Muziki: Unofficial Weekend
Unajua kabisa sitachoka kukuuliza u khali gani Kapuku mheshimika, na kama kawaida ulizo langu sio lile la swali bali ni la maelezo, majibu yanajulikana, yakiwa mazuri sawa yakiwa tofauti naypo ni sawa na kaa ukijua kukaa kimya nako ni jibu. Ni furaha sana kukuona hapa maana bila wewe KF isingekuwa jukwaa bora kabisa hapa JF.
Ulishwahi kujiuliza na kujiswalisha bila kupewa maswali, well, labda nakuchanganya na siruhusiwi kufanya hivyo maana yapo mengi yanayokuchanganya na maandishi yangu hayapaswi kuwa moja wapo ya vingi vinavyokuchanganya. naandika vitu rahisi rahisi tu na nikimaliza natoa shukrani kwa wadau waliolichangamsha Jukwa siku ya leo, mtaasisi mwenzangu
Nyagei na
Linamo asanteni kwa kutuchangamsha, siwasahau wadau wote ambao uwepo wenu hapa unalifanya Jukwaa hili kuwa sehemu bora kabisa. Niseme nini kingine.
Muziki sasa; unaweza kujiuliza kwanini jana ilikuwa vile tofauti na juzi wakati ambapo tunaishi leo na kuipanga kesho! shangaa hata wewe maana nilichoandika usikurupuke kuwa sieleweki, jipe muda na utajua ukikumbuka mabaya ya jana utajirekebisha na kama kuna lililokuliza hakika hutopenda litokee tena ama kwako au kwa mwingine na zaidi kukumbuka mambaya ya jana huwa haisaidii kwani utabaki kuumia tu. Ukitaka kuikumbuka jana usiisahau na juzi maana juzi ilikuwa ya furaha. Tuburudike na vijana wa enzi hizo waliojitwalia tuzo ya Grammy na nyingine nyingi sana.
Muziki wa wadhamini na wapendanao utakujia hivi punde