
WARUMI 8
31 Basi tuseme nini juu ya hayo MUNGU akiwa upande wetu ni nani atakuwa juu yetu?
32 Yeye asiyemwachilia Mwana wake mwenyewe bali alimtoa kwa ajili yetu sisi sote. Atakosaje kutukirimia mambo yote pamoja naye
33 Ni nani atakayewashitaki wateule wa MUNGU? MUNGU ndiye mwenye kuwahesabia haki
34 Ni nani. atakaye wahukumia adhabu? Kristo Yesu ndiye aliyekufa naam; na zaidi ya hayo amefufuka katika wafu yuko mkono wa kuume wa MUNGU tena ndiye anayetuombea
35Ni nani atakaye tutenga na upendo wa Kristo? Je! Ni dhiki au shida, au adha, au njaa, au uchi, au hatari, au upanga?
36 Kama ilivyoandikwa, ya kwamba, kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa, na tumehesabiwa kuwa kama kondoo wa kuchinjwa
37 Lakini katika mambo yote hayo tunashinda, zaidi ya kushinda, kwa yeye aliyetupenda
38 Wala yaliyo juu wala yaliyo chini wala kiumbe kinginecho chote hakitaweza kututenganisha na upendo wa MUNGU Ulio katika Kristo Yesu Bwana wetu

MUNGU ANATUPENDA SANA NDIO MAANA TUPO MPAKA MUDA HUU HAKUNA CHA KUTUTENGANISHA NAE TUKAZE MWENDO TUMSHUKURU TUMPENDE ANATUPA KUSHINDA

KILA WAKATI. MBARIKIWE MCHANA MWEMA