini alishuka tu mana hawezi kukaa moja kwa moja katika gari
Lakini sasa sahi alipomwangalia, alimwona kavalia nguo zake zile za uchangudoa.. Yaani kigauni kilikuwa chepesi alafu kifupi kilichoishia katika mapaja juu kabisa... Sahi alimsogelea mpaka karibu yake na kumuuliza
"ivi huna nguo nyingine katika mkoba wako"
"mh mh sina kaka angu"
Jamani leah ni mzuri acheni utani, ni mtoto aliobarikiwa vyote kasoro kazi tu,.
"ukiwa na mimi hizi ngu hazifai, ni kqeli si kweli"
Aliongea sahi huku akikashika kale kagauni
"afu hata chupi hujavaa, ni kweli si kweli"
"kweli kaka angu, umejuaje"
"si nnaona hapo jinsi ulivyo mlaini"
"Samahani kwa hilo"
"siwezi kwenda na wewe hio safari ukiwa na nguo hizo... Naomba twende Kariakoo ukachukue nguo"
Aliongea sahi huku akirudi katika gari, leah hakukataa aliingia katika gari kisha haooo wakatoka
Jijini Dar es Salaam, ikifika saa mbili za usiku, utafikiri ndio kumekucha mana biashara ndio zinashamiri kwelikweli,.. Na ndio wakati wenyewe wa majira ya saa mbili za usiku,.. Kariakoo katika duka kubwa la nguo ambalo hata leah hakutazamia kuingia hapo mana ni maduka ya nguo za kike za matajiri... Na ni sehemu inayouza nguo aina zote
"fanya fasta twende"
Aliongea sahi huku leah akishuka na kuuliza swali
"nani atalipa"
"we kachague nguo mi nakuja kulipa"
Sahi anamueshimu leah kwakiwa anampa msaada mkubwa sana juu ya kupata dom,.. Mara kinasa sauti cha sahi kinasikika kikisema
"GU"
Ukisikia tu hio GU ujue ni raisi GU anampigia simu kupitia simu ya siri ambayo ipo oni muda wote,
"yes GU"
"BB, kesho una misheni gani"
"kesho naelekea tanga mkuu"
"kuna nini huko tanga"
"Nimemisi dom ipo eneo hilo"
"ok, kuna kazi nilitaka kukupa ya kumpeleleza waziri wa fedha.. Sasa maliza kwanza hio kisha utafanya kwa wakati mwingine"
"sawa..."
"afu hii sauti ya mtoto wangu,.. Uliirekodi ukiwa wapi"
"nilikuwa TSS"
"na alimpigia nani"
"alimpigia General Nyange"
"ahaaaa.... Ngoja kesho nitawaita Ikulu wote, nataka niwatumbue mbele ya kadamnasi"
"mzee, hata mtoto wako"
"hata baba yangu, kama ana kosa mlete nimtumbue jipu"
"mama yako je"
"BB, unaleta utani na kazi"
"nalo pia ni swali, mfano nimemkuta mama yako ni Jipu"
"aahhhhh mama tutaangalia na kosa bwana.... Weww fanya kazi maswali ya kijinga sitakic
"ahahahahahahahahahahaah.... Nimeshaju mama yako huezi mtumbua majipu wewe"
"pumbavu wewe"
Simu ilikata, lakini sahi aliingizia utani kidogo na mzee GU,.. Ila kale a taarifa kuwa General nyange na Joseph John kesho ni jipu mbele ya kadamnasi, shuguli nzima itafanyika Ikulu jijini Dar es Salaam....
Huku ndani ya duka, leah kachukuwa nguo nyingi kweli, Madera, mahijabu na wakati yeye Mkristo, sketi za heshima magauni marefu, yaan nguo nyingi sana zilikuwa ni za heshima, mana kuambiwa na sahi kuwa akiwa naye hataki nguo aina hizo fupi fupi, hivyo leah kachagua nguo nyingi za heshima... Dukani palikuwa na mama wa makamo aliokuwa akiuza duka hilo,... Kumbe yule mama ndie aliekuwa akimchagulia nguo nzuri tena mama alikuwa akimsifu sana leah,...
"naona umekuja na mumeo.... Kiukweli ni wanawake wachache sana tulio bahatika kuwa na wanaume kama wakwako"
Aliongea mama huyo huku leah akitabasamu na kusema
"Ahsante mama angu"
"unajua binti, nyinyi wasichana wengi hamjui jinsi ya kuishi na wanaume zenu, na ndio mana hamuishi kuachwa"
Aliongea mama huyo, lakini alipomwangalia leah aligundua hakuwa na chupi, yaani nguo nyepesi ukivaa, lazima ijulikane
"hata hili nalo ni kosa... Unapotoka na mumeo kwenda sehemu yeyote ile nje ya nyimba yenu, unatakiwa uvae kiheshima, ili mumeo asifiwe kapata mke bora,.. Hiki kingua ulichovaa, unatakiwa ukivae chumbani kwako... Hii ni ishara ya kumtamanisha mwanaume mwingine ingali unae wakwako... Hili nalo ni tatizo wanaume wengi hawapendi kuona wake zao wanatoka nje na nguo za ajabu ajabu,.. Hebu njoo huku kuna taiti nzuri za kischana"
Mama alizidi kumtapikia leah maneno. Mazuri yaliomfanya leah kukaa kimya muda wote..
"ukivaa taiti kama hii, makali yako hayawezi kutetemeka na kumtamanisha mwanaume asie wako"
Leah alichukuwa nguo hizo, lakini sasa ni kazi bure kwa leah mana kazi yake haimruhusu kuvaa nguo kama hizo, na akivaa atakosa wateja, mana hatovutia tena...
"njoo huku kwenye chupi... Sasa hapa chagua chupi ambazo mumeo anapenda kuziona.."
Masikini ya mungu leah machozi yalimtoka, yqani maneno anayo yapewa laiti kama ingelikuwa ni kweli sijui ingelikuwa, sasa hapa leah ndio anajua kuwa changudoa, yaani anajuta mno...
"ona kama hii, yaani ukivaa chupi nyepesi kama hii, mmeo lazima apande mlima hata kama kachoka kiasi gani,.. Sikiliza binti yangu, mimi najua wasichana wengi hamjui sheria za ndoa, hamjui jinsi gani ya kuwashawishi waume zenu,.. Sio lazima umuite apande mlima... Nguo tu yenyewe inamuita"
Leah ndio kabisa machozi yanamtoka masikini ya mungu, wakati huo kawa mpoleew, maneno ya huyo mama yalimuingia vizuri sana..
"ivi ulisema unaitwa nani vile"
"naitwa leah"
"sasa unalia nini leah?"
"maneno yako Anti,.. Nahisi maneno yako yananitoa pangoni"
Leah alimaanisha kuwa maneno ya mama huyo yanamshawishi kuacha uchangudoa...
"una maana gani binti"
"anti, mimi nilikuwa siyajui hayo, naona unanifumbua maskio"
"usijali binti yangu, nanhata siku nyingine ukipenda kuja hapa njoo tu nikufundishe jinsi ya kuishi na mume wako"
"sawa anti, nitakuja tu"
"ok sasa hapa, pia una kosa moja tu"
"kosa gani anti"
"hapa kwenye nguo za ndani, unatakiwa uje na mumeo akuchagulie nguo anazopenda yeye... Hebu muite"
Maskini Leah ndio anazidi kuumia roho yake,.. Mtu huyo sio mume wake tena hapo anamtendea msaada tu wa kumpeleka tanga,..
"binti, we binti"
"abee anti"
"una nini??...muite baba watoto mje msaidiane kuchagua... Mana sharti mume ajue vigagula vyako, mana ni kazi yake kuvivua... Hebu muite"
Leah anafikiria ataanzia wapi, sahi wala hana mazoea nae tena ndio kwanzaa wamekutana leo, sasa aanzeje kumuita mume, na mbaya zaidi ni changudoa, yaani hata yeye mwenyewe anajionea aibu kujiita mke wa fulani,... Leah alilia sana huku akifikiria jinsi ya kumuita sahi aje wachague nguo za ndani, na mbaya zaidi hata jina la sahi halijui.. Yaani hamjui kabisaaaaaa... Leah anatamani kumwambia huyo mama kuwa yeye ni changudoa tu, na huyo sio mume wake.. Wakati huo mama anakazania leah amuite mume wake waje wachague nguo za ndani na hio ndio furaha ya ndoa mahaba ya dhati katika ndoa......
Je? Nini kitaendelea???... Leah atafanyaje na wakati keshasifiwa vya kutosha??? USIKOSE