Makapuku Forum

Makapuku Forum

je wajua..??
Kuwa baba sio tu kuwa na uwezo wa kumpa mwanamke ujauzito na kuzaa mtoto. Kuwa baba sio suala la kibaiolojia tu. Kuwa baba sio wadhifa. Kuwa baba ni jukumu na utayari wa kubeba majukumu. Kuwa baba ni nafasi ambayo sifa na pongezi huja baada ya matokeo, kuwa baba nikuwa na uwezo wa kujitoa mhanga kuhakikisha familia yako inatabasamu hata kama gharama ya tabasamu lao inatokana na wewe kununa au kuteseka. Kuwa baba ni uwezo wa kuhakikisha furaha ya watu wa familia yako inaitangulia furaha yako na sio kuitanguliza furaha yako mbele na kuisahau ya wanaokuita baba. Being a father is a serious business that deserve serious people.
 
Pole na TANESCO nadhani ni tatizo kubwq huku kwetu sijui kama wametuacha salama ni kuzima na kuwasha mara umeme kuwa mdogooo na kurudi ghafla tena...tuombe uwe umetulia sasa.

RIP Chiku na mtoto so sad mama na mtoto kupotea pamoja tena kwenye hospitali kongwe hadi uzazi unakuwa tishio kwa wanaotafuta watoto..Mungu awatie nguvu na kuwapa faraja Mzee Yusuph, ndugu, jamaa na marafiki kwa msiba huu mzito .

Asante kwa ratiba na mambo ya michezo mkuu Nyagei kazi yako ni njema ubarikiwe
Ahsante mama mchungaji



Ubarikiwe
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom