Muziki: Jumatano ya Majoka
Ni siku nzuri kabisa kwa kila mmoja hapa (hata kama ni mbaya mimi najiaminisha tu kuwa umekuwa na siku nzuri), kwani uongo jamani, si wote ni mashuhuda hapa KF kumechangamka utasema mtindi uliotiwa ndimu. Vitu vingine havijaribiwi, na kwa kuwwa wewe u sehemu ya makapuku basi Jukwaa hili ni sehemu bora kabisa kuwepo. Mimi nipo, wewe pia, na yule asiyekuwepo bado akija hatokosa kitu.
Ni furaha kuonana kila mmoja akiwa amechangamka, kuna vingi vinavyochangamsha na ukichangamshwa vinachangamka na vingine vinasisimka. Unajua nini, uchangamfu ni jambo zuri kwa sehemu yake na inapotokea unachangamka kupitiliza basi wengine watachangamka kupita kiasi. Asante sana kwa
mzeewakungoa kwa kulichangamsha Jukwaa leo, you rock! Kile sijui ni kilugha gani me nikaishia maneno utamu na sikukunda, anyway.
Muziki sasa, mnajua pale mwanzo nilitaka kutunuku wimbo kwa
husna muba , huyu ni mtu muhimu kwangu, ikiwa hujui jua hilo. Baadaye nikapata ombi la
Sakayo ambalo namshukuru sana
Transcend kwa kutupia wimbo wa Z-Anto kijana wa Kigamboni. Well, nimetafakari nikagundua kutokana na kibaridi hiki wengine kuoga mtihani, ni mwemndo wa pasport tu. Sasa
husna muba nitamtunuku wimbo siku kila mmoja akiwa ameoga mwili mzima.
Kujiandaa na kuoga mwili mzima lazima uchangamke na ninakuchangamsha kwa chaguo la anko wangu
lee empire akiungana na pedeshee mwenzake Koffi Olomide, Mopao muzee ya batoto anahgawa cheni za gold wewe gawa shanga zifuliwe kwa foma gold.
Nakupenda Kapuku mwenzangu na unalijua hilo. Burudika
NB: Nawashukuru wote ambao mnakuwa na nafasi ya kupendekeza wimbo, heshima kwenu sana