Makapuku Forum

Makapuku Forum

Muziki: Jumatano ya Majoka

Ni siku nzuri kabisa kwa kila mmoja hapa (hata kama ni mbaya mimi najiaminisha tu kuwa umekuwa na siku nzuri), kwani uongo jamani, si wote ni mashuhuda hapa KF kumechangamka utasema mtindi uliotiwa ndimu. Vitu vingine havijaribiwi, na kwa kuwwa wewe u sehemu ya makapuku basi Jukwaa hili ni sehemu bora kabisa kuwepo. Mimi nipo, wewe pia, na yule asiyekuwepo bado akija hatokosa kitu.

Ni furaha kuonana kila mmoja akiwa amechangamka, kuna vingi vinavyochangamsha na ukichangamshwa vinachangamka na vingine vinasisimka. Unajua nini, uchangamfu ni jambo zuri kwa sehemu yake na inapotokea unachangamka kupitiliza basi wengine watachangamka kupita kiasi. Asante sana kwa mzeewakungoa kwa kulichangamsha Jukwaa leo, you rock! Kile sijui ni kilugha gani me nikaishia maneno utamu na sikukunda, anyway.

Muziki sasa, mnajua pale mwanzo nilitaka kutunuku wimbo kwa husna muba , huyu ni mtu muhimu kwangu, ikiwa hujui jua hilo. Baadaye nikapata ombi la Sakayo ambalo namshukuru sana Transcend kwa kutupia wimbo wa Z-Anto kijana wa Kigamboni. Well, nimetafakari nikagundua kutokana na kibaridi hiki wengine kuoga mtihani, ni mwemndo wa pasport tu. Sasa husna muba nitamtunuku wimbo siku kila mmoja akiwa ameoga mwili mzima.

Kujiandaa na kuoga mwili mzima lazima uchangamke na ninakuchangamsha kwa chaguo la anko wangu lee empire akiungana na pedeshee mwenzake Koffi Olomide, Mopao muzee ya batoto anahgawa cheni za gold wewe gawa shanga zifuliwe kwa foma gold.

Nakupenda Kapuku mwenzangu na unalijua hilo. Burudika




NB: Nawashukuru wote ambao mnakuwa na nafasi ya kupendekeza wimbo, heshima kwenu sana

Hapo kwenye cheni za gold wewe gawa shanga umetisha bila kinyago

......
 
ISAYA 49

14.Bali Sayuni alisema,YEHOVA ameniacha,BWANA amenisahau.

15.Je!Mwanamke aweza kumsahau mtoto wake anyonyaye,hata asimuhurumie mwana wa tumbo lake?Naam hawa waweza kusahau lakini mimi sitakusahau wewe.

16.Tazama,nimekuchora katika vitanga vya mikono yangu,kuta zako ziko mbele yangu daima.

WAPENDWA..MUNGU NI BABA YETU,HATUSAHAU KAMWE AMETUCHORA KATIKA VITANGA NI UPENDO WA MILELE

ASANTE BABA kutufikisha usiku huu salama,asante kwa yote uliyotutendea,asante kwa neema mchana kutwa..tuma malaika walinzi watuzingire mpaka asubuhi,tunavunja kazi zote za muovu shetani usiku huu ,Damu ya YESU itufunike...ponya wagonjwa,fariji wafiwa,watie moyo waliovunjika moyo tuguse BABA majeraha yetu ni mengi tupate uponyaji wa mwili na roho katika jina la Yesu Amen

USIKU MWEMA MBARIKIWE MAKAPUKU WOTE..MUNGU HAJAWASAHAU,HATAWASAHAU AMEWACHORA KATIKA VITANGA ..ANAWAGUSA MGUSO MTAKATIFU AMEN

Sent from my TECNO H6 using JamiiForums mobile app
 
ISAYA 49

14.Bali Sayuni alisema,YEHOVA ameniacha,BWANA amenisahau.

15.Je!Mwanamke aweza kumsahau mtoto wake anyonyaye,hata asimuhurumie mwana wa tumbo lake?Naam hawa waweza kusahau lakini mimi sitakusahau wewe.

16.Tazama,nimekuchora katika vitanga vya mikono yangu,kuta zako ziko mbele yangu daima.

WAPENDWA..MUNGU NI BABA YETU,HATUSAHAU KAMWE AMETUCHORA KATIKA VITANGA NI UPENDO WA MILELE

ASANTE BABA kutufikisha usiku huu salama,asante kwa yote uliyotutendea,asante kwa neema mchana kutwa..tuma malaika walinzi watuzingire mpaka asubuhi,tunavunja kazi zote za muovu shetani usiku huu ,Damu ya YESU itufunike...ponya wagonjwa,fariji wafiwa,watie moyo waliovunjika moyo tuguse BABA majeraha yetu ni mengi tupate uponyaji wa mwili na roho katika jina la Yesu Amen

USIKU MWEMA MBARIKIWE MAKAPUKU WOTE..MUNGU HAJAWASAHAU,HATAWASAHAU AMEWACHORA KATIKA VITANGA ..ANAWAGUSA MGUSO MTAKATIFU AMEN

Sent from my TECNO H6 using JamiiForums mobile app
Ubarikiwe ....!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom