NUKUU YA LEO
There have been some people and non-governmental organizations advocating for this idea, but it will not happen when i am in office, this is against our ethics.
Kumekuwepo na baadhi ya watu na mashikira yasiyo ya kiserikali kuunga mkono hoja hii, lakini hii haitatokea katika utawala wangu, hii ni kinyume na maadili yetu.
Haya maneno yalitamkwa na Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dr. Johj Pombe Magufuli Tar. 22/06/2017. Rais Johj P Magufuli alizaliwa tar. 29 /10/1957 katika wilaya ya Chato, mkoa wa Kagera wakati huo nchi ikiitwa Tanganyika.
Rais Johj Magufuli anakuwa kiongozi wa juu kabisa kuja na kauli hii ambayo watanzania na ulimwengu kwa ujumla wameipokea kwa mtazamo hasi, kwa kuwa duni na ulimwenguwa sasa umekuwa ukipigania sana elimu na kundoa vikwazo hasa kwa wasichana na wanawake ambao ndio kundi kubwa linaloathirika kwa kukosa elimu.
Hii kauli itabaki kuwa kati ya kauli tata kutolewa na rais huyo, kwani wiki 2 zilizopita makamu wa rais alitangaza kuunga mkono na kuwakumbushia wazazi wote wenye watoto waliojifungua kwa mimba za utotoni kuwarudisha shuleni kwa kuwa hiyo ni
sehemu ya ilani ya ccm ambayo yeye na magufuli wanaitekeleza.
Vyombo vingi vya habari vya kimataifa, mitandao ya kijamii imechukulia suala hili
kama ukosefu wa busara, ukandamizaji na unyanyasaji wa kijinsia.
Wakati Rais akisema hayo alikuwa mbele ya Mke wa Rais wa zamani mama Salma Kikwete ambae pia ni mwenyekiti wa WAMA(Wanawake na maendeleo Foundation) NGO ambayo pia inapigania haki na usawa kwa wanawake na wasichana.
Wakuu ; Hii kauli ya rais ni ya kupigwa, sidhani kama kuna mtu atakuwa anaunga mkono juhudi ya ajabu namna hii, tutapoteza kizazi kwa mwendo huu.
Picha ikiwa inamuonesha mmoja ya wanafuzi wajawazito.
Maisha baada ya kujifungua.
mwanafunzi mwenye mimba akiwa shuleni.
Rais JPM
Moja wapo ya mambango elimishi yaliyochapiswa mtandaoni na NGO ya WAMA.
Hapo chini niweka link ! Ni video ya dakika 2:30...


Hii nimeileta kwa hisan ya
Sakayo ,
Shunie Tumosa Madame S,
Clkey ukhuty Jimena BlessedHope,
demi Jovitha na wanawake wengine woote.