Makapuku Forum

Makapuku Forum

eef30f85a4064a91281d90dbb2c1130f.jpg
 
WARUMI 8

31 Basi tuseme nini juu ya hayo MUNGU akiwa upande wetu ni nani atakuwa juu yetu?

32 Yeye asiyemwachilia Mwana wake mwenyewe bali alimtoa kwa ajili yetu sisi sote. Atakosaje kutukirimia mambo yote pamoja naye

33 Ni nani atakayewashitaki wateule wa MUNGU? MUNGU ndiye mwenye kuwahesabia haki

34 Ni nani. atakaye wahukumia adhabu? Kristo Yesu ndiye aliyekufa naam; na zaidi ya hayo amefufuka katika wafu yuko mkono wa kuume wa MUNGU tena ndiye anayetuombea

35Ni nani atakaye tutenga na upendo wa Kristo? Je! Ni dhiki au shida, au adha, au njaa, au uchi, au hatari, au upanga?

36 Kama ilivyoandikwa, ya kwamba, kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa, na tumehesabiwa kuwa kama kondoo wa kuchinjwa

37 Lakini katika mambo yote hayo tunashinda, zaidi ya kushinda, kwa yeye aliyetupenda

38 Wala yaliyo juu wala yaliyo chini wala kiumbe kinginecho chote hakitaweza kututenganisha na upendo wa MUNGU Ulio katika Kristo Yesu Bwana wetu

MUNGU ANATUPENDA SANA NDIO MAANA TUPO MPAKA MUDA HUU HAKUNA CHA KUTUTENGANISHA NAE TUKAZE MWENDO TUMSHUKURU TUMPENDE ANATUPA KUSHINDA KILA WAKATI. MBARIKIWE MCHANA MWEMA
 
WAFILIPI 4

1 Basi ndugu zangu, wapendwa wangu, ninawaonea shauku, furaha yangu, na taji yangu, hivyo simameni imara katika BWANA, wapenzi wangu.

4 Furahini katika BWANA siku zote tena nasema furahini

5 Upole wenu na ujulikane na watu wote BWANA yu karibu

6 Msijisumbue kwa neno lolote, bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru haja zenu na zijulikane na MUNGU

7 Na amani ipitayo akili zote itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu

MUWE NA JIONI NJEMA MBARIKIWE
 
Ndoo maana mm kiroho safi napachika picha tu


Ha ha ha ahaha, hata hiyo kupachika picha tu ingekuwa rahisi kila mmoja wetu angeweza. Si lazima uisome picha na uone kamainaweza kuwa na maana hapa jukwaani.

Unafanya kazi sana anko na tunaipenda, sio rahisi na ingekuwa ni hivyo hata mimi ningeweza, sema nilichonacho ni saa na simu ya tachi tu, sio simu ya kamera
 
WAFILIPI 4

1 Basi ndugu zangu, wapendwa wangu, ninawaonea shauku, furaha yangu, na taji yangu, hivyo simameni imara katika BWANA, wapenzi wangu.

4 Furahini katika BWANA siku zote tena nasema furahini

5 Upole wenu na ujulikane na watu wote BWANA yu karibu

6 Msijisumbue kwa neno lolote, bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru haja zenu na zijulikane na MUNGU

7 Na amani ipitayo akili zote itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu

MUWE NA JIONI NJEMA MBARIKIWE

Asante BH, kufurahia ni haja ya kila mmoja ila la kujiuliza unafurahia nini? Ukifurahi katika Bwana basi hiyo ni heri sana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom