Makapuku Forum

Makapuku Forum

JEREMIA 33

BWANA MUNGU ASEMA

3.Niite nami nitakuitikia,nami nitakuonesha mambo makubwa ,magumu usiyoyajua

BABA Asante kutuamsha salama,asante kwa zawadi hii nzuri kabisa ya uhai asante kwa kuitika kila tunapokuita,unatujua vyema na wala hujawahi kutuacha...tunakuona MUNGU wetu daima unatuitikia.
Tunaomba toba tunapoanza siku ya leo tuanze tukiwa tumeyaacha yote ya nyuma na kuanza upya maana ni siku mpya kabisa uliyoifanya BWANA.

Tunaomba utujalie afya njema,amani,mshikamano,msamaha,uvumilivu,upendo na yote yanayofanana na hayo.

Ponya wagonjwa,watie moyo waliopondeka mioyo,wafungulie wafungwa na wape faraja yatima na wajane.

Bariki kazi za mikono yetu na utufundishe kufanya kazi kwa bidii.

Tuopoe katika hatari zote za mwili na za roho,tuwe salama.

Asante BABA kwa kutuitikia

Tunaomba kwa
jina la Yesu Amen

MUWE NA SIKU NJEMA MBARIKIWE
Ameen Mama ubarikiwe
 
Tafakar ya kirat. ..
4c040f7ff79cb74a02fa267987cbd0eb.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom